Posts Tagged ‘kinyerezi’
Dar es Salaam: Daraja Kinyerezi – Maendeleo
Hili ndilo Daraja la Kinyerezi-Majumbasita linaloendelea kujengwa. Hatua ya ujenzi iliyofikiwa inatia moyo. Lakini ni muhimu mkandarasi aongeze kasi. Wananchi wamechoka kuvunjikiwa na daraja la muda kila baada ya miezi michache. Ili kasi ya maendeleo iwe ya kutosha, ni muhimu miundombinu kama hii ijengwe katika kasi ya uhakika na kwa viwango bora. Endapo haya yamezingatiwa katika ujenzi wa daraja hili, basi litakuwa na mchango mkubwa sana kwa ukuaji wa uchumi wa Taifa hili.
Mungu ibariki Tanzania.
‘Daraja Hili … Thamani Yake ni Mvua ya Saa Tatu’
Ndivyo hali ilivyo katika daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea. Ni daraja muhimu kwani linategemewa na maelfu ya wakazi wa upande huo wa Dar es Salaam. Daraja la muda lilijengwa kwa muda wa miezi kadhaa. Malori ya mawe yalimwagwa hapo. Wajenzi wakatumia maarifa yao. Mamilioni ya fedha yaliingia hapo … sijui ni milioni ngapi. Kudumu kwa daraja hilo miezi michache tangu lijengwe kumekomeshwa na mvua iliyodumu kwa saa 3 tu! Hapa ndipo ninakumbuka kauli ya dereva wa daladala aliyetubeba ‘Thamani ya Daraja hili ni saa tatu ya mvua’!
Abiria wengine walijiuliza … ‘hasara hii ni ya nani’? Nani atabeba gharama za ujenzi mwingine wa daraja la muda? Miongoni mwa abiria hakuna aliyekuwa na majibu.
Hapa tunaona umuhimu wa kutumia maarifa yetu vema. Mwezi Desemba 2011 wakati wa mafuriko ya Dar, daraja lililokuwa hapo kwa miaka mingi lilisombwa. Hiyo ilitosha kabisa kutoa angalizo kwa wakandarasi walioshinda zabuni hiyo. Daraja la muda lilipaswa liwe madhubuti na kubwa kuliko lililokuwepo awali, na daraja la kudumu linalopaswa kuwa hapo linatakuwa kuwa kubwa sana, lililopanda juu sana na pana vizuri ili lisije kusombwa na mafuriko.
Tanzania ni yetu sote. Kila mmoja ajisikie uchungu na kuchukua hatua kukabili magumu yanayotusibu!
Ajali … Kinyerezi
Ni ya uso kwa uso … Hiace na Lorry
Viti vya kwenye Hiace … viliparaganyika na vingine kung’oka
Mparaganyiko wa viti kwenye daladala …
Barabara ilifungwa kwa muda … kisha magari yalianza kupita upande mmoja wa barabara kwa kusubiriana
Ni majira ya saa 2 usiku. Wakati ninawasili eneo la tukio, kiasi cha kama dakika kumi zilikwishapita. Ni basi dogo, Hiace, na lorry la kama tani tatu yaliyohusika na ajali hii. Magari haya kwa yanavyoonekana, yaligongana uso kwa uso. Baada ya kutazama, inaelekea kwamba dereva wa lorry ndiye aliyehama kutoka upande wake wa barabara na hatimaye kugongana na daladala hilo. Baadhi ya abiria waliokuwa kwenye daladala hilo bado wapo. Wengine bado wana mshtuko wa kuhusika kwenye ajali. Wananieleza kwamba walioumia hasa ni madereva wote wawili wa magari hayo. Madereva hao hawapo hapo lakini wamekwishatoka, hakuna aliyejua hasa wako wapi. Lorry lilikuwa likiteremka kwenye kilima kutoka upande wa Kinyerezi na Haice ilikuwa ikipanda kilima hicho kutoka Njia Panda Segerea.
Ajali. Barabara ni nyembamba na ina miteremko mikali kidogo na madaraja daraja. Ingawa hakuna aliyepoteza maisha katika tukio hili, lakini mtu unapata maswali mengi. Linaloumiza kichwa zaidi ni kuhusu umahiri wa madereva wetu hapa nchini. Ajali zilizo nyingi zinasababishwa na uzembe wa madereva. Mtu unajiuliza, hivi hizi leseni zilizo mikononi mwa madereva … wanazistahili kweli? Je, vigezo vyote na masharti yalizingatiwa kabla ya kuwapa leseni hizo? Je, polisi wa usalama barabarani wanafanya kazi yao kikamilifu … au ndiyo baadhi wanawalinda wahalifu wa makosa ya barabarani baada ya kulambishwa shilingi mbili tatu?
Tupige vita ajali. Tunaweza kuwa na barabara zilizo salama katika nchi yetu. Kila mmoja atimize wajibu wake vizuri. Pamoja sana!
Ajali … Segerea darajani … barabara nusu yafungwa
Kwanza nimekuta basi hili katika hali hii … na ni basi la shule … katika barabara inayounganisha Segerea na Kinyerezi Mbuyuni … mbele ni msululu wa magari uliokuwa ukienda kwa mwendo wa kinyonga …
Msululu wa magari yanayoelekea Kinyerezi …
Haya … hii ndiyo iliyokuwa sababu ya kasheshe nzima usiku huu … ni katika daraja linalounganisha Segerea na Kinyerezi …
Hali ilikuwa hivi …
Kwa mujibu wa mashuhuda … au waliodai kuwa mashuhuda, lori hilo lenye shehena ya mchanga lilishindwa kupanda mlima. Baada ya hapo lilianza kurudi nyuma. Hiyo pick up ilikuwa ikija kwa nyuma. Basi kasheshe yake ndiyo kama unavyoona. Habari zaidi zilieleza kwamba waliokuwa kwenye pick up walijeruhiwa na mpaka mimi nafika eneo la tukio walikuwa wamekwenda police ili kupata PF3 kwa ajili ya kwenda hospitali kwa matibabu.
Haya … karibu na Daraja linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita, kwenye barabara ya kwenda Mongo la Ndege, nimekutana na hii tena.
Kwa maelezo niliyopata hapa. Mbele ya hiyo gari ndogo kulikuwa na gari lingine lililoshindwa kupanda mpando mdogo ulio mbele kidogo. Dereva wa pick up, pengine alikuwa na haraka sana, aliamua kuovertake gari hili dogo … matokeo yake ndiyo hiyo pasi …
Ndiyo niliyoshuhudia usiku wa leo wakati narejea kijijini kwetu … Ya barabarani ni mengi, mengine makubwa.