simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Posts Tagged ‘ajali

Hali tete Daraja la Kinyerezi na Majumba Sita

leave a comment »


Darajani 22 march 1

Darajani 22 march 4

Darajani 22 march 2

Darajani 22 march 7

Darajani 22 march 6

Kwa ufupi, hii ni kuhatarisha maisha ya wapiga kura katika nchi hii. Ni zaidi ya wiki mbili sasa tangu daraja la muda livunjike wakati lori la kuchanganya zege likipita juu yake. Hadi wakati huu, sijasikia tamko lolote kuhusu mpango uliopo wa kurekebisha hali ya mambo. Sijamsikia Mbunge wa Ukonga wala Madiwani wa Kata za Ukonga, Kipawa, Segerea wala Kinyerezi akizungumzia suala hili. Sijamsikia Waziri wa Ujenzi akisema lolote kuhusiana na tatizo lililopo.

Pengine wakuu hao wanasubiri mtu au watu wapoteze maisha na mali zao kisha ndio wajitokeze. Hivi sasa hali ni tete katika eneo hilo. Watu wanaojaribu kuvuka kwa kutumia vyuma vya daraja lililovunjika wanafanya hivyo kwa kuhatarisha maisha yao na mali zao. Eneo si salama. Mawasiliano kati ya pande mbili hakuna. Hakuna gari wala pikipiki inayoweza kuvuka hapo wakati huu. Na huu ni mwanzo tu wa mvua za masika.

Chondechonde, serikali ilitazame eneo hili kwa namna ya pekee. Naamini tuna wahandisi wengi wazalendo wenye uwezo wa kubuni suluhisho la muda wakati daraja la kudumu likiendelea kujengwa. Hakika katika hili hatutawaelewa ikiwa hamtakuja na majibu ya haraka.

Ni muhimu hatua za haraka zichukuliwe. Kuna wazee, watoto, akina mama na wananchi wengine wengi wanaotumia barabara na daraja hili. Hivi sasa watoto wa upande mmoja wanaosoma shule upande mwingine, hawana tena fursa ya kwenda shule. Pale hapavukiki. Vivyo hivyo kwa watoto wa upande mwingine. Kwa watu wazima, watalazimika kupata adhabu ya kuzunguka njia ndefu ili kwenda kutafuta riziki za watoto wao na kodi mbalimbali wanazolipa serikalini. Maana yake, maisha yatakuwa ghali zaidi.

Kinachotakiwa hapa ni uamuzi mgumu. Mtuthibitishie kuwa mnaweza kufanya uamuzi mgumu na kuwarejeshea mawasiliano wapiga kura wenu.

Kwa pamoja, tunaweza.

Ghorofa Laporomoka … Ni Mumbai, India

leave a comment »


Ndugu, jamaa, mashuhuda na mtoto aliyeokolewa kutoka kwenye janga hilo ... huzuni imetanda.

Ndugu, jamaa, mashuhuda na mtoto aliyeokolewa kutoka kwenye janga hilo … huzuni imetanda.

Eneo la tukio, umati ukifuatilia kazi ya uokoaji inayoendelea.

Eneo la tukio, umati ukifuatilia kazi ya uokoaji inayoendelea.

Harakati za uokoaji zikiendelea ... kuondoa kifusi ... kila kinachoweza kutumika kinafanya kazi.

Harakati za uokoaji zikiendelea … kuondoa kifusi … kila kinachoweza kutumika kinafanya kazi.

GHOROFA LAPOROMOKA INDIA

Mashuhuda walisema jengo hilo liliporomoka “kama karata zilizokuwa zimepangwa wima moja juu ya nyingine”, anaripoti Rajini Vaidyanathan

Walau watu 40 wameripotiwa kupoteza maisha, wakiwemo watoto 11, baada ya jengo lililokuwa likiendelea kujengwa kuporomoka karibu na jiji la kibiashara la Mumbai nchini India, polisi nchini humo wameripoti. Dazeni kadhaa nyingine wameumizwa huku wengine wakihofiwa kunaswa katika jengo hilo lililokuwa na orofa saba katika mji wa Thane.

Polisi walisema jengo hilo lilikuwa likijengwa kinyume cha sheria na kwamba ujenzi ulikuwa ukiendelea huku baadhi ya orofa zikiwa tayari na wakazi ndani yake. Kuporomoka kwa majengo kunakotokana na ujenzi usiozingatia kanuni na taratibu, ni jambo linaloshutumiwa sana.

Mwandishi wa habari wa BBC, Sameer Hashmi, aliyekuwa katika eneo la tukio alisema waokoaji walikuwa wakiendelea na kazi ya kuondoa kifusi cha jengo hilo.

Janga hili limeibua ukosefu wa udhibiti katika ujenzi wa majengo nchini Inida. Polise wanasema mjenzi alitumia vifaa duni vya ujenzi na hakuwa na vibali vilivyomruhusu kujenga. Kuna mamia ya ujenzi haramu yanayoendelea katika jiji la Mumbai. Kwa sababu ya kasi ya ongezeko la watu, daima kumekuwa na mahitaji makubwa ya nyumba za gharama nafuu. Nyumba duni huuzwa kwa bei nafuu zaidi kuliko zile zilizojengwwa kwa kuzingatia vigezo vyote.

Wanaharakati wanatuhumu kwamba wajenzi hawa wenye tamaa ya utajiri wa harakaharaka hutoa rushwa kubwa kwa mamlaka zinazohusika ili wafumbie macho majengo haya haramu na huwa hawachukuliwi hatua zozote za kisheria. Wengi ya wale waliokuwa tayari wamehamia kwenye jengo hilo ni wale wa kipato cha chini hadi cha kati.

Mashuhuda walisema kwamba ujenzi wa jengo hilo ulianza yapata wiki sita zilizopita na kwamba hadi ajali inatokea, jengo hilo lililojengwa kwa kasi kubwa, tayari lilikuwa limeshafikia orofa ya saba na ile ya nane ilikuwa mbioni kukamilika. Hata kabla ujenzi haujakamilika kabisa, tayari wapangaji waliruhusiwa kuhamia na kushika orofa nne kati ya zile saba.

Chanzo: BBS World News kupitia mtandao

ANGALIZO

Tukio hili linakuja wiki moja tu baada ya jengo la orofa 16 kuporomoka jijini Dar es Salaam. Yapata watu 30 walipoteza maisha. Hapa nchini na kule India — matukio hayo hayakuwa ya kwanza. Yamejirudia mara kadhaa. Sababu za kuporomoka, ingawa uchunguzi bado unaendelea, kwa kiasi kikubwa ni kukosena kwa udhibiti wa kutosha ili kuhakikisha kwamba viwango vya ujenzi vinazingatiwa kikamilifu. Kama ilivyoripotiwa huko nchini India, tatizo la rushwa pia linajitokeza. Rushwa ni kama kansa. Inapoingia mwilini, mwili unapoteza mwelekeo wake wa asili wa ukuaji, vivyo hivyo kwa taifa linaloanza kupenywa na kansa ya rushwa. Dunia hivi sasa inazidi kufunguka. Katika uingizaji wa mambo nchini … ni muhimu kuhakikisha tunachuja sana. Kuna matatizo yanayotokea katika mataifa mengine, hayo ni vema kuyachuja na kuyaacha huko huko. Tuchukue tu yaliyo mazuri.

Blogu hii kwa mara nyingine inatoa pole kwa wafiwa wa matukio yote mawili — lile la hapa nchini na la huko nje.

Madereva na Mafunzo … Ajali Kupungua?

leave a comment »


Majuma ya karibuni nilikutana na hii -- gari linalotumiwa na VETA Dar es Salaam  kutoa mafunzo ya udereva. Hii ni hatua muhimu sana. Mara nyingine ninapopata nafasi ya kuwasikiliza waliopitia mafunzo ya udereva miaka ya 60 hadi 70, huwa ninajiuliza ikiwa bado umakini katika kutoa mafunzo ungalipo. Takwimu za ajali na jinsi watu wanavyopoteza maisha ni baadhi ya mambo ambayo yanaonyesha dhahiri kabisa kwamba tuna watu wengi wanaojua kuongoza magari/vyombo vya moto ... lakini si madereva kwa maana ya SANAA na SAYANSI. Ni muhimu sana kwa Idara ya Jeshi la Polisi-Usalama wa Barabarani wasimamie, wamiliki na kumudu vema namna taaluma hiyo ya udereva inavyopanuka. Mahitaji ni makubwa kulinga na kasi ya kukua kwa uchumi ... lakini lazima kutoa wanataalama walio bora na wanaozingatia maadili ya taaluma. Hiyo ni ikiwa tunataka kudhibiti matukio ya ajali ambayo kila kukicha tunayasikia na mara nyingine kuyashuhudia. Pamoja sana.

Majuma ya karibuni nilikutana na hii — gari linalotumiwa na VETA Dar es Salaam kutoa mafunzo ya udereva. Hii ni hatua muhimu sana. Mara nyingine ninapopata nafasi ya kuwasikiliza waliopitia mafunzo ya udereva miaka ya 60 hadi 70, huwa ninajiuliza ikiwa bado umakini katika kutoa mafunzo ungalipo. Takwimu za ajali na jinsi watu wanavyopoteza maisha ni baadhi ya mambo ambayo yanaonyesha dhahiri kabisa kwamba tuna watu wengi wanaojua kuongoza magari/vyombo vya moto … lakini si madereva kwa maana ya SANAA na SAYANSI. Ni muhimu sana kwa Idara ya Jeshi la Polisi-Usalama wa Barabarani wasimamie, wamiliki na kumudu vema namna taaluma hiyo ya udereva inavyopanuka. Mahitaji ni makubwa kulinga na kasi ya kukua kwa uchumi … lakini lazima kutoa wanataalama walio bora na wanaozingatia maadili ya taaluma. Hiyo ni ikiwa tunataka kudhibiti matukio ya ajali ambayo kila kukicha tunayasikia na mara nyingine kuyashuhudia. Pamoja sana.

Written by simbadeo

December 9, 2012 at 9:16 pm

Treni ya Mwakyembe … Madereva Kaeni Chonjo

with 2 comments


Garimoshi la abiria wa Dar es Salaam likiwa katika moja ya safari zake kati ya Posta na Ubungo Maziwa.

Gari dogo la binafsi likiwa kwenye moja ya foleni za magari jijini. Hata hivyo, gari hilo lipo katikati ya njia ya reli.

WAKATI ambapo wakazi wa baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam wanaendelea kunufaika na kuanzishwa kwa usafiri wa abiria wa ndani ya jiji (Commuter train) — tangu katikati ya mwezi Oktoba — kuna haja tupeane hadhari.

Njia ya reli inayotumika kwa usafiri huu wa aina yake — asante kwa juhudi za Dkt Harrison Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi — inakutana na barabara kuu na ndogo na hata njia na vijia vingi sana. Katika baadhi ya makutano hayo kuna wasimamizi na vizuizi vilivyoanziswa, hata hivyo kuna mahali pengi ambapo hakuna watu na nyenzo hizo. Kumbe basi, badala ya madereva na waenda kwa miguu kutegemea tu nyenzo hizo pamoja na king’ora cha garimoshi, ni vema tukajifunza kuheshimu sehemu hizo za makutano na kuongeza uangalifu na umakini.

Binafsi sioni kwa nini mtu unayeendesha gari ulisimamishe kwenye njia ya reli. Hebu fikiri kama garimoshi litatokea ghafla, utafanya nini wakati mbele na nyuma na pembani kote umebanwa na magari? Hivi, unapoteza nini kwa kusimamisha gari lako walau mita tatu kutoka njia ya treni?

Inafaa tujifunza kuepuka ajali zisizo za lazima. Tuache kumjaribu Mungu (na bahati mbaya). Tufuate kanuni ya ‘akili ya kuzaliwa nayo’ (common sense). Si lazima Dkt Mwakyembe aje kusimamia na jambo hili.

Vivyo hivyo kwa waendesha pikipiki, baiskeli, mikokoteni, bajaj na hata waenda kwa miguu … umakini tuwapo barabarani saa zote utatusaidia sana kupunguza ajali, hasa kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.

Nawakilisha. Pamoja sana.

Written by simbadeo

November 16, 2012 at 11:21 pm

Matumaini kwa Wakazi wa Kinyerezi … Daraja Kujengwa

with 3 comments


Wahenga wanasema dalili ya mvua ni mawingu. Hapa kwenye daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea kuna dalili hizi. Naamini ni njema na zinazoleta matumaini mapya kwa wakazi wa pande zote mbili. Kipande hicho cha darajani kwenye barabara hiyo kimekuwa kero kubwa sana kwa watumiaji. Harakati hizi zinazoendelea sasa zinaleta matumaini makubwa.

Ingawa mimi si mtalaamu wa ujenzi, lakini si vibaya nikatoa ushauri kwamba daraja linyanyuliwe juu sana kupunguza ukali wa mteremko na vilevile kulipa nafasi kubwa kabisa chini ili maji ya mvua yapite pasipo kikwazo. Vilevile, tunataraji kuona daraja pana kiasi cha kutosha hata magari manne kupishana ili kuzuia/kupunguza uwezekano wa kutokea ajali.

Na kwa kukumbushia tu. Kazi ikikamilika hapo, serikali ielekeze macho yake kwenye daraja la Kinyerezi linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita. Ni daraja finyu sana. Mara nyingi unapotokea mkwamo wa dakika mbili tu, tayari foleni pande zote mbili zinaenda umbali wa kilometa mbili. Ni vema daraja linanuliwe ili magari yapishane na iwekwe sehemu ya wapita kwa miguu — ni muhimu sana kuwalinda watoto na wazee wanaopita pale. Si vema tusubiri hadi ajali itokee kisha ndiyo tuchukue hatua. Kinga ni bora kuliko kutibu.

Pamoja sana. Wimbo: ‘Ni bora kujenga daraja … kuliko kujenga ukuta’ endelea…

Written by simbadeo

November 14, 2012 at 9:20 am

Ajali … Kinyerezi

with 2 comments


Ni ya uso kwa uso … Hiace na Lorry

Viti vya kwenye Hiace … viliparaganyika na vingine kung’oka

Mparaganyiko wa viti kwenye daladala …

Barabara ilifungwa kwa muda … kisha magari yalianza kupita upande mmoja wa barabara kwa kusubiriana

Ni majira ya saa 2 usiku. Wakati ninawasili eneo la tukio, kiasi cha kama dakika kumi zilikwishapita. Ni basi dogo, Hiace, na lorry la kama tani tatu yaliyohusika na ajali hii. Magari haya kwa yanavyoonekana, yaligongana uso kwa uso. Baada ya kutazama, inaelekea kwamba dereva wa lorry ndiye aliyehama kutoka upande wake wa barabara na hatimaye kugongana na daladala hilo. Baadhi ya abiria waliokuwa kwenye daladala hilo bado wapo. Wengine bado wana mshtuko wa kuhusika kwenye ajali. Wananieleza kwamba walioumia hasa ni madereva wote wawili wa magari hayo. Madereva hao hawapo hapo lakini wamekwishatoka, hakuna aliyejua hasa wako wapi. Lorry lilikuwa likiteremka kwenye kilima kutoka upande wa Kinyerezi na Haice ilikuwa ikipanda kilima hicho kutoka Njia Panda Segerea.

Ajali. Barabara ni nyembamba na ina miteremko mikali kidogo na madaraja daraja. Ingawa hakuna aliyepoteza maisha katika tukio hili, lakini mtu unapata maswali mengi. Linaloumiza kichwa zaidi ni kuhusu umahiri wa madereva wetu hapa nchini. Ajali zilizo nyingi zinasababishwa na uzembe wa madereva. Mtu unajiuliza, hivi hizi leseni zilizo mikononi mwa madereva … wanazistahili kweli? Je, vigezo vyote na masharti yalizingatiwa kabla ya kuwapa leseni hizo? Je, polisi wa usalama barabarani wanafanya kazi yao kikamilifu … au ndiyo baadhi wanawalinda wahalifu wa makosa ya barabarani baada ya kulambishwa shilingi mbili tatu?

Tupige vita ajali. Tunaweza kuwa na barabara zilizo salama katika nchi yetu. Kila mmoja atimize wajibu wake vizuri. Pamoja sana!

Written by simbadeo

September 18, 2012 at 10:48 pm

Changamoto za maisha … vijijini

with 2 comments


Afya. Gari la wagonjwa likiwa limekata chuma kinachounganisha gurudumu la mbele. Safari ilikomea hapo. Kwa bahati umbali kufika mjini ulibaki kama km 25 hivi, kwa hiyo mgonjwa alimalizia safari yake kwa gari lingine lililokuwa likipita hapo.

Maji. Miundombinu bado ni hafifu. Hivi ni kipi kinachotuzuia kutumia miundombinu kama hii iliyowahi kujengwa tangu miaka ya nyuma? Kwa nini wananchi waachwe kuendelea kuteseka kwa kwenda kutafuta maji mbali wakati tenki kama hili lingewapunguzia adha hiyo?

Kipato. Ni vigumu kuendesha maisha ya maana pasipo kipato cha uhakika. Je, vipi kuhusu haki za mtoto aliye mgongoni hapo? Nchi ina wajibu wa kuleta mabadiliko ya maana kwa wananchi kama huyu.

Elimu. Katika maeneo mengi hakuna madarasa ya maana. Kwa hiyo, hata watoto wanapofika umri wa kwenda shule hakuna mahali wanapoweza kwenda. Katika kijiji kimojawapo kuna vijana walioamua kujitolea kufundisha watoto. Kila mzazi anapaswa kulipa walau Sh1,000 kwa mwezi. Hata hivyo, wengi huwakatisha watoto wao masomo kwa kushindwa kumudu kiwango hicho … au pengine kwa kutoipa elimu kipaumbele. Hamasa na elimu kwa watu wazima ni muhimu ili watoto wapate fursa nzuri zaidi za kusoma.

Vitabu. Uhaba mkubwa. Kwenye darasa hilo kulikuwepo vitabu viwili tu. Mahitaji ya elimu yatakidhiwa vipi kwa mwendo huu? Kiu cha elimu ni kikubwa. Ukame wa vitabu, madarasa, walimu, madawati na vifaa vingine ni mkubwa mno.

Written by simbadeo

July 26, 2012 at 10:31 pm