simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Posts Tagged ‘daraja

Daraja la Kinyerezi: Hatimaye matumaini yarejea …

with 2 comments


Darajani 7 April xx

Baada ya mahangaiko haya …

Darajani 7 April xxxx

… na haya yaliyodumu kwa zaidi ya mwezi mmoja, hatimaye matumaini yanaanza kurejea.

Darajani 7 April x

Daraja lilifika nusu …

Darajani 7 April xxx

… na kisha jana lilifika mwisho mwingine. Kazi iliyokuwa imebaki ni kutandaza sakafu.

Kasi ilikuwa ndogo … ya kusuasua sana. Pamoja na hayo pongezi kwa mamlaka yoyote iliyovalia njua dharura hii hadi sasa matumaini yanarejea. Pengine tusiishie hapo. Daraja ni mali adimu ya umma. Gharama yake ni zaidi sana ya zile tu za ujenzi na ununuzi wa vifaa … gharama yake ni pamoja na huduma inayotolewa na daraja hilo, ni vigumu kuikadiria. Kwa sababu hiyo, miundombinu kama madaraja ni muhimu yalindwe usiku na mchana. Ulinzi wenyewe uwe mkali kwelikweli. Nchi haiwezi kumudu kupoteza au kucheleweshewa maendeleo kwa sababu ya mtu fulani mzembe au mwenye tamaa zake. Hilo ni ni muhimu lieleweke na kuwekwa vichwani.

Pamoja sana.

Hali tete Daraja la Kinyerezi na Majumba Sita

leave a comment »


Darajani 22 march 1

Darajani 22 march 4

Darajani 22 march 2

Darajani 22 march 7

Darajani 22 march 6

Kwa ufupi, hii ni kuhatarisha maisha ya wapiga kura katika nchi hii. Ni zaidi ya wiki mbili sasa tangu daraja la muda livunjike wakati lori la kuchanganya zege likipita juu yake. Hadi wakati huu, sijasikia tamko lolote kuhusu mpango uliopo wa kurekebisha hali ya mambo. Sijamsikia Mbunge wa Ukonga wala Madiwani wa Kata za Ukonga, Kipawa, Segerea wala Kinyerezi akizungumzia suala hili. Sijamsikia Waziri wa Ujenzi akisema lolote kuhusiana na tatizo lililopo.

Pengine wakuu hao wanasubiri mtu au watu wapoteze maisha na mali zao kisha ndio wajitokeze. Hivi sasa hali ni tete katika eneo hilo. Watu wanaojaribu kuvuka kwa kutumia vyuma vya daraja lililovunjika wanafanya hivyo kwa kuhatarisha maisha yao na mali zao. Eneo si salama. Mawasiliano kati ya pande mbili hakuna. Hakuna gari wala pikipiki inayoweza kuvuka hapo wakati huu. Na huu ni mwanzo tu wa mvua za masika.

Chondechonde, serikali ilitazame eneo hili kwa namna ya pekee. Naamini tuna wahandisi wengi wazalendo wenye uwezo wa kubuni suluhisho la muda wakati daraja la kudumu likiendelea kujengwa. Hakika katika hili hatutawaelewa ikiwa hamtakuja na majibu ya haraka.

Ni muhimu hatua za haraka zichukuliwe. Kuna wazee, watoto, akina mama na wananchi wengine wengi wanaotumia barabara na daraja hili. Hivi sasa watoto wa upande mmoja wanaosoma shule upande mwingine, hawana tena fursa ya kwenda shule. Pale hapavukiki. Vivyo hivyo kwa watoto wa upande mwingine. Kwa watu wazima, watalazimika kupata adhabu ya kuzunguka njia ndefu ili kwenda kutafuta riziki za watoto wao na kodi mbalimbali wanazolipa serikalini. Maana yake, maisha yatakuwa ghali zaidi.

Kinachotakiwa hapa ni uamuzi mgumu. Mtuthibitishie kuwa mnaweza kufanya uamuzi mgumu na kuwarejeshea mawasiliano wapiga kura wenu.

Kwa pamoja, tunaweza.

Dar es Salaam: Lori lavunja Daraja la Kinyerezi tena

with 2 comments


Ikiwa ni miezi michache tu tangu daraja linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita kuvunjwa na lori lililosheheni matofali, leo hii tena, majira ya saa moja usiku lori lingine la kuchanganya kokoto limevunja daraja hilo.

Alama za barabarani huonyesha kuwa daraja hilo — ambalo ni la muda na lililotengenezwa kwa vyuma tupu — lina uwezo wa kubeba uzito usiozidi tani saba (7).

Kama ilivyokuwa safari ya kwanza, kuvunjika kwa daraja hili kunasababisha kero kubwa ya usafiri kwa wanaotumia barabara hii muhimu ikiwa ni pamoja na Jeshi la Magereza kutoka katika Gereza la Segerea. Tayari kulikuwa na msururu wa mamia ya magari kila upande wa daraja, huku yakipeana muda kuvuka katika Bonde la Mto Msimbazi kwa kutumia barabara ya dharura inayopita kwenye eneo la mto. Barabara hiyo ina uwezo wa kupitisha gari moja tu kwa wakati mmoja — yaani, magari mawili hayawezi kupishana.

 

Daraja Kinyerezi 1

Picha zaidi hizi hapa (ubora wa picha zi mzuri kwa sababu ya eneo hilo kutawaliwa na giza wakati wa usiku):

Daraja Kinyerezi 2

Lori lililoanguka usiku huu.

Daraja Kinyerezi 4

Utambulisho wa lori hilo.

 

Daraja Kinyerezi 5

Sehemu ya shehena ya zege ikiwa imemwagika kutoka kwenye lori hilo. Wakati picha hii inapigwa tayari zege hilo lilikuwa limeshaanza kukauka.

 

Daraja Kinyerezi 6

Utambulisho mwingine wa lori hilo.

Kwa mujibu wa mashuhuda ambao hawakuwa tayari kutajwa kwa sababu wao si wazungumzaji rasmi, dereva na utingo wake walinusurika na kutiwa mbaroni na walinzi wa daraja.

Kwa hakika, wakati ambapo haijulikani ni lini daraja hili la muda litatengenezwa tena, wananchi wa maeneo jirani na watumiaji wengine wa barabara hii wajiandae kwa kero kubwa ya usafiri. Miongoni mwa watakaotaabika ni pamoja na wanafunzi ambao hufuatwa majumbani na mabasi ya shule wanakosoma. Wakati huohuo, mwezi Machi huwa ni mwanzo wa msimu wa masika katika Jiji la Dar es Salaam. Mara mvua zitakapoanza kunyesha, hata barabara ya muda itapitika kwa taabu sana, na hivyo kufanya eneo hili kutokuwa na mawasiliano na upande wa pili.

 

 

‘Daraja Hili … Thamani Yake ni Mvua ya Saa Tatu’

leave a comment »


Siku chache zilizopita, wengine wetu tulipolalamikia uzio huo!

Siku chache zilizopita, wengine wetu tulipolalamikia uzio huo!

Daraja na uzio na vifaa vingine vya ujenzi wa daraja jipya ... vimesombwa na maji ...

Daraja na uzio na vifaa vingine vya ujenzi wa daraja jipya … vimesombwa na maji …

Mitambo ya ujenzi ... karibu ufukiwe na udongo ...

Mitambo ya ujenzi … karibu ufukiwe na udongo …

Hivi ndivyo uvukaji ulivyokuwa ... Ni eneo lenye udongo unaoteleza. Usipokuwa makini, unavunja mguu au mkono kama si kupasua kichwa!

Hivi ndivyo uvukaji ulivyokuwa … Ni eneo lenye udongo unaoteleza. Usipokuwa makini, unavunja mguu au mkono kama si kupasua kichwa!

Hali ya usafiri ilikuwa hivi. Daladala za kutoka Kinyerezi na Majumbasita ziliishia hapa. Zile za kutoka Tabata na Segerea, nazo ziliishia upande wa pili. Hiyo haikutoa unafuu wa nauli ... au utembee hadi Segerea Mwisho, au upande gari na ulipe nauli nyingine. Kufa kufaana.

Hali ya usafiri ilikuwa hivi. Daladala za kutoka Kinyerezi na Majumbasita ziliishia hapa. Zile za kutoka Tabata na Segerea, nazo ziliishia upande wa pili. Hiyo haikutoa unafuu wa nauli … au utembee hadi Segerea Mwisho, au upande gari na ulipe nauli nyingine. Kufa kufaana.

Ndivyo hali ilivyo katika daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea. Ni daraja muhimu kwani linategemewa na maelfu ya wakazi wa upande huo wa Dar es Salaam. Daraja la muda lilijengwa kwa muda wa miezi kadhaa. Malori ya mawe yalimwagwa hapo. Wajenzi wakatumia maarifa yao. Mamilioni ya fedha yaliingia hapo … sijui ni milioni ngapi. Kudumu kwa daraja hilo miezi michache tangu lijengwe kumekomeshwa na mvua iliyodumu kwa saa 3 tu! Hapa ndipo ninakumbuka kauli ya dereva wa daladala aliyetubeba ‘Thamani ya Daraja hili ni saa tatu ya mvua’!

Abiria wengine walijiuliza … ‘hasara hii ni ya nani’? Nani atabeba gharama za ujenzi mwingine wa daraja la muda? Miongoni mwa abiria hakuna aliyekuwa na majibu.

Hapa tunaona umuhimu wa kutumia maarifa yetu vema. Mwezi Desemba 2011 wakati wa mafuriko ya Dar, daraja lililokuwa hapo kwa miaka mingi lilisombwa. Hiyo ilitosha kabisa kutoa angalizo kwa wakandarasi walioshinda zabuni hiyo. Daraja la muda lilipaswa liwe madhubuti na kubwa kuliko lililokuwepo awali, na daraja la kudumu linalopaswa kuwa hapo linatakuwa kuwa kubwa sana, lililopanda juu sana na pana vizuri ili lisije kusombwa na mafuriko.

Tanzania ni yetu sote. Kila mmoja ajisikie uchungu na kuchukua hatua kukabili magumu yanayotusibu!

Written by simbadeo

March 25, 2013 at 11:29 pm

Daraja la Kinyerezi … Mabadiliko

leave a comment »


Ni mwezi August 2008. Siku hizi barabara hiyo ina lami. Ni mabadiliko ya aina yake. Kuimarishwa kwa barabara hiyo kulipandisha sana umaarufu wa kiunga (suburb) cha Kinyerezi. Hivi sasa viwanja kule havishikiki. Pamoja sana katika kukumbuka taswira za zamani kidogo.

Ni mwezi August 2008. Siku hizi barabara hiyo ina lami. Ni mabadiliko ya aina yake. Kuimarishwa kwa barabara hiyo kulipandisha sana umaarufu wa kiunga (suburb) cha Kinyerezi. Hivi sasa viwanja kule havishikiki. Pamoja sana katika kukumbuka taswira za zamani kidogo.

Written by simbadeo

March 19, 2013 at 10:40 pm

Ujenzi … Madaraja na Miundombinu

leave a comment »


Moja ya madaraja yanayoendelea kujengwa katika barabara ya Tunduma kwenda Sumbawanga

Moja ya madaraja yanayoendelea kujengwa katika barabara ya Tunduma kwenda Sumbawanga

Ujenzi wa barabara kwa ajili ya magari yaendayo kasi katika Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani, Dar es Salaam

Ujenzi wa barabara kwa ajili ya magari yaendayo kasi katika Barabara ya Morogoro eneo la Jangwani, Dar es Salaam

Maandalizi ya ujenzi wa daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea

Maandalizi ya ujenzi wa daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea

Harakati za ujenzi wa miundombinu zinaendelea katika pande mbalimbali za nchi ya Tanzania. Uzoefu unaonyesha kwamba miradi mingi huwa na viwango vya chini vya ubora. Moja ya sababu za viwango duni ni usimamizi hafifu wa maofisa au mamlaka zinazohusika. Ni kwa sababu hiyo utasikia kwamba barabara imeanza kubomoka mara tu baada ya kukabidhiwa kwa serikali. Mwenendo huu hulitia Taifa hasara kubwa sana, kwani huhitajika fedha nyingine tena ili kukarabati maeneo yale yaliyoharibika.

Kumbe basi, badala ya kuziachia tu mamlaka zinazohusika kusimamia na kukagua miradi hiyo, kila raia wa nchi hii ni vema afungue macho atazame mienendo ya ujenzi wa miundombinu katika maeneo wanayoishi. Pale unapoona dosari fulani, si vibaya kuuliza kwenye mamlaka inayohusika ili wataalamu watoe maelezo ya kiufundi.

Picha mbili hapo juu zinaonyesha ujenzi ukiendelea. Picha hiyo hapo chini ni maandalizi ya ujenzi. Tofauti ninayoona kati ya miradi hiyo miwili hapo juu na huu wa tatu hapa chini ni suala la uzio. Inawezekana wajenzi wa mradi huo hapo chini wana sababu za maana za kujenga uzio kwenye eneo la mradi. Mathalani, huenda ni ili kuimarisha usalama wa mali zao na zana za ujenzi; au pengine wanataka wajenzi wengine wasione teknolojia yao na hivyo ‘kuiiba’ na kwenda kuitumia kwenye mradi mwingine kama huo.

Hata hivyo, na ninakaribisha kurekebishwa, binafsi sioni kama ilikuwa muhimu kuweka uzio. Sana sana mimi naona kwamba utaratibu huo unaweza kuwa na matatizo zaidi kuliko manufaa. Kwa mfano, hapo kuna hiyo kali katika barabara nyembamba ya muda na kuna daraja dogo. Uzio unatengeneza ‘blind spot’ hapo gari linapokaribia daraja. Kwa hiyo, ni rahisi kwa ajali kutokea na hatujui itasababisha hasara zipi! Lakini pia, huu kama mradi wa umma sioni kwa nini uzibwe ili watu tusione — je, wajenzi hawataki tuone ni aina gani ya nondo zinaingia kwenye daraja? Ni kiasi gani cha nondo kinahitajika kutumika?

Nafikiri wananchi tuna haki ya KUONA na kutathmini. Hatutaki tuje tushtukizwe baadaye na uduni wa daraja. Inafaa kuona ili kama ni kulaumiwa, tulaumiane sisi wenyewe kwa kutochukua hatua zinazostahili mapema.

Nawasilisha hoja. Pamoja sana.

Written by simbadeo

March 12, 2013 at 6:57 am

Matumaini kwa Wakazi wa Kinyerezi … Daraja Kujengwa

with 3 comments


Wahenga wanasema dalili ya mvua ni mawingu. Hapa kwenye daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea kuna dalili hizi. Naamini ni njema na zinazoleta matumaini mapya kwa wakazi wa pande zote mbili. Kipande hicho cha darajani kwenye barabara hiyo kimekuwa kero kubwa sana kwa watumiaji. Harakati hizi zinazoendelea sasa zinaleta matumaini makubwa.

Ingawa mimi si mtalaamu wa ujenzi, lakini si vibaya nikatoa ushauri kwamba daraja linyanyuliwe juu sana kupunguza ukali wa mteremko na vilevile kulipa nafasi kubwa kabisa chini ili maji ya mvua yapite pasipo kikwazo. Vilevile, tunataraji kuona daraja pana kiasi cha kutosha hata magari manne kupishana ili kuzuia/kupunguza uwezekano wa kutokea ajali.

Na kwa kukumbushia tu. Kazi ikikamilika hapo, serikali ielekeze macho yake kwenye daraja la Kinyerezi linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita. Ni daraja finyu sana. Mara nyingi unapotokea mkwamo wa dakika mbili tu, tayari foleni pande zote mbili zinaenda umbali wa kilometa mbili. Ni vema daraja linanuliwe ili magari yapishane na iwekwe sehemu ya wapita kwa miguu — ni muhimu sana kuwalinda watoto na wazee wanaopita pale. Si vema tusubiri hadi ajali itokee kisha ndiyo tuchukue hatua. Kinga ni bora kuliko kutibu.

Pamoja sana. Wimbo: ‘Ni bora kujenga daraja … kuliko kujenga ukuta’ endelea…

Written by simbadeo

November 14, 2012 at 9:20 am

Segerea Darajani … Uvukaji

leave a comment »


Baada ya daraja lililokuwepo kusombwa na mafuriko miezi michache iliyopita … hivi ndivyo baadhi ya magari na watu wanavyovuka bonde hili. Ni katika Mto Msimbazi, sehemu inayounganisha Segerea (upande wa Seminari) na Sitakishari (Majumbasita).

Mahali lilipokuwa daraja kabla ya kusombwa. Chora mstari wa moja kwa moja na barabara iliyo ng’ambo ya mto (bonde la mto).

Bonde la mto baada ya kupanuliwa na mmomonyoko wa udongo …

Upande mwingine wa bode … nyumba zilizokuwa karibu kusombwa na maji.

Swali la kizushi

Mamlaka inayohusika na barabara hii … daraja hili litajengwa lini? Kimsingi, barabara hii inafupisha sana umbali kati ya Segerea na Sitakishari hadi Uwanja wa Ndege. Vilevile, endapo kuna tatizo lolote katika barabara ya Kinyerezi-Majumbasita, hii inaweza kutumika. Kumbe, ni barabara muhimu na yafaa kwamba daraja litengenezwe upya. Pamoja … sana.

Written by simbadeo

April 10, 2012 at 11:27 pm