simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Posts Tagged ‘segerea

Dar es Salaam: Lori lavunja Daraja la Kinyerezi tena

with 2 comments


Ikiwa ni miezi michache tu tangu daraja linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita kuvunjwa na lori lililosheheni matofali, leo hii tena, majira ya saa moja usiku lori lingine la kuchanganya kokoto limevunja daraja hilo.

Alama za barabarani huonyesha kuwa daraja hilo — ambalo ni la muda na lililotengenezwa kwa vyuma tupu — lina uwezo wa kubeba uzito usiozidi tani saba (7).

Kama ilivyokuwa safari ya kwanza, kuvunjika kwa daraja hili kunasababisha kero kubwa ya usafiri kwa wanaotumia barabara hii muhimu ikiwa ni pamoja na Jeshi la Magereza kutoka katika Gereza la Segerea. Tayari kulikuwa na msururu wa mamia ya magari kila upande wa daraja, huku yakipeana muda kuvuka katika Bonde la Mto Msimbazi kwa kutumia barabara ya dharura inayopita kwenye eneo la mto. Barabara hiyo ina uwezo wa kupitisha gari moja tu kwa wakati mmoja — yaani, magari mawili hayawezi kupishana.

 

Daraja Kinyerezi 1

Picha zaidi hizi hapa (ubora wa picha zi mzuri kwa sababu ya eneo hilo kutawaliwa na giza wakati wa usiku):

Daraja Kinyerezi 2

Lori lililoanguka usiku huu.

Daraja Kinyerezi 4

Utambulisho wa lori hilo.

 

Daraja Kinyerezi 5

Sehemu ya shehena ya zege ikiwa imemwagika kutoka kwenye lori hilo. Wakati picha hii inapigwa tayari zege hilo lilikuwa limeshaanza kukauka.

 

Daraja Kinyerezi 6

Utambulisho mwingine wa lori hilo.

Kwa mujibu wa mashuhuda ambao hawakuwa tayari kutajwa kwa sababu wao si wazungumzaji rasmi, dereva na utingo wake walinusurika na kutiwa mbaroni na walinzi wa daraja.

Kwa hakika, wakati ambapo haijulikani ni lini daraja hili la muda litatengenezwa tena, wananchi wa maeneo jirani na watumiaji wengine wa barabara hii wajiandae kwa kero kubwa ya usafiri. Miongoni mwa watakaotaabika ni pamoja na wanafunzi ambao hufuatwa majumbani na mabasi ya shule wanakosoma. Wakati huohuo, mwezi Machi huwa ni mwanzo wa msimu wa masika katika Jiji la Dar es Salaam. Mara mvua zitakapoanza kunyesha, hata barabara ya muda itapitika kwa taabu sana, na hivyo kufanya eneo hili kutokuwa na mawasiliano na upande wa pili.

 

 

‘Daraja Hili … Thamani Yake ni Mvua ya Saa Tatu’

leave a comment »


Siku chache zilizopita, wengine wetu tulipolalamikia uzio huo!

Siku chache zilizopita, wengine wetu tulipolalamikia uzio huo!

Daraja na uzio na vifaa vingine vya ujenzi wa daraja jipya ... vimesombwa na maji ...

Daraja na uzio na vifaa vingine vya ujenzi wa daraja jipya … vimesombwa na maji …

Mitambo ya ujenzi ... karibu ufukiwe na udongo ...

Mitambo ya ujenzi … karibu ufukiwe na udongo …

Hivi ndivyo uvukaji ulivyokuwa ... Ni eneo lenye udongo unaoteleza. Usipokuwa makini, unavunja mguu au mkono kama si kupasua kichwa!

Hivi ndivyo uvukaji ulivyokuwa … Ni eneo lenye udongo unaoteleza. Usipokuwa makini, unavunja mguu au mkono kama si kupasua kichwa!

Hali ya usafiri ilikuwa hivi. Daladala za kutoka Kinyerezi na Majumbasita ziliishia hapa. Zile za kutoka Tabata na Segerea, nazo ziliishia upande wa pili. Hiyo haikutoa unafuu wa nauli ... au utembee hadi Segerea Mwisho, au upande gari na ulipe nauli nyingine. Kufa kufaana.

Hali ya usafiri ilikuwa hivi. Daladala za kutoka Kinyerezi na Majumbasita ziliishia hapa. Zile za kutoka Tabata na Segerea, nazo ziliishia upande wa pili. Hiyo haikutoa unafuu wa nauli … au utembee hadi Segerea Mwisho, au upande gari na ulipe nauli nyingine. Kufa kufaana.

Ndivyo hali ilivyo katika daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea. Ni daraja muhimu kwani linategemewa na maelfu ya wakazi wa upande huo wa Dar es Salaam. Daraja la muda lilijengwa kwa muda wa miezi kadhaa. Malori ya mawe yalimwagwa hapo. Wajenzi wakatumia maarifa yao. Mamilioni ya fedha yaliingia hapo … sijui ni milioni ngapi. Kudumu kwa daraja hilo miezi michache tangu lijengwe kumekomeshwa na mvua iliyodumu kwa saa 3 tu! Hapa ndipo ninakumbuka kauli ya dereva wa daladala aliyetubeba ‘Thamani ya Daraja hili ni saa tatu ya mvua’!

Abiria wengine walijiuliza … ‘hasara hii ni ya nani’? Nani atabeba gharama za ujenzi mwingine wa daraja la muda? Miongoni mwa abiria hakuna aliyekuwa na majibu.

Hapa tunaona umuhimu wa kutumia maarifa yetu vema. Mwezi Desemba 2011 wakati wa mafuriko ya Dar, daraja lililokuwa hapo kwa miaka mingi lilisombwa. Hiyo ilitosha kabisa kutoa angalizo kwa wakandarasi walioshinda zabuni hiyo. Daraja la muda lilipaswa liwe madhubuti na kubwa kuliko lililokuwepo awali, na daraja la kudumu linalopaswa kuwa hapo linatakuwa kuwa kubwa sana, lililopanda juu sana na pana vizuri ili lisije kusombwa na mafuriko.

Tanzania ni yetu sote. Kila mmoja ajisikie uchungu na kuchukua hatua kukabili magumu yanayotusibu!

Written by simbadeo

March 25, 2013 at 11:29 pm

Weekend … Pumzisha Akili kwa Taswira Hizi

with 2 comments


Enero la Feri jijini Dar. Ni mahali unapoweza kutembea na kuburudika. Hata hivyo, kuna changamoto nyingi. Soko la samaki limechakaa ndani ya muda mfupi sana ... kama muongo mmoja tu. Swali la kujiuliza ... kutujengea watujengee ... hata kutunza nako waje kututunzia? Sisi kazi yenu ni nini? Kukusanya ushuru tu??? Tubadilike!

Enero la Feri jijini Dar. Ni mahali unapoweza kutembea na kuburudika. Hata hivyo, kuna changamoto nyingi. Soko la samaki limechakaa ndani ya muda mfupi sana … kama muongo mmoja tu. Swali la kujiuliza … kutujengea watujengee … hata kutunza nako waje kututunzia? Sisi kazi yenu ni nini? Kukusanya ushuru tu??? Tubadilike!

Mvua inapoamua kunyesha ... Hapana budi kusubiri ... Ndivyo ilivyokuwa ... Dakika 45!

Mvua inapoamua kunyesha … Hapana budi kusubiri … Ndivyo ilivyokuwa … Dakika 45!

Haya ... ulimi unaniponyoka ... Mara nyingi huwa tunalazimishwa kutenda vitu vingi pasipo kuhiyari. Mathalani, upo kituo cha basi, unasubiri usafiri ambao nao unakuwa umeota mbawa ... huna hili wala lile ... mara anakuja jamaa na spika yenye sauti kali ... anakatisha fikra ulizo nazo kwa kuanza kukumiminia neno. Papo hapo hakukutaka radhi, hakuomba ruhusa yako kama unaridhia kusikiliza au la. Kuondoka hapo huwezi, maana ndipo mahali pa wewe kupata usafiri. Unajikuta unameza dozi bila kupenda ... sorry ... Vitendo kama hivi ... haviwezi kuwekwa kundi moja na 'ubakaji'? Vipo vingine vingi. Huu ni mfano mmoja tu! Kuuliza si ujinga ... wahenga walisema!

Haya … ulimi unaniponyoka … Mara nyingi huwa tunalazimishwa kutenda vitu vingi pasipo kuhiyari. Mathalani, upo kituo cha basi, unasubiri usafiri ambao nao unakuwa umeota mbawa … huna hili wala lile … mara anakuja jamaa na spika yenye sauti kali … anakatisha fikra ulizo nazo kwa kuanza kukumiminia neno. Papo hapo hakukutaka radhi, hakuomba ruhusa yako kama unaridhia kusikiliza au la. Kuondoka hapo huwezi, maana ndipo mahali pa wewe kupata usafiri. Unajikuta unameza dozi bila kupenda … sorry … Vitendo kama hivi … haviwezi kuwekwa kundi moja na ‘ubakaji’? Vipo vingine vingi. Huu ni mfano mmoja tu! Kuuliza si ujinga … wahenga walisema!

Weekend njema wadau wa blogu hii. Mbarikiwe sana. Natumaini nimepata ridhaa yako hapo kabla ili kukuletea makala hii. Maoni ni ruksa, tusivunje tu sheria za nchi! Pamoja sana!

Written by simbadeo

January 18, 2013 at 11:23 pm

Posted in Siasa na jamii

Tagged with , , , , ,

Bonyokwa to Kimara … Barabara Inapitika

with 2 comments


Ni barabara inayounganisha Barabara ya Morogoro na Ile ya Kinyerezi/Segerea. Nimeitumia hivi karibuni. Inapitika. Inapobidi kukwepa foleni na kufupisha umbali ... unaweza kuitumia. Ni ya vumbi bado lakini yaelekea inapata baadhi ya huduma ndogondogo. Changamoto kubwa zaidi ni kwenye mwinuko huo mkali ambapo pembeni kuna mmomonyoko wa udongo. Vinginevyo, katika kufikiria zile 'ring roads' za jiji la Dar, hii nayo ipewe kipaumbele. Tunapoanza mwaka mpya, pengine hii iwe moja ya maazimio ya serikali -- kwa malengo ya kupunguza misululu na misongamano ya vyombo vya moto kwenye barabara kuu. Pamoja sana!

Ni barabara inayounganisha Barabara ya Morogoro na Ile ya Kinyerezi/Segerea. Nimeitumia hivi karibuni. Inapitika. Inapobidi kukwepa foleni na kufupisha umbali … unaweza kuitumia. Ni ya vumbi bado lakini yaelekea inapata baadhi ya huduma ndogondogo. Changamoto kubwa zaidi ni kwenye mwinuko huo mkali ambapo pembeni kuna mmomonyoko wa udongo. Vinginevyo, katika kufikiria zile ‘ring roads’ za jiji la Dar, hii nayo ipewe kipaumbele. Tunapoanza mwaka mpya, pengine hii iwe moja ya maazimio ya serikali — kwa malengo ya kupunguza misululu na misongamano ya vyombo vya moto kwenye barabara kuu. Pamoja sana!

Written by simbadeo

December 30, 2012 at 11:15 am

Matumaini kwa Wakazi wa Kinyerezi … Daraja Kujengwa

with 3 comments


Wahenga wanasema dalili ya mvua ni mawingu. Hapa kwenye daraja linalounganisha Kinyerezi na Segerea kuna dalili hizi. Naamini ni njema na zinazoleta matumaini mapya kwa wakazi wa pande zote mbili. Kipande hicho cha darajani kwenye barabara hiyo kimekuwa kero kubwa sana kwa watumiaji. Harakati hizi zinazoendelea sasa zinaleta matumaini makubwa.

Ingawa mimi si mtalaamu wa ujenzi, lakini si vibaya nikatoa ushauri kwamba daraja linyanyuliwe juu sana kupunguza ukali wa mteremko na vilevile kulipa nafasi kubwa kabisa chini ili maji ya mvua yapite pasipo kikwazo. Vilevile, tunataraji kuona daraja pana kiasi cha kutosha hata magari manne kupishana ili kuzuia/kupunguza uwezekano wa kutokea ajali.

Na kwa kukumbushia tu. Kazi ikikamilika hapo, serikali ielekeze macho yake kwenye daraja la Kinyerezi linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita. Ni daraja finyu sana. Mara nyingi unapotokea mkwamo wa dakika mbili tu, tayari foleni pande zote mbili zinaenda umbali wa kilometa mbili. Ni vema daraja linanuliwe ili magari yapishane na iwekwe sehemu ya wapita kwa miguu — ni muhimu sana kuwalinda watoto na wazee wanaopita pale. Si vema tusubiri hadi ajali itokee kisha ndiyo tuchukue hatua. Kinga ni bora kuliko kutibu.

Pamoja sana. Wimbo: ‘Ni bora kujenga daraja … kuliko kujenga ukuta’ endelea…

Written by simbadeo

November 14, 2012 at 9:20 am

Segerea Darajani … Uvukaji

leave a comment »


Baada ya daraja lililokuwepo kusombwa na mafuriko miezi michache iliyopita … hivi ndivyo baadhi ya magari na watu wanavyovuka bonde hili. Ni katika Mto Msimbazi, sehemu inayounganisha Segerea (upande wa Seminari) na Sitakishari (Majumbasita).

Mahali lilipokuwa daraja kabla ya kusombwa. Chora mstari wa moja kwa moja na barabara iliyo ng’ambo ya mto (bonde la mto).

Bonde la mto baada ya kupanuliwa na mmomonyoko wa udongo …

Upande mwingine wa bode … nyumba zilizokuwa karibu kusombwa na maji.

Swali la kizushi

Mamlaka inayohusika na barabara hii … daraja hili litajengwa lini? Kimsingi, barabara hii inafupisha sana umbali kati ya Segerea na Sitakishari hadi Uwanja wa Ndege. Vilevile, endapo kuna tatizo lolote katika barabara ya Kinyerezi-Majumbasita, hii inaweza kutumika. Kumbe, ni barabara muhimu na yafaa kwamba daraja litengenezwe upya. Pamoja … sana.

Written by simbadeo

April 10, 2012 at 11:27 pm

Ajali … Segerea darajani … barabara nusu yafungwa

leave a comment »


Kwanza nimekuta basi hili katika hali hii … na ni basi la shule … katika barabara inayounganisha Segerea na Kinyerezi Mbuyuni … mbele ni msululu wa magari uliokuwa ukienda kwa mwendo wa kinyonga …

Msululu wa magari yanayoelekea Kinyerezi …

Haya … hii ndiyo iliyokuwa sababu ya kasheshe nzima usiku huu … ni katika daraja linalounganisha Segerea na Kinyerezi …

Hali ilikuwa hivi …

Kwa mujibu wa mashuhuda … au waliodai kuwa mashuhuda, lori hilo lenye shehena ya mchanga lilishindwa kupanda mlima. Baada ya hapo lilianza kurudi nyuma. Hiyo pick up ilikuwa ikija kwa nyuma. Basi kasheshe yake ndiyo kama unavyoona. Habari zaidi zilieleza kwamba waliokuwa kwenye pick up walijeruhiwa na mpaka mimi nafika eneo la tukio walikuwa wamekwenda police ili kupata PF3 kwa ajili ya kwenda hospitali kwa matibabu.

Haya … karibu na Daraja linalounganisha Kinyerezi na Majumbasita, kwenye barabara ya kwenda Mongo la Ndege, nimekutana na hii tena.

Kwa maelezo niliyopata hapa. Mbele ya hiyo gari ndogo kulikuwa na gari lingine lililoshindwa kupanda mpando mdogo ulio mbele kidogo. Dereva wa pick up, pengine alikuwa na haraka sana, aliamua kuovertake gari hili dogo … matokeo yake ndiyo hiyo pasi …

Ndiyo niliyoshuhudia usiku wa leo wakati narejea kijijini kwetu … Ya barabarani ni mengi, mengine makubwa.

Written by simbadeo

February 9, 2012 at 11:34 pm