Archive for September 2nd, 2012
Dar Mitaani … Siamini Macho Yangu
Kama siamini macho yangu vile! Tunaanza kuona kazi za sanaa kwenye mitaa ya Darisalama. Hizi ni katika Mtaa wa Makunganya, katikati ya jiji. Kwangu ilikuwa mshtuko kidogo … maana mambo haya hatukuzoea kuyaona hapa. Nipongeze mamlaka inayohusika na mpango huu. Ni mwanzo mzuri na hauna budi kuendelezwa. ILA tafadhali sana tuwashirikishe wanasanaa wa hapa nchini katika kufanya kazi hizi. Wao ndiyo wanaofahamu vema kabisa vionjo vya Watanzania. Kwa kuwahusisha wao, ni njia ya kukuza kazi za sanaa hapa nchini ili zipate kuthaminiwa kama zinavyostahili.
Kupitia sekta ya sanaa, nchi itapata fursa ya kukuza na kudumisha utamaduni wake; itazalisha nafasi nyingi za ajira; itachangia kuongezeka kwa kasi ya kukua kwa uchumi; itaimarisha thamani ya mwanadamu na ubinadamu na hata kukuza viwango vya kufikiri, namna ya kupanga vipaumbele katika maisha na mipango yetu ya mtu mmoja mmoja na ile ya Taifa — yaani katika kutazama hasa substance na si accident. Pamoja sana!