Archive for September 13th, 2012
Biashara … Maisha Yanasonga Mbele
Maisha ni kujumlisha na kutoa. Katika kufanya hivyo, kuna kuzidisha chenji, kuna kupunja chenji na kuna kutoa chenji iliyo sahihi. Umakini ni muhimu ili kuepeka kuzidisha au kupunja. Ni muhimu kupokea kilicho sahihi na kurudisha kilicho sahihi. Pale ulipo, usizidishe chenji wala usipunje chenji bali toa na pokea kiasi kinachostahili. Mwanafalsafa Aristotle aliandika, nanukuu:”E via media, e via aurea!”, kwa kimombo: “The middle way, is the way of gold”, yaani “njia ya katikati, ndiyo njia ya dhahabu”. Tenda haki. Upokee haki. Toa haki. Siku njema wadau wa blogu hii na wapita njia wengine.
Picha hizo ni kutoka mitaa ya Tandika, jijini Dar es Salaam.