simbadeo2000

Bono on Twaweza … a controversy

January 28, 2010
Leave a Comment

On his January 2nd, 2010, article titled People Power and the Upside-Down Pyramid, Bono (US celebrity) extols on the work of Twaweza, an entity that promotes citizen agency in bringing about positive change in societal organization. On the one hand, the column , http://www.nytimes.com/2010/01/03/opinion/03bono.html ushers in criticism from author of a blog called http://swahilistreet.wordpress.com while on the other pulls support from Owen, on his website http://www.owen.org/ who is happy about Bono’s comments.
While the general criticism on how some Non-Governmental Organisations (NGOs) operate, especially in Developing Countries, is valid, still it is important to scrutinize individual organisation’s operations and level of transparency within that particular organization. Transparency is key in ensuring that an entity is up to its objectives and has not deviated from them.
Modern means of communication offer us with ample opportunities to follow up on the activities of a targeted entity. When transparency is lacking in an organization – that is when it is important to double efforts on how we monitor its functionality. So far Twaweza has been transparent enough, as far as I’m concerned. It is this element that we first need to weigh whether it is up to standard or not.
I find that Twaweza’s targets of improving imagination, citizen agency and people’s accountability is a positive initiative that will surely bring in the much needed change in societal organization, particularly in the developing world. Above all, it is an entity that cherishes the art of learning and sharing the lessons learned. In doing that, flexibility is an important tool. All in all, it is also time to clear out the weeds in the farm so that only the crops remain.


Posted in Siasa na jamii

Why? Kwa nini? TAZARA…

January 24, 2010
Leave a Comment

Ni siku ya Jumamosi tarehe 23 Januari 2010. Eneo ni stesheni kuu ya TAZARA, jijini Dar es Salaam. Pamezubaa. Hakuna uhai. Hakuna umotomoto wa kibinadamu. Panatia huzuni.

Hivi kwa nini? Why did we let this happen? How could we have allowed this once prideful symbol of our independence decompose…sink into so much ruin … sink into such degradation?

Why did we let this place that was once full of life, full of activities, activities that generated sources of livelihoods for thousands of homes, become so inactive, lifeless?

Change. We need to change.

Hivi karibuni kulikuwa na taarifa kwenye vyombo vya habari juu ya Serikali ya China kuwa tayari kuifufua upya reli hii ya ushirikiano kati ya Tanzania na Zambia. Ni habari njema. Lakini tukiri kwamba ni habari ambayo pia inafedhehesha. Ilikuwaje kwamba turuhusu kufikia hali ya kutaka msaada kutoka kwa wengine … hata kama ni marafiki zetu … Kwa nini tuwe wa kupokea tu misaada kila wakati hata kwa miradi na biashara ambazo zingeweza kabisa kujiendesha zenyewe kibiashara na kuleta faida kubwa? Mpaka lini hali hii? Tunahitaji uhuru wa pili … uhuru wa kuwa wawajibikaji … awamu nyingine ya uhuru baada ya ule wa mwanzo uliomwondoa mkoloni mweupe na kumleta mkoloni asiye na sura. Tubadilike.


Posted in Siasa na jamii

Simba Mitaa ya Mjini / Lion in City Streets

January 23, 2010
Leave a Comment

Ili tupate mazao bora hatuna budi kufuata kanuni bora za kilimo. Maendeleo ya teknolojia yameleta zana maalumu za kusaidia kuongeza tija katika kilimo. Ugunduzi wa pekee ulioleta mapinduzi ya kilimo katika mataifa yaliyoendelea ni pamoja na ule wa matrekta.

Picha ya kwanza inatuonyesha mazao ya migomba yalivyostawi vema na kumpa mkulima (Bw Vicent wa Morogoro) uwezekano wa kuongeza ubora wa maisha yake.

Picha ya pili – ni trekta la manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam. Trekta hilo, kama yalivyo mengi kadhaa, linatumika kwa kazi ya kubeba taka kupeleka dampo. Ni kazi ya maana.

Ila, kwa maoni yangu, ijapokuwa kazi ya kuzoa taka ina umuhimu wake, mahali mwafaka kwa kulipeleka trekta ni shambani. Likalime. Likapalilie. Likapande. Likavune na kisha lisombelee mazao kupeleka ghalani. Taka zina zana zake maalumu. Kuna malori maalumu kwa ajili ya kazi ya kubeba taka. Malori hayo yameundwa vizuri kiasi kwamba yanapobeba taka – hutaona taka zikisambaa mitaani kwa kupeperushwa na upepo. Kumbe basi, trekta hili lipo MISPLACED. Ni sawasawa na kukuta Simba (mnyama mwitu) akikatiza mitaa ya katikati ya jiji. Si mahali pake. Ingawa naupongeza uongozi wa manispaa kwa kazi hiyo nzuri na ya maana, bado ninawashauri walete malori maalumu ya kusombea taka badala ya kutumia matrekta. Na matrekta hayo wayapeleke mashambani ili kuendelea Kilimo Kwanza. Ciao!

Una maoni gani?


Posted in Siasa na jamii

Msiba kwa Da Chemi

January 19, 2010
Leave a Comment
MSIBA MKUBWA: DA’ CHEMI AMEFIWA NA MMEWE

Kwa masikitiko makubwa nimepokea ujumbe na kusoma katika blogu ya dada Chemi na ukurasa wake wa Facebook taarifa ya kufiwa na mumewe. Hivi ndivyo alivyoandika katika blogu yake ya Swahili Time:

Wadau, nasikitika kutangaza kifo cha mume wangu, Reverend Douglas G. Whitlow, kilichotokea nyumbani hapa Cambridge, Massachusetts leo asubuhi.

Mipango ya mazishi ninafanya na nitawajulisha mara ikikamilika. Kwa habari zaidi mnaweza kuwasiliana na mimi: Chemi Che-Mponda Whitlow 617-497-4353 au Ezekiel Concord Luhigo 781-632-3605

Subi
NB: Kwa atakaye piga toka nje ya Tanzania tafadhali weka namba namba ya mwito ya nchi +1 mwanzoni mwa tarakimu hizo kumi zilizotolewa.

Mungu aipumzize pema roho ya marehemu Douglas G. Whitlow.

NAKUPA POLE NYINGI DA’ CHEMI. TUKO PAMOJA KATIKA WAKATI HUU MGUMU KWAKO NA FAMILIA YAKO.

Simba Deogratias
Dar es Salaam
Source: Mjengwa Majjid’s blog.

Posted in Siasa na jamii

Kwa bei hizi…

January 14, 2010
Leave a Comment

Miundombinu ya nchi kama nyaya za simu, nyaya za umeme, madaraja, alama za barabarani na kadhalika – itapona kweli? Udhibiti wa biashara hii ni muhimu sana. Vinginevyo, tutakuwa tukila hasara kubwa kila mwaka.

Pichani ni moja ya mitaa katika jiji la Dar es Salaam. Kwa wapanga miji – matukio ya kusikitisha kama hili la jana kule Haiti yanatukumbusha umuhimu wa kupanga miji katika namna inayotoa fursa ya kufanya harakati za uokoaji kwa ufanisi. Mpangilio wa jiji la Dar es Salaam hautoi nafasi hiyo. Uchipukaji wa majengo marefu katikati ya jiji unaweza kuwa wa hatari kubwa kwa siku za baadaye. Majanga ya asili hayachagui wapi na lini yatokee – ila ni vema kukaa tayari kwa njia zote daima. Nawakilisha.


Posted in Siasa na jamii

Tabasamu la 2010…

January 13, 2010
Leave a Comment

Pichani juu ni Scola. Mkazi wa Kisarawe. Bila shaka ana haki ya kutabasamu maana kuna shughuli nyingi za maendeleo zinafanyika katika wilaya yake. Mojawapo ya shughuli hizo ni ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kisarawe kuelekea Msanga na kwingineko. Tabasamu ni muhimu kwa ajili ya kuwa na afya njema. Tabasamu. Cheka.


Posted in Siasa na jamii

Utajiri wa Watanzania

January 6, 2010
Leave a Comment

Tanzania ni nchi iliyojaaliwa utajiri mwingi. Utajiri mkubwa zaidi ni ardhi. Pamoja na kuwa na utajiri huo bado Watanzania wengi ni maskini, kwa mujibu wa ripoti mbalimbali za utafiti, hususan Poverty and Human Development reports (2002, 2003, 2005 na 2007). Wengi bado wanaishi kwa kipato cha chini ya dola 2.00 za Marekani kwa siku.

Kuna mengi ambayo serikali na Watanzania kwa ujumla tunaweza kufanya ili kujikomboa kutoka katika umaskini huu. Jambo kubwa ni kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa. Lingine ni kutoa nafasi kwa watu kueleza vipaumbele vyao katika maeneo yao na kuhakikisha kwamba wanashiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi waliyoshiriki kuibuni.

Suala la ardhi na umiliki wake halina budi kuzingatiwa na kupewa uzito unaostahili. Tunayo Sheria ya Ardhi ambayo imechukua sura mbalimbali katika miaka tofauti. Umiliki wa ardhi mpaka sasa uko wa aina mbili. Kuna ule wa kimila na ule wa hati. Kwa kuwa umiliki wa aina zote hizo mbili unatambuliwa kwa mujibu wa sheria basi ni vema njia zote hizo zikapewa heshima iliyo sawa.

Upangaji wa matumizi ya ardhi ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa. Hata hivyo, ili kuepuka migogoro na manung’uniko ni vema wananchi wakapata fursa ya kuelewa vizuri mipango hiyo ya matumizi ya ardhi – pengine washiriki kikamilifu katika kuibuni na kisha wale ambao hawana budi kupisha miradi ya kitaifa na kieneo ya maendeleo, wapate kufanya hivyo kwa kuridhika baada ya kulipwa fidia inayostahili kwa kulinganisha na nguvu ya soko.

Ili basi nchi iendelee, kuna umuhimu mkubwa wa kuzingatia haki katika ushiriki wa watu kwenye mipango ya maendeleo, kusikiliza sauti zao na kuwaelimisha juu ya mipango iliyopo ili hata wanapolazimika kuhama kutoka eneo moja kwenda lingine wafanye hivyo kwa kuelewa umuhimu wa kuhama kwao.

Nakaribisha maoni kujadili jambo hili.


Posted in Siasa na jamii

Kadhia kuu Dar…

April 5, 2009
Leave a Comment

dscf0005

Ni katika makutano ya barabara ya Nyerere na ile iendayo uwanja wa Ndege wa zamani, Terminal One. Kuanzia hapo, ni kimbembe kuikamata Banana. Barabara ni ya lane moja, lakini mara nyingine hujitokeza lanes mpaka tatu! Kuna wanaopita kwenye kingo za barabara, kuna wanaokatisha katika njia za waendao kwa miguu! Ni uharibifu mkubwa wa mazingira. Kuna umuhimu wa kutafuta suluhu kwa kadhia hii inayozidi kukua kila kunapokucha … foleni ndeeefu katika barabara za Dar es Salaam. Suluhu si kuondoa vipanya peke yake, kuna umuhimu wa wanausalama barabarani pia kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi. Foleni hizi ni jinamizi kubwa kwa kasi ya kukua kwa uchumi wetu. Dawa itafutwe.


Posted in Siasa na jamii

Tuna historia … tuitunze

March 29, 2009
1 Comment

dscf0028

Historia hii itunzwe. Ni hazina kubwa itakayolisaidia Taifa hili katika miaka ijayo. Hao wanaoitwa ‘waendelezaji’ waende kuendeleeza jiji huko pembezoni, siyo hapa katikati.

Na mvua inapotua jijini Dar mambo huwa hivi mitaani:

dscf0034

Mitaa hubaki mitupu.

dscf0035

Na baada ya mitaro ya maji machafu kuziba, basi maji hufurika barabarani. Hali hiyo inapotokea, unachagua moja kati ya mawili – au unajitosa kukanyaka maji hayo au kulipa sh 100 ili uvushwe katika maji machafu kwa kubebwa kwenye mkokoteni. Mababa wa Jiji, kazi mnayo!


Posted in Siasa na jamii

Sitakishari Veterani yatimiza mwaka …

March 29, 2009
Leave a Comment

dscf0063

Kikosi kamili cha Sitakishari Veteran Sports Club katika Bonanza Maalumu la kusherehekea kutimiza kwa mwaka mmoja tangu timu hiyo ianzishwe rasmi. Iliichapa timu ya Ukonga kwa mabao 2 – 0. Timu nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Boko, Ukonga, Pugu, Kitunda na Air Wing. Kandanda safi ilisindikizwa na mchezo wa kuvuta kamba na burudani safi ya muziki.

dscf0061

Kulia ni Mh. Stambuli, Diwani wa Kata ya Kipawa aliyekuwa mgeni rasmi katika Bonanza hilo; kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Sitakishari Veterani Sports Club, Mr Morris; Kulia kwa Bwa Stambuli ni Mr Elly Ngwala, aliyekuwa DJ na mhamasishaji mkuu.

dscf0050

Mwanadada mshika kibendera alimudu vema mechi zote zipatazo nane alizosimamia tangu asubuhi.

dscf0075

Washikaji kibao walikuwepo.

dscf0070

Mambo ya kuvuta kamba hayakukosekana. Mpaka tunakwenda press, Bonanza lilikuwa bado likiendelea.


Posted in Siasa na jamii
Next Page »

About author

I am a citizen of Tanzania. I live in Dar es Salaam, commercial city of Tanzania. I am an editor, particularly dealing with books as well as other publications and related activities: editing, translating, supervising design and layout, monitoring printing, warehousing and dissemination of the books. I am also an author: I write children's story books, school textbooks and adult books. I undertake translation tasks from English to Kiswahili and vice versa. I do book indexing, that is preparing an index for a professional book. Contact: kakasimba@gmail.com . Feel free to get in touch with me.

Search

Navigation

Categories:

Links:

Archives:

Feeds