Posts Tagged ‘utaifiti’
Ajira: Wanawake na Maendeleo
Ajira rasmi bado ni changamoto kubwa kwa nchi yetu. Kwa mujibu wa matokeo ya ‘Utafiti wa Watu Wenye Uwezo wa Kufanya Kazi wa Mwaka 2014’ wa National Bureau of Statistics, kuna jumla ya watu 25,750,116 wenye uwezo wa kufanya kazi nchini. Miongoni mwao, Nguvu Kazi ya Taifa ni 22,321,924. Na kati ya hao kwenye kundi hilo la pili, walio kwenye ajira ni 20,030,139. Idadi hiyo ni jumla ya walio kwenye ajira rasmi na isiyo rasmi.
Kwa mujibu wa utafiti huo, sekta isiyo rasmi haijumuishi shughuli za kilimo. NBS inafafanua kuwa ni zile shughuli za kiuchumi zinazofanywa na mtu mmoja mmoja au na kaya lakini ambazo ni vigumu kisheria kuzitofautisha na wamiliki wake, kwani mara nyingi hazina akaunti zake zenyewe za benki, baadhi ya bidhaa wanazozalisha ni kwa ajili ya kuuza huku zikiajiri chini ya wafanyakazi watano.
Utafiti huo unaonyesha kuwa kuna kaya 4,338,070 zenye shughuli za kiuchumi zilizo katika sekta isiyo rasmi. Lakini utafiti unaonyesha kuwa wanaofanya kazi mmojammoja katika sekta isiyo rasmi ni watu 6,257,124.
Kwa hiyo, nchi yetu ina changamoto kubwa ya kuwaingiza hawa katika sekta rasmi. Ni kwa sababu ya ukosefu wa ajira rasmi siku hizi tunaanza kuona akina mama wakifanya shughuli za uchuuzi mijini. Shughuli hizi zilikuwa zikifanywa zaidi na akina baba. Hii ni kwa maana ya kubeba bidhaa na kuzitembeza kutafuta wateja.
Tulipe kodi ili kwa pamoja tulete mabadiliko katika uchumi wa nchi yetu.
Pamoja sana.
Written by simbadeo
April 24, 2016 at 10:47 pm
Posted in Business, Conflict, Culture, Economy, Education, Family and social life, human rights, Investment, Media, People, Places
Tagged with ajira, ajira isiyo rasmi, ajira rasmi, Integrated Labour Force Survey 2014, kaya, matokeo, National Bureau of Statistics, NBS, utaifiti