simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Archive for November 16th, 2012

Treni ya Mwakyembe … Madereva Kaeni Chonjo

with 2 comments


Garimoshi la abiria wa Dar es Salaam likiwa katika moja ya safari zake kati ya Posta na Ubungo Maziwa.

Gari dogo la binafsi likiwa kwenye moja ya foleni za magari jijini. Hata hivyo, gari hilo lipo katikati ya njia ya reli.

WAKATI ambapo wakazi wa baadhi ya maeneo ya jiji la Dar es Salaam wanaendelea kunufaika na kuanzishwa kwa usafiri wa abiria wa ndani ya jiji (Commuter train) — tangu katikati ya mwezi Oktoba — kuna haja tupeane hadhari.

Njia ya reli inayotumika kwa usafiri huu wa aina yake — asante kwa juhudi za Dkt Harrison Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi — inakutana na barabara kuu na ndogo na hata njia na vijia vingi sana. Katika baadhi ya makutano hayo kuna wasimamizi na vizuizi vilivyoanziswa, hata hivyo kuna mahali pengi ambapo hakuna watu na nyenzo hizo. Kumbe basi, badala ya madereva na waenda kwa miguu kutegemea tu nyenzo hizo pamoja na king’ora cha garimoshi, ni vema tukajifunza kuheshimu sehemu hizo za makutano na kuongeza uangalifu na umakini.

Binafsi sioni kwa nini mtu unayeendesha gari ulisimamishe kwenye njia ya reli. Hebu fikiri kama garimoshi litatokea ghafla, utafanya nini wakati mbele na nyuma na pembani kote umebanwa na magari? Hivi, unapoteza nini kwa kusimamisha gari lako walau mita tatu kutoka njia ya treni?

Inafaa tujifunza kuepuka ajali zisizo za lazima. Tuache kumjaribu Mungu (na bahati mbaya). Tufuate kanuni ya ‘akili ya kuzaliwa nayo’ (common sense). Si lazima Dkt Mwakyembe aje kusimamia na jambo hili.

Vivyo hivyo kwa waendesha pikipiki, baiskeli, mikokoteni, bajaj na hata waenda kwa miguu … umakini tuwapo barabarani saa zote utatusaidia sana kupunguza ajali, hasa kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.

Nawakilisha. Pamoja sana.

Written by simbadeo

November 16, 2012 at 11:21 pm