Hapa ni mashaka tu. Mwaga punje za mchele hapo na kila mmoja atazipigania. Hapa kila mmoja ni mjanja kwenye anga yake. Nafikiri tunaweza kuwafananisha na wanasiasa na vyama vyao … kila kimoja kina ujanja wake katika kujipatia kura yako. Kibaiolojia … kila kimoja kina umuhimu wake (negatively or positively). Tutafakari hatma ya siasa na nchi yetu … hususan hivi sasa ambapo mali-asili kibao zinazidi kuvumbuliwa, mali-asili ambazo katika nchi nyingine kadhaa zimegeuka kuwa laana badala ya baraka. Ni vema sisi tujifunze kuwa makini tusije angukia pua kama Taifa. Umimi usipewe nafasi hata chembe … tujifikirie SISI sote. Pamoja sana!
-6.822921
39.269661