simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Archive for January 16th, 2013

KIA … Kazi ya Sanaa

leave a comment »


Barabara hii inayoelekea KIA ni mithili ya mstari ulionyooka kwa kupigwa kwa rula. Ina urefu wa kiasi cha kilomita sita kutoka Barabara Kuu ya Moshi kwenda Arusha.

Barabara hii inayoelekea KIA ni mithili ya mstari ulionyooka kwa kupigwa kwa rula. Ina urefu wa kiasi cha kilomita sita kutoka Barabara Kuu ya Moshi kwenda Arusha.

Unaanza kuliona jengo la kiwanja ... takribani umbali wa kilometa moja hivi.

Unaanza kuliona jengo la kiwanja … takribani umbali wa kilometa moja hivi.

Hapa ni sehemu ya jengo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (JRO/KIA). Unapolitazama jengo hili kwa kiasi fulani unapata hisia za Jengo la Terminal One la Julius Nyerere International Airport. Kuna tofauti mbalimbali hata hivyo.

Hapa ni sehemu ya jengo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (JRO/KIA). Unapolitazama jengo hili kwa kiasi fulani unapata hisia za Jengo la Terminal One la Julius Nyerere International Airport. Kuna tofauti mbalimbali hata hivyo.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (JRO/KIA) … nao ni sanaa ya aina yake. Ingawa ni uwanja mdogo na kama unatoka ughaibuni utahisi kama vile unatua kwenye uwanja wa ndege wa Kijiji, kubwa ni kwamba aliyesanifu ramani ya jengo na mpangilio wa vitu kuwa nini kiwe wapi na wapi kiwekwe nini alifanya kazi nzuri. Upungufu uliopo unaweza kushughulikiwa na uongozi wa sasa, hasa kwa vile hivi sasa kiwanja hiki kimeanza kuwa na kazi nyingi na kwa hiyo kinaingiza mapato mazuri.

Kilicho chako, japo kidogo, yakupasa kujivunia.

Pamoja sana

Written by simbadeo

January 16, 2013 at 12:01 am

Posted in Siasa na jamii

Tagged with , , ,