simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Ufugaji Kuku …

with 500 comments

dscf0010

dscf0011

Pichani ni kuku wenye uzito kati ya kilo 4 mpaka 6 wanaouzwa kwa Amadori eneo la Uwanja wa Ndege, Dar es Salaam. Bei ya kuku ni Sh. 14,000/= kwa kuku jike na 22,000/= kwa jogoo.

Ufugaji kwa njia bora za kisasa ni moja ya njia tunazoweza kutumia Watanzania kujikwamua kutoka kwenye umaskini. Kuna somo hapo la kujifunza.

(Makala hii ilifahamika kwa jina la ‘Kuku wa Amadori’ mpaka tarehe 30 Julai 2011. Kutokana na maombi ya wadau wa webpage hii, jina la makala limebadilika kuwa ‘Ufugaji Kuku’. Tafadhali endelea kuifuatilia ili ujifunze na ufunze wengine pia).

Written by simbadeo

December 25, 2008 at 12:49 pm

Posted in Siasa na jamii

500 Responses

Subscribe to comments with RSS.

  1. Natafuta sana taarifa mbali mbali za ufugaji wa kuku lakini kwa kiswahili sipati. Ina maana wataalamu wetu wako nyuma kiasi hiki? Yaani kutokuwa na taarifa za maana za kumfaa mkulima au mfugaji katika mtandao? Mimi ni mfugaji mdogo, lakini sasa nataka kuwa mkubwa na shamba langu ni ekari 7 nje kidogo ya Dar es Salaam. Ninao kuku wa kienyeji mchanganyiko na wa kisasa. Pia ninao kanga (Guinea fowls) wengi na vifaranga wao wengi tu. Kuku wangu na Kanga wanatembea free, isipokuwa vifaranga kwa hofu ya kuchukuliwa na ndege wajanja kama Kipanga na Kuguru. Ninao pia Nguruwe 8 ambao 1 ameshapandwa tayari.

    Sasa najiuliza wapi nitapata taarifa za ufugaji bora na jinsi ya kuanzisha shamba langu sipati majibu. Kwenye net kuna taarifa nyingi kwa kiingereza. Nilidhani za Kiswahili pia zapatikana ili hata vijana wasaidizi shambani iwe rahisi kwao kusoma na kuelewa. Nisaidieni kwa hili: Wapi nitapata msaada wa kufuga kama hao Amadori Farm?

    NB: Picha nzuri, ila wanunuzi hao wakatili sana. Shambani kwangu sitaruhusu mnunuzi au awaye yote kumbeba kuku au mnyama vibaya namna hiyo. Ninawapenda sana wanyama, wana akili sana. Immagine kumni’nginiza kuku wa kilo 4 kwa mabawa yake tu!!! Soooo Sick behaviour! Am not joking, I hate it!

    MTZ halisi.

    Like

    Jenny

    March 3, 2009 at 11:22 am

    • Jamani mi naona amadori kama ni waongo mana nimelipia vifaranga vya nyama hii inaenda wiki ya nne sijui nimetapeliwa au?

      Like

      BARAZA

      February 14, 2014 at 10:02 am

      • Baraza, ungefuatilia ulikolipia tatizo ni nini badala ya kulaumu. Hatuwezi kujua pia mapatano yenu yalikuwaje, ukilipia unavipata baada ya muda gani… Wafuatilie wenyewe ili uwe na uhakika umetapeliwa ama la.

        Ufugaji mwema.

        Like

        Jenny

        February 14, 2014 at 1:57 pm

  2. Mimi natafuta soko la hawa kuku ninao wengi nauza Tsh 11000 tu kwa majogoo kama kuna mtu anahitaji awasiliane nami lakini nauza kwa jumla kuanzia 300 nakuendelea

    Like

    kuku

    June 1, 2009 at 8:23 pm

    • namba yako kaka naomba, ama chukua ya kwangu 00353860654019 nitumie text nitakupiga tafadhali

      Like

      Lui

      November 2, 2014 at 3:26 pm

  3. Du kaka simba ni kweli unayosema kuwa kuku wanaweza kupatia kipato watanzania lakini kuna tatizo kubwa sana kwa wafanyabiashara wa kuku wenyewe na ambao tunawapelekea kkuku hao. Mimi nilikuwa mfugaji wa kuku hasa hawa wa kisasa lakini imefikia mpaka nimejitoa kwenye kazi hiyo kwa sababu kubwa ya kutoko kuwa na ushirikianio na wafugaji wengine. Na ushirikiano huo ninaosema siyo wa kufanya kazi pamoja bali amawazo na bei katika soko ambalo watu woote tunakimbilia kuuza hao kuku wakisha kuwa wakubwna au wa kuuza mayai. Nilikuwa najaribu kufanya kazi hii kwa utaalamu mkubwa sana wa kuweka record ya gharama ninazotumia ili nijue ni faida gani halisi naweaza kupata wa kati wa kuuza. hadi mwaka 2008 december wakatiu mimi naacha kufuga kwa mujibu wa hesabu zangu nilizo kuwa nafanya kuku mmoja bloiler wa wiki 6 toka kumnunua hadi kumuuza alikuwa anafikisha gharama ya shs 3500 hadi 3800 na kama atakaa zaidi ya hapo gharama hizo zinaongezeka kwa sababu anaendelea kula kila siku, sasa ukuienda kwa wanunuzi hiyo ndio bei wanataka kununua kuku wako sasa hapa maendeleo utapata au unafanya kazi ya watu tu bila faida yeyote. usipo waauza kuku hao siku zinapozidi in maana gharama inaongezeka, ukiacha kuuz mwenzako anakuja hapo ulipo kataa hiyo bei ambayo uaona haina maslahi yeye anauza kwa bei hiyo wako wanabaki na gharama inaongezeka. Ukimuangalia mtu huyo unaponunu a chakula cha kuku na yeye anachukua hapahapo sasa unajiuliza mtu huyu anafanya hesabu kweli au anauza kuku kwa kuangalia bei ya kununua vifaranga na bei ya kuuzia kuku tu gharama nyingine haweki kama umeme, ulizi maji mfanyakazi (watu wengine gharama za mfanyakazi huwa hawaweki kwa sababu familia ndio inafanya kazi hiyo na hakuna malipo yeyote katika nguvu hizo za familia, umeme na maji watu wengi wanasahau kanma ni gharama katika kuku hao unaowauza kwa kuw atu maji na umeme ni bili za kawaida nyumbani wanasahau kuwa hii ni biashara ili kupata faida ni lazima gharama hizo uweke na usipo weka ndio unajidanganya kuwa umepata faida kumbe ni gharama zako mwenyewe ambazo hujaziweka.
    mambo hayo yapo vile vile kwenye kwenye kuku wa mayai watu wanaacha gharama nyingi sana na kuuza mayai kwa bei ndogo hivyo wafugaji woote wa kuku Mwanza na shemu nyinginezo mfanye mikutano ya mara kwa mara kwa ajiri ya kupanga bei na wateja wenu watanunua tu kama mtakuwa na bei ya pamoja yenye maslahi

    Like

    YOMBOP from Tanzania

    August 24, 2009 at 4:56 pm

    • uko sawa maji na umeme wanafikiri vinakuja kama upepo;kumbe ni pesa zao

      Like

      madaraka

      October 19, 2013 at 3:37 pm

    • Nimekusoma

      Like

      taniwatani

      May 29, 2014 at 11:15 am

  4. it’s true what my friends comments about the specialist,b’coz even I try to look such information but funny enough I did n’t find & we are saying KILIMO KWANZA how is it possible.To my point of view I think the committe did not think of it first,am n’t saying it’s a bad idea,but they should analyse things well, by putting polices that are condussive and can be implimented by the required society.

    Like

    p squire

    September 29, 2009 at 12:49 pm

  5. naomba kama unawezekana nikapata contact za huyu bwana muuza kuku wa Amadori wa maeneo ya uwanja wa ndege nitafurai .

    Like

    peter

    March 19, 2010 at 3:39 pm

    • Niko Moshi mjini Ninaangua viranga Chotara wa Kuku kienyeji. Vifaranga 120-150 kila wiki. Kuna vifarnga kuanzia siku moja mpaka wiki nane. Bei inaendana na umri na kiasi unachonunua. Bei inapungua kiasi kikiongezeka. Simu: +255 784 29 08 08 KARIBU !!

      Like

      drswai@yahoo.co.uk , eliafieswai@gmail.com

      January 28, 2011 at 2:06 pm

      • Ndg Swai. Asante sana kwa mchango wako na taarifa uliyotufikishia hapa. Ninaamini kwamba wadau watanufaika nazo sana. Ndugu wadau … bila shaka hii ni fursa nzuri sana. Tumempata ndugu Swai ambaye yuko kwenye nafasi ya kutushirikisha maarifa mengi sana, hususan kuhusu vifaranga. Hebu na tumwulize maswali yale ambayo pengine mpaka sasa bado hatujapata majibu yake. Karibuni.

        Like

        simbadeo

        January 28, 2011 at 11:33 pm

  6. Mimi nina shamba langu la eka 3 maeneo ya bunju ninafuga mbuzi wa nyama na ng’ombe wa maziwa nataka kuanza ufugaji wa kuku wa kisasa wa nyama na mayai.sasa katika utafiti wangu nimegundua tatizo kubwa upatikanaji wa vifaranga na ubora wa vifaranga hivyo.kwa yoyote mjasilia mali mwenzangu anisaidie katika upatikanaji wa vifaranga kwa urahisi.

    Like

    seddy farm

    April 29, 2010 at 6:14 pm

    • Seddy farm, umefuatilia alichotueleza Jenny? Nadhani ni jambo linalofaa kujaribu, huenda litasaidia sana, au siyo?

      Like

      simbadeo

      May 18, 2010 at 2:49 pm

  7. Hello Seddy Farm,

    Vifaranga ni tatizo sugu. Lakini ili upate vifaranga bora na wazuri, huna budi kuwapata kutoka katika sehemu ambako tunapanga foleni kuwapata. Nakushauri kwa vile unaishi Bunju, uweke order pale Interchick, wana vifaranga wazuri sana na mimi huchukulia hapo. Ila tatizo ni foleni utakayoikuta, ukilipia mwezi huu vifaranga unaweza wapata baada ya mwezi mmoja na nusu ama miwili lakini kwa uhakika kwamba utawapata, na wanatoa ushauri mzuri kwa wafugaji wanaoanza kufuga.

    Kutokana na kuibiwa sana mazao ya kuku shambani na vijana niliokuwa nikiwaweka, niliamua kubadilisha ufugaji. Kwa sasa ninafuga kuku wa kisasa wa mayai, lakini nawafuga kienyeji kabisa. Wanatoa mayai mazuri sana na mimi na familia yangu tunayatumia pia, mayai yenye kiini cha njano na ladha kama mayai ya kuku wa kienyeji. Nimegundua mayai mazuri ya kuku yanatokana na namna unavyowatunza na kuwalisha. Ninao wachache ili kumudu kuwahudumia kienyeji. Nimebakiza pia kanga wachache kwa ajili ya ulinzi wa shamba na kufukuza wadudu na nyoka. Changamoto ni nyingi sana, I wish kungekuwa na mshikamano wa pamoja hata online ili tuweze kupeana uzoefu na namna ya kutatua matatizo mbali mbali yahusuyo mifugo na kilimo.

    Like

    Jenny

    May 17, 2010 at 10:16 am

    • Asante Jenny, umetupa maelezo safi na yenye kutoa mwanga sana. Cheers!

      Like

      simbadeo

      May 18, 2010 at 2:50 pm

    • Mimi nafuga kuku wa nyama na matatizo uliyoyasema ni ya kweli kabisa kiasi kwamba nami natatka kuanza kuku wa mayai na nimevutiwa na njia yako ya ufugaji wa mayai kwa kutumia njia za kienjeji, Jee waweza tuelimisha zaidi?.

      Like

      Nassib

      July 8, 2010 at 3:28 pm

      • Ndugu Nassib

        Asante kwa maoni yako. Nimefurahi kusikia kuhusu juhudi zako. Soma vizuri maoni ya Dada Jenny kwenye post hii. Naamini kuna mengi ya kujifunza hapo. Unaweza pia kuwasiliana naye kwa maelekezo ya kina zaidi.

        Wasalaam

        Simba Deo

        Like

        simbadeo

        July 9, 2010 at 3:51 pm

    • Hello Jenny,

      Nimefurahi saana kwa commens zako hapo nikupate wapi ili unipe darasa la kuku wa kisasa wa mayai maana na mimi nataka kuanza kufuga wa biashara mapema iwezekanavyo maana ninapenda saana yaani kufuga, please naweza kupata mawasiliano yako kama hutojali, iliniweze kukutembelea nakupata ushauri wako hata kununua kwako kama inawezekana

      Rachel

      Like

      Rachel

      February 4, 2011 at 4:02 pm

    • Hello Jenny,

      Nimefurahi saana kwa commens zako hapo nikupate wapi ili unipe darasa la kuku wa kisasa wa mayai maana na mimi nataka kuanza kufuga wa biashara mapema iwezekanavyo maana ninapenda saana yaani kufuga, please naweza kupata mawasiliano yako kama hutojali, iliniweze kukutembelea nakupata ushauri wako hata kununua kwako kama inawezekana

      Pia naomba ushauri wenu mimi nina banda langu nymbani tu kijitonyama ni kubwa lakini na ninatamani saana kufuga kuku wa mayai, na lengo langu nikununua kuku kesho jumamosi ya tarehe 5 Feb 2011, sasa nifikiria kutonunua kwanza ili nipate elim ya kutosha, mwanzo nilifuga wa kienyeji wa nyama tu sikua serious nao saana, lakini sasa hivi nimeamua kufuga wa kisasa wa mayai, please waungwana nisaidieni nahitaji elim hii ya ufugaji,

      ninachotaka kujua ni mwanzo wake, mimi nina banda tayari, kilichobaki ni kununua tu kuku nakuanza sasa najiuliza,

      1. je nanunua vifaranga na kuwa kuza mpaka waanze kutagia mayai kwangu?

      2. je haiwezekani kununua waliokaribia kutaga? yaani wakubwa wakubwa kidogo,

      3. Je nikisha nunua kuku kinachofuata ni nini? nawatibu (kuwadunga sindano)ndo naanza kuwalisha au inakuwaje?

      4. Je banda linatakiwa liweje? mimi banda langu liesakafiwa na simenti ile lakini halijawekwa kwenye hali ya kusakafiwa vizuri, je niweke hivyo hivyo kuku au inakuaje? kuna mtu aliniambia ni lazima niweke randa za mbao, je ni kweli?

      5. Na je, inatakiwa kuwatibu mara ngapi kwa mwezi? au nipale tu wanapougua?

      Naomba mniwie radhi kwa maswali yangu, mimi ni mgeni hapa na nimara ya kwanza kuandika hapa, nafikiri mtanisaidia, napenda saana biashara hasa hii ya ufugaji

      Asanteni saana

      Rachel

      Like

      Rachel

      February 4, 2011 at 4:49 pm

      • Rachel, karibu katika kijiwe chetu. Kila tunapopata mwanachama mpya, sisi hufarijika sana. Moja ya malengo ya blogu hii ni kuunganisha watu walio na fikra/nia/malengo yanayofanana ili kwa pamoja waweze kujiletea aina ya mabadiliko wanayoyataka. Kama utakuwa umesoma maoni karibu yote katika makala ya Kuku wa Amadori, bila shaka umeona kwamba kuna mengi ya kujifunza na kwamba bado tunahitaji maarifa zaidi kutoka kwa wenye nayo. Kwa hiyo jisikie nyumbani, uliza maswali yote uliyo nayo pasipo kusita … kwa kufanya hivyo utawasaidia na wengine pia. Karibu.

        Like

        simbadeo

        February 4, 2011 at 5:14 pm

      • Wadau, tumemsikia Rachel. Wenye majibu kwa maswali yake, tafadhali wamsaidie kwa majibu.

        Like

        simbadeo

        February 5, 2011 at 1:20 pm

    • Hey nimefurahi sana kusoma email yako mimi niko moshi na nataka kuanza kufuga ao kuku wa mayai lakini watakao kuwa wanataga mayai yenye kiini cha njano kama utojali unaweza kunielekeza ni vipi unavyowafuga kuku hao .

      Asante,

      Nasra.

      Like

      nasra

      November 3, 2011 at 2:41 pm

  8. Hello,

    Hao kuku wa mayai nawanunua na kufuata utaratibu wote kama inavyotakiwa wakiwa vifaranga wadogo. Nawapa chanjo na matunzo yao yote wakingali wadogo hadi wanapokaribia kutaga ndio naanza kugeuza kidogo kidogo mwenendo wao, wanakuwa wameshakuwa resistant sana kwa magonjwa wanapokua wakubwa.

    Hawa nilionao nilianza kuwatoa nje na kuwaachia wiki chache kabla ya kuanza kutumia chakula cha kutagia. Wakizoea nje wanafurahia sana hawataki hata kurudishwa ndani, inakuwa taabu kuwarudisha hadi muwe 2 au 3 muwazingire huku na huku kuwaelekeza mlangoni. Kwa vile nafugia shambani, eneo ni kubwa na hivyo wako huru japokuwa watu wa shambani huwatoa wakati wanapokuwa na hakika ya wao kuwepo macho kuangalia na kuwafuatilia. Pia huwatoa nje wakishataga wengi hasa muda wa mchana.

    Ni vizuri ukianza kuwaachia nje pia kujifunza kuchanganya chakula chao mwenyewe. Kuna wateja wengine hawapendi baadhi ya vitu vinavyowekwa kwenye vyakula vya kuku mfano damu, hivyo ukiweza kuchanganya chakula mwenyewe inakuwa vizuri zaidi. Nawapatia pia treats ya dagaa wanapokuwa nje, wanapenda sana ila sio mara kwa mara na kwa wingi maana la sivyo hata mayai yatanuka samaki. Kuna aina ya majani laini wanapendelea sana kula, ukiyafahamu wakati wa mvua yako mengi unawapa wanapokuwa hawajatoka nje.

    Mayai yao hayana tofauti kabisa na yale ya kuku wa kienyeji. Japo ninao wachache, najitahidi kuwafuga kwa njia hiyo na mayai yangu yanapendwa sana na watu walioyatumia. Nauza tray TShs. 7,000/= badala ya bei ya kawaida kati ya TShs. 5,000/= hadi 5,500/= ambayo niliona hailipi.

    Natarajia kuongeza wengine, lakini nitakaposhindwa kuwafuga wote kwa njia hii kwa kuwa wengi, nadhani bado nitatenga kundi fulani kwa ajili ya mayai hayo ninayotoa sasa au kuwapatia zamu za kufurahia maisha ya nje ambako wanakula majani na vidudu mbali mbali.

    Nadhani hadi hapo nimesaidia ya kutosha.

    NB: Ninapotaka kupata mbegu mchanganyiko pia huwa natenga majike kadhaa na majogoo wa kienyeji kabisa, wakiwapanda yanapatikana mayai yenye mbegu ambayo nawapatia kuku wa kienyeji kuatamia. Bado sijaweza kununua mashine ya kutotoleshea. Katika kuku wa aina hii pia nimewahi kupata majike wanaotaga tu kama hao wa kisasa, hawajui kuatamia, wanataga tu mfululizo hadi wanaposimama kupumzika wenyewe na ni wakubwa.

    Kuna uzoefu mwingi endapo tutasaidiana, mimi najua hiki na wewe unafahamu kile, tukiunganisha tunasaidiana kufika mbali. Siku njema.

    Like

    Jenny

    July 12, 2010 at 2:53 pm

    • Dada jenny ,

      Nimefurahi sana na hilo somo lako na mimi nimmoja wapo ambaye natamani sana kuanzisha iyo biashara ya kufuga kuku wa mayai lakini yellow york ila ndo sijui ntaanzia wapi kwa sasa naishi moshi ntashukuru kama utanisaidia kunielimisha zaidi.

      Asante,

      Nasra.

      Like

      nasra

      November 3, 2011 at 2:49 pm

    • Bei ya Kuuzia ni Nzuri.. Tofauti ya 1500.. Aise!

      Like

      Abiyamu Solomon

      July 7, 2012 at 11:08 am

      • Abiyamu, hiyo ilikuwa bei ya 2010. Sasa tuko 2012 na tray yangu ni 10,500/= kwa mayai ya layers, yanajiuza tu yenyewe kwa jinsi yalivyo mazuri. Karibu.

        Like

        Jenny

        July 9, 2012 at 8:04 am

  9. Pia, nje wanapata nafasi nzuri ya kuota jua na kuoga mchanga. Unawafaa sana mchanga kwa ngozi. Kwao inaitwa “Sand Bath”. Ni maisha ambayo mnyama angetakiwa apate lakini watu tunasahau hilo na kuangalia faida tu. Mayai bora yanatokana na namna kuku wanavyotunzwa vizuri na chakula wanachokula. Nafasi kati ya kuku na kuku ni kubwa sana, wako huru sana bandani kwao maana banda ni kubwa. Linatosha kuongeza wengine 50 hivi na bado wakawa na nafasi nzuri ya kutosha kwa hivyo ukiwapa raha, wanyama nao watakupatia raha, wana hisia na akili pia japo sifahamu kwa kiwango gani kutofautisha na binadamu.

    Like

    Jenny

    July 12, 2010 at 4:34 pm

    • Asante sana Da Jenny kwa darasa zuri. Naamini wafuatiliaji wa post hii juu ya ufugaji wa kuku kwa njia zenye tija wamenufaika sana. Mie pia napata hamu ya kuanza biashara hii. Fursa ikipatikana Da Jenny unikaribishe shambani kwako nipate kujifunza zaidi. Shukrani. Tuendelee kuchangia.

      Like

      simbadeo

      July 14, 2010 at 11:18 am

      • Habari ya Kazi Kaka Deo, Mimi ninahitaji ng’ombe na mbuzi wa nyama wa kisasa. Kama kunamtu unamjua anao hao ng’ombe wa kisasa wa nyama na/au mbuzi wa kisasa tafadhali naomba unijulishe pamoja na gharama zake na ni wapi wanapatikana.

        Like

        Christian Maembe

        August 15, 2012 at 5:28 pm

      • Ndugu Christian Maembe. Karibu katika jukwaa hili. Kwa hakika, wewe leo umetuingiza kwenye mstari mpya — ufugaji wa mifugo kama ng’ombe na mbuzi. Hadi wakati huu tangu tumeanza majadiliano hapa, hatujazungumzia kuhusu mifugo hii. Ila kwa kuwa kuna mahitaji na hapa ni jukwaa huru na wazi, naamini watajitokeza wanaofahamu vema zaidi na kutushirikisha sote. Ninakukaribisha na ninawakaribisha wengine pia kuchangia. Karibuni sana. Deo Simba.

        Like

        simbadeo

        August 15, 2012 at 11:14 pm

  10. Nashukuru kwa daras ulilototoa dada jenny. Suala jingine ni kuhsus soko kwa mayai napata wasiwasi kuanza biashara ya kuku wa mayai nikiwa sioni soko la uhakika kwani nikiona waendesha baisikeli wakiwa na mayai hata mchana hivyo kunipa picha kwamba soko ni gumu; wengine wanasema kwamba watu hufuata mayai nyumbani kwa wafugaji hiyo ni vizuri lakini una mayai yako kila siku unaHANGAIKA madukani kupeleka mayai inanipa wasiwasi kuanza biashara hii. Naomba unipe shule ya soko la mayai. Ahsante

    Like

    Nassib

    July 15, 2010 at 9:35 am

  11. Soko la mayai kusema UKWELI ni ujanja na bidii zako mwenyewe katika kulitafuta. Nadhani kwa swali lako nimeelewa kwamba unapungukiwa -ujanja (ambao unaweza kuwa ni wa kuzaliwa nao), -ujuzi (ambao inabidi upitie mafunzo fulani kuupata) wa namna ya kutafuta wateja kwa bidhaa zako. Kuna Maduka Makubwa, Supermarkets, Hoteli, Masoko, Mashule, Hospitali, Vyuo, Magereza, Majeshi, Wenye baiskeli wanaonunua kwako nao wakauze, maduka madogo, watu binafsi, wakaanga chips na kadhalika. Unataka kuuza ukiwa umekaa nyumbani bila kutoka wateja wafuate kwako hilo ni uamuzi wako kutegemea na UJANJA/UJUZI wa namna ya KUSHAWISHI wateja waweze kukufuata badala ya kukaa wakisubiri kupelekewa. Utakuwa kwenye mashindano na wale wanaopeleka huduma kwa mteja badala ya mteja kufuata huduma. Kwa maana hiyo nadhani unahitaji kupata UJUZI wa namna ya kutafuta masoko, kama UJANJA huna maana tunatofautiana talanta. Kozi fupi na ndefu za Ujasiriamali zipo na kwa bei nafuu, nyingine zina sponsorship kabisa na zinatolewa kwa watu wa kawaida tu kama sisi na nimeshuhudia hilo, Chuo Kikuu – UDSM – UDBS wanatoa kozi hizo, nadhani na taasisi zingine za elimu pia.

    Like

    Jenny

    July 15, 2010 at 1:13 pm

    • dada jenny nakushukuru sana

      Like

      Nassib

      July 15, 2010 at 2:00 pm

    • Dada Jenny nimefarijika sana. Nimejifunza jambo kubwa kuhusu uanzishaji miradi. Nalo ni kwamba … haitoshi tu kuanzisha mradi … bali lazima kuhakikisha kwamba mradi huo unakuwa endelevu … na unapata uendelevu huo kwa kutafuta masoko … na kwamba kazi ya kutafuta masoko hiiishii kuwa na product tu. Lazima kutumia mbinu za kijasiriamali ili kuhakikisha kwamba bidhaa ulizo nazo zinauzika.

      Ndugu Nassib na wengine tunaofuatilia mjadala huu natumaini tumepata elimu kubwa. Sasa pengine ni wakati wengine nao watushirikishe maarifa waliyo nayo. Kila mmoja anakaribishwa – inaweza hata kwa kuuliza maswali. Tunaweza kujiletea mabadiliko chanya katika jamii yetu – tunaweza.

      Like

      simbadeo

      July 16, 2010 at 10:33 am

  12. Hello Kaka Simba
    Naona watu hawachangii. Mimi nitaendelea tu maana nahitaji msaada bado wa vitu vingi. Leo nauliza wapi naweza kununua mashine ya kutotolesha vifaranga inayotumia mafuta ya taa? Asante

    Like

    Jenny

    July 27, 2010 at 12:49 pm

    • Hi Jenny, asante kwa kutupa changamoto hiyo. Ni kweli … watu hupita hapa na kusoma na kuondoka kimyakimya bila kuacha alama za kuonekana sana. Lakini hiyo isikukatishe tamaa kwani ujue kwamba watu wengi wananufaika na maelekezo ambayo wewe huwapa kupitia uwanja huu.

      Nafikiri wasomaji watakuwa wamepata swali ulilotutupia leo. Jamani, mwenye kufahamu wapi mashine hiyo inauzwa tafadhali atushirikishe. Au kama wewe ni mwuzaji wa mashine aina hiyo, tayari hapa una mteja mmoja na si ajabu wengi zaidi wakaibuka.

      Tupo pamoja!

      Like

      simbadeo

      July 27, 2010 at 1:42 pm

    • hbr.huwa tunatengeneza hizo incubator za mafuta.tuwasiliane kama bado unaitaji 0755524433

      Like

      albert

      July 29, 2013 at 4:53 pm

      • Habari
        Naitwa Pilly, mimi pia ni mfugaji wa kuku wa kisasa nilikuwa najiulia siku nyingi hivi hizi mashine za kutotoleshea vifaranga zinapatikana wapi? Bahati nzuri nimeweza kukupa.Mfano nataka mashine ya kutotoleshea vifaranga 500 ni kiasi gani? na vifaranga 5000 pia ni kiasi gani.napendelea zaidi ya mafuta ya taa au kama za umeme mnazo pia si mbayanina shamba ambalo nataka kufanyia hiyo kazi nipo mbioni kutafuta mtaalum anielekeze jinsi linavyotakiwa kuwa/Kuliendesha kwa ajili ya hiyo shughuli au kama kuna mtu anayejua anaweza kunielekeza zaidi,shamba langu ni ekari 1.5

        Like

        PILLY

        September 20, 2013 at 6:59 pm

  13. Nawashukuruni sana kwa elimu hii. Mimi nina swali, tafadhali naomba anayejua mchanganyiko unaotakiwa kwa vyakula vya kuku wa mayai anisaidie. Kwa mfano kama unataka kutengeneza kilo mia za starter, growers na layers unatakiwa kuweka kiasi gani cha mahindi, mashudu, soya beans nakadhalika?. Ahsanteni

    Like

    Elizabeth

    August 12, 2010 at 10:00 am

    • Da Eliza

      Asante sana kwa swali lako. Naamini Da Jenny atatumwagia somo zaidi hapa … na wengine wote wenye maarifa haya … msisite kutupatia. Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      August 12, 2010 at 11:44 am

  14. Mhhh kaka Deo, watu wanamsubiri dada Jenny tu wao hawachangii chochote jamani? Hata mimi nahitaji msaada tupeane maarifa.

    Kuhusu kuchanganya chakula, nakushauri dada Eliza uwaone madaktari wa wanyama wao watakupatia mchanganuo mzuri zaidi kulingana na mahitaji yako na aina ya kuku unaotaka kufuga. Mimi kwa mfano wateja wangu fulani kwa sababu za maadili yao ya dini, hawataki kutumia mayai ama nyama ambayo kuku wake walipewa vyakula vilivyochanganywa na vitu fulani mfano damu. Kwa hiyo uchanganyaji wa chakula unaomfaa mnyama, ni vizuri kuwaona madaktari wa wanyama. Sifahamu unaishi wapi, lakini mimi ninawafahamu baadhi ambao ni wazuri sana na wanapatikana katika maduka ambako kunauzwa pia madawa ya mifugo, na ambako huduma za wanyama zinapatikana. Usiwaone tu wauzaji wa hicho chakula, waone madaktari watakupa vipimo kamili kulingana na mahitaji na aina ya wanyama wako.

    Like

    Jenny

    August 13, 2010 at 8:23 am

    • Da Jenny,

      Asante sana kwa mchango wako. Ni mkubwa mno. Kiufupi unatupa changamoto sote tunaofuatilia darasa hili la mtandaoni kwamba ni muhimu kufanya utafiti. Na ili tupate matokeo mazuri kutokana na utafiti tunaofanya ni vema tulenge kupata wataalamu haswa wa hicho tunachokitafiti. Natumaini Da Eliza umemwelewa vema Da Jenny. Kwa mara nyingine tena ametufungua macho. Asante sana Da Jenny. Na, jamani, tusisahau changamoto nyingine aliyotupa – nasi wengine tushirikishe wengine yale tunayojua – tusikae kimyaa – kama unajua mawili matatu basi yamwage hapa. Tuendelee kuwepo!

      Like

      simbadeo

      August 13, 2010 at 10:22 am

  15. du namfurahia sana dajenny kwani ananigusa mi nafuga wa nyama wa kanga na wamayai ila bado sijawa mtaalamu sana ila ninaomba kama kuna mtu anafahamu sehemu napoweza kupata mashine ya kusaga chakula cha kuku ahsante

    Like

    damariam

    August 20, 2010 at 6:22 pm

    • Da Mariam, karibu kijiweni. Nimefurahi kusikia kwamba unafuatilia mjadala na huwa unakusaidia katika kukuza maarifa yako katika shughuli zako za ufugaji. Haya jamani, Da Mariam anaomba kufahamishwa juu ya mashine hiyo … anayejua jamani atuelekeze na wengine.

      Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      August 21, 2010 at 12:42 pm

    • Damariam
      mimi ni mpya sana katika njadala huu mzuri unaoendelea lakini nimependa kushiki. pamoja nanyi
      kuhusu mashine ya kuchangayia chakula hebu tembelea SIDO – MBEYA nilionana nao maonyesho ya nanenane Dodoma wana mashine nzuri zinazoweza kufanya kazi kwenye umeme wa kawaida single phase ni bei cheap zipo kwa ajili ya wafugaji medium size like you and me thanks

      Like

      atupele

      April 5, 2011 at 3:12 pm

      • Karibu sana Atupele na ninaamini taarifa uliyoingia nayo hapa uwanjani itakuwa ni habari njema kwa wadau wengi hapa. Asante sana kwa taarifa hiyo. Wadau tuchangamkie fursa hiyo.

        Like

        simbadeo

        April 6, 2011 at 12:02 am

  16. Mashine za kusaga na kuchanganya chakula cha kuku zinapatikana SIDO. Unachotakiwa kufanya ni kupiga simu Dar es Salaam (ya offisini) ukaomba kuongea na manager wa karakana. Mweleze unachokitaka atakupa ushauri. Hata kwenye maonyesho ya Nane Nane walikuwa nazo.

    Like

    Elizabeth

    August 25, 2010 at 4:18 pm

    • Da Eliza, asante sana kwa maelekezo haya. Naamini Da Mariam na wengine waliokuwa na mahitaji hayo sasa wamepata mwanga wapi kwa kwenda. Nadhani umefika wakati sasa SIDO kufanya matangazo zaidi ya bidhaa zao – kweli kutumia maonyesho ya Nane Nane na mengine kama hayo kuna nafasi yake, lakini pia kutangaza magazetini, kwenye blogu, kwenye redio na TV kwa wingi zaidi kutasaidia. Tuendelee kupeana maarifa. Jukwaa ni lenu.

      Like

      simbadeo

      August 25, 2010 at 7:32 pm

  17. Ahaaa! Sasa nimetabasamu kwa wengine kuongezeka na kuchangia. Nimefurahi nami kujua zinakopatikana mashine za kuchanganya chakula. Asante. Bado sijajibiwa, anayejua zinakopatikana za kutotolesha vifaranga zinazotumia mafuta ya taa si umeme. Asanteni.

    Like

    Jenny

    August 26, 2010 at 9:27 am

    • Da Jenny, ni kweli, hata mie kicheko mpaka jino la sikukuu linaonekana! Tanzania ina watu wengi wenye weledi mkubwa katika fani mbalimbali … tushirikishane weledi wetu kila mmoja kwa nafasi yake … kupeana taarifa ni kuzikuza taarifa hizo na kuziongezea thamani … ukibaki nazo mwenyewe hazikui … au siyo jamani. Mnisahihishe.

      Like

      simbadeo

      August 26, 2010 at 10:55 am

    • kwanza napenda nikushukuru dada jenny kwa mchango wako mkubwa katika kuelimisha jamii. nimefarijika sana na maelezo yenu wadau. kwa kweli kuna haja ya kuanzisha blogs, kwa wajasilia mali ili tumweze kujengana namna hii. kuhusiana na mashine ya kuangulia vifaranga inayotumia mafuta ya taa unaweza kupata kwa jamaa mmoja songea. samahani kwa sasa simu yake sina lakini ninakuahidi naweza kuitafuta.antengeneza mashine inayoweza kuzalisha vifaranga 100 hadi 150, kwa wastani wa bei ya 30000 hadi 500000. huyu jamaa ni malufu sana maana ameshashiriki maonyesho makubwa ya kitaifa. na kwa kweli anasaidia sana pia kutoa elimu baada ya kukuuzia mashine zake. unaweza kuwasiliana nami kwa namba 0752191920 au 0714805510. pia naomba namba yako ya simu dada jenny nahitaji sana kujifunza kutoka kwenu, pia ningefurahi kama unaweza kuniruhusu kufika shambani kwako. nawatakia wote heri ya mwaka mpya wenye baraka tele.
      manase mwakagali

      Like

      manase mwakagali

      December 29, 2010 at 11:08 am

      • Hello Kaka Manase,

        Asante kwa jibu lako. Nashukuru kwa taarifa ya mashine ya kutotolesha inayotumia mafuta ya taa. Nilishapata mtu anayezitengeneza hapa hapa Dar es Salaam na bei ni hiyo uliyotaja yaani TShs. 500,000/=, nje ya Dar ina maana niongeze gharama ya kuisafirisha na ikileta shida kumpata fundi aliyeitengeneza sio rahisi.

        Namba yangu ya simu sipendelei kuiweka hapa kwenye mtandao lakini tuendelee kuwepo hapa kwa Kaka Deo tunavyofahamiana tutaaminiana kiasi cha kutembeleana, utufahamishe nawe unafanya nini au unafuga nini na unapendelea kujifunza nini toka kwetu. Wapo ambao tumeshatembeleana kupitia hapa. Kwa hivyo inawezekana kabisa. Pengine nikuahidi kuwa baada ya sikukuu hizi kupita na pilika pilika za kulipa ada za watoto shule zitakapotulia nitakutafuta kupitia namba ulizotoa tuwasiliane.

        Karibu.

        Like

        Jenny

        December 29, 2010 at 2:11 pm

  18. Da Jenny
    Nimefurahi na elimu yako uliyojitolea kutufundisha na mimi imenigusa sana kwani nami ni mjasiriamali. Hiyo mashine ya kutotolea vifaranga inapatikana SIDO, RUVU JKT na pia kuna mtu mmoja anaitwa Shabani Singa anatengeneza hizo mashine na anaziita(Mgana Incubeta)
    au MGANA POULTRY POINT anakaa Mbezi barabara ya Tegeta A: ila tu hajaandika namba yake ya simu hiyo ndio ingerahisisha kazi.

    Like

    Da Jenny

    September 3, 2010 at 1:25 pm

    • Da Jenny
      Huyo mtu anayetengeneza hizo mashine za kutotoleshea vifaranga anapatikana mbezi ya wapi? na hiyo mashine ya 500,000 ni ya vifaranga wangapi? Nategemea kupata msaada toka kwako.

      Like

      PILLY

      September 20, 2013 at 7:03 pm

    • Msinichoke wadai nina maswali mengi.
      Ukitaka kuwa agent wa best arusha chicks ,interchick au amadori inakuwaje.
      Mnisaidie kuna mtu ananiulizia mara kwa mara nami sijawahi kuulizia katika ofisi zao inakuwaje.Anayefahamu anifahamishe

      Like

      PILLY

      September 20, 2013 at 7:07 pm

  19. Da Jenny
    Samahani badala ya kuandika jina langu nikaandika jina lako tena kwa haraka za maenedleo niliyokuwa nayo mimi ndio niliokuandikia hiyo msg ya mashine ya kutotoleshea vifaranga na zinapopatikana huko SIDO, RUVU JKT na kwa bwana Sahabani Singa wa Tegeta naomba ufuatilie utafanikiwa tu

    Like

    Fatma

    September 3, 2010 at 1:48 pm

  20. WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.
    Kuku wa Amadori

    with 32 comments

    dscf0010

    dscf0011

    Pichani ni kuku wenye uzito kati ya kilo 4 mpaka 6 wanaouzwa kwa Amadori eneo la Uwanja wa Ndege, Dar es Salaam. Bei ya kuku ni Sh. 14,000/= kwa kuku jike na 22,000/= kwa jogoo.

    Ufugaji kwa njia bora za kisasa ni moja ya njia tunazoweza kutumia Watanzania kujikwamua kutoka kwenye umaskini. Kuna somo hapo la kujifunza.

    * Share this:
    *
    * Email
    * Print
    * Facebook
    * Press This
    * Reddit
    * Digg
    * StumbleUpon
    *

    Possibly related posts: (automatically generated)

    * Why? Kwa nini? TAZARA…
    * Simba Mitaa ya Mjini / Lion in City Streets
    * Twiga Cement na Aurora … pongezi
    * Kinondoni inaongoza kwa uchafu Tanzania

    Written by simbadeo

    December 25, 2008 at 12:49 pm

    Posted in Siasa na jamii
    « Merry Christmas and Happy New Year 2009
    Ujumbe kutoka Kisarawe… »
    32 Responses

    Subscribe to comments with RSS.

    1.

    Natafuta sana taarifa mbali mbali za ufugaji wa kuku lakini kwa kiswahili sipati. Ina maana wataalamu wetu wako nyuma kiasi hiki? Yaani kutokuwa na taarifa za maana za kumfaa mkulima au mfugaji katika mtandao? Mimi ni mfugaji mdogo, lakini sasa nataka kuwa mkubwa na shamba langu ni ekari 7 nje kidogo ya Dar es Salaam. Ninao kuku wa kienyeji mchanganyiko na wa kisasa. Pia ninao kanga (Guinea fowls) wengi na vifaranga wao wengi tu. Kuku wangu na Kanga wanatembea free, isipokuwa vifaranga kwa hofu ya kuchukuliwa na ndege wajanja kama Kipanga na Kuguru. Ninao pia Nguruwe 8 ambao 1 ameshapandwa tayari.

    Sasa najiuliza wapi nitapata taarifa za ufugaji bora na jinsi ya kuanzisha shamba langu sipati majibu. Kwenye net kuna taarifa nyingi kwa kiingereza. Nilidhani za Kiswahili pia zapatikana ili hata vijana wasaidizi shambani iwe rahisi kwao kusoma na kuelewa. Nisaidieni kwa hili: Wapi nitapata msaada wa kufuga kama hao Amadori Farm?

    NB: Picha nzuri, ila wanunuzi hao wakatili sana. Shambani kwangu sitaruhusu mnunuzi au awaye yote kumbeba kuku au mnyama vibaya namna hiyo. Ninawapenda sana wanyama, wana akili sana. Immagine kumni’nginiza kuku wa kilo 4 kwa mabawa yake tu!!! Soooo Sick behaviour! Am not joking, I hate it!

    MTZ halisi.

    Jenny

    March 3, 2009 at 11:22 am
    Reply
    2.

    Mimi natafuta soko la hawa kuku ninao wengi nauza Tsh 11000 tu kwa majogoo kama kuna mtu anahitaji awasiliane nami lakini nauza kwa jumla kuanzia 300 nakuendelea

    kuku

    June 1, 2009 at 8:23 pm
    Reply
    3.

    Du kaka simba ni kweli unayosema kuwa kuku wanaweza kupatia kipato watanzania lakini kuna tatizo kubwa sana kwa wafanyabiashara wa kuku wenyewe na ambao tunawapelekea kkuku hao. Mimi nilikuwa mfugaji wa kuku hasa hawa wa kisasa lakini imefikia mpaka nimejitoa kwenye kazi hiyo kwa sababu kubwa ya kutoko kuwa na ushirikianio na wafugaji wengine. Na ushirikiano huo ninaosema siyo wa kufanya kazi pamoja bali amawazo na bei katika soko ambalo watu woote tunakimbilia kuuza hao kuku wakisha kuwa wakubwna au wa kuuza mayai. Nilikuwa najaribu kufanya kazi hii kwa utaalamu mkubwa sana wa kuweka record ya gharama ninazotumia ili nijue ni faida gani halisi naweaza kupata wa kati wa kuuza. hadi mwaka 2008 december wakatiu mimi naacha kufuga kwa mujibu wa hesabu zangu nilizo kuwa nafanya kuku mmoja bloiler wa wiki 6 toka kumnunua hadi kumuuza alikuwa anafikisha gharama ya shs 3500 hadi 3800 na kama atakaa zaidi ya hapo gharama hizo zinaongezeka kwa sababu anaendelea kula kila siku, sasa ukuienda kwa wanunuzi hiyo ndio bei wanataka kununua kuku wako sasa hapa maendeleo utapata au unafanya kazi ya watu tu bila faida yeyote. usipo waauza kuku hao siku zinapozidi in maana gharama inaongezeka, ukiacha kuuz mwenzako anakuja hapo ulipo kataa hiyo bei ambayo uaona haina maslahi yeye anauza kwa bei hiyo wako wanabaki na gharama inaongezeka. Ukimuangalia mtu huyo unaponunu a chakula cha kuku na yeye anachukua hapahapo sasa unajiuliza mtu huyu anafanya hesabu kweli au anauza kuku kwa kuangalia bei ya kununua vifaranga na bei ya kuuzia kuku tu gharama nyingine haweki kama umeme, ulizi maji mfanyakazi (watu wengine gharama za mfanyakazi huwa hawaweki kwa sababu familia ndio inafanya kazi hiyo na hakuna malipo yeyote katika nguvu hizo za familia, umeme na maji watu wengi wanasahau kanma ni gharama katika kuku hao unaowauza kwa kuw atu maji na umeme ni bili za kawaida nyumbani wanasahau kuwa hii ni biashara ili kupata faida ni lazima gharama hizo uweke na usipo weka ndio unajidanganya kuwa umepata faida kumbe ni gharama zako mwenyewe ambazo hujaziweka.
    mambo hayo yapo vile vile kwenye kwenye kuku wa mayai watu wanaacha gharama nyingi sana na kuuza mayai kwa bei ndogo hivyo wafugaji woote wa kuku Mwanza na shemu nyinginezo mfanye mikutano ya mara kwa mara kwa ajiri ya kupanga bei na wateja wenu watanunua tu kama mtakuwa na bei ya pamoja yenye maslahi

    YOMBOP from Tanzania

    August 24, 2009 at 4:56 pm
    Reply
    4.

    it’s true what my friends comments about the specialist,b’coz even I try to look such information but funny enough I did n’t find & we are saying KILIMO KWANZA how is it possible.To my point of view I think the committe did not think of it first,am n’t saying it’s a bad idea,but they should analyse things well, by putting polices that are condussive and can be implimented by the required society.

    p squire

    September 29, 2009 at 12:49 pm
    Reply
    5.

    naomba kama unawezekana nikapata contact za huyu bwana muuza kuku wa Amadori wa maeneo ya uwanja wa ndege nitafurai .

    peter

    March 19, 2010 at 3:39 pm
    Reply
    6.

    Mimi nina shamba langu la eka 3 maeneo ya bunju ninafuga mbuzi wa nyama na ng’ombe wa maziwa nataka kuanza ufugaji wa kuku wa kisasa wa nyama na mayai.sasa katika utafiti wangu nimegundua tatizo kubwa upatikanaji wa vifaranga na ubora wa vifaranga hivyo.kwa yoyote mjasilia mali mwenzangu anisaidie katika upatikanaji wa vifaranga kwa urahisi.

    seddy farm

    April 29, 2010 at 6:14 pm
    Reply
    *

    Seddy farm, umefuatilia alichotueleza Jenny? Nadhani ni jambo linalofaa kujaribu, huenda litasaidia sana, au siyo?

    simbadeo

    May 18, 2010 at 2:49 pm
    Reply
    7.

    Hello Seddy Farm,

    Vifaranga ni tatizo sugu. Lakini ili upate vifaranga bora na wazuri, huna budi kuwapata kutoka katika sehemu ambako tunapanga foleni kuwapata. Nakushauri kwa vile unaishi Bunju, uweke order pale Interchick, wana vifaranga wazuri sana na mimi huchukulia hapo. Ila tatizo ni foleni utakayoikuta, ukilipia mwezi huu vifaranga unaweza wapata baada ya mwezi mmoja na nusu ama miwili lakini kwa uhakika kwamba utawapata, na wanatoa ushauri mzuri kwa wafugaji wanaoanza kufuga.

    Kutokana na kuibiwa sana mazao ya kuku shambani na vijana niliokuwa nikiwaweka, niliamua kubadilisha ufugaji. Kwa sasa ninafuga kuku wa kisasa wa mayai, lakini nawafuga kienyeji kabisa. Wanatoa mayai mazuri sana na mimi na familia yangu tunayatumia pia, mayai yenye kiini cha njano na ladha kama mayai ya kuku wa kienyeji. Nimegundua mayai mazuri ya kuku yanatokana na namna unavyowatunza na kuwalisha. Ninao wachache ili kumudu kuwahudumia kienyeji. Nimebakiza pia kanga wachache kwa ajili ya ulinzi wa shamba na kufukuza wadudu na nyoka. Changamoto ni nyingi sana, I wish kungekuwa na mshikamano wa pamoja hata online ili tuweze kupeana uzoefu na namna ya kutatua matatizo mbali mbali yahusuyo mifugo na kilimo.

    Jenny

    May 17, 2010 at 10:16 am
    Reply
    *

    Asante Jenny, umetupa maelezo safi na yenye kutoa mwanga sana. Cheers!

    simbadeo

    May 18, 2010 at 2:50 pm
    Reply
    *

    Mimi nafuga kuku wa nyama na matatizo uliyoyasema ni ya kweli kabisa kiasi kwamba nami natatka kuanza kuku wa mayai na nimevutiwa na njia yako ya ufugaji wa mayai kwa kutumia njia za kienjeji, Jee waweza tuelimisha zaidi?.

    Nassib

    July 8, 2010 at 3:28 pm
    Reply
    o

    Ndugu Nassib

    Asante kwa maoni yako. Nimefurahi kusikia kuhusu juhudi zako. Soma vizuri maoni ya Dada Jenny kwenye post hii. Naamini kuna mengi ya kujifunza hapo. Unaweza pia kuwasiliana naye kwa maelekezo ya kina zaidi.

    Wasalaam

    Simba Deo

    simbadeo

    July 9, 2010 at 3:51 pm
    8.

    Hello,

    Hao kuku wa mayai nawanunua na kufuata utaratibu wote kama inavyotakiwa wakiwa vifaranga wadogo. Nawapa chanjo na matunzo yao yote wakingali wadogo hadi wanapokaribia kutaga ndio naanza kugeuza kidogo kidogo mwenendo wao, wanakuwa wameshakuwa resistant sana kwa magonjwa wanapokua wakubwa.

    Hawa nilionao nilianza kuwatoa nje na kuwaachia wiki chache kabla ya kuanza kutumia chakula cha kutagia. Wakizoea nje wanafurahia sana hawataki hata kurudishwa ndani, inakuwa taabu kuwarudisha hadi muwe 2 au 3 muwazingire huku na huku kuwaelekeza mlangoni. Kwa vile nafugia shambani, eneo ni kubwa na hivyo wako huru japokuwa watu wa shambani huwatoa wakati wanapokuwa na hakika ya wao kuwepo macho kuangalia na kuwafuatilia. Pia huwatoa nje wakishataga wengi hasa muda wa mchana.

    Ni vizuri ukianza kuwaachia nje pia kujifunza kuchanganya chakula chao mwenyewe. Kuna wateja wengine hawapendi baadhi ya vitu vinavyowekwa kwenye vyakula vya kuku mfano damu, hivyo ukiweza kuchanganya chakula mwenyewe inakuwa vizuri zaidi. Nawapatia pia treats ya dagaa wanapokuwa nje, wanapenda sana ila sio mara kwa mara na kwa wingi maana la sivyo hata mayai yatanuka samaki. Kuna aina ya majani laini wanapendelea sana kula, ukiyafahamu wakati wa mvua yako mengi unawapa wanapokuwa hawajatoka nje.

    Mayai yao hayana tofauti kabisa na yale ya kuku wa kienyeji. Japo ninao wachache, najitahidi kuwafuga kwa njia hiyo na mayai yangu yanapendwa sana na watu walioyatumia. Nauza tray TShs. 7,000/= badala ya bei ya kawaida kati ya TShs. 5,000/= hadi 5,500/= ambayo niliona hailipi.

    Natarajia kuongeza wengine, lakini nitakaposhindwa kuwafuga wote kwa njia hii kwa kuwa wengi, nadhani bado nitatenga kundi fulani kwa ajili ya mayai hayo ninayotoa sasa au kuwapatia zamu za kufurahia maisha ya nje ambako wanakula majani na vidudu mbali mbali.

    Nadhani hadi hapo nimesaidia ya kutosha.

    NB: Ninapotaka kupata mbegu mchanganyiko pia huwa natenga majike kadhaa na majogoo wa kienyeji kabisa, wakiwapanda yanapatikana mayai yenye mbegu ambayo nawapatia kuku wa kienyeji kuatamia. Bado sijaweza kununua mashine ya kutotoleshea. Katika kuku wa aina hii pia nimewahi kupata majike wanaotaga tu kama hao wa kisasa, hawajui kuatamia, wanataga tu mfululizo hadi wanaposimama kupumzika wenyewe na ni wakubwa.

    Kuna uzoefu mwingi endapo tutasaidiana, mimi najua hiki na wewe unafahamu kile, tukiunganisha tunasaidiana kufika mbali. Siku njema.

    Jenny

    July 12, 2010 at 2:53 pm
    Reply
    9.

    Pia, nje wanapata nafasi nzuri ya kuota jua na kuoga mchanga. Unawafaa sana mchanga kwa ngozi. Kwao inaitwa “Sand Bath”. Ni maisha ambayo mnyama angetakiwa apate lakini watu tunasahau hilo na kuangalia faida tu. Mayai bora yanatokana na namna kuku wanavyotunzwa vizuri na chakula wanachokula. Nafasi kati ya kuku na kuku ni kubwa sana, wako huru sana bandani kwao maana banda ni kubwa. Linatosha kuongeza wengine 50 hivi na bado wakawa na nafasi nzuri ya kutosha kwa hivyo ukiwapa raha, wanyama nao watakupatia raha, wana hisia na akili pia japo sifahamu kwa kiwango gani kutofautisha na binadamu.

    Jenny

    July 12, 2010 at 4:34 pm
    Reply
    *

    Asante sana Da Jenny kwa darasa zuri. Naamini wafuatiliaji wa post hii juu ya ufugaji wa kuku kwa njia zenye tija wamenufaika sana. Mie pia napata hamu ya kuanza biashara hii. Fursa ikipatikana Da Jenny unikaribishe shambani kwako nipate kujifunza zaidi. Shukrani. Tuendelee kuchangia.

    simbadeo

    July 14, 2010 at 11:18 am
    Reply
    10.

    Nashukuru kwa daras ulilototoa dada jenny. Suala jingine ni kuhsus soko kwa mayai napata wasiwasi kuanza biashara ya kuku wa mayai nikiwa sioni soko la uhakika kwani nikiona waendesha baisikeli wakiwa na mayai hata mchana hivyo kunipa picha kwamba soko ni gumu; wengine wanasema kwamba watu hufuata mayai nyumbani kwa wafugaji hiyo ni vizuri lakini una mayai yako kila siku unaHANGAIKA madukani kupeleka mayai inanipa wasiwasi kuanza biashara hii. Naomba unipe shule ya soko la mayai. Ahsante

    Nassib

    July 15, 2010 at 9:35 am
    Reply
    11.

    Soko la mayai kusema UKWELI ni ujanja na bidii zako mwenyewe katika kulitafuta. Nadhani kwa swali lako nimeelewa kwamba unapungukiwa -ujanja (ambao unaweza kuwa ni wa kuzaliwa nao), -ujuzi (ambao inabidi upitie mafunzo fulani kuupata) wa namna ya kutafuta wateja kwa bidhaa zako. Kuna Maduka Makubwa, Supermarkets, Hoteli, Masoko, Mashule, Hospitali, Vyuo, Magereza, Majeshi, Wenye baiskeli wanaonunua kwako nao wakauze, maduka madogo, watu binafsi, wakaanga chips na kadhalika. Unataka kuuza ukiwa umekaa nyumbani bila kutoka wateja wafuate kwako hilo ni uamuzi wako kutegemea na UJANJA/UJUZI wa namna ya KUSHAWISHI wateja waweze kukufuata badala ya kukaa wakisubiri kupelekewa. Utakuwa kwenye mashindano na wale wanaopeleka huduma kwa mteja badala ya mteja kufuata huduma. Kwa maana hiyo nadhani unahitaji kupata UJUZI wa namna ya kutafuta masoko, kama UJANJA huna maana tunatofautiana talanta. Kozi fupi na ndefu za Ujasiriamali zipo na kwa bei nafuu, nyingine zina sponsorship kabisa na zinatolewa kwa watu wa kawaida tu kama sisi na nimeshuhudia hilo, Chuo Kikuu – UDSM – UDBS wanatoa kozi hizo, nadhani na taasisi zingine za elimu pia.

    Jenny

    July 15, 2010 at 1:13 pm
    Reply
    *

    dada jenny nakushukuru sana

    Nassib

    July 15, 2010 at 2:00 pm
    Reply
    *

    Dada Jenny nimefarijika sana. Nimejifunza jambo kubwa kuhusu uanzishaji miradi. Nalo ni kwamba … haitoshi tu kuanzisha mradi … bali lazima kuhakikisha kwamba mradi huo unakuwa endelevu … na unapata uendelevu huo kwa kutafuta masoko … na kwamba kazi ya kutafuta masoko hiiishii kuwa na product tu. Lazima kutumia mbinu za kijasiriamali ili kuhakikisha kwamba bidhaa ulizo nazo zinauzika.

    Ndugu Nassib na wengine tunaofuatilia mjadala huu natumaini tumepata elimu kubwa. Sasa pengine ni wakati wengine nao watushirikishe maarifa waliyo nayo. Kila mmoja anakaribishwa – inaweza hata kwa kuuliza maswali. Tunaweza kujiletea mabadiliko chanya katika jamii yetu – tunaweza.

    simbadeo

    July 16, 2010 at 10:33 am
    Reply
    12.

    Hello Kaka Simba
    Naona watu hawachangii. Mimi nitaendelea tu maana nahitaji msaada bado wa vitu vingi. Leo nauliza wapi naweza kununua mashine ya kutotolesha vifaranga inayotumia mafuta ya taa? Asante

    Jenny

    July 27, 2010 at 12:49 pm
    Reply
    *

    Hi Jenny, asante kwa kutupa changamoto hiyo. Ni kweli … watu hupita hapa na kusoma na kuondoka kimyakimya bila kuacha alama za kuonekana sana. Lakini hiyo isikukatishe tamaa kwani ujue kwamba watu wengi wananufaika na maelekezo ambayo wewe huwapa kupitia uwanja huu.

    Nafikiri wasomaji watakuwa wamepata swali ulilotutupia leo. Jamani, mwenye kufahamu wapi mashine hiyo inauzwa tafadhali atushirikishe. Au kama wewe ni mwuzaji wa mashine aina hiyo, tayari hapa una mteja mmoja na si ajabu wengi zaidi wakaibuka.

    Tupo pamoja!

    simbadeo

    July 27, 2010 at 1:42 pm
    Reply
    13.

    Nawashukuruni sana kwa elimu hii. Mimi nina swali, tafadhali naomba anayejua mchanganyiko unaotakiwa kwa vyakula vya kuku wa mayai anisaidie. Kwa mfano kama unataka kutengeneza kilo mia za starter, growers na layers unatakiwa kuweka kiasi gani cha mahindi, mashudu, soya beans nakadhalika?. Ahsanteni

    Elizabeth

    August 12, 2010 at 10:00 am
    Reply
    *

    Da Eliza

    Asante sana kwa swali lako. Naamini Da Jenny atatumwagia somo zaidi hapa … na wengine wote wenye maarifa haya … msisite kutupatia. Tuendelee kuwepo.

    simbadeo

    August 12, 2010 at 11:44 am
    Reply
    14.

    Mhhh kaka Deo, watu wanamsubiri dada Jenny tu wao hawachangii chochote jamani? Hata mimi nahitaji msaada tupeane maarifa.

    Kuhusu kuchanganya chakula, nakushauri dada Eliza uwaone madaktari wa wanyama wao watakupatia mchanganuo mzuri zaidi kulingana na mahitaji yako na aina ya kuku unaotaka kufuga. Mimi kwa mfano wateja wangu fulani kwa sababu za maadili yao ya dini, hawataki kutumia mayai ama nyama ambayo kuku wake walipewa vyakula vilivyochanganywa na vitu fulani mfano damu. Kwa hiyo uchanganyaji wa chakula unaomfaa mnyama, ni vizuri kuwaona madaktari wa wanyama. Sifahamu unaishi wapi, lakini mimi ninawafahamu baadhi ambao ni wazuri sana na wanapatikana katika maduka ambako kunauzwa pia madawa ya mifugo, na ambako huduma za wanyama zinapatikana. Usiwaone tu wauzaji wa hicho chakula, waone madaktari watakupa vipimo kamili kulingana na mahitaji na aina ya wanyama wako.

    Jenny

    August 13, 2010 at 8:23 am
    Reply
    *

    Da Jenny,

    Asante sana kwa mchango wako. Ni mkubwa mno. Kiufupi unatupa changamoto sote tunaofuatilia darasa hili la mtandaoni kwamba ni muhimu kufanya utafiti. Na ili tupate matokeo mazuri kutokana na utafiti tunaofanya ni vema tulenge kupata wataalamu haswa wa hicho tunachokitafiti. Natumaini Da Eliza umemwelewa vema Da Jenny. Kwa mara nyingine tena ametufungua macho. Asante sana Da Jenny. Na, jamani, tusisahau changamoto nyingine aliyotupa – nasi wengine tushirikishe wengine yale tunayojua – tusikae kimyaa – kama unajua mawili matatu basi yamwage hapa. Tuendelee kuwepo!

    simbadeo

    August 13, 2010 at 10:22 am
    Reply
    15.

    du namfurahia sana dajenny kwani ananigusa mi nafuga wa nyama wa kanga na wamayai ila bado sijawa mtaalamu sana ila ninaomba kama kuna mtu anafahamu sehemu napoweza kupata mashine ya kusaga chakula cha kuku ahsante

    damariam

    August 20, 2010 at 6:22 pm
    Reply
    *

    Da Mariam, karibu kijiweni. Nimefurahi kusikia kwamba unafuatilia mjadala na huwa unakusaidia katika kukuza maarifa yako katika shughuli zako za ufugaji. Haya jamani, Da Mariam anaomba kufahamishwa juu ya mashine hiyo … anayejua jamani atuelekeze na wengine.

    Tuendelee kuwepo.

    simbadeo

    August 21, 2010 at 12:42 pm
    Reply
    16.

    Mashine za kusaga na kuchanganya chakula cha kuku zinapatikana SIDO. Unachotakiwa kufanya ni kupiga simu Dar es Salaam (ya offisini) ukaomba kuongea na manager wa karakana. Mweleze unachokitaka atakupa ushauri. Hata kwenye maonyesho ya Nane Nane walikuwa nazo.

    Elizabeth

    August 25, 2010 at 4:18 pm
    Reply
    *

    Da Eliza, asante sana kwa maelekezo haya. Naamini Da Mariam na wengine waliokuwa na mahitaji hayo sasa wamepata mwanga wapi kwa kwenda. Nadhani umefika wakati sasa SIDO kufanya matangazo zaidi ya bidhaa zao – kweli kutumia maonyesho ya Nane Nane na mengine kama hayo kuna nafasi yake, lakini pia kutangaza magazetini, kwenye blogu, kwenye redio na TV kwa wingi zaidi kutasaidia. Tuendelee kupeana maarifa. Jukwaa ni lenu.

    simbadeo

    August 25, 2010 at 7:32 pm
    Reply
    17.

    Ahaaa! Sasa nimetabasamu kwa wengine kuongezeka na kuchangia. Nimefurahi nami kujua zinakopatikana mashine za kuchanganya chakula. Asante. Bado sijajibiwa, anayejua zinakopatikana za kutotolesha vifaranga zinazotumia mafuta ya taa si umeme. Asanteni.

    Jenny

    August 26, 2010 at 9:27 am
    Reply
    *

    Da Jenny, ni kweli, hata mie kicheko mpaka jino la sikukuu linaonekana! Tanzania ina watu wengi wenye weledi mkubwa katika fani mbalimbali … tushirikishane weledi wetu kila mmoja kwa nafasi yake … kupeana taarifa ni kuzikuza taarifa hizo na kuziongezea thamani … ukibaki nazo mwenyewe hazikui … au siyo jamani. Mnisahihishe.

    simbadeo

    August 26, 2010 at 10:55 am
    Reply
    18.

    Da Jenny
    Nimefurahi na elimu yako uliyojitolea kutufundisha na mimi imenigusa sana kwani nami ni mjasiriamali. Hiyo mashine ya kutotolea vifaranga inapatikana SIDO, RUVU JKT na pia kuna mtu mmoja anaitwa Shabani Singa anatengeneza hizo mashine na anaziita(Mgana Incubeta)
    au MGANA POULTRY POINT anakaa Mbezi barabara ya Tegeta A: ila tu hajaandika namba yake ya simu hiyo ndio ingerahisisha kazi.

    Like

    Fatma

    September 3, 2010 at 1:56 pm

  21. Asante sana …. kwa jibu lako. Nakushukuru. Hizo za Mgana nilishazisearch online, lakini bahati mbaya ni kwamba hajaweka jinsi ya kumpata huyo mtu ama contacts zake. Lakini hata maelezo yako yanatoa mwanga wa mimi kumtafuta. Pia nitaanzia na za SIDO. Nashukuru kwa ufumbuzi.

    Like

    Jenny

    September 3, 2010 at 2:34 pm

    • Maendeleo mazuri. Tuendelee kupeana taarifa na kubadilishana uzoefu. Maendeleo hayaji bila kushikamana. Karibuni tuchangie zaidi.

      Like

      simbadeo

      September 4, 2010 at 4:20 pm

  22. Sasa hiyo Mgana Incubeta nichacharika na kuzipata contact zake huyo bwana kwa Da Jenny unaweza kuwasiliana nae kwa Mobile hizi: 0717-621777,0754-502805, 0718-203221.
    Nakutakia kila kheri.

    Like

    Fatma

    September 6, 2010 at 7:47 am

    • Fatma, asante sana kwa kazi nzuri uliyofanya. Haya, wadau, kazi kwetu. Tunaweza kuwasiliana na Mgana kwa ajili ya incubeta hizo. Tuendelee kupeana mbinu na kubadilishana taarifa muhimu kama hizi. Asante.

      Like

      simbadeo

      September 6, 2010 at 10:02 am

  23. Da Fatma asante sana. Msinichoke, leo tena nauliza contacts za watu wanaochimba visima virefu na kama kuna yeyote anayefahamu utaratibu wa kufuata ama gharama zao, nahitaji kuchimba kisima kirefu shambani. Asanteni sana.

    Like

    Jenny

    September 6, 2010 at 10:04 am

  24. Da Jenny wala hatutakuchoka kwani haya yote maendeleo, ila naomba unifahamishe unakaa wapi kuna mtu mmoja namfahamu yeye anachimba visima virefu. Naweze kumwambia na pia kukupa contacts zake ili uweze kuwasiliana naye.

    Like

    Fatma

    September 6, 2010 at 1:45 pm

  25. Da Fatma, naishi Mbezi Beach, shamba liko Madala. Yaani nafurahia sana hii site tungeongezeka, maana badala ya kunipa contacts za mtu kwa kitu fulani, siku nyingine unaweza kukuta ni wewe unayetoa huduma hiyo na wateja ukawapata hapa hapa. Asante.

    Like

    Jenny

    September 6, 2010 at 2:58 pm

  26. Da Jenny nashukuru kwa kinifahamisha unapokaa, kwa hiyo subiri kidogo niwasiliana na huyu bwana nikimpata kwenye simu yake nitamueleza kisha nitakurushia namba yake. Mimi naomba nikurudishe nyuma kidogo kwani umesema kuku wako wa mayai unawaachia nje wapandwe na majogoo, sasa mimi nina kuku wa mayai 200 wanataga hivi sasa lakini ningependa na mimi niwatenge baadhi yao sasa sijui niwatenge wangapi na pia niwaweke na majogoo wangapi ili niweze kupata mayai ya kienyeji eneo langu sio kubwa sana kama lako ila nina uzio hivyo hawatoki nje naomba unielekeze tafadhali.

    Like

    Fatma

    September 7, 2010 at 8:37 am

  27. Da Jenny naomba tusichokana, ukisikia hizo semina zinaendeshwa naomba unijulishe na mimi ili niweze kwenda kupata ujuzi zaidi kama ulisema mimi nikijua hivi na wewe unajua vingine tukuchanganya pamoja naamini tutafika mbali kimaendeleo na iko siku tutatoka tu kwa baraka za Mwenyezi Mungu. Kwa mawasiliana zaidi Namba yangu ya Mobile ni 0715-025723
    Nawaomba na kaka zangu pia muendelee kutupanua mawazo zaidi ya kufuga au kilimo hata na vitu vingine zaidi, ka Nassib na ka Simbadeo.

    Like

    Fatma

    September 7, 2010 at 9:03 am

  28. Hello Fatma, Asante kwa maelezo. Kuku wangu nawaachia nje ila sina majogoo wengi kuwatosha wote. Kwa hivyo, ninapohitaji mayai ya kutotolesha – (kumbuka natotolesha kwa kutumia kuku wa kienyeji, sijanunua mashine) kama post yangu ya juu ya July 9 inavyoeleza mwishoni. Kuku wangu nawaachia ili kupata mayai yenye quality sawa na kuku wa kienyeji. Hiyo ndiyo sababu yangu kuu ya kuwapa uhuru wa nje, pia nawapenda wanyama, nahisi ni ukatili sana kuwaweka kwenye banda masaa 24 miaka yote watakayotaga wasijue jua wala kukunjua mabawa wala kuoga mchanga.

    Ninapohitaji kupata mayai yaliyorutubishwa na jogoo, huwa natenga baaddhi kwa kuwawekea alama miguuni ili niwatambue na kuwaachia nje pamoja na majogoo muda wote hadi nitakapoona sihitaji tena kutotolesha. Nawawekea alama miguuni kwa sababu wenzao wanapoachiwa nje wanachanganyika na kama hawana alama huwezi kuwatambua na mara nyingine uliowatenga wanaweza kuingia bandani na wenzao, ila asubuhi nawatoa ili watage sehemu ambayo ni maalum kwa sisi kuokota mayai yao yaliyorutubishwa. Kwa hiyo hao wanaokuwa nje pamoja na majogoo, mayai yao tunayakusanya kwa sababu hata kutaga watataga eneo tofauti na wale wengine. Hao wengine kama nilivyoeleza kwenye hiyo post ya mwanzoni, huwa nawafungulia wakati ambapo tuna uhakika wengi wao wamekwishataga. Hao pia wanakutana na majogoo nje ila kwa kuwa ni wengi na jogoo ni wachache, huwezi kutambua yupi amepandwa, ndio maana kwa kupata uhakika huwa nachagua baadhi tu kwa kazi ya kurutubisha.

    Nakushauri pia kutafuta jogoo wa kienyeji kabisa, sio wale ambao ni mchanganyiko ili kupata mbegu nzuri kwa sababu mchanganyiko na kisasa kidogo haileti matokeo mazuri sana kwenye kutotolesha/vifaranga. Kinyume chake ni kwamba, jogoo mchanganyiko anafaa zaidi kwa majike wa kienyeji. Jogoo 1 wa kienyeji huwa namhesabia majike 4 hadi 5 kwa hivyo kama ninao jogoo 5 nitaweka kuku 20 nje wa mayai pamoja nao. Kwa jogoo mchanganyiko wanapanda majike wengi zaidi, hata 10 kwa jogoo mmoja hivyo inategemea una majogoo wa aina gani.

    ** Pia nikisikia kozi za ujasiriamali zinakaribia kuanza nitakuarifu au ukihitaji mawasiliano na taasisi husika pia nitakupatia. Zipo fupi za miezi 4 muda wa jioni (nzuri zaidi kwa kuanzia) na ndefu ya mwaka mmoja. Hiyo ya mwaka 1 ina sponsorship ila wanapata zaidi watu wasioajiriwa, watu waliojiajiri kwenye miradi yao. Tutawasiliana na asante kwa namba yako.

    Kwa ufafanuzi zaidi waweza kusoma maelezo yafuatayo: (Mimi hupenda pia kufanya utafiti kwenye net kupata maarifa mbali mbali kuhusu wanyama) –
    1. Pen mating
    In this type of mating, ten hens are kept in a breeding pen and one cock is permitted to mate and live with them freely. Eggs collected, a week after letting in the cock, will normally be fertile.

    2. Flock mating
    Here a large flock of hens is kept with a number of cocks in the proportion of one cock for every ten hens. But under confined conditions, the males develop a tendency to fight each other and generally one male becomes the aggressor preventing the others from mating. This may affect the fertility seriously. The eggs also cannot be traced to the cock concerned and so pedigree breeding is not possible. On the other hand, on a free range, there will not be much scope for fighting and the birds are free to run about. Flock mating is preferred where ordinary farm conditions are prevalent and no pedigree breeding is undertaken. It also permits housing for a large number of fowls as one unit and thereby reduces the overhead costs.

    3. Stud mating
    Stud mating consists of keeping the cocks and hen in separate pens or confining the males in separate coops in the pen of the females. The hens are let into the male’s pen one by one at intervals, and after mating they are removed to their own pen.

    4. Alternate males
    In this method two males are used for mating, but only one is allowed to serve the hens at a time for one full day, while the other is confined to the coop. The following day the male that had been employed is removed to the coop, and the second one is let in with the flock. In this method, too, the paternity of the off-spring cannot be determined.

    Like

    Jenny

    September 7, 2010 at 9:45 am

    • hellow jane and fatma. ne wapenda kwa mahojiano ya kitaalam. na mmenisaidia kuandika business plan yangu hapa chuo…. udsm,,

      Like

      israel ezekia

      December 26, 2012 at 9:40 pm

      • Ndugu Israel. Karibu sana. Tumefurahi jinsi ulivyofaidika na jukwaa hili na yale yanayoungana na hili katika uwanja huu. Tafadhali washirikishe na wengine ili nao pia waweze kujikomboa … kielimu na kiujasiriamali.

        Like

        simbadeo

        December 28, 2012 at 11:27 pm

  29. Hello Da Fatma, jogoo hasababishi mayai kuwa kama ya kienyeji, ni namna kuku anavyotunzwa na chakula anachokula. Ubora wa yai lenye mbegu na ambalo halina mbegu ni ule ule. Jogoo ana kazi moja tu, Kurutubisha. Kwa hivyo kama utapenda kupata mayai hayo ambayo ni mazuri, haijalishi kama kuku watapandwa ama la, cha msingi ni chakula wanachokula, na vitu vingine mfano nafasi na mwanga n.k. Nadhani nimefafanua vema.

    Like

    Jenny

    September 7, 2010 at 10:05 am

  30. Da Jenny
    Kwa kweli kama nisipo sema asante na kutoa shukrani zangu za dhati kwako basi nitakuwa mwizi wa madhila. Umenieleza kwa kina na mimi kama ni mwanafunzi basi hapo sikuachii hata maksi moja ujue nitachukua mia kwa mia jinsi nilvyoelewa. Mimi naona nianzie na kozi fupi kwanza zikiwa tayari naomba uniambie tu dada yangu hata na hizo taasisi pia itakuwa vizuri nikizijua ili niweze kufuatilia baada ya kumaliza kozi fupi nitajaribu na hizo ndefu nitashukuru ukinijulisha taasisi za kozi ndefu. Nashukuru sana sana. Tukiwepo watu wengi kama sisi tutaleta maendeleo haraka sanaa.

    Like

    Fatma

    September 7, 2010 at 12:29 pm

  31. Naomba kuuliza kama kuna mtu anaejua fomular ambayo wanatumia Amadori kuwalisha kuku wao anitumie na mimi ili niweze kuwapa kuku wangu kwani kuku wao ni wazuri na wakubwa mpaka wanatamanisha kuwaangalia.

    Like

    Fatma

    September 7, 2010 at 2:28 pm

    • Fatma na Jenny nimefurahi kusoma maelezo yenu kuhusu ufugaji wa kuku… ni mada nzuri.. mimi nataka kufuga pia… nina kiwanja hapo bunju kimepimwa. kwa hiyo wakati sijajenga nataka kuanza ufugaji
      dada Fatma kwa kuwa nimeona namba yako nitakutafuta ili tubadilishane mawazo. aidha Jenny kwa kuweli nashukuru sana kwa somo ulilotoa
      naomba nitawasumbua ili niweze kupata maelezo zaidi ya jinsi ya kuanza,…. ahsante sana,,,,,,,
      maelezo mengine juu ya ufuagaji wa kuku unaweza kuyapata
      http://mitiki.blogspot.com/2009/10/kuku-wa-kienyeji-ufugaji-bora.html
      Ngemera

      Like

      mwemezi

      September 7, 2010 at 4:59 pm

    • Fatma na Jenny nimefurahi kusoma maelezo yenu kuhusu ufugaji wa kuku… ni mada nzuri.. mimi nataka kufuga pia… nina kiwanja hapo bunju kimepimwa. kwa hiyo wakati sijajenga nataka kuanza ufugaji
      dada Fatma kwa kuwa nimeona namba yako nitakutafuta ili tubadilishane mawazo. aidha Jenny kwa kuweli nashukuru sana kwa somo ulilotoa
      naomba nitawasumbua ili niweze kupata maelezo zaidi ya jinsi ya kuanza,…. ahsante sana,,,,,,,
      maelezo mengine juu ya ufuagaji wa kuku unaweza kuyapata
      http://mitiki.blogspot.com/2009/10/kuku-wa-kienyeji-ufugaji-bora.html

      Like

      mwemezi

      September 7, 2010 at 4:59 pm

  32. Hello Mwemezi, karibu sana tusaidiane. Usione shida kutuuliza, kama unavyoona kwenye post zetu sisi pia tunauliza. Hakuna anayejua kila kitu. Karibu.

    Like

    Jenny

    September 8, 2010 at 9:02 am

    • Jenny,
      kama nilivyoainisha hapo juu, nimepata kiwanja cha Sq. meter 1700 (yaani ni kama 50mx35m). na kwa kuwa sitakuwa na uwezo wa kuanza ujenzi kwa sasa wa nyumba nimeona labda nitumie opportunity hiyo kufuga kuku. aidha kiwanja chenye kipo barabarani kabisa njiani kabisa barabara ya kwenda bagamoyo maeneo ya bunju…
      sasa kwa ukubwa huo je ni aina gani ya kuku wanaweza kufugiwa hapo wa kienyeji, wa mayai au wa nyama?

      Like

      mwemezi

      September 8, 2010 at 9:37 am

      • Ama kwa hakika nimefurahia sana maarifa yaliyomiminwa humu jukwaani. Japo mie si mfugaji lakini ni mtu ninayependa kujielimisha kuhusu masuala mbalimbali yanayolenga kuikwamua jamii kiuchumi – kuwapa watu uhuru wa kiuchumi – bila shaka kwa kuanzia na hili hata uhuru wa maeneo mengine pia utafuata – kijamii – kisiasa n.k. Tuendelee kuelimishana namna hii. Pengine tunaweza kupanga siku moja tufanye ziara ya mafunzo – kwa mfano wale walio na nia ya kujifunza zaidi na kwa kuona tunaweza kujiorganise na kutembelea shambani kwa Da Jenny – hili ni wazo tu na bila shaka kukutana kwa watu wenye nia moja kwa pamoja kutakuwa na tija kwa kila atakayejitokeza, au siyo jamani? Ni pendekezo tu hili. Tuendelee kuwepo.

        Like

        simbadeo

        September 8, 2010 at 10:01 am

  33. Hello Mwemezi, aina ya kuku wa kufuga eneo lako ambalo liko barabarani inategemea na vitu vingi na pia utashi wako binafsi. Mimi napendelea sana ufugaji wa kuku wa kienyeji au mchanganyiko wa kienyeji na kisasa kuliko kisasa tupu. Zipo sababu mbali mbali. Kwa eneo lako ningelipenda kuuliza maswali kidogo ili tukushauri pamoja na wengine.
    1. Shamba liko eneo ambako kuna usalama wa kutoibiwa mifugo? Mfano, endapo utafuga kuku wa kienyeji ambao inabidi uwaachie nje muda mwingi. Usalama ni pamoja na watu au majirani wanaokuzunguka, wezi wanaoiba bandani, wanyama wakali n.k.
    2. Unaweza kuweka au umeweka uzio kulizunguka? Uzio ni kitu muhimu sana kwa ufugaji kuepuka kero za aina mbali mbali mfano wizi, kesi na majirani, wanyama walao kuku n.k. (japo mimi binafsi sijaweka uzio, inanisumbua sana pia).
    3. Uandae bajeti ya mabanda kulingana na idadi ya kuku unaotaka kufuga. Mabanda ni pamoja na sehemu ya kuishi mtu ama watu watakaokusaidia kufanya kazi hiyo. Kuna mabanda aina mbali mbali, kulingana na uwezo but ujiandae kwa bajeti nzuri ili kujenga mabanda mazuri na imara, hata kama ni hatua kwa hatua taratibu.
    4. Majirani zako ni watu wanaokubali kuwa karibu na mifugo? Ujiandae kuangalia namna ya kuondoa uchafu wao na kuupeleka sehemu ambako hautasumbua watu wanaokuzunguka.

    Kutokana na maswali hayo, aina ya kuku utakaofuga ni utashi wako kulingana na soko lako unavyoliandaa na faida unayoiona. Kama shamba lina uzio, ni rahisi kufuga kuku hata wa kienyeji wengi tu. Kama halina uzio, kuku wa mayai na wa nyama ni rahisi zaidi kwa kuwa wao wanafungiwa zaidi, labda kama utapenda kuwapa uhuru wa nje.

    Natumaini wengine pia watachangia kukujibu swali lako.

    Like

    Jenny

    September 8, 2010 at 11:03 am

    • Habari za kazi dada Jeni.
      Nime furahia sana na somo lako.
      Mimi niko ulaya lakini nimesha choka na maisha ya ulaya. Nataka kurudu nyumbani angalau nikae huko kwa muda. Nimejaribu kufikiria kufanya biashara za aina tofauti lakini naona cha muhimu ni intrest ya mtu. Intrest yangu na shamba na mifugo.
      Miaka miwili iliyopita nilikuja huko TZ nikaenda kwa bwana mmoja anaye fuga kuku wa mayai, anao kama kuku 9000 hivi lakini wana kaa ndani tu, na si rahisi kuingia kwake mpaka upitie kwenye dawa. tuliongea sana na akanishauri sana nianze nami kufuga hawa kuku lakini nilipo kuja kufanya utafiti kwa watu wengine nikapata story nyingi tu. Ni kwamba ni rahisi kupata hasara kubwa kama wataingiliwa ma magonjwa. hapo nika back up kidogo,

      Leo niliposoma soma lako hapa nikafurahi sana na ikaniamsha kidogo. Ningependa nifahamu step by step jinsi ulivyo wafuga hawa kuku wako mpaka ukawaoesha kutoka nje. Nina shamba la hekari 15 na nategemea kununua hekari 50 au 100 ambako lanbda nitafuga na ngombe pia wa maziwa.

      Tusema hawa vifaranga unawatunza kama kawaida, ndani ya mabanda mpaka wanapo kua? Na kutumia njia zote za kufuga kuku wa mayai?
      Na je unapo wazoesha kutoka nje, inakuaje na magonjwa?

      Maana naona kazi kubwa itakua kuja kuwazoeesha kutoka nje na wasipate magonjwa.

      Thanx in advance

      Like

      boras22

      April 21, 2012 at 12:50 pm

  34. Kaka Deo, asante kwa ushauri. Wazo lako ni zuri. Tuendelee kuwepo ili tunavyoendelea kufahamiana na kuongezeka tupate muda wa kutembeleana na kujifunza kwa vitendo. Asante.

    Like

    Jenny

    September 8, 2010 at 11:07 am

  35. Aunt Mwemezi nashukuru sana kwa kujiunga nasi kwani ndivyo mtandao wetu utakavyo kuwa kwa kasi sana. Kwani unajua ujuzi ni kama mwenge unatakiwa kupokezana wewe unatufundisha unachokijua na sisi tutakufundisha tunachokijua na ndivyo tutakavyo jikwamua. Kwa hiyo aunt karibu sana kwenye ukumbi huu wa maendeleo

    Like

    Fatma

    September 8, 2010 at 2:54 pm

  36. Kaka Simba mimi naungana na wewe hundrend pacent wazo ulilolitoa ni zuri mno kwani ukitaka kujifunza unatakiwa utembelee kwa wenzako na pia unatakiwa uwe na wivu wa maendeleo hapo ndio utasonga mbele. Kwangu mimi binafsi niko tayari kwenda kwa Dada Jenny ili nikajifunze zaidi na wakati mwingine nitawakaribisha kwangu ili mje mnifundishe mengi zaidi kwani mimi bado mchanga sana katika hii fani.

    Like

    Fatma

    September 8, 2010 at 2:58 pm

  37. Dada Jenny, ahsante kwa ushauri wako.. kwa ufupi… sehemu niliyoeleza hapo juu ni kiwanja kilichopimwa na ndo kwanza nimekinunua… mawazo yako ni mazuri… mimi ninachopanga kufanya ni kukizungushia kwa ukuta ili nniweze kufanya vitu/ufugaji ndani…

    kwa kweli naonelea nifuge kuku wa kienyeji na wale wa mayai..

    Fatma, mimi siyo dada ni KAKA. ila nataka kushirikiana na mke wangu katika ufugaji..

    nakubaliana na pendekezo la Simbadeo la kuweza kukutana na kubadilishana mawazo… naamini hiyo inasaidia sana katika kupeana mawazo zaidi.. Je mnaonaje tukipanga kuonana. Hata tukikutana SIMBADEO, JENNY, FATMA, MIMI NA WENGINEO itakuwa si mbaya. Tupange.
    ahsanteni

    Like

    mwemezi

    September 11, 2010 at 6:21 pm

  38. Samahani sana KAKA Mwemezi kwa kukugeuza jinsi naomba uniwie radhi kaka yangu.

    Like

    Fatma

    September 13, 2010 at 4:33 pm

    • FAthma,
      haina neno!! Hivi unafugia wapi wewe

      Like

      mwemezi

      September 14, 2010 at 2:50 pm

  39. Mimi nakaa Ukonga na nafugia hukuhuku Ukonga

    Like

    Fatma

    September 15, 2010 at 9:41 am

  40. Ndugu Jenny,
    Moja ya makampuni ya uchimbaji wa visima ni Mamlaka iliyopo Wizara ya Maji. Search kwenye mtandao upate contacts zao uongee nao wako pale Ubungo Maji watakupa maelezo zaidi ya uchimabaji wa visima. Pia nakupongeza kwa kuchukua muda wako kuwaelimisha jamii kuhusu ufugaji kwani wengi wa wafugaji wanakuwa na ubinafsi akijua kitu hataki kumfundisha mwezake kuhofia kwamba atafaidika na kuneemeka. ila wewe u tofauti Mungu akubariki

    Like

    Nassib

    September 30, 2010 at 12:36 pm

  41. Hello people, mpo??

    Like

    Jenny

    October 4, 2010 at 2:16 pm

  42. Jenny mimi nipo ila majukumu yamenibana tu ila kama unataka bado unaitaka ile mashine ya kutotolea naomba tuwasiliane nipigie simu ili nikuelekeze mahali ukanunue kwani zipo nyingi na ni za mafuta ya taa.

    Like

    Fatma Maundi

    October 6, 2010 at 7:27 am

    • Habari dada Fatma.
      na mimi ningependa kujua mahali panapouzwa hizo incubators na bei zake na idadi ya mayai inayoweza kuangulia. Kwa hapa sweden zipi za aina nyingi lakini all they use electricty na unafahamu matatizo ya umeme hapo kwetu labda kutumia solar energy.

      Like

      boras22

      April 21, 2012 at 2:24 pm

  43. Jamani mbona mmekuwa kimya hivyo wajasiriamali wenzangu hamna changamoto yoyote au elimu yoyote ya kufundishana?

    Like

    Fatma

    October 12, 2010 at 8:20 am

  44. Hello Fatma, mimi nipo ila nimebanwa na shughuli, nina vifaranga wapya basi si unajua kazi ya vifaranga? Japo sikai shambani ufuatiliaji ni wa karibu sometimes narudi saa 4 usiku? Lakini ukiandika utajibiwa nadhani watu wapo wamejaa tele. Hata wewe unayo ya kutuambia tafadhali toa changamoto tuendelee. Ukiniona kimya nimebanwa tu na shughuli lakini mara nyingi napenda kuwepo hapa.

    Labda niulize wafugaji wenzangu wa kuku: Baadhi ya kuku wangu wanavimba kati ya vidole vya miguu yao uvimbe unaanza kidogo hatimae unakuwa mkubwa. Hii inatokana na nini na nini tiba yake? Wapo 5 sasa ambao nimewaona wako hivyo, alianza mmoja lakini na wengine wameshaanza kuvimba pia.

    Like

    Jenny

    October 12, 2010 at 9:31 am

    • Habari gani? Poleni kwa hekaheka nyingi. Ni kitambo sasa tangu tuendelee na darasa letu hapa. Bila shaka kila mmoja amebanwa na shughuli kwa namna yake. Haya Da Jenny katutupia swali, kwa mwenye jawabu, ni fursa yako kuchangia kile unachokijua … mshikamano daima, au siyo?

      Like

      simbadeo

      October 13, 2010 at 2:26 pm

  45. Kaka Deo asante. Bado nasubiri jibu la tatizo la kuku wangu.

    Kaka Nassib, niliwasiliana na hao jamaa wa Maji, wakanipa kwa ujumla gharama na utaratibu wao looooh! Nilikimbia mwenyewe. Gharama ya kunichimbia hicho kisima ni karibu milioni 7. Kwa hali yangu ya sasa sikiwezi. Nikatafuta wale wachimbaji wa mtaani wakaniambia milioni 3.5. Nayo kwa sasa sijakaa sawa. Nikatamani kuwaleta wachimbaji local toka kwetu Ukerewe wanaochimba kwa sululu jembe na makoleo hadi wanaupasua mwamba. Wakaniambia Dar es Salaam ni kichanga na wao wanaogopa sana mchanga. Kwa hivyo uchimbaji wa kisima nimesitisha kidogo. Nasubiri nijitahidi kwenye mradi wa kuku nikifanikiwa kuwa na akiba ya kutosha nitachimba. Duh! Kila kitu ghali. Sijui wenzangu mwaonaje.

    Like

    Jenny

    October 13, 2010 at 3:10 pm

    • Ni kweli Da Jenny. Kama nchi changa bado tuna changamoto nyingi likiwemo suala la udhibiti wa bei kwa ujumla pamoja na kushuka kwa thamani ya shilingi yetu. Lakini tufunge mkanda na kuendelea kuzalisha kwa wingi ili tujiletee aina ya mabadiliko tunayotaka. Ukiacha changamoto ya gharama za kuendesha miradi kuna changamoto ya kupata soko la uhakika … na nyinginezo nyingi.

      Like

      simbadeo

      October 13, 2010 at 4:32 pm

  46. Dada Jenny kuhusu tatizo la kuvimba miguu kuku wako nakushauri njia nzuri ni kuwapeleka kwa wtaalamu wa mifugo pale veterinary au kwenye sehemu kama Ilala Amana pale wana daktari wanaweza kumpasua kuku na kukwambia tatizo lake, ni vyema hata wewe ukiumwa bila shaka unaenda hospitali hali kadhalika na kuku pia kama unaona wankufa =basi wapeleke hospitali yao

    Like

    Nassib

    October 13, 2010 at 5:19 pm

    • Hi Nasib, asante sana kwa ushauri huo mzuri, nafikiri inafaa kuuzingatia. Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      October 13, 2010 at 10:40 pm

  47. za siku jaman habari za ufugaji nashukuru kwa majibu mazuri dec nitakuja likizo dar nitajitaid niende huko tegeta nikaonane na huyu mr icubuleta na sido huku kwetu vyakula tunatengeneza wenyewe na ubaya geita hakuna kiwanda kati yenu nani anchokiwanda nikija nijifunze zaid au anae rafiki anakiwanda pia nitaongea nae ili niwe na mwanga nashukuru sasa ndugu zangu ivi wenzangu kuku wakivaa makoti wakalegea miguu wakasinzia mnawapa dawa gani kuna kuku wa kanga wamenitesa sana ingekua ndo naanza kufuga naisi ningehairisha good day all

    Like

    da mariam

    October 14, 2010 at 1:08 pm

    • Da Mariam, karibu tena baada ya siku nyingi. Maswali yako ni muhimu katika kuendeleza mjadala na mazungumzo. Naamini kwamba jopo lililopo hapa litatupatia majibu kwa maswali uliyouliza na mengineyo mengi. Tuendelee kuwa pamoja.

      Like

      simbadeo

      October 14, 2010 at 11:53 pm

  48. Hello Kaka Nassib, nashukuru kwa ushauri wako. Madaktari walishawaona kuku wangu wakatoa dawa lakini tatizo linaendelea ndio maana niliona niulize kama kuna anayeweza kuwa na uzoefu na hicho kitu. Sometimes hata mimi nafuga kutokana na uzoefu zaidi nikiunganisha na utaalamu wa madaktari wa wanyama. Sometimes ukifuata sana ushauri wao unakwama. Ni 50 50 fulani hivi.

    Da Mariam, karibu sana Dar, utapata majibu yako toka kwa wengine ila ningelipenda kuzungumzia tatizo la kuku wako kuvaa makoti. Kwanza nauliza endapo unawapa chanjo muhimu hao kuku wanapokuwa wadogo kabisa mfano Newcastle, Gumboro, Ndui na kadhalika. Pia kuna magonjwa hayana chanjo inatakiwa USAFI wa mazingira unayowafugia kuku na lishe yao bora kuyadhibiti. Lakini pia kama wanavaa makoti, manyoya yanavurugika, hawakui vizuri, wanatoa mavi ya njano njano fulani sometimes mchanganyiko na kama damu basi ni Coccidiosis. Ni ugonjwa mbaya ukiingia kwenye kundi. Ila uhakika sana uwaone wataalamu wakusaidie ni njia sahihi zaidi. Ukishakuwa mzoefu ndipo utagundua mara tu tatizo linapoanza na wakati mwingine kulishughulikia mwenyewe bila hata kuhitaji msaada wa madaktari. Coccidiosis inastawi kwenye unyevunyevu na mayai yao yanakaa kwenye vinyesi vya kuku. Hakuna tiba kwa ugonjwa huo ila unaweza kuwasaidia kwa kuwapatia Amprolium 20% kulingana na vipimo vilivyoshauriwa kuwasaidia wale ambao hawajazidiwa waweze kujenga kinga ya mwili wao na kuushinda ugonjwa wenyewe. Wakiweza kuvuka wanakuwa sugu wa Coccidiosis, unawapiga sana vifaranga wa umri fulani hivi, wanapoanza kushamiri na kupendeza na wewe ukafurahia kwamba vifaranga wamechipua, ndipo ikiingia inawafagia.

    Like

    Jenny

    October 15, 2010 at 8:57 am

  49. Da Jenny Kuhusu huo ugonjwa wa kuku wako kuvimba miguu mimi sio mganga ila kuku wangu wakiwa labda amevunjika mguu na hawezi kabisa kutembea huwa nampa au nawapa Dox, ampicillin au tetasyqline hizo ni dawa za binadamu, unatakiwa kuwapa moja wapo kati ya hizo na unawapa kidonge kimoja asubuhi, mchana na jioni kwa siku tatu, kutwa mara tatu na kwa siku tatu, unammezesha kidonge na unamnywesha na maji ili kidonge kiweze kuingia tumboni na kupasuka ni kama vile unavyompa mtoto dawa baada ya siku tatu utakuta wameshapona, naomba ujaribu kwa kuku mmoja ukiona anaendelea vizuri basi utawapa na hao weninge. Pia kuna kinga ya kienyeji ambayo ni katani unachukua katani unatwanga kwenye kinu na maji yake unayaweka kwenye madude unayowekea maji yao ila yana mapofu lakini siyo mbaya nayo ni kinga nzuri sana hasa kwa kuku wa kienyeji huwa unawapa wakiwa wadogo ili kuwakinga na kideri.
    Kama ukishindwa nashauri usichoke kwenda kwa madaktari.

    Like

    Fatma

    October 15, 2010 at 1:11 pm

    • Asante Da Fatma kwa ushauri. Nadhani tunajifunza kitu hapa … ili kuwa mfugaji wa kuku mwenye ufanisi … huna budi kutumia mambo mawili makubwa. Mosi, utalaamu wa kisasa (kutoka kwa wataalamu wa fani ya sayansi ya mifugo – kwa tiba na ushauri); Pili, uzoefu (uwe wa kwako mwenyewe au kutoka kwa wenzako wanaofanya shughuli kama yako – yaani ufugaji). Kumbe basi tuendelee kushirikishana hapa ili kubadilishana uzoefu na pengine kuelekezana nini kinapatikana wapi/ kwa nani na kwa namna gani. Kupitia ushirikiano huu bila shaka ufanisi wetu katika kazi/biashara ya ufugaji nao utakuwa na hivyo kukuza tija. Tuwepo.

      Like

      simbadeo

      October 17, 2010 at 12:29 pm

  50. Asante Kaka Simba hiyo yote ni ushirikiano tulionao na ndio unaoleta kusaidiana katika maswala mbalimbali ili tuweze kufikia malengo na kujikwamua kimaisha.

    Like

    Fatma

    October 18, 2010 at 8:00 am

  51. Hello da’Fatma nashukuru sana kwa ushauri wako. Nitajaribu hiyo njia uliyosema. Kwa katani mimi hutumia majani ya Aloe Vera na Mwarobaini, nachanganya natwanga na kuchuja nawapa kama maji ya kunywa. Ni kinga nzuri. Kwa vile ninayo Aloe Vera basi situmii katani, naona kama vinafanana fanana na Aloe ni nzuri zaidi. Hiyo ni kinga nzuri kwa magonjwa japo sijajaribu katani.

    Hapa sasa panavutia sana kuwepo. Kaka Deo naomba utusaidie namna ya kukutumia picha, mimi nitapenda kuweka na picha mbali mbali za kuku wangu na kanga, pengine baadae tutabahatika kumpata daktari wa kutushauri hapa hapa. Pia nyumbani ninao mbwa 2 ninaowapenda sana Cheetah na Didi wote jike. Ni rafiki zangu sana.

    Like

    Jenny

    October 18, 2010 at 11:36 am

    • Hi Da Jenny, asante sana kwa kutushirikisha njia hiyo ya kutibu na kuwapa kinga vifaranga vya kuku na kuku kwa ujumla. Ndiyo, unaweza kutuma picha kwa anwani ya barua pepe: kakasimba@gmail.com nami nitazipandisha mara moja kwenye mtandao wetu. Hiyo ni njia nyingine muhimu sana ya kuelimishana – maana watu wataona kwa macho yao. Karibuni sana kutuma picha. Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      October 18, 2010 at 1:19 pm

  52. mambo rum huwa nafurai sana nikikuta mambo mazuri yanaongezaka nina vifaranga wa miezi miwili naweza wapa juice ya alover au katani hasa inasaidia nini kwani ninawenzangu huku ambao hawapati bahati ya kuchat mambo mazuri km haya ili nikiwambia waweze kuelewa faida mbona tutazidi kuyapanda majumban ahsanten sana mungu abariki hii rum

    Like

    damariam

    October 18, 2010 at 3:00 pm

  53. Hi, damariam hao vifaranga vyako vya miezi miwili ni wa aina gani?. Kama ni wa kienyeji ni sawa kuwapa juice ya aloe vera,majani ya mwarobaini au katani. Kwa sababu unawapa hivyo kwa ajili ya kinga hata ugonjwa wa kideri unapoingia basi kuku wako hawatakufa wengi. Inategemea wewe una nini hapo karibu na nyumbani kwako kama una aloe vera muarubaini au katani. Matumizi yake ni kama ifuatavyo: unaweza ukachukua aloe vera ukatwanga na kuwapa juice yake lakini unachanganya na maji usiwape yenyewe tu, unakaa kama wiki mbili au tatu ukawapa muarubaini au katani kama upo karibu yako. Lakini hii ni kinga tu sio tiba kwani wakiumwa inabidi ufuata ushauri wa daktari.

    Like

    Fatma

    October 19, 2010 at 7:35 am

  54. Hi, da Jenny nilikuambia kuhusu zile mashine za kutotolesha vifaranga (Incu better) kuna mtu mwingine anatengeneza na hazina usumbufu ukitaka unafanya order baada ya siku tatu anakupatia lakini anauza Shs.500,000.00 ina uwezo wa kutotolesha vifanga vya kuku 100 na 120 viranga vya kanga na hiyo mashine inatumia mafuta ya taa. Mtu yeyote kwenye ukumbi huu kama anataka anieleze ili niweze kuwapa ramani ili muweze kufika mahali penyewe au nitawapeleka.

    Like

    Fatma

    October 19, 2010 at 7:45 am

  55. Hello Da’Mariam,

    Kama alivyosema Fatuma ni kweli kabisa. Mimi huwapa kila mwezi mara 1 mfululizo wa siku 5 lakini kama wanakuwa hawana dozi ya dawa zingine. Kama wana dozi ya dawa za Vet inabidi usubiri wamalize, uwapumzishe kidogo ndio uwape. Mimi huchanganya Aloe na Mwarobaini. Kama vinatibu binadamu waliohangaika kwa Malaria sugu, basi ni zaidi hata kwa wanyama. Ni vizuri ukiyapanda nyumbani uwe nayo karibu, madaktari wa wanyama wanafurahi sana wakiyakuta unayo wewe mfugaji, wanatambua umuhimu wake.

    Hiyo ni kinga tu kuwasaidia wasipatwe magonjwa mara kwa mara au yanapoingia wasipukutike kwa wingi au wawe wamejenga kinga kushindana nayo. Majani ya mpera pia yanasaidia kama kuku wanaharisha na tiba za Vet hazionyeshi kuwasaidia. Ila kwa mimi huwa nachanganya majani hayo yote. Kama hakuna kuku anayeharisha bila mpangilio kwa kinga tu huwa nachanganya Aloe na Mwarobaini, kama nina tatizo la miharo isiyoeleweka, ambayo dawa zingine hazifui dafu naongeza Mpera. Kwa vile ni dawa ambazo hazina kipimo, usiweke makali sana ama mepesi sana, ukadirie na usizidishe siku nyingi sana kuwapa ama karibu karibu sana.

    Kuku aliyezidiwa hawezi kula wala kunywa mwenyewe huwa nawapikia uji wa lishe wa watoto laini sana, naongeza sukari kumpatia nguvu namnywesha. Kama utamnywesha dawa tu wakati hali chochote ni wazi atakufa tu. Akipata vijiko vichache vya uji ama chakula cha mezani kilichopondwa sana na dawa na maji baada ya muda utaona anaanza kula na kunywa mwenyewe.

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 7:51 am

  56. Da Fatma, Sijasahau mashine hiyo. Bado naihitaji ila kwa sasa unipe muda kidogo, nina vifaranga wapya, changanya na kuku wangu wakubwa wa siku zote na vinanigharimu somehow mfuko umepwaya. Nitakuarifu nikishakuwa tayari. Nilikuwa nazitafuta sana hizo mashine. Nipe muda kidogo nitarudi kwako, hope hutahama hapa kwa kaka Simba. Asante na tuendelee kuelimishana. Nasubiri picha zenu wandugu, na zangu soon mtazipata hapa. *(smiling)*

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 7:55 am

  57. Kuna washirika hawaonekani sana kutembelea hapa, naomba mrudi jamani, nao ni:
    PSquire
    Peter
    Eliza
    Seddy
    Yombo
    Kuku na
    Mwemezi

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 8:14 am

  58. Da Jenny ulisema una uhaba wa majogoo sasa kuna mahali wanauza majogoo ya Austrelia jogoo moja 25,000.00 lakini ni wakubwa sana na ni mbegu nzuri sana. Unaweza ukamuweka jogoo mmoja na majike au mitamba mitano kwa hiyo utapata chotara wazuri sana, na kama unataka pia kujifunza zaidi kutoka kwa watu wengine nitakupeka kwa dada mmoja yuko msasani ndio anao hao kuku na pia ukajifunze vitu vingine ambavyo huvijui. Mimi nilipokwenda huko mwenyewe nilishangaa lakini nimejifunza vitu vingi sana. Kwa jinsi ninavyokuona una bidii na ari ya kufuga ukiwa tayari nieleze nitakupeleka mimi nafanya kazi Magereza Makao Makuu ni karibu na chuo cha IFM na shule ya Bunge.

    Like

    Fatma

    October 19, 2010 at 11:39 am

  59. Da Fatma asante sana. Napenda sana kujifunza na kutembelea wengine waliobobea kwenye ufugaji, kila nilipoishatembelea sikuondoka mtupu, nilijifunza mengi na kuyafanyia kazi. Nafasi yangu ni Jumamosi na Jumapili, ninaishi Mbezi Beach – Goig. Namba yako ninayo na nitakutafuta tupange.

    Aina ya kuku wamekuwa wengi hata nachanganyikiwa mbegu gani nzuri. Vifaranga nilionao sasa ni wa Malawi. Ninao pia niliochanganya mwenyewe wachache na wa kwetu wa kienyeji. Ninao wa mayai toka Interchick. Ninao Kanga. Nilishauriwa na Daktari wa mifugo kununua wanaotoka Israel kwa madai ni wazuri. Sasa Australia! Inaonekana tuna aina nyingi sana za kuku ila tusiposhirikishana kama hivi hatutafahamu. Nadhani nitakuwa nazo hizo mbegu zote na halafu itakayotokana na hizo mbegu itakuwa ni aina ya Tanzania. Ubarikiwe Da’ Fatma nitakutumia sms.

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 12:36 pm

  60. Jenny, damariam, fatma na simbadeo.

    kwa kweli mimi nimefarijika kwa maelezo ambayo yanatolewa hapa kwenye blog hi. Kwa kweli walio wengi hasa ambao ndo kwanza tunataka kuanza tunajifunza mengi. nimegundua kwamba kuna njia mbalimbali za kukabiliana na magonjwa mbalimbali ya kuku ikiwemo matumizi ya majani ya miti.. this is good.

    nimefurahi pia wazo la kuweka picha hapa ili tuweze kuona kwa macho.. picture speaks more than words.

    kwa kweli hii blog inanifumdisha mambo mengi kiasi kwamba natamani tushirikiane tuandike kitabu cha ufugaji wa kuku tena kwa lugha nyepesi…

    mwemezi

    Like

    mwemezi

    October 19, 2010 at 2:16 pm

  61. Kaka Mwemezi asante.

    Hapo kwenye kuandika kitabu nadhani Kaka Deo ndio mwenyewe na umumbe umemfikia haswaaa!

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 2:32 pm

  62. sahihisho: ujumbe sio umumbe…

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 2:36 pm

  63. Unajua da Jenny mimi nina madume matatu ya kanga ambayo nilinunua wanne nikafikiri wawili ni madume na wawili ni majike kumbe yote ni madume kwa hiyo kama unao kanga majike naomba uniuzie hata wawili kwani naogopa kununua kwenye mabanda wasije wakanibambikia tena

    Like

    Fatma

    October 19, 2010 at 3:04 pm

  64. Kumtambua jike na dume wa kanga angalia masharubu yao. Dume wana masharubu makubwa kuliko jike. Na jike wana mlio ambao dume hawauwezi, “Buckweet! Buckweet Buckweet” Dume wanaweza mlio mmoja tu ambao jike pia wanauweza, “Krrrriaaaaaaakkakakakaka!”

    Kanga wangu kwa sasa wanataga na kama una mazoea na kanga wanaishi in pairs, jike na dume. Nisingelipenda kuwatoa kwa sasa wanapotaga wengine wameatamia. Pia niliwapunguza kutokana na wizi na kesi ya mazao ya watu, sinao wengi. Labda usubiri kidogo wakitotoa nikupe vifaranga ukuze maana sikusudii kuwa nao wengi tena. Sijazungusha fence.

    Hao madume ulionao jike ni mmoja tu? Kama ndio basi inabidi uwapunguze madume wengine abaki jike na dume tu. Wakitotoa kama utapenda kusubiri nitakupa mbegu ya kutosha.

    Like

    Jenny

    October 19, 2010 at 4:10 pm

    • Hi, asanteni nyote kwa kushiriki. Mijadala hii ina tija kubwa kwetu na kwa wengine ambao huifuatilia kimyakimya. Tunawaalika pia ili nao watushirikishe yale wanayoyafahamu au hata kuuliza swali/maswali. Asanteni.

      Like

      simbadeo

      October 19, 2010 at 7:12 pm

      • Kuhusu uandishi wa kitabu. Hilo ni wazo zuri sana. Na ni jambo linalowezekana. Ni mchakato mrefu kidogo, lakini unawezekana. Tuendelee kulifikiria na ikiwezekana kuona namna ya kuanza. Asanteni sana.

        Like

        simbadeo

        October 19, 2010 at 8:02 pm

  65. Nashukuru sana da Jenny kwa ukarimu wako wa kutaka kunisaidia nitasubiri wakitotoa unigaie vifaranga. Kwani mimi nilinunua kanga wanne nikaambiwa na muuzaji hawa wawili ni jike na wawili ni madume kumbe wote ni madume, na hivi juzi tu mmoja alikuwa anaumwa nikajitahidi kumpa madawa lakini ilishindikani nikamchinja, kwa hiyo hivi sasa nina madume matatu na yana mwaka mmoja na nusu. Ndio maana natafuta majike lakini nataka kwa wafungaji sitaki tena kununua kwenye mabanda.

    Like

    Fatma

    October 20, 2010 at 7:19 am

  66. OK Da’Fatma, Mimi mbegu nilinunua kwenye mabanda miaka 3 iliyopita ila nilipata muuzaji mstaarabu au aliyekuwa anawafahamu kanga vizuri. Ni vigumu sana kuwatofautisha jike na dume hadi uwe umewafuga ama kufahamu habari zao mbali mbali. Hawaugui kirahisi. Mara nyingi wakiugua, pia ni vigumu kugundua labda uwe mfuatiliaji sana maana mgonjwa huwa pamoja na wenzake tofauti na kuku ambaye hujitenga. Kanga mgonjwa utamuona anakuwa mzito kula. Wenzake wanapopiga kambi kula chakula ama kunywa maji yeye mgonjwa anabaki nyuma anapumzika akiwa amejikunyata. Ukimstua anatimua mbio kama wale wazima. Sio rahisi kugundua japo ukiwazoea unagundua mapema ukiwa mfuatiliaji. Mimi tangu nimewafuga tatizo kubwa linalowaathiri japo mara chache ni MAFUA. Jaribu Doxycol ni nzuri sana kwao. Daktari wa kwanza kunitibia kanga aliposikia tu maelezo yangu aliandika hiyo na toka wakati huo nikiona wanaanza kuzubaa ndio dawa ninayoikimbilia. Magonjwa mengine ni wagumu sana, nadhani kwa mazingira yetu mafua ni tatizo kwao. Pia Aloe inawasaidia kwa minyoo na tayari unayo unawapatia. Vinginevyo, akifa tena mwingine mpeleke Vet wakampasue wakujulishe tatizo. Wakitotoa nitakuarifu uchukue mbegu.

    Like

    Jenny

    October 20, 2010 at 7:32 am

  67. Asante sana da Jenny nitaendelea kusubiri. Unajua hawa nimekaa nao muda mrefu bila ya kujua kuwa nina madume watupu lakini nao naona wameshazeeka kwa hiyo nitafurahi ukinipa vifaranga ili nianze nao mwenyewe na ndio nitawafuatilia vizuri. Mimi ninataka kufanya mchanganyiko mmoja kama majaribio wa kuchukua bata kanari au bata maji ambao tunao kule ubena nataka nikanunue majike matatu na madume mawili halafu niwachanganye na bata wa kawaida kwa hiyo ukipata vifaranga vinakuwa ni chotara wazuri ila nasikia tu sasa nataka nijaribu kama ikifanikiwa nitakualika uje uvione vifaranga vyangu.

    Like

    Fatma

    October 20, 2010 at 8:09 am

  68. Yaani madume ya bata kanari au bata maji nawaweka na majike ya bata wa kawaida na majike ya bata kanari au bata maji nayaweka na madume ya bata wa kawaida. Kwa hiyo vifaranga vitakavyotoka hapo ndio utakuwa mchanganyiko au chotara.

    Like

    Fatma

    October 20, 2010 at 8:13 am

  69. Da Fatma nashukuru kwa taarifa ya Bata. Nawapenda sana Geese nadhani ndio hao bata maji. Nitakufuatilia utakapokuwa nao. Siku njema.

    Like

    Jenny

    October 20, 2010 at 8:48 am

  70. Wandugu, naomba mnisaidie kwani nina vifaranga kila siku vinakufa kati ya wanne na watano ma dr. wanasema ni ugonjwa wa vitovu. tumepewa dawa lakini vinaendelea kufa tu. kipindi cha wiki moja wamekufa vifaranga 40 yaani na kila siku vinakufa. msaad unaombwa maana mtaji unakatika

    Like

    Nassib

    October 29, 2010 at 9:21 am

  71. Hello Nassib,

    Pole sana. Kuna dada niko nae ofisi moja alipata tatizo kama lako na vilipukutika 100+. Sijawahi kupatwa na tatizo la aina hiyo hivyo sielewi sana jinsi ya kukabiliana nalo. Nadhani inabidi kuwa makini tu na wapi tunanunua vifaranga maana watotoleshaji wamekuwa wengi. Labda ushauri wangu ni kuvisaidia kwa vitamin, joto la kutosha, usafi na chakula toka kampuni nzuri. Vinginevyo sijui kweli utafanyaje, nasikitika maana hiyo hali ilimpata mwenzangu hapa na hakuna alichozuia hadi vilivyokuwa dhaifu zaidi vilipokwisha ndio vilivyobaki vikawa stable.

    Wengine walio na uzoefu na hilo jambo ama wanaelewa cha kufanya watakushauri. Nasubiri kuona pia ushauri wao.

    Like

    Jenny

    October 29, 2010 at 9:49 am

  72. Hell Dada Jenny,
    Nashkuru kwa maelekezo yako. Tulichofanya tuliwaendea wale waliotuuzia vifaranga na wakasema kwamba kuna mteja mwingine naye amepata tatizo hilohilo hivyo wanalifanyia kazi inawezekana vifaranga vyao vina matatizo. kwa hiyo kama ulivyosema ukipata vifaranga ambavyo vimetotolewa kwenye mayai yenye matatizo basi vifaranga hivyo vitakuwa na matatizo. Labda kwa ujumla nambie vifaranga wazuri ni wepi au kampuni gani inatoa vifaranga vizuri maana nao ni mtihani kubwa

    Like

    Nassib

    October 30, 2010 at 10:12 am

  73. Hello Dada Jenny,
    Nashkuru kwa maelekezo yako. Tulichofanya tuliwaendea wale waliotuuzia vifaranga na wakasema kwamba kuna mteja mwingine naye amepata tatizo hilohilo hivyo wanalifanyia kazi inawezekana vifaranga vyao vina matatizo. kwa hiyo kama ulivyosema ukipata vifaranga ambavyo vimetotolewa kwenye mayai yenye matatizo basi vifaranga hivyo vitakuwa na matatizo. Labda kwa ujumla nambie vifaranga wazuri ni wepi au kampuni gani inatoa vifaranga vizuri maana nao ni mtihani kubwa

    Like

    Nassib

    October 30, 2010 at 10:13 am

  74. pole sana kaka nassib hiyo huwa inatokea wape hao vifaranga otc na vitamin otc niantibayotic inasaidia kukausha vitovu wape maji ya otc vitamin kwa siku nzima kwa siku 3 mpk 5 bila meupe naiman tatizo litakwisha polee

    Like

    damariam

    October 30, 2010 at 11:44 pm

  75. Hello Kaka Nassib,

    Nadhani ni tatizo la dharula kwa watotoleshaji wengine, labda niseme watotoleshaji wamekuwa wengi hivyo kuna ambao ni wazuri, wazoefu, wanaelewa mambo mengi na kuna ambao wakikosea kidogo tatizo kama hilo linatokea. Mimi huchukulia Interchick, safari hii vya Malawi nimenunua Mbezi Beach (Samaki) na sijawahi kupata tatizo la aina hiyo. Labda wataalamu wangesaidia kutuambia kinachotokea. Kaka Simba huwezi kutusaidia tuwe na Daktari wa wanyama hapa kwenye baraza? Ingetufaa sana kwa shida ambazo ni ngeni kwetu n.k.

    Nadhani mtotoleshaji inabidi awafidie. Maana tatizo liko upande wake na hamna jinsi ya kulizuia. Huyo dada ambaye niko naye kazini vya kwake alinunulia Buguruni. Walinunua 2 na wote walipatwa tatizo moja la vitovu, hadi vidhaifu vilipokwisha vyote ndio vilivyobaki vimeendelea lakini kwa dawa sana hata inatia huruma.

    May be member mwingine atatoa ushauri zaidi. Asante Da’Mariam.

    Like

    Jenny

    November 1, 2010 at 6:34 am

  76. Pole sana kaka Nassib hiyo hutokea kwa bahati mbaya vifaranga kuwa na ugonjwa wa vitovu. Kwani vifaranga vyote tunavyo vichukua kwa maajenti au kiwandani huwa hawapewi kinga hivyo basi unapofika nao nyumbani unatakiwa uwape maji ambayo yana glucose na dawa hizi 3 moja wapo Fluquine, Aqwa Acid au Fulban ili uweze kukausha vitovu unawapa kwa muda wa siku 5 hiyo inasaidia sana kuwaweka sawa wakiwa wadogo. Naomba uwape hizo dawa halafu utaona maendeleo yake. Na kama unataka kuku wazuri ukanunue Kibo, kuku wa Arusha Interchick au hata Ideal

    Like

    Fatma Maundi

    November 1, 2010 at 7:55 am

  77. Wandugu,
    Nawashukuru sana kwa msaada wa mawazo kwa ushauri mlionipa. Mungu awbariki

    Like

    Nassib

    November 2, 2010 at 11:22 am

  78. Da Jenny unaendeleaje na kuku wa Malawi kwani na hapo uliponunua ni kwa ajenti na kila wakati wanakuwepo, na mimi nahitaji kununua hivyo vifaranga vya Malawi ili niweze kuwachanganya na kuku wangu ambao nimbegu ya Australia. Hivyo basi naomba unifahamishe vizuri ili nami niweze kwenda kununua hivyo vifaranga.
    Asante.

    Like

    Fatma

    November 4, 2010 at 7:13 am

  79. hamjambo jamani mifugo haijambo si huku wazima

    Like

    damariam

    November 7, 2010 at 1:20 pm

  80. Napenda kuwapongeza sana mlioanzisha website hii, pamoja na wadau wote mnaochangia mada. Mimi ndiyo mara yangu ya kwanza kufungua website hii, mimi pia nataka kuanza kufuga kuku wa mayai nikaona ni bora nianze kutafuta data jinsi ya kufuga kuku wa mayai. Naomba mnieleweshe zaidi wapendwa kwanza kabisa ujenzi wa banda, jinsi ya kujenga banda hilo, na je nianze kwa kufuga kuku wangapi? pia mnielekeze mafunzo yanapatikana wapi. nitazidi kuuliza maswali mengi sana naomba uvumiluvu wenu wadau.

    swali langu la mwisho lakini msinishangae ni addres yenu ya website hii manake nimeuliza tu kwenye google jinsi ya kufuga kuku wa mayai zikaja nyingi nikabahatika kufungua hii ya kwenu. sasa nataka niwe nayo kabisa manake google nayo wakati mwingine inazingua.

    Mungu awabariki sana.

    Like

    Judith

    November 9, 2010 at 2:26 pm

  81. Mimi sina shamba lakini nina nafasi kubwa kiasi inayoweza kuniwezesha kujenga banda, lakini kwangu ninatatizo moja mwisho ya kiwanja changu unapita mfereji mkubwa unaopitisha maji kutoka kwenye nyumba nyingine, pia jirani yangu anafuga nguruwe na kuna vicheche wengi na kenge ambao wananisumbua sana kwani nina fuga kuku wakienyeji kidogo kwaajili ya familia yangu. lakini wamekuwa wakila sana mayai.

    Like

    Judith

    November 9, 2010 at 2:32 pm

    • Mpendwa Judith, karibu sana kwenye kijiwe chetu hiki. Hapa tunabadilishana mawazo, ujuzi, fikra, uzoefu, contacts n.k. kuhusu suala zima la ufugaji, hususani ufugaji wa kuku. Ukipata nafasi, jaribu kupitia maoni yaliyotolewa siku za nyuma katika makala hii ya Kuku wa Amadori. Bila shaka huo utakuwa mwanzo mzuri na utajifunza mengi sana.
      Hata hivyo, mshiriki yeyote mwenye maoni mawili matatu anaweza kutuwekea hapa kwa faida ya Judith na wengine ambao bila shaka hupita kimyakimya.
      Anwani ya site hii (blogu) ni https://simbadeo.wordpress.com/ na makala inayohusika ni hiyo yenye kichwa cha habari Kuku wa Amadori.
      Da Jenny, asante sana kwa pendekezo lako la kumkaribisha daktari wa mifugo kwenye site yetu ili tuchangiane naye maarifa. Nitajaribu kuzungumza na daktari mmoja ninayemfahamu ili kama nafasi inamhurusu basi aingie kwenye kijiwe chetu walau mara moja moja ili kuona aina ya maswali yanayoulizwa na yeye anaweza kutupatia ushauri upi. Hata hivyo, ninamkaribisha mwingine yeyote anayefahamiana na daktari wa mifugo ili amwelekeze kwenye kijiwe chetu hiki. Nina imani jambo hili halitakuwa na tija kwetu tu tunaofuatilia makala hii ya ufugaji bali hata kwa daktari mwenyewe. Kwani wengi wetu tulio wafugaji au tunaotarajia kuwa wafugaji tutahitaji huduma yake, yaani, zaidi ya ushauri ambao atakuwa akiutoa hapa. Kwa hiyo basi kama kuna daktarai unamfahamu, mwambie anayo fursa hiyo nzuri hapa.
      Vinginevyo, niwashukuru nyote kwa michango mnayotoa, na zaidi sana niwapongeze kwa kushiriki kudumisha amani nchini kwetu baada ya uchaguzi mkuu uliokuwa wa kihistoria.

      Asante.

      Like

      simbadeo

      November 9, 2010 at 2:42 pm

  82. Asante sana kaka Simbadeo, nashukuru sana kwa msaada wako na kwa majibu yako ya haraka. nitazidi kufuatilia. nimejaribu kusoma japo kwa kiasi kikubwa sana japo nasomo huku nafanya kazi, kakini kwa baadhi ya niliyosoma sikuona hayo niliyo yauliza, jinsi ya kujenga panda ukubwa wa banda na ushauli wa nianze na kuku wangapi? kusema kweli mimi ni mgeni kabisa katika maswala ya ufugaji wa kuku wa kisasa.

    naomba msinichoke wadau

    Like

    Judith

    November 9, 2010 at 2:59 pm

  83. Habari za siku jamani. Nimekuwa kimya siku nyingi lakini ni Mzima kabisa na kuku wangu sasa wameanza kutaga.

    Judith, mimi mwenyewe nimeanza kufuga kuku wa mayai tangu mwezi wa tano mwaka huu, nilikuwa sijawahi kufuga kabisa. Idadi ya kuku wa kufuga inategemea na mfuko wako, ukubwa wa eneo, mtaji wa kujenga banda, kununua vifaranga, kuwahudumia na kuwalisha hadi kufikia kutaga. Ni vizuri utembelee wafugaji wengine uone wanachokifanya na umtafute daktari akague na eneo unalotaka kufugia ili akupe ushauri kwasababu umesema kuna mifereji ya maji na mwingiliano wa wanyama wengine. Kuku wa kisasa hawataki vurugu la sivyo watakufa.

    Suala la ukubwa wa banda ni kwamba mita moja ya mraba inatosha kuku 4-6 wa mayai na 9-12 wa nyama. Hivyo kama unataka kuanza na kuku 1,200 inabidi uwe na banda lisilopungua ukubwa wa mita za mraba mia mbili. Hakikisha hewa ya kutosha na sehemu kubwa ya banda isiangalie upande wa jua. Chakula cha kuku wa kisasa bei yake iko juu inabidi uwe umedhamiria na ujipange la sivyo unajikuta unashindwa kuwalisha wanadumaa.

    Kwa mfugaji anayeanza na kama kuku ni wengi ni vizuri uwe na daktari wako akuongoze. Mimi nina daktari anayewakagua kila baada ya muda na kunipa ushauri pale unapohitajika. Kwakweli nakiri kuwa ni mradi mzuri ambao nimejikuta naupenda na siku za weekend nasaidiana na mfanyakazi kuwahudumia. Hivi sasa situmii hela yangu tena angalau wanajilisha wenyewe ila nimeteseka kuwafikisha hapa walipo.

    Nawatakia kila la kheri, tuendelee kuwepo.

    Like

    Elizabeth

    November 9, 2010 at 4:58 pm

    • Asante sana Elizabeth, nashukuru sana, yani nimejikuta sasa napata moyo wa kufuga. Sijui unaishi wapi mpendwa, mimi nakaa Kibamba, je hao madaktari naweza kuwapata wapi, kwani inabidi umpate anayeweza kuwa karibu na maeneo ninayo ishi. Pili naomba kujua chakula cha kuku kwa sasa ni bei gani naomba pia unishauri niandae kama bei gani nikitaka kufuga kuku kama 1000. na je 1000 wanaweza kunipatia faida au inabidi wawe wengi?

      Yani naomba unisaidie kunieleza wewe umetumia kiasi gani cha pesa kuanzia maandalizi ya banda, ununuzi wa vifaranga, vyakula mpaka madawa hadi ulipoacha kutoa pesa yako mfukoni.Na umefunga kuku wangapi? Naweza kupata picha walau ya niandae kiasi gani.

      Like

      Judith

      November 9, 2010 at 5:12 pm

  84. Judith,

    Gharama ya kujenga banda inategemea ni la aina gani. Banda zuri la kisasa la kutosha kuku 1,000 si chini ya Milioni Nane. Vifaranga kila kimoja ni Tshs 2,000. Jumla Tshs 2,000,000/=. Chakula, bei inategemea kama ni starter, growers au layers, bei yake ni Tshs 22,000 – 27,000 kwa mfuko wa kilo 50,000. Wataalamu wanakadiria kuku mmoja wa mayai anahitaji Tshs 6,000 kumuhudumia mpaka atage (chakula na madawa. Nimeifanyia majaribio naona ni sawa. Wanahitaji maji ya kutosha na masafi pamoja na joto (wakiwa wadogo). Vifaa vya kulia chakula pamoja na kunywea maji. Kwa data hizo utapiga mahesabu mwenyewe kiasi gani uandae.

    Madaktari wako wengi. kwa mfano ukinunua vifaranga vya Tanzania Poultry Farm wa Arusha (wana office zao Temeke Kwa Sokota). Watakupatia vipeperushi na utamkuta daktari atakueleza yote unayotaka kujua. Idadi yoyote ya kuku kama umewafuga vizuri huwezi kukosa faida. Kwa mfugaji wa kati kuku 1,000 ni idadi nzuri kuanzia.

    Mimi nafugia Tabata Kinyerezi, nimeanza na kuku 1,200.

    Like

    Elizabeth

    November 10, 2010 at 12:11 pm

  85. Asante sana, mpendwa ubarikiwe sana, kweli dada ndo mana unafanikiwa katika ufugaji wako.

    Unajua watu wengi sana ukiwauliza kuhusu habari za kuku wanakatisha tamaa kabisa. Ndo mana nikaamua kutafuta humu kwenye mtandao.

    Nashukuru sana dada nikipata contact zako naweza kukutembelea siku moja, kwani natumia njia hiyo ya kinyerezi mara nyingi sana kwenda nyumbani kwangu Kibamba.

    Naomba msinichoke kwa kuomba ushauri.

    nawatakia ufugaji mwema.

    Like

    Judith

    November 10, 2010 at 1:22 pm

  86. Dada Elizabeth, nami nimefarijika kwa taarifa hiyo ya kuku wa mayai; ila nauliza tu umesema Wataalamu wanakadiria kuku mmoja wa mayai anahitaji Tshs 6,000 kumuhudumia mpaka atage (chakula na madawa) jee hiyo ni kwa mwezi kwa siku au ?? nami pia nataka nianze kuku wa mayai ndio maana nfatilia mijadala hiyo

    Like

    Nassib

    November 11, 2010 at 10:24 am

  87. Dada Elizabeth,
    Nashkuru nami nimepata taarifa nzuri kwa ajili ya ufugaji wa kuku wa mayai. jee wakianza kutaga matumizi kwa kila kuku inakuwa Tshs ngapi?

    Like

    Nassib

    November 11, 2010 at 10:42 am

  88. Kaka Nassib,

    Hiyo ni kwa kipindi chote mpaka kutaga, week 18. Unaweza kuiona ndogo lakini kumbuka kama una kuku 1,000 ni Tshs 6,000,000 kwa chakula tu na chanjo. Wakati wanataga kuku mmoja anakula gram 120 kwa siku na vitamin mara mbili kwa wiki. Mfano mimi kuku wangu wote wanakula mifuko miwili na nusu ya kilo 50 kwa siku. Wakishaanza kutaga gharama za dawa si kubwa, labda wakiugua, Wanakuwa wameishamaliza chanjo.

    Nawatakia kila la kheri,

    Like

    Elizabeth

    November 11, 2010 at 3:21 pm

    • Wandugu, salama? Da Eliza, asante sana kwa mchanganuo huo uliotuwekea hapa. Naamini kwa mtu anayetaka kuanza biashara hii ya ufugaji atakuwa amejifunza mengi sana – na kujipima kwamba aanze vipi na katika hatua gani. Basi wengine mnakaribishwa kutupatia uzoefu wenu zaidi kuhusu namna gani mtu aanze kufuga – aanze vipi na ajiandae vipi – ajitahidi kuwa na ‘liquid capital’ ya muda gani ili asikwame katikati ya mradi. Asanteni sana kwa ushauri na michango mnayotoa kupitia kijiwe chetu hiki. Karibuni.

      Like

      simbadeo

      November 18, 2010 at 10:31 am

  89. Hodiiiii!

    Nilikuwa bize kufuatilia matokeo ya uchaguzi. Kwa jinsi kampeni zilivyokuwa zilinihamasisha kufuatilia hivyo nilikuwa nafungua mitandao inayozungumzia uchaguzi nikasahau kuja hapa.

    Da Fatma nilikujibu, lakini kwa faida ya wengine hao kuku wa Malawi wanapatikana Mbezi Beach. Pale Tangi Bovu kuna Veterinary Clinic/Shop inaitwa Tangi Bovu iko barabarani kabisa, ukifika hapo watakuelekeza kwa mama muuza vifaranga na kukupa mawasiliano yake.

    Da Mariam nashukuru sana kwa ufafanuzi ulioutoa, umeniongezea maarifa, ubarikiwe. Mimi nilianza kidogo kidogo sana kwa mtaji mdogo na bado niko katika hali ya mtaji mdogo, meaning bado ninawekeza. Ujenzi wa mabanda nilianza na banda ambalo nilijenga kwa kutumia used materials, zipo nyingi pale Buguruni ukielekea TAZARA upande wa kushoto. Utapata kila kitu kuanzia mabao yaliyotumika, mabati, milango n.k. Banda langu nililoanzia nimetumia mitumba ya kila kitu, tofali kidogo ndio nilifyatua ama kununua lakini nazo kuna mahali nilipata wamebomoa nyumba, nikazipata kwa unafuu. Fundi alikosea ku-set hivyo likawa kubwa, nikaezeka nusu na nusu nikamalizia baadae nikiwa tayari ninafuga kulingana na kuku walivyokuwa wakiongezeka. Nilianza na kuku wa kienyeji. Hivyo kwa wafugaji wadogo inawezekana kuanza kidogo kidogo. Nimefurahishwa na uchambuzi wa Da’ Mariam kwa wafugaji wa kati imenipa moyo kwamba karibu nitaingia kwenye hilo kundi. Wafugaji wadogo pia inawezekana kwa kuanza kidogo kidogo. Nilianza na kuku wachache sana. Wa mayai nilikuwa nao 100 tu ukitoa kanga na wale wa kienyeji. Nimeongeza vifaranga 300 ambao sasa wanatunzwa na hao 100 wanaotaga. Mwisho wa mwezi huu tena nitaongeza wengine 300. Malengo nifikishe kuku 1,000.

    Kama alivyoeleza Da’Mariam, ni kweli ni kazi sana kuwalisha na kuwahudumia ingawa kwa hao 100 sikuona shida sana, nilikuwa na kuku wa kienyeji nyumbani ambao kwa kiasi fulani walifidia ugumu. Lakini kwa sasa hao 300 wanakula kama mchwa na ninapokwenda kuongeza wengine 300 wiki ijayo nimeshaona jinsi itakavyokuwa kufunga mkanda. Kama nilizoea kununua vyakula na vitu muhimu kwa mwezi mzima, kwa sasa ninapima vibaba. Kila senti inaliwa na hao kuku, lakini ni kwamba inawezekana pia kuanza kidogo kidogo, na kama una mtaji wa kutosha ni vizuri uanze kwa kundi kubwa ili kupata faida mapema.

    Ni katika kupeana maarifa. Nashukuru kwa hayo niliyosoma. Mimi yananisaidia sana sana. Asanteni wadau.

    Like

    Jenny

    November 18, 2010 at 12:04 pm

  90. Sorry, Da Elizabeth ndiye aliyetutumia ufafanuzi mzuri wa ufugaji ambao nimeuzungumzia hapo juu. Eliza nakushukuru sana sana sanaa! Wote asanteni pia.

    Like

    Jenny

    November 18, 2010 at 12:06 pm

    • Da Jenny, asante sana kwa kututia moyo. Nimefurahia sana maoni yako, hasa msisitizo, kwamba TUNAWEZA hata kidogokidogo. Nakubaliana nawe, maana Waswahili husema: ‘Hata mbuyu ulianza kama mchicha’. Na kwa hakika huo ndiyo ujasiriamali! Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      November 18, 2010 at 2:43 pm

  91. Hamjambo wadau, poleni na mchakato wa uchaguzi.

    Da Jenny umenifurahisha sana, kwani hesabu za da Eliza zilikuwa zimenichanganya kidogo, manake niliona mambo yanakuwa magumu sana. Kumbe unaweza kuanza kidogo kidogo, manake niliona pesa zangu zitaishia kwenye panda kumbe unaweza kutumia vifaa vya mtumba.

    Tatizo langu jingine ni kwamba, nawaomba sana wale mlio na mabanda basi yapigeni picha mtuwekee kwenye mtandao tuweze kuyaona tupate ramani nasisi, manake mafundi nao wanatuzingua sana.

    nawashukuru wote mnaozidi kutuelimisha, bila kumsahau kaka yetu mwenye blog.

    Like

    Judy

    November 18, 2010 at 4:59 pm

    • Haya wadau, tuendelee kujadili na kubadilishana mawazo. Kuna wazo hili la kuweka picha zinazohusiana na ujenzi wa mabanda ya kufugia na bila shaka picha zinazohusu mbinu/njia za ufugaji bora. Ninawakaribisha kunitumia picha hizo nami nitaziweka hapa. Pia kama una mradi ambao unafikiri watu wanaweza kujifunza kwa njia ya picha, basi nikaribishe, nami nitatafuta wasaa wa kuja kupiga picha hizo na kuwawekea hapa wadau wetu. Lakini kila kitu hapa ni hiyari kabisa … mtu ujisikie huru. Binafsi, nafasi ikiniruhusu nitatembea huku na kule ili kupata taswira ambazo nitazipandisha hapa kwa manufaa yetu sote. Asante mdau kwa changamoto hiyo.

      Like

      simbadeo

      November 18, 2010 at 10:52 pm

  92. Hello Judy, Karibu kwenye baraza (nilisahau kukukaribisha!).

    Da Eliza alikupigia hesabu kwa swali ulilouliza maana uliuliza kuku 1,000. Na hayo ndiyo mahesabu yake kwa wafugaji wa kati. Mimi binafsi niliona hizo ni hela nyingi kwa sisi wafugaji wadogo na kwa vile watu wengi hupita hapa katika kutafuta tafuta habari na kuuliza, nikaona ni vema niwasaidie wale ambao bado tuko katika mtaji mdogo wasikate tamaa. Maana hesabu za kuku 1,000 banda peke yake na kuku ni mil 10,000,000/=. Ukijumlisha na kuwalisha na dawa hadi waanze kutaga ni + mil 6,000,000/= ambazo jumla ni mil 16,000,000/= (bila kuweka mishahara ya wafanyakazi, maji, umeme, mafuta ya taa etc.) Kwa wafugaji wadogo hizo ni hela ambazo huwezi kupata mwamko wa kufuga. Ndio maana nikasema pia kwamba, kama mtaji unakuruhusu, ni vizuri sana kuanza kwa hesabu hizo kama Da’Eliza alivyoainisha maana utakwenda haraka. Lakini kwa wale ambao mtaji ni kidogo na pengine tunategemea mshahara toka tulikoajiriwa, tusikate tamaa, unaweza kwenda taratibu kama mimi. Kama nilivyosema, hao wa mayai pekee ukitoa wa kienyeji nilianza na 100. Na hao 100 waliweza kujilisha na kuwalipa vijana mishahara yao bila kugusa mfuko wangu. Lakini sasa ninapoongeza ili kukimbilia 1,000 kazi ipo. Lakini hao 300 ambao wataanza kutaga Februari watawalisha kundi zima nitakalokuwa nalo na pengine kulipa mishahara kwa vile nikiwajumlisha na waliopo wote watakuwa kama 450 hivi kuondoa 300 ninaoongeza mwisho wa mwezi huu. Da’Eliza amesema ukweli, inatesa kuanza lakini baadae inalipa hivyo kama una mtaji mzuri anza na idadi nzuri ili ukimbie haraka. Nitajitahidi sana kuwatumia picha, Da’Eliza pia please tutumie picha kama itawezekana utusaidie kupiga hatua kufikia kati, binafsi nimefaidika na maelezo yako. Nimependa sana ulivyoanza na 1,200 na pole maana loh! sio rahisi kwa vitendo.

    Kuhusu picha nasubiri kijana wangu afunge shule yeye ni mzuri zaidi kwa picha. Kaka Deo pia kama unaweza kunitembelea karibu ila kwa weekend hii sitakuwa na nafasi. Labda mwisho wa mwezi say tarehe 28 hivi au baada ya hapo, kama utaweza ili upate hizo picha kiufundi zaidi.

    Naamini tukisaidiana kama hivi tutafika mbali. Jamani tuungane tusaidiane. Namshukuru sana Da’Eliza, amenisaidia mengi kwa post zake za ufafanuzi. Nimeshapiga hesabu tayari ninapokwenda kuongeza kuku kutokana na hesabu alizotupatia.

    Kaka Deo Karibu “Poultry Garden” yangu, hehehehehe!

    Like

    Jenny

    November 19, 2010 at 7:48 am

    • Hi, Da Jenny, asante sana kwa picha. Nimeipandisha kwenye blogu. Wadau wote kwa ujumla – Ukipata shida ya kuifungua … maana mtandao haukuwa stable sana leo asubuhi … jaribu kuidouble click. Itafunguka katika size kubwa zaidi. Nakaribisha picha zaidi.

      Like

      simbadeo

      November 19, 2010 at 9:33 am

  93. du banda zuri sana da jane nami nimepata kitu nikihamia mkoa mwingine nitajenga la hivyo hongera sana

    Like

    damariam

    November 19, 2010 at 3:49 pm

  94. Da Judith, Mbona unajichanganya. Tarehe 9/11/2010 uliomba tukupe mchanganuo wa kufuga kuku 1,000 nikakupa. Leo hii unasema nimekukatisha tamaa. Mchanganuo huo unaweza kuutumia hata kwa kuku 20 tu na ndo maana nikasema inategemea na jinsi ulivyodhamiria. Mimi mwenyewe nimekiri kwamba nimeteseka haswa, kama anavyosema Da Jenny hadi budget ya familia inapunguzwa kwa ajili ya kulisha kuku.

    Da Jenny, nimefurahi kama information hizo zimekuwa useful kwako, endelea kupambana kwa juhudi zako malengo yako yatafika tu.

    Mungu awabariki sana.

    Like

    Elizabeth

    November 22, 2010 at 11:34 am

  95. Asanteni sana kwa kunishauri wapendwa, si kwamba nimesema wewe ndo umenikatisha tamaa no, labda sikueleweka vizuri, yani ni kwamba baada ya kuona hayo mahesabu nikajua kwamba ukianza na kuku kidogo uwezi kupata faida, ndo mana nikasema nilikata tamaa baada ya kuona kumbe kuku 1000 wanakula pesa kiasi hicho? na nikajua ukifuga kidogo uwezi kupata faida. Lakini nilishukuru sana da Eliza kwani mchanganuo wako nimeupenda na nilimpelekea mwenzangu akafurahishwa nao lakini akasema tunatakiwa kujipanga sana. sasa baada ya kuona wa Da Jeny nikao kumbe wakati nasubiri mtaji naweza kuanza na kidogo ili nipate usoefu.

    Like

    Judith

    November 22, 2010 at 2:03 pm

  96. Nashukuru pia kwa kujibu maombi yetu kwani banda nimeliona na nimelipenda sana linatia hamasa. Hongera sana wafugaji.

    Naomba wadau wetu kina Da Jeny, Da Eliza na wengineo tusaidieni pia kutupatia hesabu za mapato na matumizi ili tuweze kupata mwanga kuhusu faida na hasara, na vipi ukipata hasara ufidie wapi. yani tuseme jinsi ya kukeep recods zako, (kwani mali bila daftari upotea bila kujua). Wengine tunakosa muda wa kwenda kwenye masomo ya ujasiliamali, kutokana na ajira zetu hizo za kubembeleza, ili tuweze kujikwamua.
    Nazidi kuwashukuru na Mungu azidi kuwabariki
    Nitawashukuru

    Like

    Judith

    November 22, 2010 at 2:11 pm

    • Wadau, nafurahi naona kumekuwa na kuelewana baada ya fafanuzi mbalimbali. Da Judith … ni kweli ‘mali bila daftari, hupotea bila habari’ … nafikiri hili ni eneo lingine ambalo inafaa tupeane maarifa.
      Sifa kuu za mjasiriamali ni pamoja na uthubutu (ujasiri), ubunifu, umakini na ufuatiliaji wa taarifa zinazohusiana na kile anachofanya. Biashara ya ufugaji kuku inahitaji sifa hizi … maana nao ni ujasiriamali wa hali ya juu.
      Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      November 22, 2010 at 2:22 pm

  97. Hi wadau, natumaini wote hamjambo, mnaendelea vizuri na mifugo yenu. Leo naomba nije na mada nyingine inayohusu Jinsi ya kutunza kumbukumbu (Records) naomba wadau mtutumie jinsi ya kutunza kumbukumbu zinazoonekana (Physical records) km. chakula, vifo, ukuaji na afya. na kumbukumbu za kifedha (Financial Records) mauzo ya mayai, manunuzi ya chakula+dawa n.k, kwa siku/wiki/mwezi/mwaka.

    Nitashukuru iwapo ombi langu mtalifanyia kazi wataalam.
    Tuzidi kupeana mawazo na mafunzo.

    Like

    Judy

    November 23, 2010 at 11:27 am

  98. Hello Da Juddy,

    Mimi binafsi sina utaalam wa kuweka kumbukumbu lakini ninaweka kumbukumbu zangu very localy ama kienyeji kwa namna ambayo inaniwezesha kuelewa na kujua ninapata faida ama la. Kwa hivyo kwa ufupi, niliamua kuweka ledger books au vitabu vya kumbukumbu nyumbani na shambani. Nyumbani ninavyo vitabu ambavyo vinaonyesha manunuzi na maingizo. Upande wa manunuzi unajumuisha kila senti ninayoitoa kwa ajili ya huo mradi ikiwemo mishahara na kila kitu. Upande wa maingizo ni mauzo yoyote ninayoyafanya mfano mayai, kuku etc kutokana na mradi. Hata ujenzi kwenye kitabu changu hicho naweka huko huko. Nikihitaji kujua mwezi huu kuku pekee wamegharimu kiasi gani kutoa mambo ya ujenzi mdogo mdogo ninaoendelea nao hatua kwa hatua narudi kwenye kitabu na kutenganisha kwenye karatasi tofauti napata jumla. Ila nina kitabu kidogo kwa ajili ya vifaranga hadi wanapoanza kutaga ili kujua wamenigharimu kiasi gani. Hesabu hii pia inakuweko kwenye kitabu kikubwa isipokuwa kitabu cha vifaranga natenga mambo ya vifaranga tu.

    Shambani nimewapa vijana vitabu ambavyo viko tofauti.

    Kuna kitabu cha vifaa ambacho kinaonyesha vifaa vyote vilivyopo shambani, na kila baada ya muda hukagua kuona kama vipo vyote ama vimeongezeka ama kuna vilivyopungua na kwa namna gani, vimechorwa kwa chati ambazo wao hujaza. Katika kitabu hiki kuna sehemu inayoonyesha vyakula wanavyopokea, gunia ngapi n.k. na kiasi wanachotoa stoo kila siku kwa ajili ya kuku. Kwa hali hiyo tunafahamu kuku wanatumiaje na tupeleke kiasi gani na kitakuwa ni kwa muda gani, kama kimekwisha kabla ya muda tunaulizana wamekosea wapi maana inabidi kwenda kwa mahesabu kamili. Kabla ya hapo nilikuwa napeleka tu matokeo yake hata pumba liliuzwa pamoja na madawa kwa majirani.

    Kuna rejesta ya mayai inayoonyesha kwa siku yametagwa mangapi, mangapi yameharibika mfano yamepata nyufa au kupasuka n.k. na kwa siku wamepata tray ngapi. Kwa mwisho wa mwezi jumla yalitagwa mayai mangapi, mangapi yalikuwa hayafai, na tray ngapi kwa mwezi mzima zilipatikana na mgawanyo wake wa kutolewa shambani kuja kwangu kama muuzaji. Idadi ya tray walizotoa inatakiwa iendane na idadi ya mauzo ya tray zitakazokuwa kwenye kitabu changu nyumbani kwa vile kila zinapouzwa ninaandika.

    Pia kuna rejesta ya mapato na matumizi shambani kwa pesa walizopewa kununua pengine dawa ama mafuta ya taa au chochote na namna zilivyotumika na kwa mayai yaliyouzwa shamba na namna pesa zilivyotumika ama kuwasilishwa kwangu.

    Kwa kifupi, sina ujuzi kwenye upande huo kwa hiyo nina aina ya vitabu ambavyo nimevibuni mwenyewe na kuviweka katika namna ambayo mwisho wa mwezi huniwezesha kujua faida na hasara kama zipo.

    Natumaini wenye ujuzi juu ya hili watatusaidia.

    Like

    Jenny

    November 24, 2010 at 1:04 pm

    • Da Jenny, well, nimependa namna unavyotunza mahesabu yako. Nafikiri kuna matumizi makubwa tu ya njia zinazokubalika kitaalamu. Kikubwa ni kwamba unazo data zote na mtu akitaka kuziaccess anaweza. Pengine njia za kisasa zaidi zinasaidia katika upatikanaji wa haraka wa data zinazohitajika, lakini nafikiri njia hiyo ni mwafaka kabisa na pengine wengine pia tunaweza kuifuata – kama sio katika ufugaji kuku basi katika biashara/shughuli zetu nyingine. Asante sana Da Jenny kwa mchango wako.

      Like

      simbadeo

      November 24, 2010 at 5:05 pm

    • Da. Juddy hizo mbinu unazotumia kutunza hesabu ni za kitaalamu kabisa.Hongera. Hiyo ndio mbinu ya kitaalamu ya kutunza hesabu katika biashara ya mifugo..inabidi watu wa jifunze kutoka kwako

      Like

      sisa

      December 23, 2010 at 5:20 pm

  99. […] […]

    Like

  100. Habari za siku wadau,

    Maendeleo ya mifungo vipi? Kama mnavyojua hiki ni kipindi cha joto ambacho uwa kigumu kwa wafugaji wa kuku hasa wa mayai maanake wanashindwa kula vizuri na utagaji unashuka. Wenzangu mnafanyaje kuhusu hili?

    Wenu, Katika Ujenzi wa Taifa

    Like

    Elizabeth

    December 1, 2010 at 12:45 pm

  101. Hello Eliza, maendeleo mazuri.

    Mimi Kuku wangu wa mayai wako nje wanazurula kama wa kienyeji tu, wanapumzika vivulini wanapozidiwa joto n.k, hivyo sielewi inakuwaje. May be wengine wenye uzoefu watatuhabarisha. Asante.

    Like

    Jenny

    December 1, 2010 at 1:26 pm

  102. Habari za siku ndugu zangu wote kwenye ukumbi huu
    Nilikuwa bussy kidogo na majukumu ya maisha vipi kuku wenu wanaendeleaje. Yeyote anaejua jinsi ya kutengeneza chakula cha kuku mwenyewe naomba anifahamishe ili niweze kutengeneza mimi mwenyewe kwani cha kununua kimekuwa bei mbaya sana.

    Like

    Fatma

    December 6, 2010 at 3:14 pm

  103. Watu wako wapi jamani? Habari za mifugo zimekwisha ama mko bize na mivugo yenu?

    Like

    Jenny

    December 20, 2010 at 4:43 pm

    • Da Jenny, watu wapo. Lakini kama unavyojua, kipindi hiki watu wako busy kwelikweli kufanya biashara ya kuku … maana Krismas ndiyo hiyo imebakiza siku tatu tu … au siyo wandugu?

      Niwatakie kila la kheri katika Msimu huu wa Sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya.

      Mwenyezi Mungu atulinde, atukinge na mabaya yote na atupe nguvu za kuanza Mwaka Mpya kwa malengo makubwa zaidi: kimwili, kiakili, kiroho, kiuchumi na kijamii. Sikukuu njema.

      Like

      simbadeo

      December 21, 2010 at 9:39 am

  104. KAKA SIMBA NA WENGINE WOOOTEEEE HAPA UKUMBINI, NASSIB, JUDY, FATMA, MARIAM, ELIZA, NA INVISIBLE WOTE WANAOPITA HAPA BILA KUSEMA KITU BALI KUTABASAMU NA KUFURAHIA:

    HERI YA MWAKA MPYA 2011 NA MAENDELEO NA MAFANIKIO YAWE TELE, WALIOKUWA WAFUGAJI WA KATI WAPANDE DARAJA KUWA WAKUBWA, WALIOKUWA WADOGO TUPANDE KUWA WA KATI, NA WANAOTAKA NA WANAOANZA WAANZE KWA MAFANIKIO.

    MUNGU AWE NASI SOTE DAIMA NA MBARIKIWE SANA SANA.

    Like

    Jenny

    December 29, 2010 at 2:02 pm

    • Da Jenny, asante sana kwa salamu za Mwaka Mpya 2011. Tunaomba Mungu dua zako zipokelewe ili wadau katika sekta hii tuongezeke.

      Nami pia ninawatakia nyote heri, baraka na mafanikio tele katika Mwaka Mpya wa 2011. Uwe mwaka wa kushirikiana zaidi. Tuombe Mungu kwamba atuwezeshe kukutana na kuwa na semina ya pamoja ambapo tutapata fursa ya kufahamiana zaidi, kubadilishana uzoefu, kuelimishana na hata kufungua milango ya kutembeleana.

      Labda kwa kuuliza tu, je, tukisema tuandae semina, na mimi ninafikiri semina ya aina hii si kama zile za kufanyia katika mahoteli ya 5 star, bali hii itabidi tutafute namna ya ‘shamba darasa’ ambapo tutatumia siku nzima hapo, sasa, ni wangapi ambao wangependa tufanye kitu na namna hiyo? Kama kutakuwa na gharama kidogo (basics), ni wangapi watakuwa tayari kuchangia … na mathalani kama shamba darasa linapatikana hapa Dar es Salaam … tunaweza kukisia kiasi gani cha gharama.

      Hilo ni wazo tu ambalo limekuwa kichwani kwa muda mrefu … tupeane mawazo namna gani tunaweza kulifanikisha. Nawasilisha.

      Like

      simbadeo

      December 29, 2010 at 2:51 pm

  105. Mimi naona wazo la shamba darasa ni zuri sana labda nimngemwomb dada Jenny yeye tuandalie shamba darasa watu tutembelee shambani kwake kama atakubali. Kuhusu gharama nagdhani gharama ni ya kwenda huko labda vinywaji kidogo kila mtu atajigharamia mwenyewe. Ni wazo tu na wengine wanaweza kuchangia. Pia mapenda kuwapa hongera kwa kukaribia kumaliza mwaka na nawatakia mafanikio mema kwa shughuli mzifanyazo

    Like

    Nassib

    December 30, 2010 at 8:40 am

  106. Wazo hilo ni zuri sana na nashukuru kwa watu kuchagua tuanzie na shambani kwangu. Nawakaribisha sana maana najua mkija darasa litanifaa sana mimi kwa vile niko bado kwenye ufugaji mdogo najitahidi nifikie wa kati.

    Sasa tupange lini, nashauri baada ya mwaka mpya na watoto wakishaenda skuli. Siku pia iwe lini? Kwangu siku nzuri ni Jumamosi japo naweza kujipanga kulingana na wengine watakavyopendekeza.

    Asanteni na karibuni tusaidiane.

    Like

    Jenny

    December 30, 2010 at 10:08 am

  107. Nawashukuru na karibuni sana shambani kwangu. Shamba nitaliandaa ila pengine darasa itabidi tujumuike pamoja kwa vile na mimi nategemea kujifunza mengi na kupata mawazo mapya toka kwa watakaokuwa wanafunzi wenzangu siku hiyo. Mwalimu/Kiongozi napendekeza awe Kaka Deo na atuandalie masomo.

    Siku nzuri kwangu huwa ni Jumamosi, pia ningelipendekeza tupange tarehe ambayo itakuwa imetuweka huru kidogo kutoka kwenye sikukuu za mwaka mpya na pilika pilika za kupeleka watoto shule. Labda watu wapendekeze na tarehe kabisa ili tuiangalie kwa pamoja.

    Like

    Jenny

    December 30, 2010 at 10:13 am

  108. Kaka Deo naomba ufute msg mojawapo ya hizo hapo juu, nilipost ya kwanza nikaona kama haikwenda nikarudia kuandika. Asante.

    Like

    Jenny

    December 30, 2010 at 10:15 am

    • Hi, Da Jenny na Nd Nassib. Asanteni kwa michango hiyo ya mawazo. Pengine tuendelee kusikia na wengine watakuwa na maoni gani. Jamani karibuni ili tukifika mahali tukakubaliana modalities zote ili kufanikisha siku hiyo, basi itakuwa vema zaidi, au siyo.

      Ijapokuwa, kama alivyodokeza Da Jenny, itabidi kwanza kila mmoja amalize hekaheka zinazotokea mwezi wa kwanza … kupeleka watoto shule … kukamilisha mahitaji yao ya shule …n.k.

      Like

      simbadeo

      December 30, 2010 at 2:41 pm

  109. Mimi naungana na kaka Nassib ni vizuri tuanzie kwa da Jenny tukajifunze anavyofanya mwenzetu na kubadilishana mawazo kutokana na tutakachokiona hapo. Kwa sababu ni shamba itabidi kila mtu abebe kinywaji chake na kitafunwa kama ikiwezekana, ila cha msingi ni kwenda kujifunza ujasiriamali. Tukitoka hapo basi labda mwingine nae anaweza kujitokeza na kusema twende kwake basi itakuwa ndio tumeshaanza mzunguko kama alivyosema kaka Deo hatimae tutajikuta tumetembeleana wote. Nawatakieni kila la kheri na mwaka mpya mwema.

    Like

    Fatma

    December 31, 2010 at 2:34 pm

    • Asante Da Fatma kwa mchango wa mawazo. Heri na Fanaka kwa mwaka Mpya 2011 kwa wadau wote.

      Like

      simbadeo

      December 31, 2010 at 2:41 pm

  110. […] Kuku wa Amadori December 2008142 comments 3 […]

    Like

  111. HERI YA X-MA NA NEW YEAR WAPENZI WOTE WA BLOG HII, KWELI MWAKA MPYA NA MAMBO MAPYA.

    Natumaini wote tumesalimika kwa kuwezo wake Mwenyezi Mungu. Namshukuru sana kaka Simbadeo kwa wazo lake na wadau wengine wote mlio changia mada. Nimefurahi sana nami naunga mkono hoja na mawazo yenu ya kwamba tusubiri kabisa mwezi huu wa kwanza upite, then February ndo tupange tarehe ya kukutana. Ni wazo zuri sana nasi tunaosua sua tuzidi kuelimika zaidi, wakati tunaandaa mabanda ya kufugia. Jumamosi ni siku nzuri sana naiunga mkono.

    MUNGU ATUBARIKI SANA, NA AIBARIKI BROG HII.

    Like

    Judy

    January 4, 2011 at 2:46 pm

  112. jamani sahamahani kwa kupotea siku nyingi,,
    na mimi nitafurahi tukiweza kutemebeleana na tukaanzia kwa dada Fatuma

    Like

    mwemezi

    January 9, 2011 at 10:27 am

  113. ‘HERI YA MWAKA MPYA WADAU’

    Hilo ni wazo zuri tunaliunga mkono. Tutapata mengi ya kujadili baada ya hapo na kwa kufanya hivyo tutasaidiana sana. Tukitoka kwa da Jenny nitawakaribisha na kwangu.

    Like

    Elizabeth

    January 10, 2011 at 10:25 am

  114. Dada Jenny,
    Hivi shamba lako liko sehemu gani nafikiria kipindi cha sikukuu ya Mapinduzi niweze kupita shambani kwako kuja kuangalia na wife wangu ambaye yeye ndiye mjasiriamali mi napiga support tu. Ahsante

    Like

    Nassib

    January 10, 2011 at 12:30 pm

  115. Habari za siku ndugu zangu wapendwa kwa jina la Bwana
    Kaka Mwemezi nashukuru sana kunipendekeza tuanzie kwangu ila tunaanzia kwa da Jenny tukitoka hapo tunakwenda kwa da Elizabeth labda baada ya hapo mtakuja kwangu. Nawatakia mchana mwema wote.

    Like

    Fatma

    January 17, 2011 at 7:50 am

  116. heri ya mwaka mpya rum jmn nawaonea tamaa sana na shamba class natamani nami niwepo ila mnaniamasisha nianze kufuga na dar japo naogopa kwani napenda kufuga nami niwepo da jenny vp kuku wa malawi nami nimesikia ni wazuri kuna kaka tazara agent ninamawasiliano nae anao je ni wazuri jamani shamba darasa karibuni na geita kila la kheri 2011

    Like

    da mariam

    January 18, 2011 at 6:00 pm

  117. Hello Da Mariam,

    Kuku wa Malawi kwa kuwaangalia ni wazuri, wana umbo kubwa kidogo kuliko wa kwetu tuliozoea, ni kuku wa kienyeji na mm focus yangu kubwa ni kurudia ufugaji wa kuku wa kienyeji ambao kusema ukweli ndio nilianza nao kabla ya kuuza kuku wote na kuhamia wa mayai.

    Naona majogoo wao wameanza kung’ara manyoya ya mkiani na mgongoni, ni weusi na macho yao meusi kabisa. Nasikia wanaanza kutaga wakiwa na miezi 4 na nusu hadi 5. Tunawatarajia wataanza kutaga mwezi wa 2 watakapofikisha miezi 4 na nusu hadi 5 maana sasa wana miezi karibu 4. Wenzao kundi linalofuata wana wiki 6 na hao pia karibu nitawaachia nje wakifikisha wiki 8.

    Hadi watakapoanza kutaga ndipo nitaweza kutoa maelezo vizuri kama ni wazuri ama vipi maana uzuri wa hawa mifugo wetu unategemea na kama wanataga mayai mengi muda mrefu, wanaishi sana na kama wana nyama nyingi, hawaugui ovyo kwa wale wa kuuza kwa ajili ya nyama.

    Kaka Nassibu samahan sikukujibu. Mimi binafsi siishi shambani, kuna watu wanaokaa kule na sio kwenye barabara kuu, ni ndani ndani kidogo ambapo kwenda ingebidi twende pamoja. Nadhani utakuwepo na mkeo siku ya kutembelea wote tupate kujifunza. Karibuni.

    Like

    jenny

    January 19, 2011 at 7:56 am

  118. DadA jenny
    Nashkuru kwa kunijibu. Nadhani sasa ni wakti muafaka kwa kwenda huko kwani kama wengi walivyotoa ushauri wa kususbirir pilika za watoto shule kwisha ndio tupange kukutembelea. Nashauri wandugu wote wa blogg hii tubaliane lini ili tumtembelee ndugu Jenny

    Like

    Nassib

    January 20, 2011 at 7:48 am

  119. ndugu zangu. kwa siku kadhaa nimekuwa nikifuatilia website hii na nimevutiwa nayo sana.

    mimi kwa upande wangu nimejikita zaidi kwenye kilimo.. na nina marafiki wengi JAMiiforums. nimesoma kwenye Jamiiforums na kuona kwamba kutakuwa na mkutano wa kujadili masuala ya kilimo (fursa za uwekezaji na wenye uzoefu kutoa mada). itakuwa 5 February 2011 Dar es salaam.

    kwa yeyote aliye interested naomba tuwasiliane nitam-link na waandaaji nat867@gmaio.com

    Like

    mwemezi

    January 23, 2011 at 12:38 pm

  120. ndugu zangu. kwa siku kadhaa nimekuwa nikifuatilia website hii na nimevutiwa nayo sana.

    mimi kwa upande wangu nimejikita zaidi kwenye kilimo.. na nina marafiki wengi JAMiiforums. nimesoma kwenye Jamiiforums na kuona kwamba kutakuwa na mkutano wa kujadili masuala ya kilimo (fursa za uwekezaji na wenye uzoefu kutoa mada). itakuwa 5 February 2011 Dar es salaam.

    kwa yeyote aliye interested naomba tuwasiliane nitam-link na waandaaji nat867@gmail.com

    Like

    mwemezi

    January 23, 2011 at 12:38 pm

  121. jamani habari za siku naomba msaada kwa wote huku kwetu shamba kupata vifaranga ni tabu sana unaweza kukaa hata 7 month bila kupata na kapesa kako kanahodhiwa na mleta kuku nia yangu nami nianze uagent ila sijui vizuri vifaranga wa kampuni gani ni wazuri yani wanahimili kwani kuna mtu analeta wa interchic weusi wanakufa sana hivyo wateja wanatafuta njia nyingine nikasema niulize ili nianze mie nilijaribu kutafuta kwa mtandaon nikawapata wanaitwa tz potryl farm sijajua vizuri ubora wa vifaranga vyao naomba ushauri mawazo wadau
    thx all

    Like

    da mariam

    January 31, 2011 at 1:58 pm

  122. Habari za siku wandugu?

    Kuna comments nimeona zimeongezeka, lakini hapa sizioni. Ziko upande gani? Rachel naona umeandika lakini sioni comments zako. Kunitembelea naomba ujiandae kuja na kundi la hao watu wengine wote ambao tutaingia kwa darasa amoja kujifunza. Kukuuzia vifaranga sio rahisi, kama umesoma comments zetu hapa utagundua mimi ni mfugaji mdogo, sina kuku wengi kwa sasa. Ila maelekezo ya mahali pa kununulia kuku utapata. Mimi wa mayai huchukulia Interchick.

    Da’Mariam nadhani ni vizuri ukanunua mashine ya kutotoleshea hata kama itakuwa ndogo utotoleshe mwenyewe. Endapo mfuko unakuruhusu, wapo watu wanazitengeneza kubwa za umeme.

    Like

    jenny

    February 7, 2011 at 8:37 am

    • Dada Jenny asante saana kwa maelezo yako, na mimi nashangaa niliandika lakini sioni nilicho post, asante kwa kujibu baadhi ya maswali niliyo uliza, sikuweza kuja na watu ulioniambia kwasababu flani flani hivi, lakini nahisi hakija haribika kitu, nita join msafara ujao

      mengine niliyo uliza ni kwamba,
      1. Je ni lazima saana kuanza kwa vifaranga? au naweza kuchukua walio kua kua kidogo

      2. Je banda la kuku wa mayai linatakiwa liweje? maana mimi la kwangu nilishauriwa kuweka simenti nikaweka, na pia niweke randa za mbao, sasa hapo kwenye randa je nikweli? maana huyo mtu kama simwamini hivi,na je nikiweka hizo randa, kuhusu kulisafisha banda itabidi niwe na weka kila mara au inakuaje,

      3. Je nikisha leta hao kuku au vifaranga kwenye banda, natakiwa niwape chanjo au ni mpaka nitakapo ona dalili za ugonjwa,

      4. Je kwa vifaranga wadogo ni lazima taa?

      samahanini kwa maswali yangu kama hayatowafurahisha kwa njia moja ama nyingine, nahitaji tu kujua maana nilikua nafuga kuku wakienyeji lakini sasa nataka kufuga wa kisasa wa mayai,

      Ninachohitaji hasa ni hatua zile za kwanza kabisa katika kuwa fuga hawa kuku wa kisasa, maana nimesoma comments za watu hum ni nzuri na zitanifaa saana kwa baadae nikishaanza lakini sijaona comments zinazozungumzia mwanzo mtu afanyeje, sorry kama nitakua nje ya mada.

      Like

      Rachel

      February 7, 2011 at 4:43 pm

  123. Habari za hapa kwa wote jamani nilikuwa pembeni kidogo kwa maswala ya kijamii, haya mnaendeleaje na ujasiriamali vipi da Jenny unaendeleaje na ufugaji na kujitayarisha na shsmba darasa. Kwani ni lini mmepanga tuje kwako da Jenny?. Naomba unihabarishe ili niweze kujiandaa na safari.

    Like

    Fatma

    February 8, 2011 at 7:34 am

  124. Nitakujibu kulingana na uzoefu wangu, lakini naamini wapo watu wazoefu zaidi na wanaoelewa zaidi hapa ukumbini, watakapopatikana watakusaidia zaidi.

    1. Ni vizuri sana uanze na vifaranga hasa kwenye shamba lako jipya kwa sababu hutakuwa na magonjwa ya kuhamia shambani kwako. Hiyo ndiyo sababu yangu kubwa ya mimi kupendelea vifaranga. Hujui unakotoa kuku wakubwa kulikuwa na magonjwa gani na magonjwa mengine ya kuku hayana tiba hivyo utakuwa umeyaleta mwenyewe shambani. Niliwahi kununua kuku sokoni na kuwaleta nyumbani wakati naanza kufuga nikiwachanganya na wale wachache sana niliokuwa nao, magonjwa ya hao kuku wa sokoni mengine yananisumbua hadi leo hayajaondoka kabisa. Pia waliokua kua kidogo kama unavyosema gharama yao ni kubwa kuliko vifaranga wa siku 1.

    2. Vifaranga wa siku moja wanahitaji uangalifu wa karibu zaidi. Wanahitaji joto la kutosha kwa vile hawana mama yao wa kuwafunika chini ya mwili wake wapate joto. Wanahitaji maji safi, chakula kipo kinaitwa starter japo mimi huanza na growers moja kwa moja. Maelezo mengine nadhani ni vizuri upate wataalam wa mifugo ama uhudhurie hilo shamba darasa ama kwa wafugaji wakubwa ambao wanakuwa na vifaranga ili ujifunze kwa vitendo. Vifaranga wa siku 1 siweki maranda kwa sababu bunch iliyopita dada wa shamba alikosea (aliona ameshakuwa mzoefu) akaweka maranda, matokeo vifaranga walipatwa mafua wakiwa na siku 3 tu! na tulipoteza karibu 14 hivi kwa mafua. Maelekezo ni mengi kidogo.

    3. Vifaranga wadogo wa siku 1 na kuendelea hata kuku wakubwa wanazo chanjo. Wasiliana na wataalam wa mifugo kwa maelekezo.

    4. Vifaranga wadogo taa ni muhimu kwa vile zinawapatia joto linalotakiwa na utakuwa ukizipandisha juu kila baada ya wiki moja moja kupunguza makali ya joto lake kulingana na mahitaji. Kama ni taa za umeme zipo za 200 Watt zina joto sana na kama utatumia taa za chemli uongeze na mkaa pia.

    Maswali yako ni mazuri na hapa tunaulizana chochote tusichoelewa ilmradi kinahusu mifugo hasa ndege haijalishi topic inahusu nini.

    Ushauri wangu wa mwisho, usianze hadi umepata msaada wa kitaalam au kutoka kwa wafugaji wenzako waliopiga hatua kukusaidia kuanza maana vifaranga wa kisasa wako delicate kuliko wa kienyeji japo matunzo yao ni sawa tu wanapokuwa wadogo. Karibu sana.

    Da Mariam, habari za siku? Shamba darasa bado, watu hawajapanga sijui pilika pilika zimezidi? Likiwa limekubalika ni lini utaarifiwa kupitia hapa ama Kaka Deo atakuhabarisha.

    Nawatakia kazi njema, pale nilipopungua maelekezo wengine watakusaidia nami napenda sana kufuatilia hayo maelezo ya ziada.

    Like

    jenny

    February 8, 2011 at 7:53 am

    • asante saana Jenny, yaani umenifungua sana kwa hatua za mwanzo hizi umenielewesha saana. nimeshajua kwamba kuanza unapaswa kununua vifaranga na kuwaweka bandani nakuwapa chanjo……

      maswali ya mwisho Da Jenny,au yeyote yule
      – Je hilo jiko la mkaa hawa wezi kurukia kweli na kuungua au naweka juu ya kitu flani.

      – Je taa na jiko kuweka ni usiku tu, au 24hrs lazima viwe on?

      -Na je nikiamua kuweka taa nyingi zaidi nikaacha jiko ni vibaya? maana banda langu sio kubwa saana saana ni la kiasi tu, nahisi kama naogopa kuweka jiko la mkaa

      jamani msichoke kwa maswali yangu, nawapenda wote nakuwa takia mafanikio katika ujasilia mali wenu kokote mliko

      Like

      Rachel

      February 8, 2011 at 3:37 pm

  125. karibu rachel jiko ni zuri pia chemli kwa kupunguza gharama ya umeme mara nyingi mi huwa naweka kitu chini hawlifikii pia mkaa unatakiwa uwe umekolea mpk uwe mwekundu kwani gesi ya mkaa sio nzuri nkkuhusu taa kwa huku kwetu tunaweka 24 hrs kwani ni baridi pia vifaranga vinakula 24hrskwani wapo wajanja wanaokula haraka wakakaa pembeni pia wazembe kuweka taa nyingi si vibaya ili bei ya umeme iko juu ni mfuko wako tu hayo ni yangu wengine watakushauri zaidi

    Like

    da mariam

    February 8, 2011 at 7:12 pm

  126. Jiko la mkaa hawawezi kurukia kwa juu, wanakuwa wadogo sana bado hawana mabawa. Lakini mlango wake ufungwe kwa sababu wanaingia, bado hawana akili kutofautisha hatari.

    Taa na majiko ni 24hrs hadi watakapoanza kufunika manyoya.

    Sio rahisi taa pekee za chemli zifanye kazi ya kuleta joto linalotakiwa sawasawa, pia kumbuka chemli zinatoa moshi fulani kwa juu sidhani kama ukizidi ni mzuri. Kama alivyosema Da’MAriam, mkaa pia unatakiwa uwe umewaka kwanza nje na kuwa mwekundu ndo uweke jiko kwa vifaranga baada ya moshi moshi wa mkaa kuondoka.

    Kwa msaada zaidi:

    Instructions.Things You’ll Need:
    a draft free location safe from predators.
    a source of heat(such as a heat lamp)
    a thermometer (optional)
    sand and grit
    a chick waterer
    chick starter (food)
    a chick feeder.
    chicks
    1.1
    First priority in brooding your chicks is to provide them with a safe draft free location in which to grow that is safe from predators. Ideally this location is circular and without corners. The size of this area depends on how many chicks you have. For as few as twenty-five chicks, a tub covered with a metal mesh may be adequate at least initially but never try to raise your chicks in the house because the chicks create a dust that can be harmful to you and your family. Be sure there is no way for the chicks to escape or any other animal can get into the pen.

    2.2
    The next item to consider is the heat source. Be sure that your heat source is adequate but not too intense because you don’t want to roast your little birds. I use a heat lamp with a 100 watt bulb to keep 25 or so chicks warm. If you are using a thermometer, the temperature should be close to 90 degrees to begin with gradually decreasing the temperature over the next month until the chicks no longer need the heat. The best way I have found to be sure the temperature is right for the chicks is to listen to them. If they are peeping loudly and are huddled under the lamp, they are too cold and you need to get the heat lamp closer to them. If they are trying to get away from the heat lamp, the lamp is too close and putting more distance between the lamp and the chicks thus lowering the temperature in the pen.

    3.3
    Once you have the pen ready and the heat source in place, pour some sand and grit at the bottom of the pen to line the pen. Some people use newspaper to line the floor of the pen but chicks naturally scratch so they have a tendency to scratch up newspapers. Chicks need grit at the bottom of the pen because they need grit to help them digest their food. With just a few chicks, you can buy the same grit they use for parakeets.

    4.4
    The next item needed to prepare for the arrival of your chicks is a waterer. The waterer I use for very young chicks is a round plastic dish that fits to an inverted mason jar that is filled with water. You can buy one of these from the local animal feed store. The water used should be warm, about 90 degrees to prevent chicks from getting chilled from drinking the water.

    5.5
    The next thing needed for the chicks is the feeder. I buy my feed from the local animal feed store. When you ask for the chicken feed they will ask you what kind. Tell them you want either chick starter or chick crumbles. They will then ask you if you want medicated or unmedicated. For chicks, the choice is yours. For me, when I buy chicks from a hatchery, I use one bag of medicated then switch to unmedicated. when I incubate my own chicks, I ask for unmedicated exclusively. I don’t want to be exposed to any more chemicals than I have to be. When I get the chick food home, I put the feed in a small chick feeder. I have two different sized feeders that I use as the chicks grow. I have used screw top jar lids to start and then switched to paper egg cartons with the tops cut so that the chicks couldn’t scratch in the food. Like I said before, the chicks like to scratch. If using egg cartons for feeder, don’t use Styrofoam because the chicks will peck the Styrofoam and that isn’t good for the chicks.

    6.6
    When the chicks arrive, gently place them into the pen and watch them. Introduce them to the waterer by dipping their beaks into the water. Make sure only to wet the beaks and not the feathers. Chicks are easily chilled. The chicks will figure out how to eat on their own.

    7.7
    Now that the chicks are in their new home and you are sure they are drinking and eating and staying warm, keep an eye on them and keep their food and water clean. They are dependent on you to make sure they have a long and birdie life.

    NB: Mchanga huwa siweki, wanaula. Natumia majani makavu yaliyokatwa katwa na magazeti kwa siku za mwanzo sana, wakishafikisha kama wiki 1 hivi wakaweza kutofautisha chakula na takataka ndio naweka maranda lakini baada ya kuyaanika tena juani na kuhakikisha ni masafi na hayana vumbi vumbi.

    All the best!

    Like

    jenny

    February 9, 2011 at 8:22 am

  127. Jamani poleni na harakati za maendeleo.

    Da Jenny, vifaranga wa Interchick utagaji wake ukoje percentagewise kama unawatunza vizuri? Namaanisha kwa mfano una kuku mia unapata mayai mangapi kwa siku.

    Hapa nina kipeperushi cha Tanzania Poultry Farm kilichoandaliwa kwa kiswahili ningewatumia wale wanaoanza kufuga kitawapa mwanga lakini nashindwa ku-attach, anayejua anieleweshe.

    Like

    Elizabeth

    February 9, 2011 at 11:42 am

  128. Kipeperushi hiki kinanisaidia sana kwani hata vijana wa shamba huwa nawatolea copy nawapa wanasoma wenyewe. Kimeonyesha na mpangilio wa chanjo kiasi kwamba mimi nikijisahau wananikumbusha.

    Like

    Elizabeth

    February 9, 2011 at 11:52 am

  129. Hello Elizabeth,

    Kipeperushi mtumie kaka Deo atatumuvuzishia. Asante.

    Hao kuku wa Interchick upande wangu niliwaona ni wazuri, natarajia kulipia wengine wiki hii hapo hapo. Nilinunua kuku 100 nikapewa 102, vikafa 2 nikabakiwa na 100. Siku ya kuwahamisha toka nyumbani kwenda shamba kulifanyika uzembe wakafa 2 wakabaki 98. Hao 98 walikuwa wanataga hadi 96, 92, 88 kabla hawajashuka baada ya miezi 7 ya kutaga (inaitwa molting period). Waliposhuka walishuka hadi mayai 10 kwa siku, kwa sasa wameanza kuongezeka tena na tunapata 40+ kwa siku. Kw asasa wapo 86 tu. Watakapoongezeka kutaga sina hakika kama watataga kama awali kwa sababu taarifa nilizosoma kwenye tafiti zinasema wakianza tena kutaga hawatagi kama awali. Ndo najifunza, labda mwingine anayechukulia pia Interchick ataelezea zaidi.

    Like

    jenny

    February 9, 2011 at 1:41 pm

    • Wadau, Da Jenny, Da Eliza, Da Mariam, Da Rachel. Nawashukuru kwa maswali na michango mbalimbali ambayo umekuwa mkiivurumisha hapa jukwaani. Nimetingwa kidogo, lakini tuko pamoja. Da Eliza, waweza kunitumia hicho kipeperushi ili niwawekee hapa wadau, naamini watafaidika nacho sana. Au waweza kunipigia 0754 488916 nitakuelekeza namna ya kufanya attachment kwenye email. Au nikipata muda nitakuandikia email na maelekezo namna ya kuattach. Asanteni na tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      February 10, 2011 at 10:27 am

  130. Ahsante Kaka Deo, nimeishakutumia kwenye email yako kama attachment, bila shaka utaiona.

    Da- Jenny nashukuru kwa maelezo hapo juu, naona ni wazuri labda hiyo molting ya kwenda mpaka 10% ndo imenitisha kidogo. Sijui imewachukua muda gani mpaka kurudi kwenye production hiyo ya 40%+? Mimi nilionao ni wa Tanzania Poultry Farm Arusha, wanaendelea vizuri ila 90% production sijawahi kuifikia. Ninataka kujaribu na wengine.

    Like

    Elizabeth

    February 11, 2011 at 10:11 am

  131. Da Eliza,

    Kutoka kwenye 10% imewachukua wiki 6 kuanza tena kurudia uzalishaji ambao kwa sasa wamefikisha 40%. Mimi natafuta layers wekundu, nisaidieni niwapate wapi maana naona kote waliopo sasa ni weusi tu. Asanteni.

    Like

    jenny

    February 11, 2011 at 11:16 am

  132. Da Jenny, Da Eliza,na wengine woote jamani yaani ninawashukuru saana kwa maelezo yenu, kesho naenda kuweka oda na mimi interchick, kujaribu si kushindwa japo kuna watu mtaani wanakatisha tamaa jamani, mh, lakini Mungu naamini atanisaidia tu, kwasababu mimi nawiwa moyoni kufanya na ninaona nitafanikiwa tu, asanteni saana kwa mchango wenu wakunielekeza hatua za mwanzo za ufugaji huu,

    natumaini tutaendelea kuwasiliana hapa na kufundishana zaidi na zaidi. kumbe mwanzo naweka magazeti sikujua nilifikiri nawaweka tu na simenti hivyo hivyo,

    shukrani saana nasubiri tu hicho kipeperushi kwa maelezo zaidi,

    naamini na mimi nitakua kama Da Jenny hata zaidi na mimi niwe nawa elekeza watu hahahah, ili nijue zaidi

    Like

    Rachel

    February 11, 2011 at 4:00 pm

  133. Jenny, unamaanisha kama wale uliotutumia kwenye picha? Mimi ninao kama hao nachukua Tanzania Poultry Farm. Ni wazuri ila inabidi uweke order mapema, Uzuri wao unaweka order mapema lakini unalipia mwezi mmoja kabla. Juzi nimechukua batch ya pili ya vifaranga 1,500, order niliweka December 2010 mwanzoni nakulipia January 2011 mwanzoni. Kama ni hao unaowataka nitakupa contacts za offisi zao hapa Dar es Salaam ili uende uweke order.

    Like

    Elizabeth

    February 11, 2011 at 4:45 pm

  134. wandugu wote
    Nawashukuru kwa michango mikubwa amabayo wadau tunaipata katika blogg hii. Mi napenda tu kuchangia kwamba vifaranga sio lazima kuwaweka katika jiko la mkaa ila unaweza kuchukua sufuria ukaweka mkaa wako uliokuwa mwekundu usiwe na moshi ukawawekea katika tofali ambalo haliwezi kuiangusha sufuria yako na ukaiweka katikati kawani itakuwa inatoa joto kila mahali unajua sufuria inatoa joto kila pande hivyp vifaranga wanafurahia hali hiyo kama joto ni kali utawaona wansogea wenyewe mbali kujiadjust na joto lililopo ; naona ni njia nzuri kuliko kuweka jiko la mkaa halina joto sna au jotop lake linaenda juu tu siyo kama sufuria inatambaa hirizontally, Sie huwa tunafanya hivyo na vifaranga wanfurahia hali hiyo. Jamani darasa lini dada Jenny? Pia swali kwamba kuku wa mayai kadiri anavyotaga basi utagaji hupungua siku hadi siku?

    Like

    Nassib

    February 14, 2011 at 10:48 am

  135. Kaka Nassib, nakubaliana nawewe kabisa. Mimi natumiaga taa za watts 200, ila weekend hii mimi nimeteseka na vifaranga kwasababu umeme umekatika kama siku mbili mfululizo. Vifaranga wana siku tatu tu. Nimeweka majiko nikaona bado wanatetemeka. Tukatumia masufuria ndo ikawa nafuu na mpaka sasa ndo tunayatumia. Mawazo ya kuweka tofari nilikuwa sijapata, sasa nawambia waweke matofari au mawe. Ahsante sana kwa ushauri huo.

    ‘Kilimo Kwanza Oyeee’

    Like

    Elizabeth

    February 14, 2011 at 12:02 pm

  136. kaka kasim na wengine wote,

    jamani yaani nimefurahi kusikia ishu ya sufuria maana nilikua napiga hesabu jiko la mkaa tena kupikia hilo hilo hahah, lakini kweli ishu ya sufuria ni poa saana, tena nitatafuta la bati nyepesi ndo linashika joto haraka.

    nina swali leo bakumbuka dada jenny ulisha jibu lakini nahisi nahitaji ufafanuzi zaidi,

    Vifaranga wadogo dada Jenny ulisema unaweka magazeti,
    sasa unayatandaza chini au? samahani jamani sikuelewa vizuri

    na je dirishani tunaweka nini? maana banda langu lina space ya madirisha makubwa mawili sasa nauliza hapo naziba au vipi, maana huwa kuna upepo saana vumbi isije kuathiri labda, lakini dirisha hizo zina nyavu, so wapendwa nielewesheni.

    Na magazeti hayo nitandaze chini kwa muda gani? na nikitoa nini kifuatie kuweka ambacho hakita athiri vifaranga?

    Asanteni saana kwa kuendelea kunivumilia na maswali yangu maana yanaweza kuwakera to some point lakini ni vile tu ninaanza so nakuwa namaswali saana

    Like

    Rachel

    February 14, 2011 at 3:03 pm

  137. habari rum naona mabo yanazidi kuwa bambam nami nategemea kuingiza wajukuu wiki ijayo na huu mgao unanichanganya kabisa kwan kwetu umezidi ila nitajitahidi majiko pia ntaweka hayo hayo machcemli kuhusu kuku wekundu nasikia habari zisizo rasmi kuwa tz imezuia vifaranga toka kenya ndo hali hiyo ila mi ntawapata hao pia da jane nipigie kwa namba hii 0713549140 au 0769549140 nikupe namba ya kaka anaewaleta hao kama bado analeta

    Like

    da mariam

    February 14, 2011 at 3:10 pm

  138. Hello Wandugu,

    Nawashukuru sana kwa ushauri wenu hasa wa masufuria bunch ijayo nitaujaribu. Hapa panatufaa sana kujifunza, hakuna ajuaye sana kuliko mwingine.

    Magazeti huwa tunatanguliza chini kabisa halafu majani makavu yaliyokatwa katwa saizi ya toothpick 2 ukiziunga, saizi ambayo vifaranga hawawezi kula. Tunabadili kila yanapochafuka ama kuloa, vifaranga wanahitaji kuwa sehemu kavu na si sehemu iliyoloa na pia kukiwa na kinyesi chao kingi maana hawajatofautisha chakula na mavi yao wanakula kila kinachoweza kupita mdomoni kwao. Wakishaanza kukimbia kwa spidi wakichangamka tunaongeza majani zaidi ili wasiteleze kwenye magazeti. Magazeti ukitumia utumie yasiyoteleza kwa sababu wakiteleza miguu hupitiliza wakateguka nyonga.

    Vifaranga nimepata Buguruni, nimeweka order tayari nitawapata wiki ijayo. Da, Mariam asante kwa namba zako nitawasiliana na wewe.

    Shamba darasa watu wamekaa kimya, sijui bado wako bize? Mimi niko tayari wakati wowote baada ya Januari.

    Asanteni sana kwa mafundisho.

    Like

    jenny

    February 15, 2011 at 11:18 am

    • Asante wote kwa comments zenu,

      kwasasa nime elimika vya kutosha kwa kuanza naweza sasa,

      ila tu nachanganyikiwa kila mtu ana nadi sehem aliyo nunulia vifaranga wake kuwa ni pazuri, mpaka nachanganyikiwa nikanunue wapi, maana kote kote wazuri

      nitapita kote nione then nitachagua pa kwenda lakini si mbaya kama mkinishauri,

      Like

      Rachel

      February 15, 2011 at 2:36 pm

  139. Da Mariamu kuhusu vifaranga nimeona bango kule kwetu Ukonga limeandikwa tunauza vifaranga vya nyama na vya mayai kutoka Mwanza siku moja nikapita pale na kuchukua namba, nikafanya mawasiliano nao mimi nilidhani ni vya kienyeji wakaniambia ni vya nyama na mayai. Nafikiri ungefanya utaratibu wa kuasiliana nao labda utaweza kupata kwa urahisina mimi nitafanya taratibu nikupatie namba zao.

    Like

    Fatma

    February 15, 2011 at 3:01 pm

  140. Da Jenny za siku nyingi mimi mwenzio nina msiba wa kuku wangu kwani hapa juzi kati nilipata safari ya ghafla kikazi nikawa sipo kwa wiki mbili nimerudi kuku wangu wote wamekufa wale tuliochukua pamoja hivi naugulia machungu kwanza na hata kwenye blog naona tabu kuingia. Kijana alizembea kwa makusudi alikuwa hawapi maji wala chakula nilimuweka ndani siku tano ili angalau nipunguze machungu lakini wapi mwisho nimemfukuza. Hivi sasa ninajipanga tena kama nitaweza.

    Like

    Fatma

    February 15, 2011 at 3:05 pm

  141. Wandugu,
    Kwanza nampa pole Bi Fatma kwa kupoteza kuku wake. Kwa ushauri tu tusiwaamini wafnyakazi hata sekunde moja kwani walio wengi hawana uchungu, Kwa kweli hata kama una mfanayakazi ni vyema na wewe ukapitia kucheki nini wanafanya maana wanaweza kukupa ugonjwa wa moyo kama dada yetu Fatma. Sio wa kweli kabisaaa. Kwa hiyo biashara ya kuku kama huna mtu wa kazi basi ussifanye maana utalia. Bahati mabay kama fatama kupata safari ndio inakuwa hakuna budi umwamini ila tu kila mara laziam tu countercheck wanavyfanya kazi zao haswa kwa wale wa mama wa nyumbani. Wafanyakazi walio wengi hawajali hata kidogo. Pole Da Fatma

    Like

    Nassib

    February 15, 2011 at 3:18 pm

  142. Asante sana kaka Nassib mimi huwa ni mwangalifu sana ila sikuwa na jinsi kwani ilibidi niende tu hiyo safari ndio maana yakatokea hayo yaliyotokea hata hivyo nashukuru sana kwa kunifariji. Pia nitazingatia hayo uliyonieleza pia kwa wengine watajifunza

    Like

    Fatma

    February 15, 2011 at 3:25 pm

    • Wadau wote. Nawashukuru kwa maarifa mnayoendelea kushirikishana na wengine. Ni jambo la maana sana.

      Natoa pole nyingi kwa Da Fatma kwa masaibu yaliyomkuta katika biashara yake ya ufugaji. Ama kwa hakika, kama alivyosema Kaka Nassib, maadili ya wafanyakazi wetu katika maeneo mbalimbali ni changamoto kubwa. Kikubwa ni kuona namna gani tunaweza pia kukuza maadili ya vijana wetu ili nao wawekeze katika uaminifu ili kuongeza tija na hivyo hata wao kipato chao kuongezeka.

      Kuhusu shamba darasa. Hapa naomba tubadilishane mawazo zaidi. Mimi nitaanza kwa kueleza machache.

      1. Tunahitaji sana shamba darasa ili kwamba tupate kujifunza kwa marefu na mapana kuhusu biashara hii ya ufugaji. Ili tufanikiwe hatuna budi kujiandaa kikamilifu – kwani siku hiyo haina budi kuwa ya kujifunza kwelikweli.

      2. Najaribu kufikiri namna ya kuhusisha wadau zaidi – mfano – Interchick – ili tupate wataalamu katika siku hiyo tunaoweza kubadilishana nao mawazo kwa njia ya maswali na ushauri. Kupata watu hao – kama tunavyofahamu ni kazi – wako bize kwelikweli.

      Kwa hiyo, pengine tushauriane kuhusu mahitaji yetu ya siku hiyo – kwa maana ya kwamba tunahitaji kujifunza nini hasa, je, wataalamu tuwatoe wapi, je, tutembelee mashamba mangapi n.k.

      Nakaribisha fikra zaidi na vilevile mapendekezo ya siku tunayoweza kufanya hiyo shamba darasa. Karibuni.

      Mtaniwia radhi, mara nyingine uingiaji mtandaoni unakuwa wa kusuasua … mdudu bize mbaya sana …

      Like

      simbadeo

      February 15, 2011 at 11:24 pm

  143. Habari zenu wadau wote, Kwanza nawapeni pole sana na janga lililotupata la mabomu Gongolamboto, hasa ndugu zetu wanaoishi huko na wale walio karibu, vipi dada yetu Jenny wa Kinyerezi umesalimika? na mifugo je poleni sana sana. Pia nampa pole dada Fatma, kweli inatia uchungu sana, unajua ukiwa na mtu asiyejua uchungu wa pesa inauma sana na hasa kwa uzembe wa kutowapa kuku chakula, bora ingekuwa ugonjwa lakini chakula wakati kipo inauma sana.
    Mimi bado nasua sua kuanza kwa kuofia hilo ndiyo maana bado naweka mipango vizuri ili nipate uhakika wa mimi kupata muda wa kutosha kuhudumia kuku wangu kwa asilimia kubwa.

    Like

    Judy

    February 19, 2011 at 1:08 pm

  144. Kaka Simbadeo mimi naomba nichangie kwa sie ambao tunajiandaa kufuga, ningependa kama tungejifunza maandalizi ya banda jinsi ya kuandaa kuanzia kujenga mpaka unapoweka vifaranga banda liweje, chakula unachotakiwa kuwa nacho na chanjo zote kuanzia unapoleta kuku siku ya kwanza mpaka wanapoanza kutaga, utunzaji wa kumbukumbu zote, jinsi ya kutafuta soko. mengine nitazidi kuchangia jinsi nitakavyo kuwa nakumbuka. Natumaini na wadau wengine watazidi kutoa mawazo yao. Nawatakia weekend njema.
    JAMANI TUSISITE KUFAHAMISHA KAMA KUNA WADAU WALIOKUMBWA NA MAAFA HAYO, KWA HIVI SASA SISI NI NDUGU MOJA

    Like

    Judy

    February 19, 2011 at 1:15 pm

  145. Tunashukuru mungu katunusuru. Wa Kinyerezi ni mimi Eliza sio Jenny. Mifugo tuliitelekeze kwa muda lakini mungu bariki tulikuta bado iko hai. Kaka Simba, nilikutumia kipeperushi, je ulikipata?

    Like

    Elizabeth

    February 21, 2011 at 4:20 pm

    • Wadau wote … napenda kuungana na waliotangulia kutoa pole kwa wote walioguswa kwa namna moja au nyingine na janga la mabomu ya Gongo la Mboto. Kama ilivyokwishasemwa na Serikali … ni janga la kitaifa … limetusibu wote kila mmoja kwa namna yake. Tunasikitika sana kwa wale waliopoteza uhai wao … na kwa wale waliopoteza ndugu, jamaa, watoto, marafiki, majirani na wengine wanaowahusu. Tuchukue mioyo ya ujasiri katika kipindi hiki na kuhakikisha kwamba tunakivuka na kuvuka simanzi zetu ili maisha yaendelee na pengine kwa namna ambayo itazuia kujirudia kwa hali kama hii au inayofanana na hii… Kila mmoja wetu ana wajibu. Niwakaribishe tena kuendelea na tafakari na michango ambayo tumekuwa tukitoa na kubadilishana katika jukwaa hili. Mwenyezi Mungu atuongoze na kutulinda sote na Taifa letu. Amina.

      Like

      simbadeo

      February 21, 2011 at 5:01 pm

  146. Ohoo Da Eliza Poleni sana mi nawachanganya, Mungu mkubwa jamani. nami nakisubiri kwani nilivutiwa na maelezo uliyotoa juu ya hicho kipeperushi. Nawatakia siku njema Mwenyezi Mungu azidi kutusimamia sote.

    Like

    Judy

    February 21, 2011 at 4:32 pm

  147. Kaka Simbadeo,
    nawapa pole kwa mabomu na pia nafarijika na michango mizuri kuhusu fugaji, Bado naona hujatupatia hicho kipeperushi. tWAKISUBIRIA

    Like

    Nassib

    February 22, 2011 at 8:29 am

    • Hi Ndugu Nassib na wadau wengine, nimemwomba Da Eliza anitumie upya kipeperushi hicho ili niwafikishie wadau hapa. Kwenye email yangu sikukiona, inawezekana kiliingia kwenye spam na hivyo kuwa deleted. Naomba tuvute subira tunapofanya mawasiliano. Asante kwa kukumbushia.

      Like

      simbadeo

      February 22, 2011 at 9:50 am

      • Ndugu Nassib na wadau wote katika ufugaji kuku … nimepata kipeperushi kutoka kwa Da Eliza … nami nimekiweka ubaoni kwa manufaa ya wote. Asante sana Da Eliza kwa kipeperushi, naamini kitawasaidia wadau hapa pamoja na wengineo katika jamii yetu. Tuendelee kubadilishana fikra.

        Like

        simbadeo

        February 22, 2011 at 11:46 am

  148. tunashkuru kwa kipeperushi kina mafunzo makubwa ya ufugaji

    Like

    Nassib

    February 22, 2011 at 4:02 pm

  149. Hello ukumbini,

    Da Eliza asante kwa kipeperushi. Da Fatma POLE ya herufi kubwa maana yaliyokupata kwa mifugo yako yanasikitisha. Sielewi watu wengine wameumbwaje kuwaangalia wanyama wakifa kwa kiu na njaa wakati chakula cha kuwapa anacho. Inatia uchungu kweli. Wao hawasahau kula hata siku moja… Kanga walipona au wapo? Wa kwangu wanaendelea vizuri, tumeshawaachia nje sasa.

    Pamoja na kusikitishwa na mabomu ya Gongolamboto kwa binadamu, siachi kujiuliza wanyama walifanyaje na kama wamepata msaada wowote ama walikimbia na wao pia ama walirudi majumbani baada ya mabomu, ukitoa waliokufa….. Nawapenda sana wanyama, japo upendo tofauti na wa watu. Nawatakia shughuli njema na tuzidi kuelimishana.

    Like

    Jenny

    February 22, 2011 at 4:22 pm

  150. Da Jenny usipime siku ya mambomu ilikuwa mbaya sana kwani mimi niko karibu sana na Gongo la Mboto ilibidi tujijali sisi wenyewe kwanza wanyama tulikuja kuwakumbuka baada ya mambomu kustop, hata hivyo kuku waliokuwa wanataga walisimama kutaga kwa mstuko wa mambomu mimi jirani yangu amefariki kwani bomu liliingia ndani kwake watu wakamwambia toka nje ukimbie ile anatoka tu kipande cha bomu kikampiga kifuani akaanguka chini na kufa hapo hapo. Sisi kama unavyojua tuliitwa kambini na tukawa tunapewa maelekezo ya nini cha kufanya. Yote kwa yote tunashukuru kila kitu kimekwenda salama kwa upande wangu. Pia nawashukuru wote walionipa pole na kunifariji kwa uzembe wa kijana wangu na kupoteza kuku wangu 200. Lakini sitokata tamaa nakusanya nguvu ili nikachukue tena kwani ukiogopa hasara huwezei kufanya biashara. Asanteni nyote kwenye blogg hii naomba tuendelee na moyo huu huu wa kusaidiana.

    Like

    Fatma

    February 25, 2011 at 7:47 am

    • Pole sana Da Fatma kwa yaliyowasibu katika familia yako kutokana na milipuko kule Gongo la Mboto … na pia poleni kwa msiba wa jirani yenu aliyepoteza maisha katika tukio hilo. Kwa hakika, Taifa zima limeguswa na kutikiswa na tukio zima. Tunachohitaji kipindi hiki ni subira, uvumilivu na kusimamia haki katika mchakato mzima wa ‘kujaribu’ kufidia wale waliopatwa na hasara ya namna moja ama nyingine. Tupo pamoja.

      Like

      simbadeo

      February 25, 2011 at 4:52 pm

  151. habari wadau, pole sana da fatma kwa kweli hilo limeniusa ila nashukuru mungu amekupa ujasiri bila ugumu kuku huwezi kufuga na wkt huu tuko ktk hali ngumujuu ya vifaranga

    Like

    damariam

    February 26, 2011 at 10:14 pm

  152. Kaka Deo nashukuru sana kwa kunipa pole ndio kidunia pia damariam nashukuru sana na wengine wote nawashukuru sana cha msingi ni kukaza buti tu ili tuweze kwenda mbele kimaisha.

    Like

    Fatma

    March 1, 2011 at 11:51 am

  153. Hamjambo jamani ukumbini? Da Fatma kanga wapo au nao walikufa?

    Kuku wangu wametoa mpya:
    1. Wanakula majani ya Aloe Vera wenyewe kidogo kidogo hadi kinabaki kisiki. Mvua iliponyesha yalinawiri yana maji maji mengi sielewi kinachowafurahisha kuku. Tumeamua kuhamisha mbegu kupanda mbali zaidi.

    2. Wanachimbua mihogo kwa miguu yao wanaidokoa na kuila. Miti yake wameirukia wameiangusha, wanakula majani yake japo sio sana kama mihogo yenyewe. Imepandwa mita chache tu toka kwenye nyumba wanafika kwa urahisi. Mwaka huu itabidi tupande mbali kidogo. Sio kwamba majani hakuna, mvua mvua zinaponyesha zimeotesha majani majani mengi, lakini pamoja na kula hayo majani mengine kama jua halijawa kali wako bize kuchimba na kula mihogo na kula majani ya Aloe Vera.

    Wengine mnaendeleaje jamani na mifugo? Nimeongeza vifaranga wa mayai wekundu 200, wanaendelea vizuri. Ni mbegu ile ya Australia uliyoniambia Da Fatma. Sasa natamani weupe… Anaejua wanakopatikana anijulishe. Asanteni.

    Like

    Jenny

    March 3, 2011 at 3:36 pm

  154. NB: Hao kuku wangu wanakula kipimo kilichoshauriwa na wanazidishiwa kidogo. Gramu 120 kwa siku, sio kwamba wanachimba mihogo hawashibi la, ila sielewi utukutu umekuja vipi.

    Like

    Jenny

    March 3, 2011 at 3:41 pm

  155. Da Jenny nafikiri hiyo ni dalili nzuri kwamba wako active kwani kuku dhaifu hawezi kufanya hayo. Suala la kushiba kuku uwa anakula akishiba anajisaidia harafu anaanza tena kula. Tunashauriwa kuwapa kiwango kinachowafaa tu ili wasinenepe sana wakashindwa kutaga. Hata mimi huwa nawapa hizohizo 120gm kwa siku lakini kuna wakati nikiingia bandani wananifuata kila ninakoenda na kupiga kelele, siku nyingine nawaonea tu huruma nawaongezea, ila daktari amenikataza kufanya hivyo.

    Like

    Elizabeth

    March 4, 2011 at 9:27 am

  156. Natumaini wote wazima na mnaendelea vizuri, Jamani mbona mimi sijakiona hicho kipeperushi? au nafungua vibaya naomba mnielekeze.

    Like

    Judy

    March 5, 2011 at 10:21 am

    • Da Judy, asante kwa swali lako. Naamini kwa kufuata ushauri aliotoa Da Eliza utapata kipeperushi hicho. Unaweza pia kucheki ‘old posts’ kwenye blogu ya https://simbadeo.wordpress.com/. Ikishindikana, usisite kutuandikia hapa nasi tutafuta njia nyingine ya kukusaidia ukipate. Asante.

      Like

      simbadeo

      March 7, 2011 at 10:16 am

  157. Da Judy, angalia kwenye website http:/simbadeo.wordpress.com au unaweza uka-google search ‘Je Unafuga Kuku?’ itajitokeza ukibonyeza kinatoka.

    Vipi umeishaanza kujenga mabanda? Ni mradi mzuri unaolipa pamoja na risk zilizokuwepo za magonjwa, mimi ni shuhuda na hivi sasa nimeongezea wengine.

    Like

    Elizabeth

    March 7, 2011 at 9:29 am

  158. habari wandugu mwenzenu niko hoi niliagiza vifaranga kenya 400 ijumaa iliyopita wakafanikiwa kuja mpk tarime kufika hapo wakashindwa kupita wakaguzi kila beria ukipitisha vifaranga vya kenya wanachoma moto ikabidiniuze tarime ukweli nina hali mbaya mwenzenu sijui nifanyeje nisaidieni

    Like

    damariam

    March 7, 2011 at 1:17 pm

  159. Da Mariam poleee! Haya mauza uza ya kukosekana kwa vifaranga sijui yatatuishia lini? Wanapatikana kwa taabu na kwa kupanga foleni sana wakati umeshalipia hela watu wanaizalisha kisha ndio wakuletee vifaranga. Ni huo uhaba unafanya hadi watu waagize Kenya japo sijui sababu zako Da’Mariam. Usife moyo, tafuta tena kwingine japo miezi inayoyoma.

    Like

    Jenny

    March 7, 2011 at 3:48 pm

  160. Asante sana Da Eliza nimekipata, nimegoogle. Kwa website ya kaka simba sijakipata bali nimekuta habari nyingine ya kusikitisha ya mtoto aliyepata ulemavu kutokana na kuugua malaria. Da Eliza ndo najiandaa kuanza nilikwama hapa kati, sasa kama vifaranga havipatikani tutafanyaje wapendwa? au ni kwa msimu tu baadae vitapatikana?

    Like

    Judy

    March 8, 2011 at 1:43 pm

  161. Ni kweli vifaranga ni shida lakini kwa wanaoishi Dar es Salaam ukiwa aggressive unavipata. Kwa mfano ukianza kujenga banda weka na plan kabisa unataka vifaranga waingie lini ili uweke order. Mimi uzoefu wangu uko na Tanzania Poultry Farm. Unaweza kuweka order leo kwa vifaranga wa kuchukua August 2011. Malipo unafanya mwezi mmoja kabla ya siku ya kuchukua (July 2011) unawapelekea bank slip wanakupa receipt ambayo siku ya kuchukua unakwenda nayo. Kwa aliye kanda ya ziwa nasikia kuna vifaranga wanatoka mwanza unaweza kufuatilia kama ni kweli na kuangalia uwezekano wa kuchukua hao.

    Unajua wanaozalisha vifaranga nao wako kwenye biashara, ni ngumu kuvizalisha wakati hauna confirmed order kwasababu ni vigumu kuvitunza. Tumeshuhudia wengine wanavifanya chakula cha nguruwe pindi wanapokosa soko, kitu ambacho ni hasara kwao. Nafikiri inabidi tuvumiliane.

    Like

    Elizabeth

    March 8, 2011 at 4:27 pm

  162. Asante sana mpendwa, kwa ufafanuzi wako mzuri, kama ukitoa order unapata basi hilo siyo tatizo sana. Ni kiasi cha kujipanga tu, kweli bila shaka nao wana muda wa kukaa na vifaranga baada ya kuvizalisha sasa kama muda utazidi bila kupata wa kuvinunua hilo nalo ni tatizo na hasara pia kwao. Nakushukuru dada.

    Like

    Judy

    March 9, 2011 at 9:51 am

  163. Dada Elizabeth,
    Vifaranga vya Tanzania Poultry Farm vikoje kwa ubora maan sie hatujavitumia tunataka kupata uzoefu wako. Nassib

    Like

    Nassib

    March 16, 2011 at 2:42 pm

  164. Kwakweli sijakutana na tatizo kubwa tangu nianze kufuga, nikiona dalili zisizokuwa za kawaida kuna daktari wao hapa Dar es Salaam nampigia simu anakuja na kunipa ushauri. Nilionao mimi naona utagaji wao una-range kati ya 70-80%. Joto ndo linawasumbua kwani kipindi cha joto ndo wanataga 70% i.e wanaotaga hivi sasa ni 1,200 napata kwenye tray 28 wakati wa joto, mvua zikinyesha kukawepo na kibaridi zinafika tray 30 kwa siku. Wataalamu wanasema ni kwasababu wanashindwa kula vizuri na wanakunywa maji mengi zaidi. Ili kuwafanya angalau wale, kipindi cha joto uwa tunawapa chakula kuanzia saa 10 za usiku angalau wanakula pale ambapo joto halijawa kali. Rangi yao ni gold kuelekea nyekundu kama wale aliotutumia Da Jenny kwenye picha.

    Da Jenny, ile picha uliyotutumia imenisaidia sana kwani banda la pili nimelijenga vilevile, ila tu lakwangu linashuka kwa steps maana ninakofugia kuna bonde. Nili-print nakuwapatia mafundi. Kwa kiasi fulani linaserve gharama.

    Nawatakia kila la kheri.

    Like

    Elizabeth

    March 17, 2011 at 10:35 am

  165. Asante Da Eliza, nashukuru kwa maelezo uliyomjibu kaka Nassib, nilikuwa nasubiri sana ajibiwe. Unajua mimi binafsi nafaidika sana hapa ninaposoma utaalamu na ushauri mbali mbali.

    Nami pia nimepanua banda nimejenga mfano wa hilo nililowatumia. Kila mtu anasema ni sehemu nzuri sana kwa kuku maana nimenyanyua kwenda juu na sehemu kubwa ni waya, linapiga feni nzuuuuriii nadhani sasa kuku watafurahia.

    Like

    Jenny

    March 17, 2011 at 11:22 am

  166. Da Jenny, siku nilipofuata vifaranga wa mayai nilikuta broiler 200 ambao mwenyewe hakuja kuwachukua nikawanunua nakuondoka nao kwavile banda ni kubwa na wa mayai bado wadogo hawapajazi nikawachanganya humo. Nilimuuliza daktari kama ina shida akasema kwasababu wote wametoka sehemu moja haina shida sana. Sasa hivi wana wiki sita. Wamenenepa kwelikweli, kama mchezo nimeuza 170 kwa shilingi 4,000 kila mmoja na kupata 680,000 ya ghafla. Niliwanunua Tshs 260,000 ila sijapiga mahesabu ya nime-invest kiasi gani kwenye chakula kwasababu walikuwa wanakula chakula kilekile wanachokula wengine.

    Nia yangu hapa nikutaka kukupa uzoefu mwingine wa broilers. Nimewapenda sana wanaitwa voda faster. Nakitulia nitawafuga kwa ajili ya kipato cha haraka haraka ila nimegundua wanahitaji more dedication in terms of time.

    Like

    Elizabeth

    March 17, 2011 at 1:03 pm

  167. Dada Elizabeth,
    Nashkuru kwa majibu yako. Naomba hilo banda picha yake sijaiona ambalo ametuma dada jenny.

    Like

    Nassib

    March 17, 2011 at 2:27 pm

  168. Uki-google search ‘Kuku Wa Amadori’ au ‘Ufugaji Kuku – Banda la Kuku’ itatokea website lililopo. Ukiibonyeza litakuja kwenye screen.

    Kila la Kheri.

    Like

    Elizabeth

    March 17, 2011 at 3:13 pm

  169. Hello Da Eliza,

    Asante sana. Binafsi nimejikita kwa kuku wa mayai na wa kienyeji kwa ajili ya mayai. Sijaanza kufuga Broiler, sina mtu mzuri kuwahangaikia na kwa sababu sikai mwenyewe shambani naona vigumu kuwafuga kwa sasa. Angalau wa mayai tunahangaika nao mwanzoni then wakishafika umri fulani basi. Tunasubiri tena batch nyingine lakini broiler ni bandika bandua ambayo ingehitaji niwe karibu. Unajua kazi ya kutuma mtu, sio sawa na ukifanya mwenyewe. Hata hao wa mayai bado nafuatilia kwa karibu sana kama sio kwenda mwenyewe kwa simu. Sometimes unaambiwa tatizo wakati limeshasambaa kwa kuku wengi linapoanza mtu hatoi taarifa au anaona ni kitu cha kawaida au anadhani ameshazoea kiasi anaweza kulitatua kumbe linakuwa tatizo jipya au ambalo halifahamu. Ila ni vizuri ukinipa ka-uzoefu na maarifa, nitautumia muda muafaka ukifika. Mbarikiwe!

    Like

    Jenny

    March 17, 2011 at 3:48 pm

  170. Hello wana ndugu,

    Nilimtumia kaka Simba vijarida kwa ajili ya kozi za ujasiriamali zimeshatangazwa, sijui kasafiri kwenda Loliondo? Maana sioni majibu, ni kama vile hayupo around. Hapa siwezi kuvituma, anayejua namna rahisi ya kumpata amuombe avitundike watu wawahi. Wanawake 30 wanapata schorlaships kila mwaka kwa kozi hii ya ujasiriamali. Wanaoweza kujilipia wanaruhusiwa na wanaume wanasoma pia ila wao hawajapata organization ya kuwa sponsor. Ni hayo tu.

    Like

    Jenny

    March 21, 2011 at 12:43 pm

  171. Tunashukuru sana kwa habari motomoto, mimi binafsi ninapenda, labda utusaidie tu kutwambia ni wapi na utaratibu unakuwaje na je ukikosa sponsor unaweza kujilipia ni bei gani? Na kama kaka simba hayupo pia unaweza kutusaidia kututumia wengine kwenye email zetu kama inawezekana.
    Asante kwa taarifa.

    Like

    Judy

    March 21, 2011 at 1:32 pm

    • Hi Wadau

      Asante sana kwa maoni mbalimbali yanayoendelea kutolewa hapa. Da Jane na Da Judy, nipo … vijimambo vimenikamata kidogo. Hata hivyo, niliweka bloguni vile vipeperushi. Hiyo nilifanya ndani ya wiki moja iliyopita. Link ya kumpeleka msomaji kwenye vipeperushi hivyo ni hii: https://simbadeo.wordpress.com/2011/03/18/fursa-ya-kujif…na-scholarship/

      Kwa kutembelea blogu hii na kutazama makala kadhaa zilizopita, utapata hiyo inayotangaza kuhusu fursa ya kujifunza Ujasiriamali pamoja na nini kinahitajika.

      Karibuni wadau, hii ni fursa adimu kupatikana, hasa upande wa kina mama ambapo kuna scholarship. Asante. Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      March 21, 2011 at 4:53 pm

  172. Wapendwa hamjambo?

    Nilikuwa kimya kidogo, niliibiwa shambani kuku 80. Vibaka walivizia vijana wamelegea au wameacha mwanya mdogo tu kwenye maelekezo, wakavunja mlango chumba kimojawapo kilichokuwa na kuku 250 wakaiba kuku 80. Kuamka asubuhi wakakuta mlango wa chumba wazi na kuna upungufu wa kuku. Mbwa walilishwa sumu, 2 wamekufa amebaki 1. Kosa lililofanyika ni kutowafungia kaka katika hicho chumba, badala yake kuwafungia wote chumba kingine ambako hawakuwa wakiona yanayotokea huko walikoibiwa kuku, vinginevyo kivuli tu cha mtu ama mnyama huwa wanapiga kelele mfano hakuna na hivyo wangeliwaamsha. Kwa vile vibaka inaelekea wanawatembelea mara kwa mara, siku hiyo walipokuta hakuna kelele za kanga wakafanya kweli kwa kuwaua mbwa kwa sumu na kuvunja mlango. Wavu uliwashinda kukata, chumba hicho nimeweka wavu fulani mgumu.

    Hizo ni changamoto wadau, tunajipanga kila siku kupambana nazo. Sasa katika idadi yangu ya kuku 950 niliyokuwa nimefikisha, wamepungua 80. Inabidi niongeze tena vifaranga na wakati huu wa baridi sijui nitaweza? Mwenye uzoefu wa kulea vifaranga msimu huu tafadhali naomba ushauri.

    Asanteni.

    Like

    Jenny

    March 31, 2011 at 8:39 am

    • Da Jenny, pole sana kwa yaliyokusibu. Kwa kweli vitendo hivyo vinahuzunisha na kusikitisha sana. Jamii yetu inakabiliwa na changamoto kubwa ya kuhakikisha inawasaidia vijana kuona umuhimu wa kujitafutia kipato kwa njia zilizo halali – kwa kufanya kazi za uzalishaji na nyinginezo na wao kujivunia wanachokipata kutokana na kazi hizo.
      Nakupa pole na ninaamini utapata ushauri mzuri kutoka kwa wadau wenzetu hapa. Asante.

      Like

      simbadeo

      March 31, 2011 at 10:52 am

  173. Pole sana Da Jenny, kweli ni changamoto na zinarudisha nyuma maendeleo. Kufuga vifaranga wakati wa baridi si kazi sana na ni wakati mzuri ambao hauna magonjwa mengi ya kuambukizana. Kinachosumbua ni baridi tu ambalo unalizuia kwa kuziba madirisha kwa makaratasi, kuhakikisha joto la kutosha kwa kutumia bulb za watts 200 ama kuweka mkaa uliokwishawaka kwenye sufuria na kulininginiza juu kidogo (nimegundua sufuria ni zuri kuliko jiko kwasababu joto linatoka nje zaidi kupitia kwenye chuma pembeni). Mimi kuku wangu wanaotaga niliwaweka mwezi wa tano mwaka jana,ambapo baridi ilikuwa imekolea. Katika kuku 1214 walikufa 6 tu na hawa wengine niliowaweka February mwaka huu, mpaka sasa wamekufa 9 ila hawa ni wengi zaidi. Kwahiyo sioni kama kuna tofauti kubwa ni umakini tu kuwazuia wasipigwe na baridi.

    Wape pole wote ndugu na jamaa. Ila vijana wa shamba nao huwa hawaaminiki nao wachunguze vizuri pia kuhakikisha hawa-collude na vibaka .

    Like

    Elizabeth

    March 31, 2011 at 12:09 pm

  174. Asanteni kwa pole,

    Naamini Vijana hawa wa shamba hawakushirikiana na wezi, ni uzembe tu mkubwa wa kutotii maagizo uliosababisha wameibiwa. Unajua ndugu zetu na watu wa kazi wanajisahau na kuchukulia mambo ni rahisi tu kumbe sio. Yaani wezi wametumia udhaifu wa kutokuwepo kelele za kanga tu kuiba. Siku zote kanga huwa wanawaamsha. Huwa wanalala juu ya miti hapo nyumbani na chochote kinachokaribia shamba wanapiga kelele, walishajaribu sana kuwapandia juu ya miti lakini wakianza tu kupanda kanga wote wanaruka wanatua juu ya paa la nyumba na kelele zao ni taharuki tupu hivyo wote ndani wanaamka vibaka wanatimua.

    Sasa wakati huu wa kilimo nimelalamikiwa na majirani wanakula mahindi niwafungie yarefuke kidogo ndipo niwaachie. Nikaagiza kanga wakubwa ambao ndio walinzi zaidi wawafungie banda hilo ambalo liko mbali kidogo na wao wanapolala, Kwa kutofuatilia na kuchukulia maagizo kirahisi, kijana mgeni akawafungia banda tofauti lililo karibu na wanapolala hivyo kanga hawakuona kilichokuwa kinaendelea nje vinginevyo wangewaamsha.

    Inaweza kuonekana kama walikula njama, nakubali, lakini kwa hao ilikuwa ni uzembe na kujisahau. Aliyefungia kanga banda chumba tofauti ni kijana mgeni, hajamaliza hata mwezi.

    Kanga, nawapenda sana. Walinzi wazuri kuliko mbwa.

    Like

    Jenny

    March 31, 2011 at 1:31 pm

  175. Nashukuru kwa ushauri wa vifaranga, nitachukua hata wakati huu na nitazingatia ushauri wako da’Eliza.

    Like

    Jenny

    March 31, 2011 at 1:36 pm

  176. Pole sana Da Jenny, ni kweli kabisa kama Deo alivyosema, yani tunatabu sana yani wakati unapigana na maisha ukijitahidi kudhibiti kuku wako wasikumbwe na maradhi, watu wengine nao wanawapigia mahesabu jinsi ya kuwaiba, yani watu wanapenda sana mteremko. Mimi kila siku nikikutana na watoto wa mitaani nafikiria wakiwa wakubwa watakuwa watu wa aina gani, yani serikali yetu inatakiwa kufanya kazi sana.
    Lakini pia nimefurahishwa na ulinzi wa Kanga, yani imenifurahisha sana natamani nifike huko shambani kwako.

    Pole sana Mungu atakutia nguvu na mbinu za kuziba hilo pengo

    Like

    Judy

    March 31, 2011 at 3:03 pm

  177. Hello Da Judy, asante sana. Shamba darasa naona limegota mahali. Mimi huenda shamba kila Jumamosi kama hakuna dharula nyingine. Jumamosi yoyote utakayokuwa na nafasi nijulishe tukutane hapo Goig – Mbezi Beach CRDB Bank jengo la Shamo Park halafu tutakwenda shamba pamoja. Ila mimi ni mfugaji mdogo bado hivyo, usitegemee mambo makubwa sana.

    Karibu.

    Like

    Jenny

    April 1, 2011 at 7:21 am

  178. Dada Jenny,
    Pole kwa yaliyokukuta. Ila hao wezi watakuwa ni watu wa karibu fanya uchunguzi. Mungu atakusaidia utapata wengi zaidi ya ho.NAssib

    Like

    Nassib

    April 1, 2011 at 6:11 pm

  179. Asante kaka Nassib, changamoto hazikosi kazi hizi. Nawashukuru wote.

    Like

    Jenny

    April 4, 2011 at 10:12 am

  180. Natumaini wote hamjambo, asante sana Da Jenny kwa mwaliko, nikiwa tayari nitakuomba unipatie namba yako ya simu tuwasiliane, kidogo ndo kinazaa kikubwa Da Jenny hata mbuyu ulianza kama mchicha wanasema. Nitajitahidi kutafuta muda kwani wengine vibarua vyetu mpaka J.mosi. nawatakia kazi njema

    Like

    Judy

    April 6, 2011 at 3:41 pm

  181. Wapendwa
    Nimefurahishwa na Mjadala wenu ambao nimeufuatilia kwa siku kadhaa nawapongeza sana nami ni mfugaji wa kuku wa kienyeji lakini ninataka kuwekwza kwenye kuku wa kisasa wa nyama/mayai lakini sina uzoefu nifanyeje?

    Like

    atupele

    April 8, 2011 at 8:54 am

  182. Atupele karibu jamvini!

    Labda ungetueleza kidogo unataka kujua nini kuhusu kufuga hao kuku wa kisasa (japo mimi nafuga zaidi wa kienyeji na wa mayai kiasi sio broiler), maana kama unafuga wa kienyeji basi utakuwa na kauzoefu kuhusu kuku.

    Da Juddy, kuna J2 baadhi pia huwa nakwenda shamba kama sikupata nafasi kwa Jumamosi ila isiwe siku za mvua maana gari yangu ndogo huwa haiingii shambani kabisa wakati huu wa mvua, napaki barabara kuu naingia kwa kutembea mwendo wa kama dk 25 hivi. Kama una usafiri 4 wheel poa, zinafika bila taabu au kama mwendo huo niliosema haukusumbui kutembea pia vema tu jipange. Kati ya hizo siku mbili ambayo wewe utakuwa na nafasi zaidi tuwasiliane tupange. Namba yangu kwa wote ni 071xxxxxxx (wasiliana na administrator wa blogu hii Simba Deo). Mbarikiwe.

    Like

    Jenny

    April 8, 2011 at 4:25 pm

  183. @Yombop,taka TZ UMESEMA LAKINI WAJIBU NI WAKO KUPUNGUZA ILE GARAMA YEYOTE YA CHAKULA KWA MAARIFA YAKO,LA MNO NI KWAMBA,BIASHARA YEYOTE IWE YA UFUGAJI,NAFAKA,LA MHIMU NI KUWA MAKINI NA KUJITEGEMEA TOKA MSINGINI KWANZA KABISA WAFAA KUWA MKULIMA,95% YA CHAKULA CHA KUUZA AU KULISHA MIFUGO WAFAA KUKUZA KWA SHAMBA LAKO GARAMA ITAKUWA CHINI HUKU FAIDA IKIWA YA KUDHIRISHA.
    SIRI HIYO TU,…BIASHARA NYINGINE KAMA YA SUNGURA,NYUKI PATO LAO NI MARADUFU..JARIBU LEO,KISHA UTASHEREHEKEA TUNDA LAKE.

    Like

    Khim Moot

    April 14, 2011 at 6:41 pm

    • Ndugu Khim Moot, karibu sana kwenye jukwaa hili na kwa kweli tumefurahia sana mchango wako. Ni mchango unayoonyesha uzoefu mkubwa ulio nao katika shughuli za ufugaji – katika viwango mbalimbali.

      Kwa wadau wafuatiliaji wa makala hizi za ufugaji – tumekuwa tukizungumza kwa muda mrefu kuhusu kuwa na siku ya Shamba Darasa. Katika mawasiliano ya hivi karibuni kati ya Da Jenny na Da Judy, kama nakumbuka vizuri, kupitia ukurasa wetu huu, Da Jenny alisema kwamba kipindi hiki cha mvua ufikikaji shambani kwake ni wa tabu kidogo. Kwa hiyo napendekeza tufanye siku hiyo mwezi wa Juni au Julai. Je, wengine mnasemaje?
      Naamini itakuwa siku nzuri sana kwetu kujifunza. Tuendelee kuwepo.

      Like

      simbadeo

      April 14, 2011 at 10:03 pm

  184. habari za siku wadau nilipotea kidogo majukumu yalinikaba pole sana dada jane

    Like

    damariam

    April 19, 2011 at 1:44 pm

  185. dada Jenny
    sikiweza kujibu haraka kwa vile nilikuwa nje ya kituo cha kazi. Kuhusu hao kuku wa kisasa wanyama/mayai ningependa kujua cost/benefit say kwa kuku 1000. ukweli nimejaribu sana wale wa kienyeji lakini naona return yao ni ndogo sioni profit, nina mabanda makubwa eneo kubwa nimesoma majarida nimehudhuria semina mbalimbali kuhusu ufugaji bora wa kuku wa kienyeji nimejaribu kufuga wale wa malawi lakini no profit and soko lilikuwa problem, mpaka nikahisi kuwa mimi sifugi bali naishi na kuku.Sasa nataka kujaribu hawa wa kisasa isipokuwa sina uzoefu naomba ushauri wenu

    Like

    atupele

    April 19, 2011 at 7:45 pm

  186. Hello Atupele, wafugaji wakubwa watakujibu. Zaidi nafuga wa kienyeji japo pia wa mayai ninao, utagaji wao nilishauelezea hapo nyuma kidogo. Pia ukisoma post za wengine hapa utaona mchanganuo ulishatolewa kwa kuku wa mayai mwezi November tarehe 9 – 11 2010. Dada Elizabeth alitoa mchanganuo kwa kuku wa mayai ambao nadhani uko wazi sana. Tusubiri wafugaji wakupe maelezo. Kuku wa nyama (broiler) sifugi kabisa.

    Like

    Jenny

    April 20, 2011 at 7:50 am

  187. Wandugu wote,
    Nawapongeza wote wanotoa michango yao kwenye hii blogg. Sie hapa tuanfuga kuku wa nyama na kipindi hiki kidogo kinaleta tabu kwa soko kwani kila tajiri yetu tunaemwita aje kununua kuku wanasema soko limefurika sasa tuko matatani kwani twaendelea kulisha tu. Sasa ombi kama kuna wateja wenu amabo twaweza kuwtumia kwa sasa ili kuku wetu watoke basi naomba namab zao waje kuwachukua, mtaji karibu unakwisha. Siye tuko Chng’ombe ya Temeke.
    NAssib

    Like

    Nassib

    April 20, 2011 at 4:34 pm

  188. Haa!!! mbona mmekuwa kimya wadau??? inaogopesha!!!

    Like

    Nassib

    May 9, 2011 at 1:19 pm

  189. Pole Nassib, natumaini uliuza kuku wakati wa Pasaka. Naona watu wako kimya kweli, sijui msimu huu wa kabaridi mambo yamenyooka?

    Like

    Jenny

    May 9, 2011 at 2:26 pm

    • da jenny na wadau wote kwa pamoja,nami ni mfugaji nae anza kujifunza,nina kuku wa kienyeji mbegu nyeusi wa mayai na nyama majogoo ningependa sana kujifunza kutoka kwenu naamini nitapata mafunzo bora kutoka kwenu ninaomba msaada wenu wa hali na mali hili nifike mlipo fika jamani.namba yangu ni 0715845284.nitashukuru endapo nitapata muongozo wenu kwa pamoja.(umoja ni nguvu)

      Like

      sarah

      June 28, 2011 at 6:44 pm

  190. Dada Jenny,
    Mungu alisaidia tuliwauza ila kwa mbinde kweli; ndiyo biashara ilivyo leo safi kesho kidogo taabu lakini tunaendelea ila tunajipanga tuanze na wa mayai kwa sasa
    NAssib

    Like

    Nassib

    May 18, 2011 at 11:04 am

  191. Mimi ni mgeni katika hii blog, nimesomasana michango ya watu mbalimbali waliochangia humu ndani kwa kweli inaelimisha sana .
    Mimi ni mfugaji wa kuku wa kienyeji nahitaji kuwa na kitotoleshi cha vifaranga lakini sina fedha ya kutosha kununua .Naomba msaada wenu ni wapi naweza kupata mkopo wa hiyo incubeta.
    Asante sana.
    Martina.

    Like

    martina

    July 3, 2011 at 2:40 pm

    • Dada Martina

      Karibu sana na jisikie nyumbani. Unakaribishwa kuuliza maswali yoyote unayohisi kuwa nayo kuhusiana na ufugaji kuku – wa kisasa na hata wale wa kienyeji. Katika jukwaa hili kila mmoja ni mwalimu na pia mwanafunzi. Maana yake tunaamini kuwa unayo mengi ya kutufundisha na vilevile kuna mengi utakayojifunza kutoka kwetu.

      Karibu sana.

      Deo Simba

      Like

      simbadeo

      July 5, 2011 at 8:45 am

  192. Da Martina na Sarah, karibuni sana. Kama alivyosema kaka Deo, sie wote hapa ni waalimu na pia wanafunzi kwa pamoja tunasaidiana kusonga mbele. Mkisoma maelezo yaliyopita mtajifunza mengi, na kama mna maswali pia mkiuliza mtajibiwa na wadau. Tupo, japo wakati mwingine tunapita kusoma na kudadavua yaliyopita kwa kujifunza n.k. Karibuni sana.

    Like

    Jenny

    July 5, 2011 at 11:13 am

  193. ndugu wapendwa
    habari za siku nilipotea kwa sababu nilikuwa nina kazi za vijijini na kwa sasa nimerudi rasmi.
    mimi ninaanza kufuga mwezi huu kuku wa mayai (nimeshaweka order ya vifaranga 600 pale Temeke (nimeagiza vya Arusha),. kifaranga kimoja ni Tsh 2200.
    nitafugia mbweni kwa rafiki yangu ambaye ameacha kufuga (atanikodisha mabanda yake).
    natamani lile shamba darasa liwepo ili tukajifunze kwa vitendo.
    Dada Jenny naomba nikutafute kwenye simu ili nipate uzoefu wako zaidi.
    mimi naishi Tegeta na ni mfanyakazi.
    naomba anayefahamu wapi naweza kupata source nzuri ya chakula aniambie i.e. which brand is the best na duka gani.

    katika kusoma blog hii, nimeona ushauri unatolewa kuwa ni vema kutegeneza chakula mwenyewe. kwa kuzingatia hili jana nilienda saba saba banda la SIDO nimeona kuna mashine ya kutengeneza chakula inauzwa milioni moja na laki mbili (1.2m) na inatumia umeme single phase na uwezo wake ni kuzalisha kilo 240 kwa saa.
    aidha, VETA wana mashine ambayo ni dual nikiwa na maana inatumia umeme na umeme ukikatika inakuwa manual na una-operate kwa mkono (i.e. unazungusha),. mashine hii inasaga ingredient moja moja; then unaamishia kwenye manual mixer (hii mixer haitumii umeme). gharama ya mashine ni laki tina na mixer yake ni laki 600.

    ila jamani tuzidi kupeana moyo hasa kwa sisi ambao tunaanza

    Like

    mwemezi

    July 7, 2011 at 10:17 am

  194. Hello Mwemezi, shamba darasa naona lilififia. Kama uko Tegeta basi ni rahisi zaidi mimi kukupitia tukaenda maana shamba liko Madale. Jana nilikwenda huko, sitarajii kwenda tena weekend hii watakwenda wasichana kusaidia, labda kama tutakubaliana J2 nikitoka Kanisani may be nikupeleke. Mimi pia ni mfanya kazi nategemea sikukuu na weekend kwenda huko. Nilishatoa namba yangu ya simu huko kwenye post za nyuma ila tena ni 071xxxxxxx (wasiliana na administrator wa blogu hii, Simba Deo). Ukipiga au ukiniandikia msg nijulishe wewe ni Mwemezi inaniwia rahisi kukumbuka kwa kunitajia jina. Sijawahi kutembelea shamba la mtu nikatoka mtupu, popote kwa mfugaji mwenzako hata kama anafuga kidogo ukienda unatoka umejifunza kitu ambacho hukuwa unakifahamu. Tuwasiliane.

    Like

    Jenny

    July 8, 2011 at 10:15 am

  195. Dada jenny, kama ni jumapili nitashukuru sana.. naomba tupange hiyo jumapili twende. mimi nitakushtua kwenye simu yako leo.

    Like

    mwemezi

    July 8, 2011 at 12:06 pm

    • Hello,

      Nimekuwa kwenye mbio nyingi. Shamba darasa ni tukio muhimu sana. Nipo safarini kwa sasa. Na ni safari itakayonichukua muda wa kutosha. Lakini kwa wadau … itakuwa vema kuendelea na utaratibu wa kukutana na kubadilishana maarifa, ujuzi, mawazo, experiences n.k. Ningetamani sana kuwepo ili pia tukio hilo tuliripoti LIVE … lakini … Mwenyezi Mungu atatujalia siku nyingine tena. Tupo pamoja.

      Like

      simbadeo

      July 8, 2011 at 4:27 pm

      • thanks Simbadeo kwa response!

        Like

        mwemezi

        July 8, 2011 at 4:38 pm

  196. kusema kweli hata mimi nimefurahi sana kuhusiana na njia hii ya kupeana ushauri nasaha kuhusu ujasiliamali katika mtandao. Hata mimi ni mdau wa shughuli hii pia ninakaribia kuanza hii project

    Like

    Kainika

    July 9, 2011 at 6:51 am

    • Karibu sana Kainika. Jisikie nyumbani kuuliza na kuchangia chochote kitakachosaidia katika kukuza stadi zetu za kijasiriamali katika eneo la ufugaji kuku.

      Like

      simbadeo

      July 10, 2011 at 10:03 am

  197. jamani mwenzenu jana nimefaidika sana, nilibahatika kukutana na dada Jenny. kwa kweli nilijifunza mengi sana kwake kuanzia utengenezaji banda, utunzaji vifaranga, ulishaji, ufuatiliaji magonjwa na farm management bila kusahau utafutaji masoko na uwekaji kumbukumbu. Kwa kweli dada jenny ni mtu ambaye yupo tayari kuelekeza mtu.. ahsante sana dada yangu.

    nakushukuru sana Simbadeo kwa kuanzisha blog hii kwa sababu imefanya nikutane na kuongeza rafiki ambaye tunaweza kushirikiana katika ujasiriamali.

    Like

    mwemezi

    July 11, 2011 at 7:06 am

    • Hongereni sana Ndg Mwemezi na Da Jenny. Mmefungua njia. Naamini wengine wengi watafuatia katika kujielimisha zaidi. Ama kwa hakika hii ni hatua kubwa sana katika jukwaa letu.

      Asante na tuendelee kushirikiana.

      Like

      simbadeo

      July 11, 2011 at 7:38 am

  198. Hello Mwemezi, Nashukuru kama uliambulia chochote. Naona hujajibiwa kuhusu chakula cha kampuni gani kizuri. Mimi hutumia chakula cha Hill, godown yao kubwa iko hapo Lufungira Sam Nujoma Road upande wa kushoto kama unaenda Mwenge tokea Ubungo, opposite na hicho kituo cha basi. Nimejaribu vyakula vya kampuni nyingine pia, ila wao naona wana chakula kizuri (kwa upande wangu).

    Kuhusu kuchanganya mwenyewe, waone wataalamu wa mifugo, watakupatia mchanganuo unaofaa kulingana na aina ya kuku ulio nao. Siku njema.

    Like

    Jenny

    July 11, 2011 at 3:40 pm

  199. jamani naomba mnisaidie ile link ya kupata kipeperushi cha utunzaji wa vifaranga/kuku kilichotolewa na Arusha chicks

    Like

    mwemezi

    July 15, 2011 at 4:14 pm

  200. Habari za siku wapendwa. Inafurahisha kwamba angalau kuna maendeleo. Mimi naendelea vizuri na kuku wangu hivi sasa wote wako kwenye production. Angalau nimepumzika kidogo ila bei za vyakula ndo zinanitisha kidogo. Da Jenny maendeleo vipi? bila shaka umekaribia malengo. Kwa wanaotaka machine za kutengeneza chakula, kuna karakana nyingine iko mwenge, wanatengeneza kuanzia nusu tani kwa saa mpaka capacity anayotaka mtu kwa mill na mixer, lakini zinatumia umeme wa three phase. Ukifika pale unakuta machine zenye ukubwa tofauti tofauti ambazo ni order za watu zikiwa zinatengenezwa. Mimi nilipoenda sikuamini, kwakweli hii sector inaendelea kukua.

    Like

    Elizabeth

    July 18, 2011 at 12:13 pm

  201. elizabeth, hizo mashine za kutengeneza chakula nielekeze vizuri mwenge sehemu gani, na kama una namba yao ya simu. Na je zinarange kiasi gani kwa mfano hiyo yenye capacity ya nusu tani.
    mimi ndo nafanya maandalizi, nategemea kuingiza vifaranga 600 vya kuku wa mayai tarehe 28 Julai na mzidi kuniombea na nitazidi kuwaomba ushauri kwa sababu ndo naanza ufugaji (sijawahi fuga kitaalamu).

    Like

    mwemezi

    July 18, 2011 at 12:33 pm

  202. Karibu ndugu Mwemezi, tunakutakia kila la kheri, la msingi usisikilize maneno ya watu maana yanakatisha tamaa. Kuku ukiwafuga vizuri na kufuata utaalamu ni mradi mzuri. Fuata sana masharti ikiwa ni pamoja na kuhakikisha unawapa kinga kwa muda unaotakiwa na usafi. Ukiweza vilivile tumia automatic drinkers pindi wakikua kidogo, hizi mimi ninazipenda sana zinapunguza sana uchafu wa banda ambao unaeneza maradhi na zinahakikisha uwepo wa maji muda wote.

    Machine ya nusu tani i.e mifuko 10 ya kilo 50 kwa saa ina-range kwenye TZS 3,600,000 hadi 4,000,000 kwa zote mill na mixer. Niliweka order June sasa hivi inakaribia kuisha. Karakana ilipo ni: Mwenge ukianza tu barabara ya bagamoyo ukimaliza tu petrol station mbele yake kidogo kuna mapikipiki upande wa kushoto unaingia kwenye barabara ya vumbi, ukiulizia maeneo hayo watakuonyesha panafahamika sana. Unaweza kumpigia vilevile mhusika kwa namba +255754634747.

    Like

    Elizabeth

    July 18, 2011 at 2:45 pm

    • dada eliza ahsante sana kwa kunipa moyo. aidha nashukuru sana kwa maelezo ya automatic drinker. sasa naomba unifahamishe hizo drinker zinapatikana wapi, na bei ikoje. hao kuku wangu 600 watakuwa katika mabanda 3 ya kuku 200 kila moja,. sasa Mahesabu ya drinkers yanaendaje.

      nashukuru sana kwa details za machine ya kutengeneza chakula

      Like

      mwemezi

      July 18, 2011 at 3:13 pm

      • Zinapatikana pale Farm Base Ilala au kwenye maduka ya dawa za mifugo makubwa. Bei yake ni TZS 30,000 kila moja. Kwa kuku 600, nne zinawatosha kama wako pamoja maana moja inatosha kuku 150, lakini kwa sababu wametengwa itakubidi kuweka kama mbili kila banda.

        Like

        Elizabeth

        July 18, 2011 at 3:26 pm

  203. ahsante sana ELizabeth, nitazifuatilia. hivi zinafanyaje kazi na faida yake ni nini kulinganisha na manual drinkers

    Like

    mwemezi

    July 18, 2011 at 3:48 pm

    • Ukitaka kuziona, google search website ya Tanzania Poultry Farm kuna sehemu inaonyesha picha, fungua utaziona kwenye mabanda yao. Faida yake ni kupunguza uchafu na kazi ya kuosha makopo mara kwa mara na kuhakikisha maji yapo muda wote, maana kuku wanahitaji maji sana, ila kama utapata kijana mzuri anayejituma inaweza isiwe shida sana. Mimi kwasababu muda mwingi nakuwa sipo naona zinanipunguzia makali.

      Hii yote ni katika kukupa uzoefu tu wa kufuga utakuja kugundua mwenyewe baadae faida au hasara za hiki au kile.

      Like

      Elizabeth

      July 18, 2011 at 4:14 pm

  204. nashukuru sana kwa maelezo yako kuhusiana na hii kitu. naona itakuwa bomba sana nikizifuatilia huko farmbase kama ulivyosema.

    Like

    mwemezi

    July 18, 2011 at 4:25 pm

  205. MEMBERS, ZA jumatatu, mimi wiki hii nategemea kupokea vifaranga 600 wa kuku wa mayai.
    kati soma soma hapo juu dada Jenny na Fatma mmeongelea matumizi ya Katani, Aloe Vera na Mwarobaini. naomba kuuliza yafuatayo:
    1) JE zinasaidia kuzuia au kutibu magonjwa gani?
    2) Je ni kwa ajili ya kutibu au kuzuia?
    3) Je vipimo vya uchanganyaji unakuwaje?
    4) Je dozi ipoje

    nitashukuru kwa msaada wenu

    Like

    mwemezi

    July 25, 2011 at 9:22 am

  206. Hello Mwemezi,

    Mimi nimepokea vifaranga 1600 Alhamisi iliyopita, niko bize navyo ndio maana nipo kimya. Sijawahi kuwapa vifaranga wadogo mchanganyiko huo kwa vile wao wana chanjo na dawa nyingi za vitamini, pia ninapenda kuwafuga kitaalamu wawapo wadogo, nawaachia wakishakua wakubwa – resistant.

    1. Mimi upande wangu :Mchanganyiko wa Aloe, Mwarobaini, na au Katani ni kwa ajili ya kusaidia kuzuia zaidi, sio kutibu japo naamini vinaweza kutibu kama virus ndio wanaingia wakakutana na mwili wa kuku ambao hauwavutii kuishi yaani wenye hizo dawa. Mfano nimesoma kwenye tafiti kwamba Aloe inatibu minyoo kwa Kanga, nadhani Aloe itakuwa inaweka mazingira ambayo hayawavutii minyoo kukaa kwenye mwili wa Kanga pale wanapoanza kuingia kufanya makazi. Wakiugua wanahitaji tiba sahihi ya kitaalamu.
    2. Mimi upande wangu: Huvitumia kama kinga na sio tiba, wakishaugua natafuta tiba sahihi. Vinasaidia kuweka kundi salama zaidi na bila magonjwa muda mrefu.
    3. Vipimo natumia ki-asili yaani kwa kukadiria isiwe imekolea sana au nyepesi sana. Kama ambavyo ningetengeneza kwa kunywa mwenyewe.
    4. Mimi hutoa dozi hiyo siku 5 mfululizo kila mwezi mara 1. Mara nyingine mara 1 kila wiki, inategemea tu na nafasi na wepesi wa vijana shambani.

    Kwa vifaranga wadogo unaotarajia kupokea, nakushauri kufuata utaratibu wa kulea vifaranga kitaalamu. Utakapoendelea kuzoea ndio utajifunza hizo njia nyingine zinazosaidia pia katika ufugaji.

    Nakutakia mafanikio.

    Like

    Jenny

    July 25, 2011 at 11:34 am

    • Ongera sana Da Jenny na tunakutakia kila la kheri maana vifaranga 1,600 sio mchezo. Moto wake nimeuona lakini hivi sasa napumua.

      Like

      Eliza

      July 27, 2011 at 11:10 am

      • Wadau katika jukwaa hili, naona kuna habari nyingi za kutia moyo hapa. Ninaungana na Da Eliza kutoa pongezi kwa Ndg Mwemezi na Da Jenny kwa mafanikio waliyoeleza hapa. Ama kwa hakika ni taarifa za kutia moyo. Pengine, kwa ajili ya kushirikishana zaidi, kama una picha ya moja ya hatua kadhaa katika mchakato wa ufugaji, unaweza kuituma kwangu, nami nitaiweka kwenye mtandao wetu hapa. Unaweza kunitumia kwa anwani hizi: simbadeo2000@yahoo.co.uk au kakasimba@gmail.com
        Karibuni sana ili wenzetu nao wajifunze na kuhamasika kwa njia ya picha.

        Like

        simbadeo

        July 27, 2011 at 3:14 pm

  207. Asante Da’Eliza, naelewa cha moto nitakiona lakini naamini nitavuka tuu huu mziki maana ni mnene. Nyie watu hapa mmenitia moyo sana ndio maana nimefika hapo sasa pa kuagiza hiyo namba. Angalau wale wa Malawi makundi yote 2 wanataga, na wale Layers wekundu wanaanza kutaga wakati wowote kuanzia sasa, nategemea hao watanisaidia kuucheza huo mziki. Mbarikiwe.

    Like

    Jenny

    July 27, 2011 at 3:47 pm

  208. namshukuru Mungu vifaranga vyangu vya kuku wa mayai (600 plus nyongeza ya vifaranga 6) vimefika salama toka Tanzania Poultry (arusha chick). kimsingi naviona kama vina afya njema. changamoto tuliyona nayo ni kuwa mimi na kijana wangu hatujawahi kufuga, ila kwa msaada wa blog ya simbadeo (hasa michango ya jenny, eliza, fatma, nassib, judy, n.k) pamoja, vipeperushi, ushauri wa walini-supply vifaranga ndo tunajitahidi kufuata hayo maelekezo ili tufanye kitaalamu. leo nimewapa Neoxyvital (a combination of antibiotics na vitamins), Trazium (antibiotic) na glucose.

    ila tatizo ninaloliona ni kuwa havinywi sana, nimejaribu kuvinywesha ila vinakunywa kidogo sana. mwanza niliweka drinkers 5 lakini vikawa ni vichache sana nikaongeza vingine 3 na kuwa jumla 8. chakula nitawawekea kwenye mabox waliyokuja nayo.

    nimeweka majiko mawili ya mkaa pamoja na chemli 2. ukubwa wa brooder ni kama 3mX2m

    nakaribisha ushauri kama utaona katika nilivyoeleza hapa nahitaji kurekebisha. Si unajua wanafunzi wanapotaka kujifunza zaidi!!

    Like

    mwemezi

    July 28, 2011 at 3:00 pm

    • Ongera, karibu sana kwenye fani, utafanikiwa tu. Hata mimi nilianza hivyo hivyo kama mchezo lakini sasa hivi ninao layers 2,900 wote wanataga. Ukiona wanarundikana sana tumia masufuria kuwekea mkaa na uweke juu ya tofari ni mazuri zaidi maana moto unatoka pande zote kupitia kwenye bati la sufuria. Mambo mengine ni kubuni tu, wengine chakula wanaweka juu ya magazeti, wengine kwenye ungo n.k. Mimi nilichonga vibox vidogo kwa kutumia ply-woods ndo natumiaga siku za mwanzoni.

      Ka-Simba, ahsante kututia moyo. Natarajia ku-install mashine ya kutengeneza chakula hivi karibuni nikiishaanza kutengeneza chakula nitakutumis picha za machine na mabanda ili wadau wanaohitaji waone operation nzima.

      Like

      Elizabeth

      July 28, 2011 at 3:25 pm

      • Hongera Ndg Mwemezi kwa kuthubutu. Ni hatua muhimu sana.\
        Dar Eliza, tunasubiri kwa hamu picha hizo. Inasemekana kwamba picha hufundisha mara nyingi zaidi kuliko maneno. Naamini wengi tutajifunza mengi kutokana na picha utakazotutumia.

        Kila la kheri.

        Like

        simbadeo

        July 28, 2011 at 3:42 pm

  209. ahsante sana wadau kwa kunitia moyo.
    kwa anayefahamu, mchanganyiko wa dawa (natumia neoxyvital badala ya OTC 20%) na dawa nyingine unatakiwa ukae kwenye chombo bandani masaa mangapi.. kuna mtu kaniambia isizidi masaa 3, ila maelezo yaliyo katika package yanasema dawa iliyochanganywa na maji isikae more than 24 hours. which is which.

    Eliza hongera kuwa na kuku 2900, umepiga hatua kubwa sana!! una fugia wapi na banda lako kubwa kiasi gani?

    Like

    mwemezi

    July 28, 2011 at 5:47 pm

    • Binafsi neoxyvital sijawahi kuitumia lakini antibiotic ziko nyingi. Siku saba za mwanzo natumiaga CTC pamoja na vitalyte. Naweka mchanganyiko huo kwenye makopo bila kujaza kwasababu ukijaza yanachukua muda mrefu sana kuisha na yanachafuka sana. Fuata utaalamu maneno ya watu yasikilize na kuyapima kwanza kila mtu ana jinsi yake lakini ukifuata maelekezo kwenye karatasi na ya madaktari ni nzuri zaidi. Ukimwaga kila baada ya masaa matatu si utakuwa ni ualibifu? Hiyo hela utairudishaje?

      Mimi nafugia Kinyerezi na ndo nyumbani hapohapo kwakiasi fulani inanisaidia ku-manage. Mabanda ninayo mawili ukubwa wake kwa ujumla ni sqm 480 ila nimeyatenga mara 6 kwa sqm 80 kila moja.

      Like

      Eliza

      July 29, 2011 at 9:05 am

  210. Simbadeo,
    aisee mimi napendekeza kichwa cha webpage hii ukibadilishe kisomeke “ufugaji wa kuku” badala ya “kuku wa amadori”. mantiki ya kupendekeza mabadiliko ni kuwa page hii inahusika na habari mchanganyiko wa ufugaji wa kuku badala ya kuongelea tu kuku wa amadori. ninajua inawezekana inaweza kuwa ngumu kuzingatia ombi hili (may be kwa sababu ya historia yake) lakini hebu lifikirie

    Like

    mwemezi

    July 30, 2011 at 6:21 pm

    • Hi, Ndugu Mwemezi, nimechukua pendekezo lako. Hivi sasa makala hiyo inafahamika kwa jina la ‘Ufugaji wa kuku’. Natumaini waliokuwa wakiitafuta kwa jina la ‘Kuku wa Amadori’ watapata namna ya kuunganishwa nayo.

      Asante sana kwa mchango wako. Tuendelee kushirikiana. Cheers!

      Like

      simbadeo

      July 30, 2011 at 11:17 pm

  211. nashukuru sana kwa response yako.

    jamani mimi naendelea vizuri na utunzaji vifaranga. so far wamekufa wawili na tunadhani sababu ni physical na si ugonjwa nikiwa na maaana kuwa tuliweka chemli chini badala ya kuiningiza kwa hiyo wakakusanyika kwenye hiyo taa na kimoja kikakosa hewa/na kuzidiwa na joto la chemli. ila tumesharekebisha na kuningiza juu kama nusu futi toka chini.

    tunaendelea kuwapa dawa hadi jumanne. na jumatano vitakuwa vimetimiza wiki na hivyo kuwapa chango ya New castle. Chanjo hii sijainunua, Je duka gani linauza dawa nzuri (at least unaweza kuwa imani kuwa si feki), za mwanzo nilinunua Farmers Center kule Ilala Amana. sasa kule ni mbali na tegeta.

    Dada Jenny unaendeleaje na vifaranga/vijogoo? hivi vinachukua wiki/miezi mingapi ili viweze kuuzwa kwa ajili ya nyama?

    Eliza hopefully mambo si mabaya.. hopefully sasa unaenjoy na output. wadau wengine naona wamekuwa kimya kina Nassib, Fatma, Mariam etc

    Like

    mwemezi

    July 31, 2011 at 8:57 am

  212. Wandugu Wote,
    Nashkuru kwa michango inayoendelea na kwa kweli nafarijika sana kwa michango. mie nimekuwa kimya nilikuwa na matatizo ya kuuguliwa binti hadi kupelekea kwenda India kwa matibabu tunashkuru tumerudi hajambo. Kwa hiyo kipindi chote hicho tulikuwa tumesimama shughuli ya ufaugaji kwani kama ujuavyo shughuli ukitaka ifanikiwe nawe uwe unai monotor na unajihusisha moja kwa moja bila hivyo waswahili hawaaminiki watakuangusha tu. Tuko pamoja
    NAssib

    Like

    Nassib

    August 1, 2011 at 2:55 pm

  213. Pole sana NAssib kwa kuuguliwa,. mungu amtie nguvu binti yako aweze kupona

    Like

    mwemezi

    August 1, 2011 at 3:17 pm

  214. Ndugu Mwemezi,
    Nashkuru sana.
    NAssib

    Like

    Nassib

    August 2, 2011 at 1:01 pm

    • Ndugu Nassib, pole sana kwa masaibu yaliyoikumba familia yako. Maisha yana changamoto nyingi. Kikubwa ni kutokata tamaa … kusonga mbele na kuendelea kukata mawimbi. Nafurahi kusikia kwamba kijana anaendelea vema. Hiyo ni sababu kubwa sana ambayo kwayo ni vema kumshukuru Mwenyezi Mungu. Kila la kheri katika kujipanga upya, hususan katika ufugaji kuku.

      Like

      simbadeo

      August 2, 2011 at 4:33 pm

  215. Ndugu simba
    Nashkuru sana. Na Mungu amejaalia tumeanza tena ufugaji rasmi
    Nassib

    Like

    Nassib

    August 3, 2011 at 8:52 am

  216. habari zenu,

    jamani hongereni sana kwa elimu mnayoitoa ktk jamii, binafsi nimevutiwa sana na comments zenu, mimi naishi mtwara kwenye nyumba ya kupanga lakini napenda sana kufuga kuku wa mayai najipanga nipate angalau banda dogo, niwe member. PAMOJA TUTAWEZA,

    kazi njema

    Like

    shakila

    August 10, 2011 at 12:36 pm

    • Hi Shakila, karibu sana katika kijiwe chetu. Tunakukaribisha kwa mikono miwili. Waswahili husema, palipo na njia pana njia. Weka nia nawe utafanikiwa katika mipango yako hiyo. Unakaribishwa kuuliza maswali na hata kujibu maswali. Hili ni jukwaa huru katika nyanja ya ufugaji kuku ambapo kila mdau ni mwalimu na vilevile mwanafunzi. Karibu sana.

      Like

      simbadeo

      August 10, 2011 at 9:33 pm

  217. wanandugu vifaranga vyangu vinaendelea vyema. nimegundua kwamba panya ni hatari sana kwa vifaranga. niliingiliwa na panya akaua kifaranga kimoja bahati nzuri kijana wa kazi akamuua kabla hajaleta maafa zaidi. jirani yangu alipoteza vifaranga 22 kwa ajli ya panya ndani ya siku mbili.

    ila jamani chakula cha Falcon ni very expensive (zaidi ya alfu 34,000 kwa mfuko wa Chick starter ) maeneo ya tegeta. naomba tubadilishane uzoefu wa gharama za chakula na wapi anagalau bei ni nzuri na at the same time chakula ni quality!!

    Like

    mwemezi

    August 14, 2011 at 12:26 am

  218. Wandugu,
    Kwanza niwape pole kwa shughuli za ufugaji kwani kama tujuavyo kitu muhimu ili tuweze kufanikiwa katika shughuli yoyote ile ni commitment bila hivyo hatufiki mbali. Jingine napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa bi Jenny kwa kuweza kupoteza muda wake jana jumapili na kunipeleka shambani kwake na kuona jinsi anavyoendesha shughuli nzima YA ufugaji; kwa kweil inatia moyo sana. Hana kinyongo analKelezea kila kitu bila kuficha ambapo wafrika sie wengi hatuko hivyo; miye nampongeza sana kwa hilo maana kwa kweli tumejifunza vitu vingi sana. (Isitoshe alipotuaga akatuachia tray nzima ya mayai na mayai yake ni mazuri sana!!). Nawaasa wenzangu shamba darasa zoezi lile naona tusilipuuze kwani ni njia nzuri ya kujifunza. Kutuembeleana ni muhimu kwani utajifunza mengi. Nasema tena hongera sana Dada Jenny Mungu azidi kukuzidishi mema. Asante
    Nassib

    Like

    Nassib

    August 15, 2011 at 10:15 am

  219. Duh! Nimepitwa muda mrefu, niko bize kwa kweli Da’ Eliza mziki huu step zake nyingi hadi naona kizunguzungu. Sitakuwa hewani mara nyingi kama awali, ufugaji ni kazi kama mifugo ni wengi. Nashukuru Kaka na Mama Nassib, mbarikiwe. Naamini mlipata vitu vichache vya kuongezea kwenye uzoefu wenu nami siku nikiwatembelea nitajifunza mengi tu.

    Leo nina swali:
    Mimi nafugia shambani, na sasa nakwenda kwenye ufugaji wa kati kutoka mdogo. Ninao hao vifaranga 1600 ambao natarajia kuwahamishia shambani mara tu watakapokuwa hawatoshi eneo walipo nyumbani ama wakifikisha miezi 2 kama watatosha hadi wakati huo.

    Ninapokwenda kuwahamishia shambani nitahitaji usalama kwa maana ya ulinzi madhubuti. Nauliza mnisaidie wajasiriamali, nifanyeje? Niajiri vijana zaidi, au nitafute kampuni za ulinzi niweke walinzi usiku wasaidiane na vijana 2 waliopo? Hasa mwezi Disemba wakifikisha miezi 5 ndio muda wa kukesha, na Krismasi itakuwa inapiga hodi. Naombeni ushauri wenu nifanyeje kuweka ulinzi madhubuti maana kundi kubwa linavutia kuibiwa kama ulinzi ni lege lege, wazoefu pia naombeni ushauri wenu, nauhitaji sana.

    Kaka Mwemezi hao vifaranga wanakomaa wakifikisha miezi 6. Asanteni sana.

    Like

    Jenny

    August 15, 2011 at 12:18 pm

  220. nimeona ni-share kipande hiki

    Q: HOW TO INCREASE EGG PRODUCTION IN MY HEN?

    A:make sure you feed them plenty of calcium rich foods and suppliments. if they are gogign to be laying many eggs, they use a lot of calcium to creat the egg shells. If they do not have enough in their body, they bodies will start extracting it from their bones. this will be your hens very unhealthy. be sure to give them suppliments containing fats and amino acids. also fruits, cooked meat, and veggies will aide in the process. do’n’t keep them cooped up all the time. let them run and get some exercise. also keep their cages clean so they are happy in their atmostphere
    source: http://answers.yahoo.com/question/index?qid=20070819075509AA0y88N

    A2: Lighting schedule. Egg production is stimulated by daylight; therefore, as the days grow longer production increases. In open houses, found commonly in the tropics, artificial lighting may be used to increase the laying period. When darkness falls artificial lighting can be introduced for two to three hours, which may increase egg production by 20 to 30 percent.
    (sijui applicability yake huku kwetu Tanzania).

    Note: according to FAO, Birds usually start to lay at around five months (20-21 weeks) of age and continue to lay for 12 months (52 weeks) on average, laying fewer eggs as they near the moulting period.

    Like

    mwemezi

    August 16, 2011 at 11:33 pm

    • Ndugu Mwezi, asante sana kwa kutupanua mawazo. Maarifa haya ni muhimu sana. Naamini wazoefu watakupatia majibu kwa swali lako kuhusu mazingira ya Tanzania na suala la mwanga hasa katika kuhusiana na kuku kutaga mayai. Asante sana.

      Like

      simbadeo

      August 17, 2011 at 7:05 pm

  221. Dada Jenny,
    Kuhsu ulinzi labda ujaribu kutafuta wamasai wanaweza kusaidia kwa hili ila tatizo nao wamasai wa siku hizi wankuwa hawaaminiki sana lakaini ukipata wale ambao wana wadhamini wankuwa kidogo afadhali; siye hapa tunapoishi nyumba za Jumua ya zamani tumewaajiri wamasai ndio wanaotulindia kiji chetu kwa hiyo nikaona nikupe wazo hilo; hawa wa malampuni nao pia hawaaminiki na malipo pia yanakuwa makubwa. Wamasai tunawapa mshahara wa Laki moja kwa mwezi na wako wawili.
    Nassib

    Like

    Nassib

    August 22, 2011 at 4:28 pm

  222. Asante kaka Nassib, nilikuwa nafikiria Wamasai ila sikuwa najua sana habari zao na jinsi ya kuwapata. Nadhani miezi ya hatari itakapokaribia nitapata suluhisho. Nalichukua wazo lako na nitakutafuta muda ukifika kabisa wa kuwaajiri hao watu. Asante na siku njema.

    Like

    Jenny

    August 22, 2011 at 4:43 pm

  223. habari zenu wapendwa?
    kwa kweli nimefurahishwa sana na majadiliano na mafunzo niliyoyapata, mimi pia ni mfugaji mdogo,shamba langu lipo visiga kwa sasa nina kuku wamayai 200 na wanyama 400. nimejifunza mengi sana natumaini tutaendelea kuwa pamoja.

    Like

    Erica

    August 23, 2011 at 3:48 pm

    • Hi Erica, karibu sana katika jukwaa hili. Jisikie huru kuuliza maswali yoyote uliyonayo kuhusu ulimwengu wa ufugaji na utajibiwa. Vilevile unakaribishwa kujibu maswali yatakayoulizwa hapa. Hapa kila mmoja ni mwalimu, kila mmoja ni mwanafunzi. Karibu.

      Like

      simbadeo

      August 24, 2011 at 9:45 pm

  224. Wasalaam
    kwanza nawashukuru woote wachangiaji, ni siku sasa yatimu miezi sita na nusu, nilifikiri kuwa mjasiliamali, niligoogle kupata habari kuhusu ufugaji niliposoma kidogo nikapenda sana! nikaprint page za maoni kama sabini hv wakati huo nikaenda kujisomea! leo nina kuku wa mayai 200 na wanataga tray tano na nusu kwa siku,wamenivutia niongeze zaidi yaani nianzishe shamba kabisa na mimi. Lakini sitawasahau kwani mmenifundisha kitu kikubwa sana woote mlioshiriki (Simbadeo, Jane,Eliza, Mwamizi, Juddy, Fatuma etc)ambao sijawataja naombeni radhi mchango wenu ni naushukuru hampotezi muda hapa kutuelimisha
    BenSam.

    Like

    Ben

    August 25, 2011 at 1:43 pm

  225. Habari za siku wadau, maendeleo vipi?

    Kaka Nasibu, ufugaji wa broilers ukoje? Nataka kujaribu, naleta batch ya kwanza alhamis. Nilitaka kujua broilers 100 wanakula chakula kiasi gani (mifuko mingapi) mpaka kuwauza? Kama una habari zingine muhimu za broilers tuhabarishe tafadhali.

    Like

    Elizabeth

    September 13, 2011 at 12:21 pm

  226. Dadfada Elizabeth,
    Ufugaji wa broiler si mbaya tatizo lake ni kwenye kuuza hapa maeneo yetu ya Chan’gombe bei inafluctuate kama dola vile!! leo bei ni nzuri na kesho unaona bei imeshuka ila ufugaji wake siyo mgumu na inategemea unataka kuku wako akae muda gani bandani ili afilie uzito fulani unaotaka ; ni kwamba akikaa muda mrefu na ukimlisha vizuri basi atakuwa mzito ila gharama ndio zinazidi. Kwa wastani kuku 100 hula kati ya mifuko 6 hadi 8 mpaka wanakuwa wakubwa ila usiwalishe mapumba sana kwani wengi wakiwa bado wadogo wanawalisha mapunga na chakula kidogo hivyo ukuaji unakuwa siyo mzuri unaweza kuwauza na wiki ya 20!!! kuku huhitaji kulishwa vizuri ili akue hakuna short cut ukitaka shortcut basi madhara yake utayaona.
    Nassib

    Like

    Nassib

    September 15, 2011 at 8:10 am

    • Nashukuru sana kaka Nassibu, jana ndo nimeweka broilers 1000 ngoja niwajaribu. Sasa hivi bei zake za jumla zina-range kwenye ngapi? Na je ili awe na angalau kilo moja anatakiwa kukaa kwa muda gani? Nataka nipige mahesabu ya chakula nisije nikahadhirika.

      Eliza

      Like

      Elizabeth

      September 16, 2011 at 10:02 am

      • Dad Elizabeth,
        Kukua kwa kuku inategemea chakula unachompa. Viko vyakula vingine havina vile virutubisho vinavyotakiwa na ndio maan wengine wanapenda kutengeneza vyakula vyao wenyewe. Kama nilvyokwambia kuku mia hula mifuko 6 hadi 8 kwa hiyo waweza piga hesabu hapo kwa kuku 1000. na wiki 5 hadi 6 kuku ndio anakuwa mzito. Kuhusu bei kwa kwelikama nilivyosema kwa maeneo yetu ni kama bei ya mafuta ya Tanzania leo inapanda kesho inashuka kwa hiyo maeneo mengine bei ni nzuri na maeneo mengine bei kidogo inakuwa chini kidogo.
        NAssib

        Like

        Nassib

        September 16, 2011 at 3:41 pm

  227. jamani habari zenu na za siku.

    samahanini kwa kuwa kimya kwa muda mrefu. nilifiwa na mama mzazi tarehe 6 september na tukamzika huko kijijini bukoba tarehe 10 september. nimerudi dar es salaam kama siku tano zilizopita. kwa hiyo msishangae ukimya wangu bana.

    kuku wangu 600 wa mayai (wapo wiki ya nane) wanaendelea vizuri ila bwana usiku bado wanataka mwanga, ukizima taa wanasongamana kiasi kwamba nimepoteza kuku 5 kwa ajili ya kusongamana. imebidi niendelee kuwawashia taa.

    alhamisi hii nimeongeza vifaranga 450 lengo ni kuwa na angalau kuku 1000 in total. vinaendelea vizuri na nimevinunua kwa jamaa mmoja anayevileta toka Uganda. hawana tofauti na wa Arusha Chick ila uzuri wa huyu jamaa anafanya chap chap haitakuchukua zaidi ya wiki moja au mbili kupata vifaranga.

    nitapiga picha kuku wangu na kuwatumia muone maendeleo. ila namshukuru kijana wangu ambaye pamoja na kutowahi kufuga kuku amekuwa na bidii ya kusoma majarida na vipeperushi ninavyompelekea na yeye sasa namuona kama ni mtaalamu kabisa. yupo makini kiasi kwamba akiona dalili kidogo tu tayari keshaenda Magito Pharmacy tegeta na kwa mtaalamu wa mifugo pale Tegeta kufanyiwa uchunguzi wa kina. mfano ni juzi juzi kuku walipata typhoid baada ya kunyweshwa maji ya kwenye kalo (maji yalikuwa yamekatika).. na mimi wakati huo nipo msibani bukoba. aliwahi kumpeleka kwa mtaalamu aliyegundua tatizo na kutoa dawa inayotakiwa.

    kwa uzoefu huu naamini kuwa kama mtu ni mfuatiliaji, kuku wanaweza wasife.

    ni hayo tu kwa leo
    mwemezi

    Like

    mwemezi

    September 25, 2011 at 9:33 am

  228. Pole sana Kaka Mwemezi, tunaomba mungu akupe nguvu zaidi katika kipindi hiki kigumu. Kuhusu kuku umri wao bado wanahitaji mwanga usiku, mimi nawawashia mpaka asubuhi hadi wakiishaanza kutaga kabisa ndo nazima taa mabandani kwenye saa nne usiku na kuziwasha asubuhi sana. Nakutakia kila la kheri.

    Like

    Elizabeth

    September 26, 2011 at 10:44 am

    • Ndugu Mwemezi,

      Pole sana kwa msiba huo. Ni msiba mzito. Hata hivyo ninakupongeza kwa kuubeba kwa moyo wa ujasiri. Maisha ni safari. Kila mmoja wetu huwa kwenye njia yake. Njia inapofika mwisho, basi imefika mwisho. Wale ambao njia zao zinaendelea … huendelea. Tunamwomba Mwenyezi Mungu ampe marehemu pumziko la amani. Amina.

      Wakati huohuo, pongezi kwa hatua uliyopiga katika ufugaji. Uzoefu unaoukusanya ni utajiri mkubwa. Kila la kheri.

      Like

      simbadeo

      September 26, 2011 at 8:51 pm

  229. salama jamani?
    kuku wangu wana shida, niliporudi toka kibaruani jana nikakuta wana mafua yaani hadi huruma nahisi jana walitimua vumbi sn, kuna dawa gani nzuri ya kuwatibu au huduma ya kwanza unayoweza kufanya ni ipi?
    BenSam

    Like

    BenSam

    September 27, 2011 at 5:05 am

  230. Pole Kaka Mwemezi, Mungu awafariji na kuwatia nguvu ya kusonga mbele.

    BenSam, pole kwa kuku wako kukumbwa na mafua. Mafua yanaua kuku vibaya sana yasipotibiwa, lakini habari njema ni kwamba yanatibika kwa dawa za mafua ya kuku kama watapata tiba. Wahi dawa, angalau ndio ushauri ninaoweza kukupa. Huduma ya kwanza sijui kama ipo kwa mafua. Anflox Gold ni nzuri, kuna pia nyingine nyingi uombe dawa ya mafua makali.

    Pia angalia kama una vijana wanakusaidia wasiweke maranda mabichi, yenye unyevu nyevu au yenye vumbi, kama ndiyo unayotumia kutandaza chini. Huwa ni chanzo cha mafua makali sana kwa kuku.

    Wahi dawa kabla hawajaanza kufa.

    Like

    Jenny

    September 27, 2011 at 8:22 am

    • Asalaam aleykum,
      Ndugu wadau, nilipotea nilikuwa ninamishe mishe za daslam, baada ya kuku wangu kuugua mafua wakapona, typhoid wakapona baada ya kufa takribani kuku 23 sasa wapo 180 na sasa hawataki kupandisha mayai licha ya jitihada nilizofanya za kuwapa GLP, extra eggs, vitamins, minerals na kubadilisha chakula. kwa sasa napata mayai 85 mpaka 97 hv wastani wa tray 3 ambazo ni hasara kuwa nao kwani wanamudu kujilisha wenyewe tu. hivyo nimepanga niwauze sikukuu hizi za x mass na mwaka mpya. kwa sasa wana miezi takribani kumi wana afya.

      Swali 1, naweza kupata soko kwa bei gani walau nirudishe pesa na nianze upya?
      swali 2, naomba mawasiliano ya soko sehemu ya kuuzia, i mean mnunuaji
      BenSam

      Like

      BenSam

      December 14, 2011 at 11:12 am

      • Hello Ben, umeshamleta daktari mzuri wa kuku kuwatizama? Inawezekana wako kwenye molting process! Pole, ndio ufugaji anyway. Wengine watakujuza zaidi.

        Like

        Jenny

        December 14, 2011 at 12:24 pm

      • Hi Jenny, najaribu kugoogle nijue hiyo molting maana yake ni nini, naomba nijuze nn maana yake,
        nimejaribu kuleta daktari nilikuwa namtumia toka wawe wadogo ambaye pia ni mfugaji, alafu kila kuku aliyekufa nilkuwa nampitisha pale farm base wanampasua wananiambia tatizo na nanunua dawa walizonishauri, ss sijui ni nn? labda kama kuna aliyewahi pata tatizo kama hili anishauri?
        Ben Sam

        Like

        BenSam

        December 14, 2011 at 12:46 pm

      • Molting ni process kuku wanapitia ya kupumzika kutaga. Wanaacha kabisaaa kutaga utapata mayai machache tu kwa siku kwa wale watakaochelewa, wananyonyoka manyoya yao, wanapoanza kuota mapya wanajiandaa kuanza tena uzalishaji lakini sio kwa % kama ya mwanzo, hushuka kidogo. Sometimes wanawahi ku-molt kwa sababu ambazo mimi binafsi sikuzifahamu labda madaktari wanaweza kusema ama uki-search zaidi. Pia nikuulize, umewachunguza hawana chawa ama wadudu wanaowasumbua? Je, dawa ya minyoo unatoa kila baada ya muda gani? Tatizo dogo tu kwa hao ndege wanashusha uzalishaji, utahangaika kila kitu na kubadili vyakula hadi upatie shida yao. Labda angalia na pande hizo zingine pengine kuna kitu kinawakera au kuwasumbua ndio maana. Uzoefu wangu pia wakati wa joto, kama linawasumbua wanashuka uzalishaji, na hii ndio miezi ya joto, sasa inategemea mabanda yako yakoje kuna hewa nzuri inapita ama joto lipo jingi. Siku njema.

        Like

        Jenny

        December 14, 2011 at 2:21 pm

      • Hello BenSam, hao layers waliendeleaje? Uliwauza ama ulifanikiwa kupandisha uzalishaji wao?

        Like

        Jenny

        January 19, 2012 at 1:53 pm

      • Hallow Jenny
        yaani haikuwa rahisi kuweza kuchukua uamuzi wa kuuza kuku ila ilibidi, hivi ss wapo 25 nashukuru hii x mass na mwaka mpya niliwauza japo kwa mkopo kwa bei ya 15,000/- kurudisha walau cost. nashukuru Mungu nimekuwa kwenye business kwa mwaka mmoja na nimepata xperience kiasi hicho. Ni kweli kama unavosema joto llikuwa sababu na panya walikuwa wanasumbua na kubwa kuna binti niliyekuwa namtegemea akadanganywa na majirani akaondoka so nikashake kidogo. Kiukweli iliniumiza but nitaanza upya tena nina kila sababu! safari hii nimejipanga upya tena site kinyerezi, nimeanza kidogo ujenzi wa banda.
        BenSam

        Like

        bensam

        January 19, 2012 at 4:10 pm

      • Afadhali hata ulipata bei nzuri kuwauza, kwa layers kuuza 15,000/= kila mmoja ni bahati. Wasaidizi kwa kweli ndio huwa wanatuangusha mara kwa mara. Natumaini utaanza tena vizuri na kwa ari zaidi maana huo pia ni uzoefu katika ufugaji. Nakutakia mafanikio.

        Like

        Jenny

        January 20, 2012 at 7:19 am

  231. Pole sana kaka Mwemezi kwa msiba mkubwa uliokupata (Inna lillah waina illah Rajiuna) mbele yake nyuma yetu, yeye ametangulia na sisi tuko nyuma yake, pia hongera sana kwa hatua uliyofikia. Mimi nilikuwa bussy na shughuli kidogo lakini sasa hivi nitarudi kundini.

    Like

    Fatma

    September 28, 2011 at 8:34 am

  232. Ndugu Mwemezi,
    Hongera sana kwa shughuli yako ya ufugaji na pole kwa msiba ulioupata. Nafurahi pia kwamba blog yetu imekuwa live tena kwani ni muda ilikuwa watu wako kimya . Ntaomba niwaone hao kuku wa Uganda wanafananaje, tutumie hiyo picha kama ulivyoahidi.
    Ahsante
    Nassib

    Like

    Nassib

    September 29, 2011 at 8:28 am

  233. Habari zenu wote!!

    Nimesoma michango yenu mizuri na ya kutia moyo, nimevutiwa sana sana na nimejifunza mengi sana. Nakupongeza sana kaka simbadeo kwa kuanzisha hii blog inasaidia na itazidi kusaidia wengi.

    Mimi pia ni mfugaji mdogo na ninapenda sana ufungaji na nina malengo ya kuwa mfugaji mkubwa. Kwa sasa ndio nimeanza na kuku 500 wa mayai na wamefikasha wiki ya 11, kwa bahati mbaya hadi kufika sasa wamekufa kuku 54. Walipatwa na ugonjwa wa gumboro, inaonekana chanjo tuliyotumia ilikuwa imeharibika kutokana na matatizo ya umeme. Wafugaji wengi waliokuwa wananunu dawa duka hilo walipata hasara sana na wengine wamepoteza karibu kuku wote.

    Hata hivyo namshukuru Mungu amenisaidia, waliobaki wamepona na wana afya nzuri.

    Nimependa sana michango yenu (Jenny, Elizabeth, simbadeo, Fatma, mwemezi, Nassib n.k.).

    Napenda kuwapongoza kwa hatua mliyofikia katika ufugaji wa kuku, na tena napenda kuwashukuru kututia moyo sisi ambao tunaanza, Mungu awabakiri sana.

    Pia naomba msaada wenu, mnijulishe maduka ya madawa ya mifugo ambayo ni waaminifu na wanauza dawa na chanjo za uhakika. Mimi nafufiga maeneo ya Tegeta.

    Asanteni sana!!

    Like

    EL

    October 1, 2011 at 10:38 am

  234. hongera sana EL kwa ufugaji na pole sana kwa idadi ya vifo.

    mimi nanunua dawa duka la Magito pale tegeta, na wakati mwingine nanunulia dawa pharmacy ya hapo Tegeta kibaoni karibu na opposite na Petrol filling station.

    mimi nilianza na kuku 607 na sasa wana wiki 9 na waliokufa ni 9. nilichogundua inabidi uwepo wewe mwenyewe mara nyingi na hakikisha una kijana mzuri. narudia tena kijana mzuri ambaye anaipenda kazi yake!. uwe unamletea vitabu na majarida ya kiswahili asome. Pata muda wa kukaa naye msome wote vitabu hivyo na kueleweshana!

    Aidha napenda kuwapa ujumbe huu toka kwa Rose (mtotoleshaji wa vifaranga vyeusi – Mbezi beach Karibu na Masana Hospital):…… hapa nanukuu:

    “kuna tatizo la kuku ambalo linasababishwa na ukosefu wa vitamin A hasa pale wanapokosa majani ya kutosha yenye vitamin A kwa wingi. Madhara yake ni utaona kuku kama anakunguta kichwa kwa sababu macho yanatoa machozi, baadae utaona yanavimba na ukikamua yanatoa kitu kama kipande cha mhogo, ukichelewa kutoa dawa anakuwa kipofu. kinga yake ni INTROVIT A % WS wapewe angalau kwa wiki moja kwa mwezi. kama utaona dalili za ugonjwa watenge na kuwatibu kwa dawa ya macho yenye antibiotic.

    mwemezi

    Like

    mwemezi

    October 1, 2011 at 11:28 am

  235. EL mimi naishi tegeta karibu na uwanja wa nyuki, ila nafugia mbweni

    Like

    mwemezi

    October 1, 2011 at 11:28 am

    • Ndugu mwemezi,

      Asante sana!!

      Hongera sana kwa kuendela vzr na kuku wako, pia pole sana kwa kuondokewa na mama, Mungu akutie nguvu brother.

      Nimependa huo ushauri wako wa kuwapa vijana wa kuangalia kuku vijarida/vitabu na kusoma pamoja nao. Maana baadaye kuku watakapokuwa wengi nitajenga mabanda mengine shambani goba na kule kutakuwa na kijana wa kuwaangalia.

      Mimi naishi Mbezi ya Kimara. Tegeta ninapofugia kuku ni kwa wazazi wangu na mama yangu ndio anawaangalia na mimi kila weekend huwa naenda kuwangalia. Pia alishawahi kufuga kuku wa nyama na wa mayai kipindi cha nyuma wakati wanaishi Dodoma, hivyo anauzoefu kiasi fulani.

      Hilo duka la magito ndiko tulikonunulia hizo dawa za chanjo na hazikufanya kazi, hata wenyewe walikiri kuwa watu wengi waliwaletea malalamiko ya vifo vya kuku kwa ugonjwa wa gumboro. Wewe unabahati kama ulinunu hapo chanjo ya gumboro na umepona kwa hilo, mshukuru sana Mungu. Asante pia kwa kunijulisha kuwa kuna phamacy hapo kibaoni.

      Pia tunashukuru kwa ujumbe kutoka kwa Rose. Itabidi na mimi nitafute hiyo kinga (INTROVIT A % WS) kwa ajili ya kuku wangu.

      Thanx!!!

      Like

      EL

      October 1, 2011 at 4:50 pm

  236. Asalaam aleykum wana ukumbi wote,
    Kaka Mwemezi naomba unipe contact za huyo jamaa mwenye vifaranga vya Uganda kwani na mimi ninavihitaji na yeye anapatikana wapi kama ni agent naomba unifahamishe niweze kufanya utaratibu wa kupata hivyo vifaranga.
    Nitashukuru sana.

    Like

    Fatma

    October 3, 2011 at 12:08 pm

  237. habari zenu wafugaji mimi nataka kuanza ufugaji wa kuku wa nyama nauliza idadi ya kuku 400wana uwezo wa kula chakula mifuko mingapi mpaka wafikie wiki nane

    Like

    nai

    October 8, 2011 at 11:44 am

  238. Asalaam aleykum wajasiriamali wote wapenda maendeleo yao na ya watu wengine,kwa kweli mimi ndio kwanza naanza kuingia katika fani hii ya ujasiriamali wa ufugaji wa kuku wa nyamaa, lakini kutokana na mada zetu nzuri na zilizojitosheleza, naomba mnipokee kwani ndio naanza mimi nimejenga banda lenye ukubwa wa mita 10 naomba kuuliza kwenye hilo banda niweke vifaranga wangapi? na je vifanga wa interchick ni Wazuri kwa ufugaji ikiwa maana kwamba hawafi sana? nasari yao inakuwa na ukubwa kwani? nauliza hivyo kwasababu mimi ninaishi maeneo ya Mbezi.Na chakula kizuri kwa vifaranga ni kipi kwani siku hizi vyakula ni vingi sana,ila mimi ni kufuga kuku mwenye uzito kuanzia kilo moja hadi kilo moja na nusu na kuendelea. Nawategemea sana kwa ushauri wenu.

    Like

    Johana

    November 10, 2011 at 5:05 pm

  239. Nauza bata mzinga wakubwa na kanga na bata bukini wakubwa 0757662401

    Like

    Kitomary

    November 25, 2011 at 8:37 pm

    • Ndugu Kitomary. Karibu sana katika jukwaa hili. Tunafurahi kupata taarifa za biashara yako ya Bata Mzinga na Kanga, na vilevile Bata Bukini. Ili kuonyesha kile unacholenga. Tafadhali piga picha ya bata na kanga hao kisha itume kwa kakasimba@gmail.com ili ziwekwe kwenye jukwaa hili kwa ajili ya wadau wote kuona kwa macho yao. Kuona ndiyo kuamini, au siyo?

      Kwa wadau wa jukwaa hili. Nimekuwa kimya kidogo. Naona hata mpango wetu wa shamba darasa umesimama. Kwa bahati mbaya nimekuwa kwenye ratiba ngumu ya kazi, hunichukua hadi siku za weekend na sikukuu. Lakini, inshaallah, kuna siku tutafanikisha — kama ambavyo Da Jenny alivyokwishaanza siku za nyuma. Karibuni na tuendelee kuwa pamoja, kwa ushauri, taarifa, maoni, miongozo n.k. Pamoja.

      Like

      simbadeo

      November 26, 2011 at 12:38 am

  240. Jamani katika pekua pekua yangu ya mitandao mbali mbali nimejikuta naigundua blog hii ikanifurahisha sana kwa kuwa nami najipanga kuanza ufugaji wa kuku. Nagonga hodiii kwa wenyewe.

    Like

    Vyagusa

    December 2, 2011 at 1:45 pm

    • Ndugu Vyagusa. Karibu sana kwenye jukwaahili la majadiliano. Jisikie nyumbani kutoa dukuduku lolote linalohusu fani hii ya ufugaji kuku na wanyama wengineo wa jamii hiyo. Tupo pamoja.

      Like

      simbadeo

      December 2, 2011 at 3:09 pm

      • Kaka Simbadeo,

        Nimechelewa sana kuingia tena ktk ukumbi huu kwa sababu nilitingwa sana na mambo ya makazi. Mimi ningependa kufuga kuku mchanganyiko – wa kisasa na wa kienyeji, wa nyama na wa mayai pamoja na Bata Mzinga na Bata Bukini.

        Nitapenda kuwatembelea wakongwe ktk ufugaji ili kujifunza mengi kwao

        Like

        Gubas Vyagusa

        March 16, 2012 at 2:16 pm

      • Karibu sana Gubas Vyagusa … jishirikishe katika jukwaa hili. Naamini utatufunza mengi na kujifunza mengi pia. Karibu.

        Like

        simbadeo

        March 21, 2012 at 11:35 pm

    • Vyagusa karibu, hapa utapata karibu kila kitu muhimu unachohitaji kuanza, usichoke tu kusoma posts zilizopita. Karibu sana barazani.

      Like

      Jenny

      December 14, 2011 at 2:26 pm

      • Da Jenny, nimechelewa sana kuingia tena ktk ukumbi huu kwa sababu nilitingwa sana na mambo ya makazi. Mimi ningependa kufuga kuku mchanganyiko – wa kisasa na wa kienyeji, wa nyama na wa mayai pamoja na Bata Mzinga na Bata Bukini.

        Aidha nadhani ktk michango yako inaonekana unaishi Ukonga Magereza, nami nilikuwa naishi Mombasa jirani na Hosp ya Mahita ingawa sasa nimehamia Kigamboni. Nitakupigia simu ili siku moja nije kujionea mwenyewe ufugaji wako. Simu yangu ni 0756 399 070

        Like

        Gubas Vyagusa

        March 16, 2012 at 2:14 pm

  241. Natafuta mayai ya kutotolesha ya hoa kuku wanaouzwa kwa amadori je ntawezaje kuyapata

    Like

    Jacob Mkoba

    December 13, 2011 at 1:56 pm

    • Labda ungewaona watu wa Amadori wenyewe.

      Like

      Jenny

      December 14, 2011 at 2:27 pm

  242. Hamjambo wapendwa? Wageni wote karibuni sana. Kwa wale wanaowasiliana na mimi moja kwa moja kupitia simu yangu tafadhali naomba tuanzie hapa ili kufahamiana kwanza na pia kuwa faida kwa wote. Tukiwasiliana watu 2 tu jamani kweli itakuwa na faida gani? Hata mimi nauliza mengi na napenda kujifunza kwa wengine, hivyo nawaomba wale mnao-note namba yangu ya simu na kunitafuta mkiwa hamjachangia chochote hapa tuanzie hapa. Urafiki hujengwa na dunia ya leo ni ya hatari, kuaminiana sio rahisi kama hakuna kufahamiana kwanza.

    Kaka Deo nisaidie nifanyaje ama unaweza kuifuta namba yangu pls?

    Like

    Jenny

    December 14, 2011 at 9:50 am

    • Dada Jenny nadhani mmoja wa watu walioonyesha nia ya kutembelea mabanda yako ni mimi, ila unapoanza kuhofia au kuingiza hisia za kutoaminiana nadhani haitakuwa vema. Mimi binafisi najiamini kabla sijaaminiwa na mtu mwingine hivyo haina haja ya kuhofia. Najua na wengine watasema ni waaminifu

      Like

      Gubas Vyagusa

      April 24, 2012 at 1:38 pm

      • Vyagusa, habari za siku? Nilikuwa nawazungumzia wageni wanaopita kimya wakiperuzi mtandaoni na si wenyeji au wale wanaoonekana kuwepo jamvini, ambao baadhi niliwapokea na kuwapeleka shambani kwa mara ya kwanza kuonana nao. Nadhani umesoma kwa haraka haraka bila kuelewa maana halisi ya nilichokuwa nakizungumzia. Sidhani kama wewe utachukulia ni kawaida tu, watu usiowafahamu kabisa wala kuwahi kusoma makala zao hapa wakakupigia simu na kuanza kukuuliza habari za kuku! At least kunatakiwa kuwe na ushirikiano tulio nao hapa jamvini kuweza kujua mtu unaongea na nani. Wale tulioko hapa jamvini tunafahamiana, ukinipigia ukataja wewe ni Vyagusa, napata picha kamili na tunawasiliana bila tatizo. Nilichokuwa nakwepa ni kugeuka mshauri wa kuku kwa watu ambao hata hapa jamvini hawapo. Kumbuka hapa hatusajili kuwa wanachama, mtu yeyote anaweza kusoma akachukua namba yako na kuanza kuwasiliana na wewe. Sikuwa na hofu wala hisia na chochote isipokuwa, nilikuwa nashawishi kuwepo hapa zaidi ili ushauri, maswali, majibu, maelezo na yote tunayowasiliana yatufae wote kuliko kujibu maswali ya kuku katika simu nyingi, kwa watu ambao wanapita hapa kimya kimya kabisa wakisoma tu. Nakutakia siku njema na kazi njema.

        Like

        Jenny

        April 25, 2012 at 8:19 am

      • Hello,

        Kwa kuchangia kidogo. Wazo la kuunda umoja ni zuri sana. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Hata hivyo, yafaa kupeleleza ili kuona kama hakuna umoja uliokwishaundwa tayari. Kama upo, basi huo uimarishwe. Kama hakuna, basi zifanyike taratibu za kuuanzisha.

        Ninaunga mkono hoja ya Da Jenny. Kuna wapita njia hapa. Jukwaa hili lilikuwa na madhumuni ya ‘kujengana’. Maana yake ni nini. Kiubinadamu, mtu huwezi kujua kila kitu, lakini pia huwezi kukosa cha kuchangia. Kumbe basi, mtindo hapa ni wa wewe kutoa kile unachokijua na kupokea kile usichokijua. Kwa mantiki hiyo, kila mshiriki ananufaika na kujengeka. Ni jukwaa la wazi na huru linaloheshimu ufahamu na uelewa wa kila mmoja. Kumbe basi, kama unapita hapa, anza kwanza kutoa – hata kwa kuuliza maswali – na vilevile uchukue. Hakuna mwisho katika kujifunza.

        Nawashukuru wachangiaji wote na wale wote wanaopasha moto jukwaa hili. Tuendelee kuwepo.

        Like

        simbadeo

        April 25, 2012 at 11:14 pm

  243. Jamani hamjambo wapenzi wote wa ukumbi huu kwanza Nawatakieni Kheri ya Mwaka Mpya. Pili naomba tuendelee kueelimishana zaidi kuhusu ujasiriamali ili wale ambao hawajaanza waweze kuthubutu na sisi ambao tumeshathubutu basi tuendelee ili tufikie pale tunapopata. Nawaombeni wale wenye mambo mapya watuletee ili tuweze kusoma na kuchangia hoja. Karibuni wote, asanteni.

    Like

    Fatma

    January 10, 2012 at 8:07 am

  244. wasalaam!
    Wadau habari zenu, nilipata kumtembelea rafiki mfugaji maeneo ya Kitunda karibu na njia panda ya kwenda Mbagala kwa waliofika. Nilijifunza mengi lakini kubwa tulikutana na jamaa anaitwa MUSOMA huyu kwa waliowahi fika hapo ana duka la dawa ambalo ndio kama meeting point ya wanunuzi wa mayai wa pikipiki na baiskeli na ununuzi wa madawa na chakula hufanyika hapo na wafugaji wengi kabla ya kuelekea shambani, pia huyu jamaa ni muagizaji wa vifaranga toka Uganda, lengo sio kumadvertise huyu MUSOMA lengo ni hili.

    Jamaa aliniambia kuwa wana lengo la kuitisha mkutano wa wafugaji akinitaka kuwa niungane nao nikawaambia aniambie ni lini lakini nikamwambia kuna wafugaji wengine nitawaambia ambao ni ninyi, malengo walio nayo ni mengi lakini kubwa waliloliwaza ni hii kuwa kuna tetesi kuwa mayai yanaweza kushuka tena bei, ebu fikiria chakula na gharama za utunzaji wa kuku umepanda siku nyingi alafu hy bei imepanda juzi tu then wanataka washushe sababu kubwa ninayoona hawa wanunuzi wana umoja, nikaona ni wazo zuri kwa kuanzia. Nikawaza mengi tukiwa na umoja tunaweza kufanya vizuri pamoja licha ya ukweli kuwa umoja ni nguvu, wakulima wengi hata mataifa yaliyoendelea wana umoja wao na huu unaweza kufanya kufanya mengi.. nikawaza kuboresha swala la bei(we can effect and control price), kuanzia selling point na kutafuta soko kwa pamoja ndani na nje ya nchi, kutafuta mtaji kwa pamoja, kupunguza gharama za usagaji wa chakula tunaweza kuwa na mashine zetu wenyewe, kuongeza kipato zaidi, kusaidia uongezekaji wa ajira, network, mawazo mazuri ambayo naamini humu ndani kuna watu wana capacity mbalimbali.,wadau hayo ni mawazo yangu naombeni mchangie kwa pamoja tunaweza zaidi.

    BenSam

    Like

    bensam

    January 20, 2012 at 11:32 am

    • Bensam, nashukuru sana kwaw taarifa yako nzuri. nina machache haya:

      1) naungana na wewe kuhusu kuwa na umoja wa wafugaji wa kuku; labda cha kujiuliza ni kama kuna umoja wa namna hii au hamna.

      2) huyo MUSOMA seems ni mtu muhimu sana kukutana naye (ninaomba unitumie namba yake ya simu nimtafute — my email ni unaweza kunirushia kwa ngemera@gmail.com). bila kusahau na namba yako Mh. Bensam

      3) uliposema wanapanga kushusha bei ya mayai, labda ungetujuza zaidi ni nani anapanga kushusha bei? hao watu wa pikipiki na baiskeli au nani. tatizo ninaloliona mimi ni kuwa wakulima wanashindwa kuwa na nguvu wao wenyewe na kushindwa jujitetea. mimi nilipoanza kuuza mayai nilifanya kwa alfu tano then nikaenda hadi 6500 (up to now) lakini wateja wangu walikuwa wanagoma ile mbaya na wakatishia kuwa hawatachukua tena kwangu. mimi niligoma kuuza kwa bei ya 6000/= .. na in fact nataka kupandisha kuwa 7000 kwa sababu chakula ni very expensive (mfano layers’ mash ya FALCON imepanda toka 32,500 hadi 34,500.. hapo hujaweka gharama nyingine.

      4) inabidi watu tujifunze kutafuta masoko sisi wenyewe si kutegemea waendesha pikipiki na baiskeli

      5) Binafsi naanza ku-predict watu wengi watashindwa kufuga kuku wa mayai maana gharama zinapanda kwa kasi sana. umeme umepanda, maji nayo yatapanda. Je hapo kweli mtu utaweza kumudu hii biashara?

      mwisho naomba kuuliza tena je kuna umoja wowote wa wafuga kuku?

      bensam, vipi huko ulipoenda kujifunza Kitunda pakoje. Je na baadhi yetu tukitaka kwenda kwa huyo jamaa kujifunza.

      mwisho naomba msaada wenu. mimi nakodisha mabanda ya mtu. naona ni vema nijenge ya kwangu. naombeni msaada wenu wa wapi naweza kupata sehemu yakujenga mabanda ya kuku takribani 5000 (0bvious mtaji wangu ni mdogo ila hayo ni malengo ya muda mrefu). sehemu inaweza kuwa hapa Dar au Mkuranga au Bagamoyo au Kibaha.. kikubwa iwe ni karibu na source ya maji.

      ahsante

      Like

      mwemezi

      January 20, 2012 at 12:42 pm

    • Jamani nimeona nichangie kidogo kuhusu kuanzisha UMOJA WA WAFUGAJI. Awali ya yote naungana na mdau alileta wazo la kuanzisha umoja huo kwa sababu Watanzania tumezoea kufanya shughuli zetu kibinafsi/kwa mtu mmoja mmoja.

      Ili umoja ulete manufaa yaliyokusudiwa, kwa mfano, kuboresha bei, kuanzisha selling point na kutafuta soko kwa pamoja ndani na nje ya nchi, kutafuta mtaji kwa pamoja, kupunguza gharama za usagaji wa chakula kwa kumiliki mashine wenyewe, kuongeza kipato zaidi, kusaidia uongezekaji wa ajira ni lazima umoja/chama hicho kisajiliwe rasmi na kitambuliwe na vyombo vya serikali.

      Suala la kuanzisha chama/umoja wa wafugaji nadhani linashughulikiwa na Ofisi ya Ushirika Wilayani (kwa DSM ni Manispaa) kwani ni aina ya chama cha USHIRIKA (Cooperative Society). Chama kikikua vizuri kinaweza kujenga hata kiwanda cha kusindika nyama ya kuku ili kila mfugaji auze kuku wake kiwandani badala ya kuhangaika mwenyewe kutafuta masoko. Kiwanda kikiwepo kitamaliza tatizo la masoko kwa wateja na wakati huo huo kitaingiza faida mara dufu kwa wafugaji na kutoa ajira kwa watu wengine watakaofanya kazi kiwandani.

      Hivyo basi nashauri mchakato wa kuanzisha CHAMA CHA USHIRIKA CHA WAFUGAJI KUKU uanze mara moja – Binafsi japo mimi bado ni mgeni wa jukwaa hili naahidi kujitolea kufanya kazi ya kutayarisha KATIBA YAKE, ila bado sijajua masharti mengine lakini lazima kutakuwa na idadi fulani ya wanachama waanzilishi.

      Nawasilisha

      Like

      Gubas Vyagusa

      April 24, 2012 at 1:24 pm

  245. Habari zenu wadau!
    Mimi niko Mwanza. Ni mara yangu kwanza kushiriki katika kijiwe iki kwani nilipopata wazo la kuanzisha ufugaji wa kuku, kitu cha kwanza nilichokifanya ni kutafuta taarifa za kitalaamu. baada ya kugoogle nilipata taarifa mbalimbali kwa lugha ya kiingereza. Pia katika kutaka kujua uzoefu wa wafugaji wa hapa nchini nilikutana na ukurasa huu.
    Nimesoma takribani comments zote, natoa pongezi kwa muasisi wa blog hii na wadau wote waliotoa maoni na uzofu wao kwa mazingira ya hapa TZ. Mungu awabariki.
    Kwa sas najiandaa kuanza na kuku 500 ili nipate uzoefu. nimeona vifaranga wanatoka Kenya lakini bei mkasi kweli, wana uzwa sh. 2500 kwa kifaranga. Tatitizo si bei ila ubora wa kuku hao. Naomba kama kuna mdau anafuga kuku wa kutoka Kenya anipe uzoefu kwa upande wa uzalishaji (productivity). Kraibuni Mwanza.

    Like

    bahati

    January 31, 2012 at 11:01 pm

    • Ndugu Bahati, karibu sana kwenye jukwaa hili. Tunakupongeza kwa kudhamiria kuanzisha mradi wa ufugaji kuku. Ni jambo la maana kwako, kwa familia yako na kwa jamii itakayonufaika na huduma zitakazotolewa na mradi huo. Naamini wanajukwaa wamesoma maswali yako na watakupatia majibu. Endelea kutembelea jukwaa hili ili kupata majibu hayo na vilevile wewe kuchangia hoja mbalimbali. Katika jukwaa hili, kila mmoja ana kitu cha kuwashirikisha wengine. Karibu sana.

      Like

      simbadeo

      February 1, 2012 at 8:32 am

  246. MKUTANO MKUBWA KUTHIBITI MAYAI HATARISHA KUTOKA KENYA WAFANYIKA.

    Guys, am proud of joining you in this bad time we are facing a price and market challenges.
    tumevamiwa na uingizwaji wa mayai feki kutoka Kenya ambayo yanaingia kwa njia za panya.

    kuna mdau kaongelea mkutano wa wafugaji ili tuwe na nguvu ya pamoja kuthibiti mapungufu na kuendeleza ubora na uzalishaji wa hali ya juu ili tuweze kufanikiwa!

    Hili limefanyika sambamba na kuwasilisha ujumbe kwa serikali kuhusu matatizo yanayoyukumba.
    TUTAKUWA NA MKUTANO MKUBWA TAR. 17/03/2012 PALE BANANA (GONGO LA MBOTO) – NGEMO ANNEX PEMBENI MWA BARABARA YA KUELEKEA KITUNDA.

    Naomba atakayepata taarifa hii amjulishe na mwenzie – 0713750055

    Like

    ignatus

    March 13, 2012 at 9:35 pm

    • Asante kwa taarifa Ignatus. MSHIKAMANO ni muhimu katika kupinga UONEVU au UNYONYAJI wa aina yoyote. UMOJA ni nguvu na utengano ni udhaifu. Wafugaji wa hapa nchini, ni wakati wa kujipigania na kuwapigania walaji wenu. Kwa sababu endapo watu wataanza kudhurika kwa sababu ya kula ‘mayai hayo feki’ ni wazi kwamba biashara yenu kwa ujumla wake itaathirika … Maana watu wataogopa kula mayai. Ni vema kuungana na kupambana na uharamia huu. Ni vema kujilinda na kuwalinda wateja wenu. PAMOJA sana.

      Deo Simba

      Like

      simbadeo

      March 14, 2012 at 12:04 am

      • Simba Deo,

        Asante kwa blog yako nzuri na ya kuelimisha jamii.

        Naomba muongozo wa kutengeneza chakula cha kuku kwa ajili ya kuuza kwa wafugaji, au niwaone watengenezaji gani wakubwa wa chakula cha kuku.. Asante

        Like

        Laurent Ruge

        April 16, 2012 at 1:50 pm

      • Karibu Ndg Laurent.

        Naamini wadau katika jukwaa letu watasoma swali lako na kutoa majibu mwafaka. Karibu sana wewe pia uchangie maarifa uliyo nayo. Hili ni jukwaa la kujengana ambapo kila mmoja analeta maarifa aliyonayo. Karibu sana.

        Like

        simbadeo

        April 17, 2012 at 12:24 am

  247. Ndugu wadau,

    Wakati nasubiri majibu ya namna ya kutengeneza chakula, ninaomba nifahamishwe majina ya wauzaji wa jumla wa chakula cha kuku. Nimepata majina mawili, Falcon na Eagle, je kuna wengine?? Asante kwa michango yetu.

    Ndg Simba Deo , saidia katika hili!

    Like

    Laurent Ruge

    April 17, 2012 at 2:10 pm

  248. Jamani nimeona nichangie kidogo kuhusu kuanzisha UMOJA WA WAFUGAJI. Awali ya yote naungana na mdau alileta wazo la kuanzisha umoja huo kwa sababu Watanzania tumezoea kufanya shughuli zetu kibinafsi/kwa mtu mmoja mmoja.

    Ili umoja ulete manufaa yaliyokusudiwa, kwa mfano, kuboresha bei, kuanzisha selling point na kutafuta soko kwa pamoja ndani na nje ya nchi, kutafuta mtaji kwa pamoja, kupunguza gharama za usagaji wa chakula kwa kumiliki mashine wenyewe, kuongeza kipato zaidi, kusaidia uongezekaji wa ajira ni lazima umoja/chama hicho kisajiliwe rasmi na kitambuliwe na vyombo vya serikali.

    Suala la kuanzisha chama/umoja wa wafugaji nadhani linashughulikiwa na Ofisi ya Ushirika Wilayani (kwa DSM ni Manispaa) kwani ni aina ya chama cha USHIRIKA (Cooperative Society). Chama kikikua vizuri kinaweza kujenga hata kiwanda cha kusindika nyama ya kuku ili kila mfugaji auze kuku wake kiwandani badala ya kuhangaika mwenyewe kutafuta masoko. Kiwanda kikiwepo kitamaliza tatizo la masoko kwa wateja na wakati huo huo kitaingiza faida mara dufu kwa wafugaji na kutoa ajira kwa watu wengine watakaofanya kazi kiwandani.

    Hivyo basi nashauri mchakato wa kuanzisha CHAMA CHA USHIRIKA CHA WAFUGAJI KUKU uanze mara moja – Binafsi japo mimi bado ni mgeni wa jukwaa hili naahidi kujitolea kufanya kazi ya kutayarisha KATIBA YAKE, ila bado sijajua masharti mengine lakini lazima kutakuwa na idadi fulani ya wanachama waanzilishi.

    Nawasilisha

    Like

    Gubas Vyagusa

    April 24, 2012 at 1:26 pm

  249. Wajameni, naomba msaada wenu, kama nilivyosema mwanzoni natarajia kuanza ufugaji kuku wa kienyeji na ningependa kuwa na mashine yangu ya kutotoa mayai (incubator). Lakini umeme haujafika mahali ninapoishi, hivyo ningependa kupata mashine inayotumia mafuta ya taa au dizeli.

    1. Je, naweza kuipata mashine hiyo sehemu gani/kwa nani na kwa gharama gani? Tuseme nahitaji yenye uwezo kuanzia mayai 100 na zaidi.
    2. Nimepata habari kwenye Jamii Forum kuwa kuna watu wanatotolesha kwa malipo. Je, ni njia ipi yaweza kuwa gharama nafuu kati ya kuwa na mashine mwenyewe (kununua mafuta) na kutotolesha kwa watu?

    Nitashukuru kwa maelekezo

    Like

    Gubas

    April 30, 2012 at 1:46 pm

    • Ndugu Gubas, vuta subira. Naamini utapata majibu katika uwanja huu. Karibu.

      Like

      simbadeo

      May 1, 2012 at 12:48 am

      • Bwana Simbadeo, nasubiria kwa hamu kubwa

        Like

        Gubas Vyagusa

        May 2, 2012 at 8:20 am

      • Wajameni nimepata habari za bwana mmoja anayetengeza mashine za Mgana Incubator kuwa anatengeneza zitumiazo umeme pekee, umeme na mafuta na mafuta pekee. Wakati huo huo kuna mahali nimeona mtu mmoja akilalamikia mashine hizo kuwa hazikumsaidia.

        Kwa wale waliokwisha tumia mashine hizo, je kuna ukweli wake?

        Like

        Gubas Vyagusa

        May 28, 2012 at 2:20 pm

  250. I savor, lead to I found exactly what I used to be
    looking for. You have ended my 4 day lengthy hunt! God Bless you
    man. Have a great day. Bye

    Like

    drugs journal

    July 2, 2012 at 7:48 pm

    • Siku njema,

      Jina langu ni Mr.Joe Wafalme wamekuwa kupanga mikopo kwa miaka mingi.
      3% ni maslahi yangu na kiwango cha gharama ya chini zaidi kuliko mtu mwingine katika mji. Kuwasiliana
      mimi leo E-pepe: nancy_loanfirms@yahoo.com

      Fomu ya Maombi ya mkopo

      * Jina Kamili ……………………
      * Jinsia ………………………
      * Mkopo Kiasi Inahitajika ……………
      * Mkopo Duration …………………
      * Nchi ……………………..
      * Home Anwani ………………….
      * Nambari ya simu ………………….
      * Fax ………………………….
      * Kazi ……………….
      * Lengo la mkopo ……………
      * Mapato kwa mwezi ………………..

      Asante kwa muda wako i kusubiri kusikia kwa ajili yenu,

      Mr.Nancy

      Like

      nancy

      July 17, 2012 at 11:10 am

      • Nancy nimejaribu kukuandikia kwenye e-mail naona inashindwa kukufikia. Nina shida na huo mkopo.
        E-mail ni jonasmpango@yahoo.co.uk

        Like

        Jonas

        August 9, 2012 at 9:30 am

      • Mbona hiyo e-mail inakataa, na hakuna adress nyingine hapa wala number za simu, Tutakupataje ndugu??

        Like

        Farhann Jama

        September 3, 2012 at 10:53 am

      • Ndugu Farhann. Asante kwa swali lako. Tafadhali fafanua ungependa kuwasiliana na mdau yupi kati ya wengi sana walio kwenye jukwaa hili? Utaratibu wetu pia ni kuwa kama una swali, unaliweka hapa ili kwamba ikitokea likapata majibu, majibu hayo yanawanufaisha na wengine pia. Hili ni jukwaa la wazi kwa ajili ya wote kunufaika. Wewe unatoa kile unachojua na mwingine anajazia n.k. Karibu sana. Deo Simba.

        Like

        simbadeo

        September 5, 2012 at 9:27 am

  251. Duh! Hii blog inalipa kimawazo.

    Like

    DanielMwakajila

    August 20, 2012 at 8:43 am

    • Ndugu Daniel. Karibu sana katika jukwaa hili. Hapa kila mmoja ni mchangiaji, ni mwanafunzi, ni mwalimu – hii ni kwa sababu kila mmoja ana cha kujifunza, lakini pia ana cha kuwafundisha wengine. Hakuna aliye mweupe kabisa kimaarifa. Tunakukaribisha kwa mikono miwili.

      Like

      simbadeo

      August 20, 2012 at 11:22 pm

  252. Wapendwa habari zenu!
    Mimi nina kiwanja kidogo Mbezi Makabe(20×20),nataka kufuga kuku wa mayai(chotara),kwa eneo hilo naweza kufuga maximum idadi gani ya kuku?

    Like

    Mac

    August 27, 2012 at 10:31 am

  253. Guta

    Jamani natafuta kuku wa kufuga kama hao mwenye mawasiliano na huyo mama anipe taarifa ntampateje mama huyo.

    Like

    gut

    September 3, 2012 at 9:39 am

  254. Kaka naomba nisaidie mayai ya hawa kuku wa Amadori ndugu yangu.

    Like

    Ikunda Makule

    September 18, 2012 at 10:55 am

    • Ndugu Ikunda

      Sijaelewa ombi lako. Unahitaji mayai ya kuku hawa wa Amadori kivipi? Tafadhali fafanua. Ila hii ni picha ya miaka minne iliyopita. Amadori wana ofisi zao mkabala na Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam. Ukihitaji huduma yoyote kutoka kwao, tafadhali watembelee. Hii ni hasa kuhusu huduma zinazohusiana na kuku — hasa hasa kwa kununua, au mayai au kuku wenyewe. Asante.

      Like

      simbadeo

      September 18, 2012 at 10:30 pm

      • Hee makubwa waswahili husema tembea ujionee Leo nasema Peruzi uone najua sijachelewa Nami nimeanza kushawishika kufuga kuku/Tatizo sjui nianzeje ,

        Like

        Francisca

        September 27, 2012 at 2:21 pm

  255. Habari zenu jamani mm nikijana mwanafunzi ila napenda sana kufuga nimejitaidi kufuatiliamijadala ya humu ndani na ilikuwa ni kama bahati kukutana na hii blog yenu inayoongozwa na bwana nina vifaranga wakienyeji wapatao 37 wakuzalisha mwenyewe apa nyumbani ila ningependa kupata majogoo walau yenye ujazo mkubwa ili niweze kupata vifaranga bora Dada jenny (nikama mama yangu) ila nikwavile ndo jina unalo tumia sina budi kulikiuka naombeni ushauri nikijana mdogo na ninaehitaji mafunzo mengi kutoka kwenu

    Like

    Abuu

    October 2, 2012 at 5:30 pm

    • Abuu. Karibu sana. Jukwaa hili ni la wote. Hapa tunaamini kwamba kila mmoja ana kitu cha kuchangia. Kwa hiyo, usijali sana kwamba wewe ni kijana mwanafunzi. Kwanza, kwa niaba ya jukwaa hili nikupongeze kwa kutumia muda wako wa ziada kufanya shughuli ya ufugaji. Ni jambo jema kwamba umeanza mapema, na bila shaka utafika mbali. Elimu unayopata katika kujishughulisha na masuala haya ni kubwa sana na bila shaka itakusaidia pia kufanya bidii zaidi katika masomo yako mengine. Ni vema kujiwekea njia za kumudu yote. Muda wa maisha yetu ni mfupi, kwa hiyo ni vema kuutumia kikamilifu kufanya mambo ya maana.

      Kuhusu swali lako, madhari umeliweka hapa, basi bila shaka atatokea wa kulijibu na wengine kuongezea. Usisite kuuliza maswali mengi kadiri unavyoweza. Usiache pia kueleza uzoefu wako … ambao huenda ukamsaidia mwingine. Hapa tunabadilishana maarifa. Tupo pamoja. Deo Simba.

      Like

      simbadeo

      October 2, 2012 at 11:23 pm

    • Karibu sana Abuu. Umewaza vyema, maana ili upate kuku wazuri wakubwa, jogoo wanatakiwa wawe bora, wale wakubwa. Kwa sasa mimi sina jogoo wa kutosha, ingawa ninayo mbegu ya Malawi black na kuchi toka Nzega, wale kuchi wetu wa asili wakubwa lakini sina idadi ya kutosha kwa mimi mwenyewe pia. Niliwauza nikabakisha mbegu tu inayoendana na idadi ya majike. Kingine, unaweza pia kupata kwa kununua mayai toka kwa wafugaji wenye mbegu nzuri kwa vile unatotolesha mwenyewe ili kupata mbegu. Mbegu nyingine kubwa ni kutoka kwa kuku mchanganyiko mfano wale wa Kibaha. Wafugaji wengine hapa barazani wanaweza kukusaidia kwa maelezo zaidi jinsi ya kuwapata.

      Pia ushauri wangu: Usipende kuchukua kuku wakubwa tayari, pendelea vifaranga wa siku 1 au mayai utotoleshe kwa sababu, kuku wakubwa wakiwa na magonjwa, unayahamishia kwenye yard yako. Magonjwa mengine ya kuku hayaondoki kirahisi au hata hayana chanjo wala tiba za uhakika.

      Nakutakia ufugaji mzuri.

      Like

      Jenny

      October 3, 2012 at 1:05 pm

  256. me bwana Gubas ningependa kukushauri ujaribu kutumia natural incubation kwakueaweka kuku kama kumi kwenye chumba kimoja ila jaribu kuwawekea chakula humohumo ndani ila siku moja moja uwaachie weende njee kula majani na vidudu vingine yaani wawe free ila ni kitu ambacho unaweza kufanya kwa mara mbili kwa kuku mmoja baada ya hapo unawaruhusu wapumzike mana nawao wanahitaji kupumzika na ili waanze kutaga upya na ninjia rahisi sana jaribu then utanipamatokeo mwisho wa siku chumba kiwe na kuku kumi na pia mabox kumi jaribu kufikiria kuku 1 akiatamia mayai 10 mwisho wasiku unakuwa na vifaranga 100 hayo ni makadirio mana kuku mmoja anaatamia mpaka mayai 15 jaribu mana me ndo njia ninayo tumia na vifaranga nanyang’anya ili mamazao warudi kuatamia

    nadhani tuko pamoja bwana Gubas

    Like

    Abuu

    October 3, 2012 at 1:20 pm

  257. asante sana Da Jenny kwa ushauri wako nitasubiri kuchi na hao black australop kama cjakosea utakapo kuwa unauza mayai yao au vifaranga vyake naomba unipe taarifa

    Like

    Abuu

    October 3, 2012 at 1:25 pm

    • Malawi Black unaweza kuwapata kupitia 0713296596 au 0714833335. Mimi ninayo mayai ila demand ya wateja ni kubwa sana kiasi ambacho hayatoshi. Ya kutotolesha huwa natoa wakati nikiwapatia kuku dawa, yanakuwa hayafai kuliwa kwa muda fulani kwa hiyo huo ndio muda ambao huwa natotolesha mayai. Nikiwa na hayo yasiyofaa kuliwa nitakuarifu uchukue kama utakuwa na majike wa kulalia. Sijajua kama utahitaji trays ngapi pia. Siku njema.

      Like

      Jenny

      October 4, 2012 at 7:54 am

  258. Mimi ni kijana nimeajiriwa temporary katika ajira yangu nimejiwa na wazo la kuanzisha miradi mbalimbali lakini wa kwanza ni ufugaji wa kuku wa nyama ila nina elimu kidogo sana juu ya mradi huo,tafadhali naona shule iliyo na utaalamu wa kutosha, Ahsanteni sna

    Like

    Stuart Mtunguja

    October 3, 2012 at 6:52 pm

  259. tutawasiliana usijali dajenny na asante kwa izo namba za simu nitajaribu kuwasiliana na tray moja unauza kiasi gani

    Like

    Abuu

    October 4, 2012 at 9:45 am

    • Tray ni TShs. 15,000/= lakini hayo yasiyofaa kuliwa ni TShs. 12,000/=.

      Like

      Jenny

      October 4, 2012 at 3:48 pm

    • Nipo kibamba hospital,tray moja ya kuku wa kisasa nauza 7500,kwa siku unaweza pata hata tray 200 hadi 300.My number is 0752828594.

      Like

      Muuza mayai.

      August 8, 2013 at 7:15 pm

  260. mimi nataka kujua njia zankufuga hao kuku, kwani ndio kwanza nataka kuanza na sijui nianzie wapi, Je waweza kunisaidia kunipatia steps hizo.

    Like

    khamis said

    October 9, 2012 at 10:28 am

    • Ndugu Khamis. Je,umesoma makala zote zilizoandikwa hapa pamoja na comments za wadau? Kama ndiyo, bila shaka utakuwa umeshapata ujuzi wa msingi kukuwezesha kuendesha biashara ya ufugaji kuku. Kama ulikuwa hujasoma, anza sasa.

      Like

      simbadeo

      October 12, 2012 at 11:47 pm

  261. haya jaman asanten shukrani zangu ningependa zimuenda Dajenny pamoja na KakaDeo mana nimefanikiwa kupata wale kuku kasoro wale kuchi ndo sijapata kwa mwenye nao anisaidie jaman

    Like

    Abuu

    October 9, 2012 at 9:13 pm

  262. Mimi ni mgeni kwenye mijadala hii. Lakini ni mfugaji wa siku nyingi. Namshukuru Mungu kwa hili. Ninachotafuta sasa hivi ni mayai ya bata mzinga na bukini. Yamekuwa ni vigumu kupatikana. Kwa wafugaji wakubwa hawatoi ila ni kwa mayai ya kanga tu ndio unaweza kupata. Je kuna mtu anaweza kunisaidia kwa hili? Tafadhali nifahamishe na bei zake.

    Asanteni

    Like

    Bibi Mwapombe

    October 17, 2012 at 2:04 pm

    • Hello Bibi Mwap… Karibu.
      Check Morogoro pale Bwawani ukiwa unaiacha Morogoro kama unakuja Dar utapata bila shaka. Nakutakia ufugaji mwema.

      Like

      Jenny

      October 24, 2012 at 8:31 am

      • Asante Da Jenny kwa kumwelekeza Bibi Mwapombe. Naamini na siye wengine wenye mahitaji kama hayo tutakuwa tumepata wapi pa kwenda.

        Kuna mdau ameniuliza: nifanye nini ili kuku wangu (wa kienyeji) watage mayai ambayo yana kiini cha njano? Niwape chakula gani? Niwatunze kwenye eneo la aina gani?

        Kama kawaida wadau, ninaweka swali hili mbele yenu. Yule mwenye majibu, tafadhali atushirikishe ili sote tupate kukua zaidi kimaarifa. Karibuni sana!

        Like

        simbadeo

        October 31, 2012 at 12:09 am

  263. Karibu sana bibi mwapombe nadhani wenye nao watakusaidia ila na ww vp unakuku aina ya kuuchi mana ninashida nao

    Like

    Abuu

    October 17, 2012 at 9:23 pm

    • nahitaji majogoo kumi ya amadori,nitayapataje kaka simbadeo? 0762-311700 hillary

      Like

      hillary

      December 30, 2012 at 10:08 am

      • Ndugu Hillary. Pengine nikushauri uwatembelee pale kwenye ofisi zao zinazotazamana na Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (Terminal II). Naamini watakupa unachohitaji. Pamoja sana.

        Like

        simbadeo

        December 31, 2012 at 6:59 pm

  264. Nimefuarahi sana kuipata hii network, nitapata mengi ya kujifunza na ambayo naahidi kuyafanyia kazi

    Like

    Hamidun Kweka

    January 17, 2013 at 5:02 pm

    • Karibu sana Hamidun. Tutafurahi kuona ushahidi wa ahadi yako hii. Kwa wajumbe wengine hapa, tunakaribisha picha za mafanikio mliyoyapata katika uwanja huu wa ufugaji kuku. Unaweza kutuma picha kupitia anwani hii kakasimba@gmail.com na zitachapishwa bila upendeleo, ubaguzi wala kufinywa. Hili ni jukwaa huru na kila mmoja ana haki kamili ya kusikika ili mradi havunji sheria za nchi. Karibuni sana.

      Like

      simbadeo

      January 18, 2013 at 10:52 pm

  265. Good day! I could have sworn I’ve been to this blog before but after browsing through some of the post I realized it’s new
    to me. Anyways, I’m definitely delighted I found it and I’ll be bookmarking and checking
    back often!

    Like

    Buy Followers For Instagram

    January 22, 2013 at 4:46 am

    • You’re welcome. Thank you for commenting on this blog. Keep following. Keep commenting.

      Cheers!

      Simba

      Like

      simbadeo

      January 22, 2013 at 1:58 pm

  266. Great info. Lucky me I ran across your website by chance (stumbleupon).

    I have saved it for later!

    Like

    this website

    February 5, 2013 at 12:44 pm

  267. Hamjambo wapendwa wafugaji na heri ya 2012! Wale wanaotengeneza chakula cha kuku naomba kazi ya kuwaletea dagaa toka Ukerewe. Kama pia una mtu unamfahamu unaweza kuniombea hiyo kazi nitakushukuru. Asanteni kwa ushirikiano, Mbarikiwe katika kazi na maisha yenu daima.

    Like

    Jenny

    February 6, 2013 at 9:57 am

    • Dagaa wako unauza kwa kilo bei gani?

      Like

      Muuza mayai.

      August 8, 2013 at 7:34 pm

      • Hello Muuza Mayai, sikuona msg mapema. Dagaa wanategemea na soko lilivyo. Hawana bei maalum inategemea na msimu na wanavyopatikana. Bei inayokuwa sokoni ndio bei yake japo kwangu huwa bei iko chini kidogo kuliko iliyoko sokoni. Ufugaji mwema.

        Like

        Jenny

        February 11, 2014 at 9:23 am

  268. Heri ya 2013…..

    Like

    Jenny

    February 6, 2013 at 9:58 am

  269. “Ufugaji Kuku simbadeo2000” was indeed a
    good post. If it owned much more pictures this would
    probably be even far better. Cya -Lyle

    Like

    http://google.com

    February 13, 2013 at 1:17 pm

  270. Thank you for writing “Ufugaji Kuku | simbadeo2000” carolinecountymusic .
    Iwill really wind up being back again for more reading through and commenting here soon.
    Thanks a lot, Stacey

    Like

    Freddie

    March 2, 2013 at 12:57 pm

  271. Yesterday, while I was at work, my cousin stole my iphone and tested to see if
    it can survive a 30 foot drop, just so she can be
    a youtube sensation. My apple ipad is now destroyed and she has 83 views.
    I know this is entirely off topic but I had to share it with
    someone!

    Like

    hurtownia torebek

    May 13, 2013 at 9:19 pm

  272. naweza pata wapi incubator na gharama zake

    Like

    kasain

    May 17, 2013 at 10:56 pm

    • Ndugu Kasain

      Karibu katika jukwaa hili. Labda kwa kuuliza tu, umesoma makala zote humu kuhusu ufugaji? Ukifanya hivyo, bila shaka utapata jibu la swali lako. Endelea kuperuzi.

      Asante

      Like

      simbadeo

      May 19, 2013 at 5:45 pm

    • Ndugu Kasain

      Karibu katika jukwaa hili. Labda kwa kuuliza tu, umesoma makala zote humu kuhusu ufugaji? Ukifanya hivyo, bila shaka utapata jibu la swali lako. Endelea kuperuzi.

      Asante

      Like

      simbadeo

      May 19, 2013 at 5:45 pm

      • Waza mpaka basi!

        Ni kweli, wazo unalolishughulikia kichwani likakufikisha karibu sana na suluhu tarajiwa (kwakua karibu mara zote hamna jibu moja kwa swali).

        Hongera bw. deo na wachangiaji wote kwa kutupa majibu ya maswali magumu tunayoyakabili. Ingetubidi kurejea kwa kufanya majaribio mengi ambayo tayari yamefanyika. Mmetuokolea rasilimali nyingi ambazo tungeingiza kwenye miradi isiyolipa.
        Binafsi nawashukuru sana kwa mawazo mliyo yaweka bayana humu. Nafikiri natakiwa kuanza kufuga sasa. MUNGU awabariki sana.

        Like

        Pleo

        June 17, 2013 at 6:10 pm

      • Waza mpaka basi!

        Ni kweli, wazo unalolishughulikia kichwani likakufikisha karibu sana na suluhu tarajiwa (kwakua karibu mara zote hamna jibu moja kwa swali).

        Hongera bw. deo na wachangiaji wote kwa kutupa majibu ya maswali magumu tunayoyakabili. Ingetubidi kurejea kwa kufanya majaribio mengi ambayo tayari yamefanyika. Mmetuokolea rasilimali nyingi ambazo tungeingiza kwenye miradi isiyolipa.
        Binafsi nawashukuru sana kwa mawazo mliyo yaweka bayana humu. Nafikiri natakiwa kuanza kufuga sasa.

        D4-nml

        MUNGU awabariki sana.

        Like

        Pleo

        June 17, 2013 at 6:11 pm

      • “waza mpaka basi”

        ndg simba,

        maamuzi yangu ya kuanza kufuga, yamenipelekea kuangakia nilichonacho mkononi. Nina kama matetea 3 na jogoo (wote wa kienyeji), mwanzo wa chini nafikiri. Nalenga mpaka mwisho wa mwaka kua na kundi linalo karibia jumla ya kuku na vfaranga 100.
        Nafikiri taarifa zilizomo kwenye uzi huu “ufugaji wa kuku…” unaweza kunifikisha huko, kwa kuniwezesha kushona vpande kadhaa vya mawazo kupata shuka zima.
        Siku njema.

        Like

        Pleo

        June 20, 2013 at 7:28 pm

      • Ndugu Pleo. Asante sana kwa salamu. Naam. Nimefurahi kusikia kwamba tayari umekwishaanza kuchukua hatua kuelekea lengo lako. Umefanya kama Wachina wanavyosema … Safari ya Maili elfu moja huanza na hatua ya kwanza. Hongera, na usisite kutushirikisha mafanikio, changamoto, uzoefu na mengineyo kupitia jukwa hili huru. Karibu sana.

        Like

        simbadeo

        June 21, 2013 at 11:19 am

  273. I always used to read piece of writing in news papers
    but now as I am a user of net so from now I am using net for articles or reviews,
    thanks to web.

    Like

    Additional Reading

    May 29, 2013 at 7:55 pm

  274. What’s up, its pleasant piece of writing about media print, we all know media is a wonderful source of information.

    Like

    Ira

    June 13, 2013 at 9:51 pm

  275. ninapenda sana ufugaji na ninahitaji sana kujua namna ya kufuga naomba unielekeze nitawapata wapi ili niweze pata hayo mafunzo

    Like

    magdalena lema

    June 21, 2013 at 12:44 am

    • Bi Magdalena. Karibu sana. Unachopaswa kufanya ni kusoma uzi mzima kwenye makala ya ‘ufugaji kuku’ … hapo utachota maarifa tani yako. Kikubwa tu, utushirikishe na sisi kupitia jukwaa hili mafanikio yako, changamoto, uzoefu na mambo mbalimbali. Hapa kila mmoja ana kitu cha kuwashikisha wengine, na pia ana kitu cha kujifunza kutoka kwa wengine. Karibu sana.

      Like

      simbadeo

      June 21, 2013 at 11:17 am

  276. Ndugu simbadeo,

    nimekua nikijaribu kuunga hatua za kupita kwenye mradi wa ufugaji. Unaweza nipa kwa ufupi changamoto za viatamizi vinavyotengenezwa tz.
    Kipi ni mtihani
    kuweka kiwango muafaka cha joto, unyevu kwenye hewa, au ugeuzwaji wa mayai?

    D8-nml -0.2,+0.4c

    natanguliza shukrani

    Like

    Pleo

    June 21, 2013 at 3:27 pm

  277. Ndugu Deo,
    nimefika hatua ya 15 kati ya 100, jogoo, matetea 3 na vifaranga 11.
    Furaha ni kubwa, ninapoangalia vfaranga vyenye uchangamfu na afya tele. Vinatoa matumaini mema ya safari. Japo furaha inaweza kukatishwa na hofu ya vita vikali ya kudhibiti hatua nilizofika,
    tumaini nalipata kwa wahenga, “ukimjua adui wako, vita umeishinda kwa 50%”, nafikiri nikifahamu silaha zake km. Surua ya kuku, kideli, mafua nk. na dalili zake, bila kusahau jinsi ya kujihami = chanjo, na kurejesha mapigo = tiba nafikiri inanipa 85%+ ya ushindi. Bado natumia uzi huu kushonea shuka. Twende pamoja safarini.

    Like

    Pleo

    July 5, 2013 at 4:16 pm

  278. Sasa hao kuku tume waona sasa tunaomba namber za sim ilikuwa pata

    Like

    Shikari mjema

    July 16, 2013 at 12:57 pm

    • Ndugu Shikari. Karibu sana katika jukwaa hili. Fuatilia kwa karibu mijadala inayoendelea hapa. Naamini utapata majibu kwa maswali yako. Karibu sana.

      Like

      simbadeo

      July 19, 2013 at 12:49 pm

  279. Good post. I learn something new and challenging on sites I stumbleupon on a
    daily basis. It’s always helpful to read content from other writers and use something from their sites.

    Like

    Blue Rugs

    July 19, 2013 at 12:28 am

  280. Thanks for one’s marvelous posting! I definitely enjoyed reading it, you could be a great author. I will remember to bookmark your blog and definitely will come back sometime soon. I want to encourage one to continue your great job, have a nice evening!

    Like

    Weight Loss

    July 19, 2013 at 12:53 pm

  281. Thank you for the auspicious writeup. It in fact was a amusement account it.
    Look advanced to more added agreeable from you!
    However, how can we communicate?

    Like

    减肥药排行榜

    July 21, 2013 at 8:13 am

  282. Thank you for the good writeup. It in fact was a leisure account it.

    Look complex to more brought agreeable from you! However, how can
    we keep in touch?

    Like

    Otto

    August 4, 2013 at 6:17 pm

  283. Nipo kibamba hospital dar es salaam,nauza mayai ya kuku wa kisasa,nahitaji mteja wa jumla ambaye anaweza kuchukua mayai mengi kwa siku kuanzia tray 50 na kuendelea,bei ya tray moja ni Tshs 7500,usafiri juu yako.Mawasiliano yangu ni 0752838594.

    Like

    Muuza mayai.

    August 8, 2013 at 7:27 pm

  284. Ninaomba kujua mahali pa kupata mayai ya kuku chotara kwa ajili ya kuatamisha pia incubator machine kwa bei rahisi

    Like

    Robert

    August 15, 2013 at 1:20 am

  285. Naweza kupata mayai ya kuku chotara kwa ajili ya kuatamishia na pia incubator

    Like

    Robert

    August 15, 2013 at 1:32 am

    • Ndugu Robert,

      Tafadhali vuta subira. Naamini atatokea mtu wa kueleza namna unavyoweza kufikia ndoto yako. Karibu sana.

      Like

      simbadeo

      August 17, 2013 at 8:14 pm

  286. Nashukuru sana kwa comments zenu hapo juu

    Mimi ni mfugaji wa kuku wa kienyeji nje kidogo ya mji wa Dar es salaam nimekuwa nikiahangaika kwa muda mrefu kutafuta mbegu nzuri ya kuku wa kienyeji wenye kutaga mayai mengi lakini pia wenye maumbo makubwa.

    Nianaweza kuwapata wapi hawa au ni kuku wa maeneo gani wanakuwa na sifa hizi

    Like

    ASIGWA

    August 20, 2013 at 9:23 am

  287. Habari wapendwa, Nimefurahi sana leo kupata hii link kwa sababu ninataka kufunga kuku kibiashara ila bado natafiti kati wa kuku wa kienyeji wa mayai na wa kisasa wa mayai wapi wanalipa zaidi? Nipo Kahama

    Like

    Petro

    August 22, 2013 at 12:23 pm

  288. hallow wajasiliamali wezangu .ingawa bado ni mwana chuo lakini bado nafahamu umuhimu wa ujasiliamali .kwa kweli ufugaji kuku ni miongoni mwa plan zangu.natalajia kuanza kufuga kuku tar 1 mwezi 10.2013.
    nataka nianze na kuku 100.
    mimi natokea gairo morogoro ila bado sijui wapi nitapata mbegu bora ya kuku wa kienyeji
    TAFADHARI NDUGU ZANGU KAMA UNAO AU UNAJUA WANAKO PATIKANA KWA URAHISI NAOMBA TUJURISHANE, NAMBA YANGU 0714586766.
    PIA UKUBWA GANI WA BANDA UNAFAA KWA KUKU HAO.
    NA KUKU NI WANYAMA SIO WA MAYAI.
    TUPO PAMOJA NDUGU ZANGU
    YUSUPH

    Like

    yusuph

    August 25, 2013 at 1:44 am

  289. Wapendwa habari ya kazi na poleni na majukumu, mimi nafugia kigamboni ni mfugaji mdogo nilianza kufuga kuku wa nyama tangu juni 2013, na Mungu akipenda nitaanza wa mayai juni mwakani au before. Hiyo ni ndoto yangu ya muda mrefu. Kabla nimekuwa nikifuga kuku wa kienyeji walifika mia 220, nikawauza, ila nimeanza tena kwa sasa nina 15. natafuata majogoo makubwa sababu mbegu yangu si kubwa sana.

    Like

    Elizabeth

    October 24, 2013 at 9:18 am

    • mimi pia nataka kufuga,hebu nielekeze banda lako lilikuwa dizaini gani?

      Like

      mtemi daniel

      February 10, 2014 at 3:37 pm

  290. Nataka kujifunza namna bora ya kufuga kuku wa kienyeji, nipo mwanza nawezaje kupata mahali pa kujifunza kabla ya kuanza ufugaji

    Like

    Theophil

    March 8, 2014 at 10:47 am

  291. Nataka kuhudhuria shamba darasa la ufugaji wa kuku wa kienyeji, kama lipo hapa mwanza please naomba mnijulishe niweze kuhudhuria mimi nipo mwanza 0767499590/0784499590

    Like

    Theophil

    March 8, 2014 at 10:49 am

  292. Kwa watu wa mwanza vifalanga vizuli ni bei gani pls

    Like

    Amin

    April 13, 2014 at 2:24 am

    • hellow brother simbadeo vp kuku wa kibo na intachik wanatofaut sana ktk ufugaji na wap the best sana

      Like

      gidionmario

      April 14, 2014 at 7:47 pm

  293. Theophil, unaweza ukaanza na wachache, cha msingi ni kuwa karibu na madktari wa mifugo, watakusaidia kukuelekeza mabanda bora, vyakula, chanjo na tiba. Mimi nilianza na wachache, na sasa wamekuwa.

    Like

    adam

    April 28, 2014 at 11:06 pm

  294. Kwa wale wa Morogoro, kama unahitaji kuku wa kienyeji wa kimalawi, wakubwa call. 0789121177

    Like

    adam

    April 28, 2014 at 11:12 pm

  295. Habari za leo wapendwa. mie ni mgeni hapa na naomba niulize kitu tofauti kabisa naamini wafugaji wa kuku wengi wenu mnashughulika pia na biashara zingine.
    Mimi nataka kuanzisha mradi wa kuuza chips na naomba yeyote mwenye uzoefu anielekeze jinsi ya kufanya mchanganuo wa faida au hasara kwa siku. Jinsi ya kulipa mfanyakazi na uzoefu mwingine wowote..
    Natanguliza shukrani zangu ndugu zangu..

    Like

    Nyamisi

    June 22, 2014 at 1:13 pm

  296. je unahiji kuku bora wa kienyeji?
    nipigie 0754471113
    ni wazuri sana

    Like

    kitigwa

    July 21, 2014 at 12:53 pm

    • nashukuru kwa kutujulisha !

      Like

      emmanuel msila

      September 2, 2014 at 1:34 pm

  297. Je unataka mayai ya kienyeji kwa bei nafuu? Nipigie kupitia 0658441130

    Like

    Mr. Edmund

    August 25, 2014 at 5:52 pm

  298. Nahitaji kuku wa amadori. natafta namba zenu siwapati pls mnipgie no 0767 323636. tafadhali mhusika wa amadori ndo anipigie na si vinginevyo.

    Like

    Beatrice

    September 5, 2014 at 5:53 pm

    • Vifaranga vya nyama @1300
      Vifaranga vya Mayai @2200

      Pia wana vijogoo (Male Layers-ISA brown Breed) @400.

      Tuwasiliane kwenye 0717332652

      Like

      Kitunda

      February 6, 2015 at 1:28 pm

  299. habari wajasiria mali. me napatikana mbeya ninatengeneza incubator kwa gharama nafuu sana kwa kubadiri fridge na kua mashine ya kutotorehsea vifaranga. endapo utahitaji mashine nitakufuata popote ulipo na kupata huduma iliyo bola. ufanisi wake ni 89% inategemea na ubora wa mayai yako. inacontrol joto outomatic na kugeuza ni mannual ndani ya sekunde 10 unakuwa umegeuza mayai yote yaliyopo ktk mashine. mashine ya bei ya chini ni sh. laki na 80. na mashine ya bei ghali n laki 4.6. 0754078015
    samsongimase@mail.com

    Like

    baba colli

    September 17, 2014 at 12:20 pm

    • Vifaranga vya nyama @1300
      Vifaranga vya Mayai @2200

      Pia wana vijogoo (Male Layers-ISA brown Breed) @400.

      Tuwasiliane kwenye 0717332652

      Like

      Kitunda

      February 6, 2015 at 1:27 pm

  300. hello,

    Unaendeleaje leo ?? hii ni kuwajulisha kuwa kama unahitaji ni Xmas mkopo kujaribu na tutumie na email nyuma fomu yake na kuamini kuwa wewe ni kupata hii Xmas mkopo uhamisho katika akaunti yako ya benki katika 1 Saa na kwamba sisi ni kutoa wewe 100% Dhamana ya hii uhamisho mkopo kwa benki akaunti yako Sawa.

    Hii ni mahali kampuni email: (roberth.tomson@hotmail.com) kutuma mkopo wako kiasi kwa sasa ni furaha Xmas mkopo

    kutoa Sawa.

    Jina: ===
    Kiasi inahitajika: ===
    Duration: ==
    Nchi: ===
    Kusudi: ===
    Simu ya mkononi: ==

    Hii ni mahali kampuni email: (roberth.tomson@hotmail.com)

    Regards,
    Mheshimiwa Tomson Roberth

    Like

    Roberth

    October 23, 2014 at 12:45 am

    • wewe ndugu Tomson Roberth ni mwizi jaribu kuwatapeli wengine sio watanzania wa leo, jaribu huko kwa wanaigeria wenzako

      Like

      fulgence kitigwa

      October 23, 2014 at 3:10 pm

    • Asante Kitigwa, hope kaka Deo atafuta haya ma-msg ya kijizi jizi hapa jamvini. Hatudanganyikiii!

      Like

      Jenny

      October 23, 2014 at 4:01 pm

  301. Hi am poppestone from KENYA and am looking for someone who can supply me with fertile kuchi eggs…my phone +254724153850

    Like

    Popestone Juma

    November 25, 2014 at 2:19 pm

  302. wadau habar za majukumu ya kiufugaji. Mimi ni mfugaji mchanga, humu ndani nimepata threads nyingi nzur ktk ufugaji. kwa sasa ninao brown australorp. wanakaribia kutaga. Wenye kuhitaji Mayai kwa matumiz pia kutotolesha yatapatikana. Nnayo pia majogoo safi ya mbegu. Nicheck 0769 556359/0686020495.Niko Moshi. Simbadeo hongera kubuni hii

    Like

    Micaah

    December 30, 2014 at 9:22 pm

  303. wadau habar za majukumu ya kiufugaji. Mimi ni mfugaji mchanga, humu ndani nimepata threads nyingi nzur ktk ufugaji. kwa sasa ninao brown australorp. wanakaribia kutaga. Wenye kuhitaji Mayai kwa matumiz pia kutotolesha yatapatikana. Nnayo pia majogoo safi ya mbegu. Nicheck 0769 556359/0686020495.Niko Moshi. Simbadeo hongera kubuni hii, umetukutanisha wafugaji

    Like

    Micaah

    December 30, 2014 at 10:11 pm

  304. Hodi hodi wadau habari za majukumu ya kiufugaji hasa ktk swala zima la kiujasilia mali mimi ni mfugaji mchanga, humundani nina mashine ndogo ya kutotolea vifaranga yenye uwezo wa kubeba mayai 360 na mategemeo ni kupata vifaranga vimezoeleka kusema vifaranga vya Malawi{kuku wa mayai} lengo hasa ni kufanya biashara ya kuuza vifaranga nategemea kuwa na vifaranga kuanzia tarehe 24 mwezi huu.Nicheck 0755/0655- 755506 Niko Mbeya Airpot ya zamani kwajina naitwa Emmanuel G Sigalla.KARIBUNI

    Like

    2008xvideos

    January 6, 2015 at 4:00 pm

    • Karibu Sigalla, hongera kwa mradi kwenda vema. Vifaranga wako wanapata chanjo za awali? Ukiliweza hilo mafanikio ni yako maana shida kubwa ya sasa ni vifaranga kutopewa chanjo za awali mfano Mareks inasumbua sana. Sijui kama kiwango cha chini tunaweza kumudu kununua chanjo yake. Nimeshuhudia hii shida imekuwa kubwa sana mtu ananunua vifaranga anawatunza wakifika umri wa kutaga wanapukutika. Nakutakia mafanikio mazuri mdogo mdogo hatimae mkubwa mkubwa. Heri ya 2015.

      Like

      Jenny

      January 7, 2015 at 9:28 am

      • Vifaranga vya nyama @1300
        Vifaranga vya Mayai @2200

        Pia wana vijogoo (Male Layers-ISA brown Breed) @400.

        Tuwasiliane kwenye 0717332652

        Like

        Kitunda

        February 6, 2015 at 1:26 pm

  305. kwa mwanza tunaweza kuwapata wapi tupe taharifa na hutuhelekeze

    Like

    muniru nasuhi

    January 9, 2015 at 9:37 pm

  306. Heri ya mwaka mpya, kaka Deo asante kwa kuniconnect na dada Jane amenisaidia, dada Jane asante sana, sasa kuku wangu wameanza kuangusha mayai, nimefurahi sana kutimiza ndoto zangu. Nawatia moyo wote ambao mnataka kuthubutu, msiogope.

    Like

    Elizabeth

    January 30, 2015 at 9:46 am

    • Heri ya mwaka mpya. Nakutakia ufugaji mwema wenye furaha Eliza. Umevuka pakubwa usisite kutusaidia pia uzoefu wako ambao utakutana nao na sisi hatuufahamu.

      Like

      Jenny

      February 2, 2015 at 4:27 pm

      • Vifaranga vya nyama @1300
        Vifaranga vya Mayai @2200

        Pia wana vijogoo (Male Layers-ISA brown Breed) @400.

        Tuwasiliane kwenye 0717332652

        Like

        Kitunda

        February 6, 2015 at 1:25 pm

    • Vifaranga vya nyama @1300
      Vifaranga vya Mayai @2200

      Pia wana vijogoo (Male Layers-ISA brown Breed) @400.

      Tuwasiliane kwenye 0717332652

      Like

      Kitunda

      February 6, 2015 at 1:25 pm

      • Poa, asante sana kwa taarifa. Wamechanjwa chanjo muhimu za awali?

        Like

        Jenny

        September 1, 2015 at 12:55 pm

  307. Habari zenu wadau na wafugaji wa kuku,Nina office yangu na ni Agent mkubwa wa vifaranga vya CPF,kwa kweli hivi vifaranga ni bora sana,havifi ovyo,vinakuwa vizuri,ndani ya siku 28 tayari wanakuwa na kilo1.2Kg.

    Ni kampuni ambayo imejipanga vizuri sana kuanzia chakula mpaka vifaranga.
    Kwa wale wote wanaotaka vifaranga bei zake ziko hivi;

    Vifaranga vya nyama @1300
    Vifaranga vya Mayai @2200

    Pia wana vijogoo (Male Layers-ISA brown Breed) @400.

    Kwa yeyote anayetaka ushauri wa ufugaji wa kuku,pamoja na chakula cha CP na Vifaranga unaweza kunipigia kwenye number yangu 0717332652.

    Like

    Kitunda

    February 6, 2015 at 1:23 pm

  308. unawezaje kutumia taa ya kibatari kutamishia mayai ya kuku

    Like

    abelly

    August 23, 2015 at 10:55 am

  309. habari ndugu wafugaji……..nawapenda sana naomba kuungana nayi ktk jukwaa hili.. nipo moshi…..ni mfugaji mdogo wa kuku.

    Like

    Shabani O. Matumla.

    August 28, 2015 at 1:21 pm

    • nisiwe mchoyo wa shukrani kwa michango mbalimbali kwakumtaja jina dada JANNY……Nimepata maarifa makubwa sana kwa mchango wako…..kwapamoja nasema asante. namba yangu ya simu ni 0753 379370

      Like

      Shabani O. Matumla.

      August 28, 2015 at 1:24 pm

      • Karibu Bw. Shabani, Karibuni wafugaji tuelimishane.

        Like

        Jenny

        September 1, 2015 at 12:55 pm

  310. Mungu akubariki dada Jenny sana kwa moyo wako wa kujitoa kutufundisha wa hali ya chini ili tuinuke

    Like

    GLORY

    September 2, 2015 at 4:32 pm

    • Glory hapa tunafundishana, hakuna anayejua kila kitu. Hata mimi nimepata faida sana kutoka kwa wachangiaji wengine.

      Like

      Jenny

      September 3, 2015 at 3:30 pm

  311. Balikiwa sana dada Jenny, nmepitia jumbe zako karibia zote nmejifunza mengi kama mdau wa ufugaji!

    Like

    wangese

    February 25, 2016 at 12:16 pm

    • Karibu sana Wangese. Ukisoma hayo yote na waliyochangia wengine hutakuwa na maswali mengi. Ufugaji mwema.

      Like

      Jenny

      February 26, 2016 at 11:14 am

  312. Habari zenu ndugu.

    Kwanza nitoe shukrani kwa wachangiaji wote, kaka Simba kwa kuusimamia ukurasa na hususan dada Jenny kwa maarifa uliyoyatoa. Nimeanza kusoma huu ukurasa leo but nimeshazisoma post zako toka za 2009 mpaka 2016. Nakushukuru kwa moyo huo na Mola aendelee kukubariki zaidi.

    Mi nina maswali mengi sana, mengi umeshayajibu but kuna baadhi bado nahitaji msaada wako. Kama sio tatizo ningeomba niwasiliane nawe dada Jenny kwenye whatsapp ili tuzungumze zaidi.

    Whatsapp yangu unaweza niadd at +971529784372 or unaweza nijulisha namba yako nikutafute pia.

    Kaka Simba kama una contact za dada Jenny and unadhani hana shida ukinipatia, tafadhaki nisaidie pia.

    Asanteni na mbaki salama.

    Like

    Joff

    September 12, 2016 at 12:12 am

  313. Habari zenu ndugu!

    Mimi nipo Dar es Salaam, nina kuku wa kienyeji 450 wako mchanganyiko matetea 300 na sasa wameanza kutaga na majogoo 150 sasa natafuta soko ili kuona picha tuwasiliane whatsapp yangu na kwa mawasiliano 0686-833282

    Like

    Boniface

    March 17, 2017 at 5:25 pm

  314. Mi nauza kuku wa kienyeji wakubwa jike 12000 jogoo 14000 nauza kuanzia kuku 20 kwa mawasiliano 0719639723 au 0759515825 nakuletea popote ulipo

    Like

    Evance Adelardi

    September 15, 2017 at 12:28 pm


Leave a comment