simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Merry Christmas and Happy New Year 2009

with one comment

simba-class31

Ilikuwa tarehe 22 November 1990. Ndiyo kwanzatulikuwa tumekamilisha kufanya mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne. Tulifanya safari ya kukwea Mlima Kilimanjaro. Sote tuliokuwa katika kundi letu tulifaulu kufika kileleni, Uhuru Peak. Ilikuwa safari ngumu na yenye kutoa changamoto kubwa kwetu. Tuliweka nia thabiti na lengo la kufika kileleni. Tulifaulu.

Picha hii inanikumbusha kwamba katika maisha tunahitaji kuwa na malengo, tunahitaji kuwa na nia thabiti ili kuyafikia malengo hayo, tunahitaji kujitoa sadaka ili kufikia malengo hayo. Vilevile, inanikumbusha kwamba tuweke malengo yetu juu zaidi kwani tukifanya hayo niliyoeleza hapo TUNAWEZA kufikia lengo lolote tunalojiwekea.

Natumia fursa hii kuwatakia Heri na Baraka za X-mas 2008 lakini pia kuwatakia Watanzania wenzangu na wasomaji wa blogu hii Heri na Mafanikio katika Mwaka Mpya wa 2009.

Tukumbuke kwamba TUNAWEZA – tunaweza kubadili hali zetu kama Taifa, tunaweza kubadili maisha yetu kila mmoja kwa nafsi yake.

Pichani, kutoka kushoto: John Bosco Mosha, Furaha Massawe, Reginald Mbuya, Paul (Christian) Temu, Sylivester Kusare, Valentine Tesha, Straton Mushi, Kanut Bynit na mimi Deogratias Simba (aliyechuchumaa).

Written by simbadeo

December 25, 2008 at 1:12 am

Posted in Siasa na jamii

One Response

Subscribe to comments with RSS.

  1. Ah kaka umenikumbusha mbali,ingawa hukumtaja manyasi,na Mzee Personality hukumtilia mkazo.

    Like

    Straton

    April 8, 2010 at 2:25 pm


Leave a comment