Ufukweni … Mahali pa Kutafakari
Ukitaka kuvuta fikra za ndani kabisa … nenda pwani … tembea mchangani … tazama upeo wa macho kwa makini. Sahau kuhusu mwili wako, sahau sauti za magari. Sikiliza tu upepo mwanana wa bahari na jinsi mawimbi yanavyosafiri. Miale ya jua inavyochezacheza juu ya maji. Rangi ya mchanga. Vidoti doti vya watu na vyombo vya baharini. Ibua fikra nzito, zinazomgusa kila binadamu. Upendo. Amani. Furaha. Matumaini. Maendeleo. Urafiki. Uzuri. Wema. Mshikamano.
Pamoja sana!
Si uwongo ni kweli kabisa ..ahsante kwa kutukumbusha..
LikeLike
Yasinta/kapulya
February 8, 2013 at 11:49 pm
ni kweli kabisa, nimekumbuka mbali sana.
LikeLike
eric
February 12, 2013 at 10:53 am
Ni kweli Eric. Maisha yanatupeleka puta sana. Usipoangalia, unaweza kujikuta umeshamaliza mwaka hujapata nafasi hata chembe ya kutulia na kutafakari kwa kina unatoka wapi, uko wapi, unakwenda wapi, wewe ni nani n.k. Tumejaliwa kuwa na maeneo hayo, basi na tuyatumie.
Pamoja sana.
LikeLike
simbadeo
February 12, 2013 at 5:13 pm