simbadeo2000

WAZA MPAKA BASI (THINK TO NO END).com weblog NOTE: Views or opinions expressed in this blog do NOT in any way represent those of any organisation, community, association, company, circle of friends, religious or ethnic group to which I am associated with.

Ufukweni … Mahali pa Kutafakari

with 3 comments

Ufukwe katika Bahari ya Hindi ... mkabala na Hospitali ya Aga Khan

Ufukwe katika Bahari ya Hindi … mkabala na Hospitali ya Aga Khan

Moja ya biashara ambazo hutawala kwenye ufukwe huo ni hii ya madafu. Kinywaji hiki ni bora kwani ni cha asili na madafu hayo mara nyingi yanatolewa hapo ng'ambo tu ... ukivuka hiyo bahari. Si vibaya ukanywa maji ya dafu na kula nyama yake walau mara sita kwa mwaka. Bei yake ni nafuu sana!

Moja ya biashara ambazo hutawala kwenye ufukwe huo ni hii ya madafu. Kinywaji hiki ni bora kwani ni cha asili na madafu hayo mara nyingi yanatolewa hapo ng’ambo tu … ukivuka hiyo bahari. Si vibaya ukanywa maji ya dafu na kula nyama yake walau mara sita kwa mwaka. Bei yake ni nafuu sana!

Ukitaka kuvuta fikra za ndani kabisa … nenda pwani … tembea mchangani … tazama upeo wa macho kwa makini. Sahau kuhusu mwili wako, sahau sauti za magari. Sikiliza tu upepo mwanana wa bahari na jinsi mawimbi yanavyosafiri. Miale ya jua inavyochezacheza juu ya maji. Rangi ya mchanga. Vidoti doti vya watu na vyombo vya baharini. Ibua fikra nzito, zinazomgusa kila binadamu. Upendo. Amani. Furaha. Matumaini. Maendeleo. Urafiki. Uzuri. Wema. Mshikamano.

Pamoja sana!

Written by simbadeo

February 8, 2013 at 10:18 pm

3 Responses

Subscribe to comments with RSS.

  1. Si uwongo ni kweli kabisa ..ahsante kwa kutukumbusha..

    Like

    Yasinta/kapulya

    February 8, 2013 at 11:49 pm

  2. ni kweli kabisa, nimekumbuka mbali sana.

    Like

    eric

    February 12, 2013 at 10:53 am

    • Ni kweli Eric. Maisha yanatupeleka puta sana. Usipoangalia, unaweza kujikuta umeshamaliza mwaka hujapata nafasi hata chembe ya kutulia na kutafakari kwa kina unatoka wapi, uko wapi, unakwenda wapi, wewe ni nani n.k. Tumejaliwa kuwa na maeneo hayo, basi na tuyatumie.

      Pamoja sana.

      Like

      simbadeo

      February 12, 2013 at 5:13 pm


Leave a comment