Mabibo Hosteli … Mandhari Kiduchu
Ndiyo. Ni kiduchu tu. korido hiyo ndefu na cafeteria pale Mabibo Hosteli. Kwa hakika huu ulikuwa mmoja wa miradi madhubuti kwa fedha za NSSF (au za wanachama wa taasisi hiyo?). Ukiachilia mbali baadhi ya yale ambayo hujiri hapo … Lakini hapa pamekuwa kitovu muhimu sana katika elimu ya juu nchini. Kuna wengi tu wamepita hapa katika safari yao ya elimu. Kwa wale walio hapo … wakumbuke tu parable ya Nyerere: Kijiji hakikuwa na chakula. Wakaona ni bora wamchagua kijana mmoja, wamkabidhi chakula chao cha akiba, ili yeye akitumie kwenda kutafuta chakula zaidi kwa ajili ya wanakijiji wenzake. Kijana akatoka kwenda zake … SASA, sina hakika kama alisharudi na kupeleka chakula kule kijijini kwake, au baada ya kufika nchi ya neema alisahau kabisa kuhusu wanakijiji waliotoa sadaka chakula chao ili yeye awe na nguvu za kwenda kuwaletea na wao chakula? Maana hizi habari za mabilioni kufichwa Uswisi, na jinsi watu walivyogeuka kuwa mchwa wala fedha na mali ya umma katika karibu kila taasisi … si dalili nzuri. Huenda kijana aliAMUA kuendelea kutumikia tumbo lake binafsi.
Sasa wewe uliye hapo … jitafakari, chukua hatua. Wewe uliyepewa chakula ili uwasaidie wanakijiji wenzako, tafakari, chukua hatua.
Pamoja sana!
Hapo bwana raha yake totoz tu. Unajizolea tani yako! Kiulaiiini
LikeLike
John
December 10, 2012 at 1:31 pm
Duh! John, ya kweli hayo? Naamini wapo wengi tu wanaojiheshimu … ila katika jumuiya kubwa kama hiyo, basi wanakuwepo wachache ambao ndiyo hivyo … hawajuia kusema ‘no’.
LikeLike
simbadeo
December 10, 2012 at 8:09 pm