Ufugaji Kuku … picha ya banda
Wadau wa ufugaji kuku, kutokana na majadiliano yanayoendelea chini ya makala ya Kuku wa Amadori katika blogu hii, tutaanza kuwaletea picha mbalimbali zinazohusiana na kazi hii ya ufugaji kuku. Tunamshukuru sana. Wengine pia mnakaribishwa kutuma picha zinazohusiana na kazi hii. Ni moja ya njia muhimu za kujifunza na kufundishana … kubadilishana uzoefu, maarifa na vilevile kujijengea ‘kamtandao’ fulani ka watu wenye interest zinazofanana. Karibuni sana.
Picha hiyo hapo juu ni kwa hisani ya Jane Mgaya.
samahani km nimekukwaza da jane ila nimeshindwa kuvumilia nimeweka picha yako km desktop background ya laptop yangu nimeipenda sana duh nataka niwe nawaona hawa kuku na banda lao ili nipate uchungu wa maendeleo
LikeLike
damariam
November 19, 2010 at 3:57 pm
Da Mariam
Asante kwa kuipenda picha hiyo ya banda. Ila, Da Jenny alinitahadharisha kwamba picha hiyo siyo ya banda lake (Da Jenny unisahihishe kama sikuelewa), ila ni moja ya picha alizo nazo za mabanda ya kufugia kuku. Amekuwa na picha hiyo (pamoja na nyingine) kwa sababu ya mapenzi yake makubwa katika ufugaji. Mimi nilimshukuru yeye kwa picha hiyo kwa sababu yeye ndiyo amekuwa chanzo cha mimi kuipata na kuichapisha hapa. Natumai tutakuwa tumeelewana. Jamani, kuna mwingine angependa kutuma picha inayohusiana na ufugaji kuku? Karibuni!
LikeLike
simbadeo
November 20, 2010 at 11:31 am
Hata mimi nahitaji ufugaji wa kuku 1400 wa mayai na 800 wa nyama. Je banda linatakiwa kuwa na ukubwa gani. Wapi naweza kupta cage ya kuku wa mayai kama ninazoziona sabasaba banda la JKT
LikeLike
Fatuma
July 13, 2011 at 5:58 pm
Da Fatuma, habari gani? Hapo, kama unaisha Dar es Salaam, basi jitahidi umtafute Da Jenny. Naamini utapata mafunzo muhimu kutoka kwake. Mtafute.
LikeLike
simbadeo
July 14, 2011 at 5:00 pm
safi sana nataka na mimi niaze kufuga jamani mauzoefu tupeane
LikeLike
Gonsalva Mswaga
October 23, 2012 at 3:15 pm
habari..naomba namba za dada jeni tafadhali ili niwasiliane nae kwa ushauri zaidi
LikeLike
george
December 9, 2015 at 6:09 pm
fanya mpango ujaribu kufuga kwani kila kitu ukiweka nia utafanikiwa.anza na Mungu na maliza NA MUNGU NAYE ATAKUJAZA NEEMA
LikeLike
JULIUS JOHN
January 25, 2014 at 8:44 pm
Ushaur mzuri..asante kwa kutukumbusha.hats Mimi ndio najiandaa kwa ufugaji
LikeLike
mboyadear
February 20, 2017 at 11:39 am
siyo wewe tu,binafs limenivutia na nimejifunza kitu ambacho awali sikuwa ninaona umuhimu wake..banda lake ni zuri zaid zaid nimependa halijapigwa sakafu lina mchanga,sasa swali kidogo kwa wataalam mchanga una madhala yoyote kwa kuku,na banda zuri nataman na mie nifanye hivyo
LikeLike
festo ngonyani
February 19, 2016 at 4:12 pm
Habari zenu wadau, nawashukuru sana jamani nilikuwa sijaona hii picha ya panda la kuku. Munu ambariki sana da Jenny kwa kutupa mafunzo zaidi. Nimependa sana hili panda jamani limenitia hamu sana.
LikeLike
Judith
November 22, 2010 at 12:17 pm
Pata full automatic incubator ya mayai 500 kwa sh.Laki 8.5. Ikiwa na ufanisi wa 89nangarantiiitupopkimararaPia tunauza bifaranga wa kienyeji. 0754078015
LikeLike
Gimase
December 9, 2015 at 12:39 pm
Habari zenu wadau wenzangu,
Mimi kwa kweli nimelipenda sana hilo banda la kuku na pia kuku wake kwani ukiwaona tu wanatia hamasa ya kufuga na kujiona kumbe na mimi siku moja nitafikia hapo. Shukrani nyingi zimuendee da Janny kwa moyo wake wa kujitolea kulete hiyo picha ili tuweze kuelimika vizuri M/Mungu akujaalie kila la kheri.
LikeLike
Fatma
November 22, 2010 at 4:43 pm
Duh nimevutiwa sana na panda hili pamoja na kuku hawa nilikuwa na plan ya ufugaji wa kuku nadhani kk nitakutafuta unipe walau mawazo mawili matatu. Hongera sana
LikeLike
dorine
November 27, 2010 at 7:44 pm
Da Dorine karibu sana kwenye kijiwe hiki cha maarifa na kubadilishana mawazo na uzoefu. Picha hiyo ya banda tulitumiwa na Da Jenny. Alitaka kutuonjesha utamu wa kufuga kwa nia ya kututia hamasa na hamu ya kuwa wafugaji makini. Karibu sana, kama una maswali, una majibu kwa maswali yanayoulizwa humu, basi tushirikishe. Asante.
LikeLike
simbadeo
November 28, 2010 at 10:24 pm
Hongera ndg yetu kwa ushauri wenu mzr sana mimi nimekuwa nikifuatilia habari nzr ufugaji wa kuku haswa chotara, kama kroila, kuchi, sjui wa Malawi, wa Israel,, wanatoa mchanganuo wa hadi faidakubwa sana mtu unahamaska kufanya, ila sasa mchanganuo wa chakula unakuwa haupo sasa sjui hapa inakuwaje, au hawa na garama ya chakula na kama ipo tunaomba mtuwekee na mchanganuo wake unakuwaje na garama zake
LikeLike
Mangi
July 11, 2017 at 7:53 am
Hello wadau, banda si langu, ila nililituma kuwa mfano wa banda la kisasa. Nashukuru mmelipenda, hapo ndipo tunapotakiwa kufikia ama kuzidi pia. Tuendelee kusaidiana.
LikeLike
Jenny
December 7, 2010 at 4:01 pm
Da jenny asante kwa picha ya banda, nimelipenda naamini nitalijenga ili kuweka kuku wangu wakae mahali bora na kunipa manufaa. Nina mabanda ya kuku lakini si kama hivi maana hapo nilipo vibaka kibao hivyo nasubiri nimalize kujenga uzio ili niweze kuwaacha wazi namna hiuo maana ukiacha hivyo bila uzio unakaribisha wezi. Salua
LikeLike
Nemyingwa Mhina
April 19, 2012 at 11:37 am
Da Jane unastahiki pongezi kwa imani yako ya kuchangia ujuvyi wako na wadau wengine. Je, una picha zozote zinazoonyesha mabanda ambayo yanajengwa ndani ya fensi ambapo ukuta mmoja huwezi kuweka madirisha? Banda kama hili linawezekana kama una kiwanja kikubwa lakini kwa wafugaji wadogo itakuwa kikwazo…Asante.
LikeLike
Gamdad
July 10, 2012 at 3:45 pm
Asante kwa picha ya banda ni nzuri sana.
LikeLike
japhet e. mungure
November 13, 2013 at 9:02 pm
dada jenny unapatikana wapi mimi nipo kimara dar es salaam,nahitaji elimu zaidi kuhusiana na ufugaji wa kuku wa kisasa.
LikeLike
Mwinyimvua ,M.A
June 28, 2015 at 8:04 pm
habar dada jane..naomba mawasiliano yako ili nipate ushauri kutoka kwako tafadhali
LikeLike
george
December 9, 2015 at 6:12 pm
Assalamu aleykum mimi ninataka kuanza ufugaji wa kuku na nimevutiwa na banda hili ila ningependa nikatumiwa kwa email yangu mabanda mengine ili niweze kujua namna ya kutengeza banda langu
LikeLike
HUSSEIN AHMED MOHAMED
December 24, 2010 at 9:23 pm
Ndugu Hussein, karibu sana katika jukwaa letu hili. Hapa tunashirikishana mawazo, fikra na mbinu mbalimbali katika eneo la ufugaji … kuku, bata, kanga na wengineo … lakini zaidi upande wa kuku. Kumbe basi ili kuenda sambamba na wengine katika kijiwe hiki, chukua muda wako, soma maoni mbalimbali yaliyokwishatolewa kisha nawe utupatie unachojua kuhusu ufugaji kuku, au kuuliza chochote kuhusiana na shughuli hii. Karibu sana na jisikie nyumbani.
LikeLike
simbadeo
December 28, 2010 at 10:57 am
nimeifurahia hii web je wewe ni mtaalamu wa bata.namaswali juu yao
LikeLike
chowdry
April 4, 2011 at 11:14 pm
Ndugu Chowdry
Karibu sana katika blogu hii ambayo ni jukwaa la kubadilishana fikra na maoni. Hapa kuna kikundi cha watu wenye malengo yanayofanana. Hujadiliana kuhusu ufugaji kuku, bata, kanga n.k. Unaweza kufuatilia thread iliyo chini ya kichwa cha habari KUKU wa AMADORI na bila shaka pale ukiuliza maswali utapata majibu mwafaka. Nawe pia waweza kuwashirikisha wengine uzoefu na maarifa yako. Karibu na jisikie nyumbani. Deo Simba.
LikeLike
simbadeo
April 4, 2011 at 11:53 pm
Hallo kaka uko juu sana umenitamanisha na mimi nifuge kuku nilikua na plani hiyo lakini ni mara ya tatu sasa nafuga kuku wa kienyeji lakini wanakufa nadhani sikuwa nafahamu njia bora za ufugaji lakini sasa hivi ndo najifunza naamini tu mambo yatakuwa mazuri.
LikeLike
OSCAR BAKINA
May 15, 2011 at 7:42 pm
Ndugu Oscar, karibu sana katika kijiwe hiki na jisikie nyumbani. Tupo pamoja. Hapa hakuna mwalimu wala mwanafunzi. Sote ni walimu na sote ni wanafunzi. Tunafundisha saa zote na tunajifunza saa zote. Karibu sana uanze kumwaga ‘material’ – hata katika muundo wa maswali, na wadau watakupatia majibu; na wao pia watauliza maswali ambayo wewe pia utayajibu. Kuna usemi kwamba kuanguka mara ya kwanza siyo mwisho wa jambo ulilokuwa unalifanya bali ni somo la kutosha la kukuimarisha zaidi na pia njia ya kufahamu kwamba njia hiyo ya mwanzo si ya kupita bali utafute nyingine. Asante.
LikeLike
simbadeo
May 16, 2011 at 2:31 pm
jamani natumani hamjambo.
na mimi naomba nijiunge na nyinyi
LikeLike
ahmad
June 26, 2011 at 7:11 am
Habari za asubuhi wandugu,na mimi naomba nijiunge na ninyi.Mi naomba mtu atakaye nipa mchanganuo wa kufuga kuku wa nyama 1,000. nitashukuru sana mukinisaidia.
LikeLike
JENNY OCHENG
September 15, 2011 at 8:48 am
duu maisha ndio hayo mkuu wangu panapo majariwa nitakutafuta unipe elimu sahihi ya ufugaji wa kuku wa mayai
LikeLike
sam chani
December 14, 2011 at 10:26 am
dada Jenny ,
Habari za leo.ukweli umenikuna sana na kunipa hamasa ya kufuga .niliomba ushauri kutoka wadau juu ya mchanganuo huo wa ufugaji kuku wa nyama naona mumekaa kimya kidogo mnaweza kunisaidia?
LikeLike
jenny ocheng
December 14, 2011 at 2:10 pm
Nivipi naweza kuwasiliana na mfugaji wa kuku mwenye hilo banda? Nataka kuanza kufuga kuku hivyo ningependa kupata maelezo zaidi kuhusu ujenzi wa banda la kisasa kwa kuku 1,000.
LikeLike
ben
January 12, 2012 at 8:57 am
IWANT TO BE IM MY OWN BOSS
LikeLike
mussa mwakatobe
February 15, 2012 at 11:12 am
Asante sana wadau kwa michango niliyoipata, Mimi nauliza kuwa, hivi kuku wa Kienyeji wa mayai huwa anataga kwa muda gani hadi kuacha kutaga?
LikeLike
Daudi Chale
March 22, 2012 at 12:23 pm
Ndugu Daudi. Karibu sana. Tupo pamoja sana. Swali limefika. Vuta subira na utajibiwa. Karibu.
LikeLike
simbadeo
March 23, 2012 at 10:46 pm
Halo wadau mabibi na mabwana. Hongereni sana kwa elimu hii mmenigusa sana. Cha kuvutia ni kuona dada zetu wakiwa mbele inatia moyo. Da Jane umenihamasisha asante Kuku ni utajiri uliofichika
LikeLike
Kenneth Mwazembe
March 22, 2012 at 7:40 pm
Karibu Kenneth. Jisikie nyumbani.
LikeLike
simbadeo
March 23, 2012 at 10:45 pm
Endeleeni kuelimisha jamii
LikeLike
Kenneth Mwazembe
March 22, 2012 at 7:46 pm
habari ya kazi wajasiriliamali wenzangu! nami pia ni mfugaji wa kuku za kienyeji, ila nimefurahishwa sana na banda hilo! napenda kujua kuku wanaingia hilo banda wakiwa na umri gani? chini kuna maranda au sakafu tupu? asante
LikeLike
vivianne kokulengya
May 15, 2012 at 1:16 pm
Ningependa kuanza kufuga kuku wa kienyeji lakin nipo Mbeya.Ningependa kupata elimu ya ufugaji bora na wakisasa wa kuku wa kienyeji
LikeLike
Margareth Swai
May 16, 2012 at 4:02 pm
Salaam, nahitaji kuwekeza mtaji wa 10m. kwenye ufugaji wa kuku wa nyama, au hata wa mayai lkn sijapata mchanganuo wa kuniwezesha,je naweza kupata kwako? nina hekari 4.
LikeLike
Ezekiel
May 22, 2012 at 11:21 pm
Ndugu Ezekiel. Karibu sana kwenye jukwaa hili la kubadilishana mawazo. Umeuliza swali zuri. Lakini mimi pia ningependa kukuuliza – Je, umesoma makala zote zilizo chini ya mada hii kwenye jukwaa hili? Ukisoma zote bila shaka utapata majibu kwa swali lako.
Karibu katika ulimwengu huu na usisite kutupa maendeleo ya mradi wako.
LikeLike
simbadeo
May 23, 2012 at 10:11 am
Bw.Simbadeo hizo makala ziko posted wapi ili nipate kuzisoma?
LikeLike
Ezekiel
May 26, 2012 at 8:55 pm
Kuna watu wanauza vifaranga wazuri sana nasikia kuliko wa Amadori mmewajaribu! Wanapia madakatari wao wakufuatilia vifaranga vyao kama vina matatizo ya ukuaji na magonjwa.Wapo maeneo ya Sinza.
LikeLike
Margareth
May 28, 2012 at 4:43 pm
Hi Margareth, asante sana kwa taarifa hiyo. Pengine kuna wadau hapa ambao watapenda kuwajaribu watoa huduma hao. Hivyo, itafaa sana ukitafuta contact zao kamili, taratibu zao nyingine za kibiashara na kutushirikisha hapa.
Asante sana kwa juhudi yako. Tuendelee kuwepo.
LikeLike
simbadeo
May 31, 2012 at 9:18 am
Je tunaweza tukawa partnership nikachangia kwenye ardhi?Nina eneo lenye ekari zaidi ya 20 eneo la Mkuranga kama kuna watu ambao twaweza kuingia kwenye partneship/group or wajasiriamali na tukafanya kitu kikubwa zaidi?
LikeLike
Margareth Swai
May 23, 2012 at 12:52 pm
ilo wazo thudhuri je umeandika busness plan yako
LikeLike
ahmad
May 23, 2012 at 5:31 pm
Ninayo business plan ,pia ninayo mashine ya kusaga na kuchanganya chakula cha wanyama (Kuku,ng’ombe,nk) ambayo inatoa tani 1.5 kwa saa.
LikeLike
Margareth Swai
May 24, 2012 at 1:59 pm
duh ilo banda na kuku wake wamependeza sana imenivutia sana nipo kwenye harakati za kujiingiza kwenye mladi huo ila kunamambo sija yaweka sawa nikishamalizana nayo tu nitakutafuta mdau. naitwa MUYA
LikeLike
muya Ramadhani ally
May 26, 2012 at 7:45 pm
Dear Brothers & Sisters nina shtuka sana nikiona kuku,ninataka kufanya kuku wa kienyeji kuwa biashara yangu huu na mwaka wa 3 najaribisha lakini sijawahi fanikiwa nifanyeje? Huku kwetu Mufindi tatizo ni Baridi nipeni njia ya kufanya Kwa mfano Mwezi wa 2 nilikuwa na vifaranga 150 waliokuwa waki tunzwa na mama zoa 10 lakini walikufa na kubakia 5 jamani ninajua mnanipenda hembu nipeni akili ya ya kufanikiwa kwani ninijaribu tena na sasa kuku ishirini wanaatamia mayai 13 kila mmoja ninahofu baridi itawa ua! Thanks in Advance.
LikeLike
Laigwenam
June 7, 2012 at 3:33 pm
kaka habari, mie ni mgeni kwenye hii blog, nimejiunga leo, nipe e-mail yako nikutumie notes usome, huenda zitakusaidia
LikeLike
Maduhu Lusamla
June 15, 2012 at 3:46 pm
Hi Ndugu Maduhu
Karibu. Waweza kuniandika kupitia kakasimba@gmail.com . Samahani, mara nyingine ninaweza kuchelewa kidogo kujibu kwa sababu ya uhaba wa muda. Hivyo, ukiona kimya kwa siku kadhaa usijali sana. Endelea kuvuta subira.
Tuendelee kuwepo.
LikeLike
simbadeo
June 17, 2012 at 4:24 pm
Habaru kaka maduhu naomba unisaidie na mm hizo notes
LikeLike
irene angelo
July 20, 2015 at 11:14 pm
Ndugu yangu jaribu kutumia “pharmaxine chick plus” unaweka kijiko kimoja cha chai kwa kila lita tano za maji kwa siku tano.
LikeLike
Mseya
August 28, 2013 at 1:04 pm
mimi nina vifaranga vinakufa, vinaota vipele kwenye macho na sehemu za mabawa kuoza, nimechanja chanjo ya ndui lakini wanakufa, ni vifaranga wa kuku wa kienyeji, naomba anayejua tiba anielimishe
LikeLike
Maduhu Lusamla
June 15, 2012 at 3:52 pm
Banda la kuku nimelipenda sana, je unaweza kuona banda la mbuzi nataka nikajenge shambani kwangu?
LikeLike
BAM
June 20, 2012 at 12:45 pm
Jamani mimi nina kuku wa kienyeji wanataga mayai halafu baadhi wanakula mayai tena, sasa nifanyaje ili wakome kula? kuna dawa ya kuwapa?
LikeLike
Maduhu Lusamla
June 22, 2012 at 1:21 pm
Ndugu Maduhu, Mwangaluka. Jitahidi kuwapa madini ya chokaa kwenye chakula chao. Pia maganda ya mayai baada ya kula au mabaki baada ya kuanguliwa vifaranga unaweza kusagasaga na kuchanganya na chakula chao. Hali ya madini ya chokaa huimarisha mayai yanayotagwa.
LikeLike
Kenneth Mwazembe
June 22, 2012 at 5:26 pm
Ng’wadila ndugu Kenneth; Ahsante sana kwa ushauri wako wa kitaalam, ngoja nianze kuutumia.
LikeLike
Maduhu Lusamla
June 25, 2012 at 1:39 pm
hapari wadau, mimi ni mgeni katika blog hii nina hamu ya kufuga kuku wa kisasa kama 2000 wa mayai na nyama naombeni ushauri wenu namna ya kujenga banda, chakula na mtaji ninaopaswa kuanza nao asante, email yangu ni benjahm@yahoo.com
LikeLike
benjamin
June 23, 2012 at 7:46 pm
Check hii link (https://simbadeo.wordpress.com/2010/11/19/ufugaji-kuku-picha-ya-banda/#comment-3239) utaona picha ya banda
LikeLike
Maduhu Lusamla
June 25, 2012 at 1:47 pm
habari wadau, nimependa sana hiyo picha na imenitia hamasa kubwa ya kuwa mfugaji bora wa kuku.Nataka kufuga kuku aina ya amadori na kuchi, naweza kuwapata wapi? naomba pia ushauri wa ufugaji bora.
LikeLike
Dorine Msuya
July 2, 2012 at 2:40 pm
Anayejua dawa ya kienyeji ya kutibu ndui ya kuku aniambie jamani
LikeLike
Maduhu Lusamla
July 4, 2012 at 1:53 pm
alovera
LikeLike
Jane Zum
July 5, 2012 at 2:59 pm
Nashukuru sana Jane kwa kunipa ushauri wa kutumia alovera, ngoja niitafute nitumie
LikeLike
Maduhu Lusamla
July 9, 2012 at 1:07 pm
poleni na shughuli za hapa na pale jamani, nimefurahishwa na ajira binafsi inayoendelea katika blog hii, naamin kwa jinsi hii tatizo la ajira kwa vijana litapungua sana. Nampongeza mwanzilishi wa blog hii kwa ubunifu huu wa kutukutanisasha kimawazo, naomba kujiungaa maana nami ni mdau wa aufugaji!
Ama baada ya hayo nina maswali kadhaa ambayo ningependa ku-share na wadau:
1. je kuku wa kienyeji wanaweza kuwa kuwekwa pamoja kwa wingi kama wa picha hapo juu bila kuwekewa partition?????
2. unaweza ukafuga kuku wa kienyeji kwa kuwaweka karibu na kuku wa kisasa lakini ktk mabanda tofauti na wakakua bila ya matatizo ya magonjwa n.k.?
3. kwa mujibu wa picha hapo juu, napenda kufahamu kama kuku wa kienyeji wanahitaji majukwaa ya kupumzikia au la.
Ni hayo tuu wadau wenzangu nisiwachoshe sana.
Karibu kwa maoni yenu.
LikeLike
Malimi Mojo
July 9, 2012 at 11:49 am
Habari kaka, kwa uzoefu wangu, kuku wengi ukiwaweka pamoja ni rahisi kuambukizana magonjwa, na kupigana pia maana watabanana. ni vema ukiwa na banda kubwa kama hilo, jaribu kufanya partition(Kuku wanaotaga sehemu yao, idadi kubwa ya majogoo sehemu yao, na wale wanaokaribia kutetea wachanganye pamoja na majogoo kiasi pamoja. vilevile vifaranga lazima wawe na sehemu yao maalumu. Ukiwaweka pamoja bila partition ni rahisi kupigana na kuaffect ulaji wao
LikeLike
Maduhu Lusamla
July 11, 2012 at 12:40 pm
Mimi ni mgeni wa blog hii na nimefika baada ya ku-google namna ya ufugaji wa mayai, michango ya humu inavutia sana hadi nimeshawishika kujumuika na watanzania wenzangu. Mimi ni mfugaji wa broilers, nimefuga kuanzia February na nimepita awamu tano. Sasa najipanga kuanza na ufugaji wa layers…
LikeLike
Gamdad
July 10, 2012 at 3:40 pm
Jamani chakula chenye madini ya chokaa kinapatikana wapi?
LikeLike
Maduhu Lusamla
July 11, 2012 at 12:43 pm
Mheshimiwa Maduhu. madini kwa ajili ya kuku hupatikana ktk maduka ya vyakula vya mifugo utapata premix kwa layers na broilers na chokaa. Madini mengine ni kuchemsha na kukausha damu ya wanyama, kuchoma na kusaga mifupa ili kupata calcium na phosphate. Kwa kuku wetu wanaochakula ardhini huko wanapata madini yote. Pia lisha mboga kwa wingi.
LikeLike
Ken Mwazembe
July 11, 2012 at 9:29 pm
blog hii nzuri sana.nami najiunga.naomba namba ya simu ya fundi wa banda hili da jane. pia wafugaji wazoefu naomba picha zimngine za mabanda bora ya gharam a nafuu. madani
LikeLike
madani
July 13, 2012 at 6:13 pm
nashukuru sana kaka Maduhu Lusamla, nimekusoma vilivyo.
LikeLike
Malimi Mojo
July 17, 2012 at 2:34 pm
nini maana ya layers na broilers?
LikeLike
Malimi Mojo
July 19, 2012 at 9:47 am
Kuna broiler starter ni chakula chenye chembe ndogondogo sana cha kukuzia vifaranga chenye mchanganyiko wote unaotakiwa na broiler finisher, unawapa vifaranga tu. na kuna broiler finisher ni chakula chenye mchanganyiko wa protein ambacho kuku wanaokua na wakubwa wanakula
LikeLike
Maduhu Lusamla
July 19, 2012 at 4:14 pm
Jamani nina vifaranga vya wiki moja,vingine siku nne, vikiamka asubuhi naviona vimechangamka lakini baadaye vinaanza kulia na kushusha mabawa na kufa ghafla, sijui ni ugonjwa gani? Au ni baridi? nashindwa kujua ni ugonjwa gani. mwenye uzoefu naomba mawazo.
LikeLike
Maduhu Lusamla
July 23, 2012 at 5:23 pm
Nina vifaranga vya kuanzia siku tatu hadi wiki mbili, kila siku lazima mmoja afe ghafla. anaweza akaamka asubuhi mzima lakini baadaye anashusha mabawa na kuanza kulia lia mda mwingi, na baadaye kufa bila kujua ni ugonjwa gani hasa. Anayejua sababu kuu ya kushusha mabawa na kuanza kulialia na baadaye kufa anijulishe tiba yake. Vinanipa shida sana kwani vinakufa vikiwa na afya kweli.
LikeLike
Maduhu Lusamla
August 1, 2012 at 12:35 pm
nimefurahi kujua kuna blog inayohusu ufugaji kuku,nipo tayari kujifunza na kujua zaidi kwa sasa nina kuku wa 52 wa kienyeji,napenda kujua jinsi ya uchanganyaji wa chakula cha kuku
LikeLike
kijja
August 10, 2012 at 10:33 am
mimi naitwa Raphael nataka kufuga kuku wa kienyeji kitaalamu.nahitaji kujua chanjo zake. matunzo.na wapi nitapata ifaranga wa bei nafuu.
LikeLike
RAPHAEL CHAMBO
August 25, 2012 at 12:36 am
Mimi naitwa Vicky, napenda sana ufugaji kuku wa kienyeji, lakini sijaweza kufahamu mahali wanapouza,je naweza kuvipata wapi vifaranga vya kuku hao ninunue ili nianze kazi rasmi?Mabanda ninayo na eneo la wastani tu.
LikeLike
Juliana Kimario
August 26, 2012 at 11:51 am
Hawa kuku wa kienyeji wanapatikana kila mkoa ila kwa wale weusi wa Malawi unapata Mbeya hasa wilaya ya Ileje.
LikeLike
Kenneth Mwazembe
August 26, 2012 at 12:38 pm
Asante sana Kenneth. Ni habari muhimu umetupatia. Ila kama una contacts za wauzaji na kama wanaridhia ziwekwe hapa, basi naamini itakuwa kwa manufaa ya wengi hapa. Karibu.
LikeLike
simbadeo
August 27, 2012 at 7:55 am
jamani group la wafugwaji hamjambo, mimi naitwa Judy naishi Kibamba Dsm, siku nilikuwa member lakini nikapotea kutokana na shida za hapa na pale, naomba kaka simbadeo unirudishe kundini tafadhali.
LikeLike
JUDITH
November 7, 2014 at 5:12 pm
mimi ndo kwanza nimeingia ktk hii blog..kwa kifupi mimi nataka kuanza kufuga kuku ma mayai sasa nilikua naomba kujua ni wapi nitapata vifaranga kwa bei rahisi mfano sh 2000 kwa kifaranga. Nimejaribu kufanya utafiti wa bei, wengi wanauza sh 2500 kwa kifaranga.. Pia Naomba ushauri wako, mimi kama mjasiliamali nahitajika kuanza na kuku wangapi?? na hawa kuku wanachukua muda gani mpaka waanze kutaga mayai? pia vyakula vyao nitapata wapi kwa wingi?
LikeLike
witgal
August 27, 2012 at 11:23 pm
Jaribu mjasiriamali huyu ,nimesikia anatotolesha vifaranga vizuri na anauza chakula cha kuku pia.
0783833335.Atakusaidia
LikeLike
asnath
August 28, 2012 at 11:20 am
Mimi nataka kufuga kuku wa mayai,naomba kujua uwiano wa idadi ya kuku na ukubwa wa banda; material gani hutumika ktk kujengea banda na vifaa vingine vinavyotumika ktk ufugaji wa kuku wa mayai.
LikeLike
Michael
August 28, 2012 at 6:08 am
Nimesahau kitu jaman mi nna kuku wa kienyeji sasa nataka wazaliane kwa wingi niwapatie kitu gani! Na nimepata tetesi kuanzia huu mwezi kunakuwa na ugonjwa wa kuku wanakufa ovyo sasa sijui niwape kinga gani jaman! Nomben ushauri wenu, jioni njema.
LikeLike
bertha shirima
August 8, 2014 at 6:07 pm
ni kweli tunahitaji kupanua wigo ktk ufugaji maana ujasilia mali ndo kazi iliyobaki
LikeLike
fredy kalongoti
September 5, 2012 at 10:14 am
Wadau kijiwe nimekipenda nina eneo kubwa nataka kufuga kuku wa nyama na mayai je?nitapata wapi vifaranga
LikeLike
Gratian Kasenene
September 14, 2012 at 8:44 pm
Wadau, nilianza na makoo 2 na jogoo 1 kuku wa kienyeji na kufikisha kuku 50,Kukosa umakini kuliniangusha, mawazo ya wadau yamenisaidia, ninajaribu tena , ukweli kuku wa kienyeji hawana gharama kama kuku wa ”kizungu” ,wa kienyeji wanauwezo wa kuhimili magonjwa ,
Natumia pumba za mahindi ,mashudu ya alizeti ,machicha ya nazi na mabaki ya chakula kama wali na ugali.
dawa za kienyeji ,aloevera, mlonge,zinasaidia sana,
sasa natumia kinga ya water soluble .inauzwa elfu sita ktk maduka ya kilimo. kinga imara kwa magonjwa mengi ya kuku
LikeLike
Bakari Hashimu
September 23, 2012 at 2:12 pm
Ndugu Bakari, asante sana kwa ushuhuda wako. Kila unapopata nafasi, tafadhali endelea kutushirikisha. Karibu sana.
LikeLike
simbadeo
September 26, 2012 at 9:41 am
kaka hii kinga wa water soluble inakuwaje hii? ni ya maji au unawapaje kuku?
LikeLike
Maduhu Lusamla
October 5, 2012 at 5:09 pm
Nina vifaranga 52 vina umri wa wiki moja toka kutotolewa, vinaota upele pembeni mwa macho, upele sehemu za mabawa, sehem za masikio na vinalia na kufa ghafla, nilikuwa navyo 52 lakini sasa vimebaki 25 tu, naomba msaada ni dawa gani inafaa kuwatibu kutokana na kuota vipele, ninavyovua chanjo ya ndui ni kati ya mwezi mmoja hadi miwili lakini hawa hawajafikia umri huo
LikeLike
Maduhu Lusamla
October 8, 2012 at 1:30 pm
Wadau wa ujasiriamali kupitia ufugaji wa kuku,nawasabahi,.Nami pia ni mdau katika sekta hiyo.Naomba kupata ushauri,kwenye matandiko ya kuku ndani ya banda,kati ya maranda ya mbao na pumba za mpunga zlizomenywa,kipi ni bora kuweka sakafuni,iwe ni wa kienyeji,broiler au layers?
LikeLike
Geoffrey mtelekela
October 13, 2012 at 4:42 pm
Banda lako dada Jane ni banda ni Bomba, lakini funga mabox ya vyakula na drinkers ziwe zinaning’inia ili upunguze umwagaji wa chakula na maji. Pia ili kuku wafanye mazoezi funga fito kwenye umbali unaofaa ili waweze kuruka ruka. Na pia fito hizo zitumike kwa kuwafungua kuku majani. Na kw aufahamu wangu vifaa hivyo vinafungwa kwenye nguzo hizo za kati – upande mmoja unaweka maji na mwingine unaweka chakula.
LikeLike
Bibi Mwapombe
October 17, 2012 at 1:55 pm
Habari wadau, naona kama vile nimechelewa nimevutiwa sana nami ni mdau ktk anga za ufugaji kuku haswa wa ASILI
LikeLike
KAPILIM
October 22, 2012 at 2:24 am
Ndugu Kapilim, hujachelewa. Kwenye archive ya mijadala hii unaweza kujipatia shule ya kutosha. Licha ya jambo hilo wewe pia unahaki na ruhusa kamili ya kutuelimisha wengine. Karibu sana.
LikeLike
simbadeo
October 22, 2012 at 10:15 pm
Nimefurai sana kupata brog kama hii,nami nata kufuga mara moja kuku wa asuli nadhani nitafanikiwa,nimejaribu kufuatilia maoni mbali mbali ya wadau kuku wa amadori mpaka hapa nashukuru sana
LikeLike
Emmiliana
November 1, 2012 at 4:59 pm
napenda kufuga kuku lakini cjui hata pa kuanzia tafadhali naombeni ushauri
LikeLike
rajab shomari
December 24, 2012 at 3:09 am
natamani kufuga mabata, ninatakikana niwe na nyumba ya aina gani, Naombeni ushauri
LikeLike
Happiness
January 9, 2013 at 6:39 pm
Karibu Happiness. Kwa vile umeleta hoja hiyo kwenye jukwaa hili, basi vuta subira atapatikana mtu wa kushare na wewe na sisi kwa ujumla wa nini kifanyike ili kufanya ufugaji bora wa bata. Endelea kufuatilia!
LikeLike
simbadeo
January 11, 2013 at 3:30 pm
Ufugaji wa kuku hauna tofauti kubwa na ule wa mabata, unachotakiwa kuongeza au kuzingatia ni kuwawekea bwawa dogo la wao kuogelea. Pia ulishaji wa bata chakula chake ni lazima kilowekwe kwenye maji kidogo tofauti na kuku anayekula kikavu.
LikeLike
Kenneth Mwazembe
January 11, 2013 at 5:52 pm
Jamani nisaidieni kupata makoo mazuri kama kumi na majogoo kama mawili.
LikeLike
Rhoda Kwareh
March 10, 2013 at 1:40 am
Karibu sana Rhoda Kwareh. Je, umesoma makala zote humu kwenye jukwaa letu? Kama bado, tafadhali tafuta wasaa, utulie na usome neno kwa neno. NIna imani utapata maarifa mengi na habari mbalimbali za kukusaidia kufikia azma yako.
Hata hivyo, wadau wanakaribishwa kujibu baadhi ya maswali moja kwa moja kwa kujibu comment hii.
Karibu sana jukwaani.
LikeLike
simbadeo
March 14, 2013 at 2:59 pm
habari zenu wadau katika pita pita zangu kwenye mtandao nimebahatika kukutana na glog hii na kwakweli nimenivutia sana
kiukweli nami nimo katika maandalizi ya kuanza kufuga kuku wa kienyeji, shida sijuwi wapi nitapata vifaranga wa kuanzia wenye ubora.
naomba nijulishehi wadau.
LikeLike
shafi qadir
March 13, 2013 at 10:25 am
Karibu sana Shafi Qadir.
Naam, hili ni jukwaa ambamo tunabadilishana maarifa, uzoefu na kupeana miongozo katika uwanja huu wa ufugaji. Tufahamishe maendeleo yako kuhusu eneo hili kadiri nafasi inavyokuruhusu.
Asante na kila la kheri. Pamoja sana.
LikeLike
simbadeo
March 14, 2013 at 3:01 pm
haaa!yaani nimefurahi mno kuijua blog hii, maana hata mimi nina mpango wa kufuga kuku wa kienyeji ndo najiandaa napenda kupata ushauri hasa wa uzalishaji zaidi wa kuku bora
LikeLike
Emma John Ntwale
May 26, 2013 at 7:05 pm
sijawahi kufuga kuku wa kienyeji ila nimeanza kwa ajili ya kujifunza nilianza na kuku kama kumi na nimejifunza changamoto mbali mbali ila nahitaji wazoefu kwa ajili ya ushauri zaidi
LikeLike
Emma John Ntwale
May 26, 2013 at 7:10 pm
Habari wapendwa.Naitwa Musunga.Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kugundua “machimbo haya ya dhahabu”.Kwa hakika nimefarijika sana kuona namna watanzania tulivyo na ukarimu na upendo wa ajabu.Katika jukwaa hili,nimeona watu wana utajiri mkubwa sana wa MOYO.Pasipo kinyongo wala kuchoka,mwenyekiti wetu ndugu yangu Simbadeo na wanajukwaa wote wamekuwa wana toa elimu kwa upendo bila kuchoka na bila ubaguzi Mungu awabariki sana.Baada ya kusoma maswali na maoni na ushauri mbalimbali kuanzia mwanzo,nimeshawishika nami kufuga kuku.Naamini ujio wangu hapa si wa bahati mbaya,naomba ushirikiano wenu.Maswli mengi niliyo taka kuuliza nimepata majibu yake kupitia maswali yalokwisha ulizwa na wajumbe wenzangu.Kwa sasa naomba kujua bei ya sasa ya vifaranga wa nyama na mayai,mwenye kuifahamu naomba anisaidie ili nami niwe miongoni mwenu kivitendo.Mbarikiwe nyote.Mwenyekiti naomba rasmi kuwa miongoni mwenu.
LikeLike
faustine musunga
May 30, 2013 at 9:29 am
Ndugu Faustine Musunga
Karibu sana katika jukwaa hili. Naam. Hapa kila mmoja ana maarifa ya kuwapa wengine, naye pia ana fursa ya kupata maarifa mapya kutoka kwa wenzake. Karibu sana tuliendeleze gurudumu katika kujitafutia ukombozi wa kiuchumi na kifikra.
Pamoja sana.
LikeLike
simbadeo
June 2, 2013 at 1:36 pm
Ni mara ya kwanza kuingia kwenye mtandao huu,kwa kweli nimefaidika kutokana na mambo nilio ya pata.Nawashukuruni kwa michango yenu kwani imenivutia sana
LikeLike
liston
June 23, 2013 at 5:32 pm
Karibu sana Liston.
Tupo pamoja.
LikeLike
simbadeo
June 24, 2013 at 11:52 pm
hello. ninapenda sana kufuga. ila ningeoenda sana kuwa na business pla ya ufugaji kuku broiler. nishauri please pa kupata ili nifanye kwa hakika Zaidi.
asante sana.
LikeLike
helen
October 29, 2015 at 1:09 pm
wapendwa wangu za masiku namshukuru mungu miaka miwii ya mamsomo imeisha saama nimerudi jukwani ila ntomba sn muongozo kwani niko tupu mungu akipenda ntaanza ufugaji oct nawapenda sn
LikeLike
da mariam
July 14, 2013 at 5:03 pm
Da Mariam,
Hongera sana kwa jitihada ulizofanya kujiendeleza kielimu. Naamini hiyo itatusaidia sisi pia kuchota maarifa zaidi kutoka kwako. Karibu tena jukwaani na uwe huru kushiriki kadiri Mwenyezi Mungu atakavyokujaalia.
Kila la kheri.
LikeLike
simbadeo
July 19, 2013 at 12:50 pm
mm ni mzalishaji mdogo sn wa vifaranga naomba mawasiliano yenu km mobile no so as to get different type of chickens
LikeLike
laurean mngongo
September 27, 2015 at 8:27 am
katika vi2 nilivyo kuwa natafuta ndo hivi nashukuru sana kwan nitakuwa nimefika nyumbani. Thanks sana wadau kwa kuanzisha hii blog siyo kila sehemu siasa kumbe kuna vitu vya msingi kama hivi.
LikeLike
abuu
July 23, 2013 at 4:54 pm
Abuu. Karibu sana. Milango iko wazi kwako kuchangia mawazo na maarifa kwa namna unayoona inafaa ili wanabaraza wengine nao wajifunze kutoka kwako. Karibu sana.
LikeLike
simbadeo
July 24, 2013 at 11:59 am
nmevutiwa na mijadala hii hongera kwa kila mmoja. nimekua nkifuga kuku wa nyama kwa miaka mitatu sasa. nataka kuaanza kufuga kuku wa mayai ila nmetishwa sana kwamba wanagarimu pesa nying sana mpaka kuaanza kutaga.sasa naomba mnifahamishe wapendwa, kwa kuku 100 wa mayai, mwezi wa 1,2,3,4,5 mpaka mwenz wa 6 wanakula kiasi gani au mifuko mingapi, kwa kila mwenzi wanaokua kwenye ukuaji kimmtiririko? nisaidieni kipato changu si kikubwa sana hivyo naogopa kuanza ikafika katikati nkashindwa
LikeLike
Elias Kilango
July 26, 2013 at 12:59 pm
Ndugu Elias Kilango, karibu sana jukwaani hapa. Wakati wadau wakijiandaa kutoa maoni yao kuhusu kiu chako, ni vema ukapitia pia majibu mbalimbali ambayo yamewahi kuwekwa hapa, naamini kwamba utapata mwelekeo. Hongera sana pia kwa hatua uliyofikia katika ufugaji, kwa hakika una mengi ya kutufunza. Karibu sana.
LikeLike
simbadeo
July 28, 2013 at 11:59 am
naomba na mm nijiungendugu zangu maana natamanisana kufuga ila taaluma niliyonayo haitoshi
yusuph
LikeLike
yusuph
August 15, 2013 at 2:14 am
Ndugu Yusuph
Karibu sana. Ukumbi ni wako kuchota maarifa na kutoa maarifa kupitia jukwaa hili. Karibu sana.
LikeLike
simbadeo
August 17, 2013 at 8:13 pm
Namshukuru sana mwenyenzi mungu kwa kutujalia punzi na kuweza kubuni mbinu nzuri ya kuuwaga umaskini mimi pia ni mfugaji nipo ifakara morogoro naomba mnisaidie kuna ugonjwa wa kuvimba maini na filigisi kwa kuku wa kienyeji nimeangaika kwa madaktari wa mifugo bila mafanikio kama mnauzoefu na ugonjwa huu naomba mnisaidie kwa sababu kuku wangu wanakufa sana.
LikeLike
Goodluck .J.Makari
July 4, 2014 at 4:21 pm
vizuri sana wadau
LikeLike
yusuph
August 15, 2013 at 2:19 am
Naitwa Revocatus Kasigwa, ninapenda kujua au kufahamu utaalam wa kufuga kuku, wa kienyeji na pia ujenzi wa banda bora
LikeLike
Revocatus Kasigwa
August 27, 2013 at 9:44 pm
nimeguswa sana na michango mbalimbali ya wadau. mungu awabariki kwa moyo wenu wa uwazi kuna vitu vizuri nimejifunza. nami najiunga nanyi tupeane uzoefu kwani mimi pia nafuga kuku wa kinyeji japo mwanzo nilianza na kuku wengi ila mradi ulishuka kwakuwa nilikuwa siko full commited nikaachia vijana ambao walinichakachua hivyo nimeanza upya sasa. mungu akubariki kaka simbadeo kwa blog hii na big up kwa wadau wote tuko pamoja.
LikeLike
agy
August 31, 2013 at 5:22 pm
Ni makala nzuri iendelee
LikeLike
Jane simon
September 1, 2013 at 8:09 pm
Habari wadau, hongereni kwa ujasiriamali, Mungu awatie nguvu na shetani ashindwe kabisa.Mimi ni mfugaji pia nilikuwa naomba kupata namba ya simu ya fundi wa kutengeneza cage za kufugia kuku, pamoja sana daima.
LikeLike
mama sam
September 12, 2013 at 10:43 am
mimi ni mfugaji wa kuku, hii ni mara yangu ya kwanza kuitembelea blog hii,ningependa tuwe pamoja
LikeLike
dandalla juma
September 25, 2013 at 8:21 pm
Nahitaji kujifunza kutoka kwenu mimi ni mfugaji na ninajiandaa kuwa mfugaji mkubwa zaidi ya hapa nilipo.
LikeLike
John P.Mwandika
October 5, 2013 at 6:19 pm
Habari wapendwa….
Naitwa Magreh John,nami napenda kuwa mmoja wenu ktk blog hii na ndio kwanza naanza
kwakweli sina nnalolijua kwahiyo naomba sana msaada kutoka kwenu..Kila la heri ktk ujenzi wa Taifa
LikeLike
Magreth magingo
October 24, 2013 at 4:52 pm
aisee ufugaji wa kuku naupenda sana, mafunzo yanapatikana wapi kwa wakazi wa arusha
LikeLike
Abdi Hassan
October 31, 2013 at 11:02 am
Mimi ni mfugaji mzoefu hapa kibamba,kwa sasa naandaa mabanda pale kibaha kwa ajili ya kufuga kuku wa chotara,kuku wa malawi na wa kienyeji pamoja na kuku wa mayai wa kisasa,je unaweza kuniuzia vifaranga?
John P.Mwandika
Tel 0716-800086
LikeLike
John P.Mwandika
October 31, 2013 at 11:27 am
Majina yangu ni Mgawe Revocatus, nimetamani siku nyingi sana kupata elimu kama hii. nimefarijika sana kukutatana na blog hii kwani ni sehemu ambayo mtu unajifunza vitu vingi sana kumhusu kuku na ufugaji kwa ujumla.
Mimi nimeanza na kuku kienyeji 22 natamani siku moja kuwa nao 10,000 kwa mpigo wadau naomba mnipe mbinu na njia ya kuwafikia kwa haraka
LikeLike
Revocatus Mgawe
December 29, 2013 at 12:58 am
Mdogo wangu Mgawe mwana wa kumwitu, suala la uamuzi wa kufuga ni aina gani ya kuku inategemeana na jinsi ulivyojiandaa. kwa maoni yangu ungefuga kuku wa mayai ambao utaanza kupata mauzo baada ya miezi sita. Kwa mzunguko wa haraka wa fedha kuku wa nyama kama una soko la haraka ni wazuri
LikeLike
Kenneth Mwazembe 0762246322
January 7, 2014 at 1:55 pm
asante Kenneth kwa kunifungua mawazo na mimi, maana nilikua dilema. nimejiandaa kufunga kuku by end of this jan, lakini nilikua dilema najiuliza nifuge kuku wa mayai au nyama. Kitu kingine jamani naombeni ujuzi kwa wale mlioko kwenye ufugaji tayari. hivi ukiwa unabadilisha let say magazeti uliowekewa kuku mwanzo, kuku unawatoa au wanakuwa humo humo, na je utasafishaje sasa sikutatimka vumbi na kuku watadhurika? naombeni mbinu jamani.
LikeLike
reuben_rachel@yahoo.com
January 9, 2014 at 4:07 pm
Hi Rachel
Wafugaji tuna maandalizi tofauti. Ukiwa na banda halafu ukawa na eneo lililozungushiwa uzio ni vema ukawatoa kuku nje ukimaliza usafi utawarudisha. Iwapo eneo lako dogo utalazimika kufanya usafi wakiwa humohumo cha kujali ni kufungua madirisha yote ili mzunguko wa hewa uwe mkubwa.
LikeLike
Kenneth Mwazembe
January 15, 2014 at 2:01 pm
Kaka Kenny.
Aksante kwa ushauri wako.
LikeLike
Revocatus Mgawe
January 9, 2014 at 4:35 pm
Happy New Year 2014 wapendwa, natumaini mmekua na wakati mzuri saana na biashara zenu zimeleta faida msumu huu wa sikukuu
nina siku nyiingi saana sijaandika hapa, ila nimekua nikikusanya comments zenu zooote, kuna kipindi nilitaka kuanza kufuga lakini kuna mambo yakajitokeza, sasa hivi nimedhamiria kabisa kabisa kuanza na ninatarajia kuanza by February. Lakini sasa nina mawazo 2 yanagongana kichwani kwangu, lengo langu ni kufuga kuku wa kisasa, kati ya wa nyama au mayai, yaani hapa nashindwa hata nianze na kuku gani maana mtaji niliyo sevu ni kwaajiri ya aina moja kati ya hizo mbili. wazoefu naombeni mnishauri nielekee upande upi. lengo hasa nikufanya biashara hii nakuepukana kabisa na kuajiriwa kiukweli nimechoka kupigana na daladala kila siku asubuhi kwenda ofisini nataka kujiajiri, sina eneo kubwa sana nina eneo dogo tu nyumbani la kutosha kuku wazio zidi 300.
jamani nisaidieni……..thanks a lot.
LikeLike
reuben_rachel@yahoo.com
January 6, 2014 at 4:21 pm
Heri ya mwaka mpya kwa wote! Mimi binafsi sina eneo la kutosha hapa mjini! nimeweza kutengeneza mahali padogo sana penye uwezo wa kuku kama mia moja na hamsini hivi. Ni mgeni sana na shughuli hii ya ufugaji wa ndani maana niliwahi kufuga free range system nikiwa mdogo! Nahitaji ushauri wa kina Wadau!
LikeLike
LUNDISASI MNYAKIDUNDANDZINGO
January 11, 2014 at 5:16 pm
Habari!!
Nimefurahi sana kuona blog hii ya mambo ya ujasiliamali wa ufugaji. napenda sana kufuga, ndo nimeanza kufuga. kwaiyo naendelea kupata uzoef kutoka kwenye blog hii. asanteni sana. name nitakua natoa uzoefu wangu.
Juliet
LikeLike
Juliet
January 15, 2014 at 12:40 pm
habari ndugu,mimi ni mjasiliamali wa kuku hasa chotara na ninandoto zakufikia hapo ulipo,nipo morogoro eneo la nanenane,najihusisha hasa nakuuza vifaranga vya kuku chotara,ila natamani kuingia kwenye kuku layers,nahitaji mazungumzo nawe,namba yangu 0764174288
LikeLike
thadei ndunguru
January 24, 2014 at 12:45 pm
nimependa banda lako.nitajaribu kuwafuga then baada ya miezi 3 nitakupa jibu la mafanikio
LikeLike
happygod
January 29, 2014 at 10:01 pm
Ni kweli ugonjwa wa vifaranga wa kuku kushusha mabawa ni common sana kwa wa fugaji wa kuku hata mimi umeua vifaranga 20 kati ya 220 niliokuwa nao, lakini nilibahatika kupata tiba yake, kwa maelezo zaidi ni check kwa namba 0763744794, nitakuelekeza zaidi, thx
LikeLike
Ally salala
February 7, 2014 at 6:29 pm
mr ally,nimeona maelekezo yako kuhusu ugonjwa wa vifaranga kushuka mbawa,mi natarajia kuanza kufuga kuku kwa kuwa wewe ni mzoefu najua utanisaidia kwa mambo mengi ikiwemo namna ya banda zuri,vyakula na namna nyigine kulingana na mahitaji
LikeLike
mtemi daniel
February 10, 2014 at 3:12 pm
Mr. Simba nimeipenda kazi yako. Tafadhali nisaidie no. yako ya simu ndugu yangu.
Mahdi Koosa
LikeLike
Mahdi Koosa
February 9, 2014 at 12:31 pm
jamani na mimi nataka kuwa mfugaji wa kuku niasaidieni wadau namna bora
LikeLike
mtemi daniel
February 10, 2014 at 3:07 pm
Ndugu zangu ufugaji aina h unasaidia sana. Wanajamii ya ufugaji nahitaji kufuga ndege watwao Tombo au kwa jina la wenzetu Quails naweza kupata wapi nahitaji msaada wenu. Mimi simu yangu ni 0762246322
LikeLike
Kenneth Mwazembe
February 17, 2014 at 1:46 am
Heeee sijawahi sikia hao ndege je ukishafuga wauza au?wana faida gani?
LikeLike
mama sam
February 17, 2014 at 9:35 am
N kwa ajili ya kitgoweo kama kuku na pia kwa biashara japo hapa Tz inaonekana hawajulikani sana. Wenzetu Kenya walisha anza ufugaji na bei yake ni maqra mbili kuliko ya kuku. Ndege hao inawachukua miezi miwili na nusu toka kuanguliwa hadi kuanza kutaga mayai. Wanauzwa sana katika mahoteli ya kitalii jijini Nairobi. Tombo asili yake ni porini kama kanga. Wanafugwa pia katika nchi za kiarabu.
LikeLike
Kenneth Mwazembe
February 17, 2014 at 7:07 pm
Naombeni ushauri wenu mimi nataka kufuga kuku wa mayai njiagani nitumie
LikeLike
SAMSON ELIZEI
February 23, 2014 at 10:00 am
Dada Jenny samahani, naomba nifahamishe ratios za ulishaji chakula kwa kundi la kuku 100 kwa siku moja, wanatakiwa jula kiasi gani? nitashukuru ukinijuliaha kwani huwa nalisha tu mbaka wasaze wao.
LikeLike
samwel kaluwa
March 30, 2014 at 10:19 am
nsmba kupata picha ya kiota kizuri cha kutagia mayai kuku wangu hawatulii wanapofikia kutaga.thanks
LikeLike
happygod
May 1, 2014 at 1:57 pm
Kupata maelezo juu ya viota pitia hapa http://mkulimambunifu.org/?p=891
LikeLike
Mwang'oko Milamo
July 8, 2014 at 10:48 pm
da kiukweli nikiiangalia hiyo picha inapa wivu wakimaendeleo sana natamani ingekuwa milki yangu
LikeLike
Rabson Daudi
May 6, 2014 at 11:55 am
da kiukweli nikiiangalia hiyo picha inanipa wivu wakimaendeleo sana natamani ingekuwa milki yangu
LikeLike
Rabson Daudi
May 6, 2014 at 11:56 am
sasa dada mimi ninafuga kuku wa kienyeji, ila kwasasa nataka kufuga chotara lakini kabla ya kuwanunua nilikuwa nahitaji kujua jinsi ya kuwatunza mwanzoni
LikeLike
Rabson Daudi
May 6, 2014 at 12:09 pm
Nashukuru sana kwa picha hiyo ya banda la maana na linavutia sana,lakini swali langu kwako nikwamba je ninaweza kuchanganya kuku wa nyama na wa mayai?
LikeLike
mtemi daniel
May 6, 2014 at 10:09 pm
Mpo vzuri sana naombeni mntumie nots kwa email djmkole.dm@gmail.com
LikeLike
Denis mkole
May 26, 2014 at 1:19 pm
Habar zenu wapendwa.nimefurah kukutana nanyi kwenye hii blog.mimi nataka kuanza ufugaji wa kuku wa nyama kama 1000.naomba mnijuze ujenzi bora wa banda kwa idadi hyo ambao ni banda lenye ubora unagharimu sh ngapi?email yangu dijaothman@yahoo.com
LikeLike
hadija athuman
June 1, 2014 at 6:31 pm
Na etie ni upi ufugaji rahis kati ya kuku wa kienyej na kisasa
LikeLike
hadija athuman
June 3, 2014 at 4:16 pm
Kwa ufugaji wa kuku kama ukifuata kanuni za ufugaji bora wa kuku hakuna ufugaji mgumu. Watu huwa na mtazamo ya kwamba ufugaji wa kuku wa kienyeji ni rahisi. Si kweli kama hauta fuata kanuni bora za ufugaji wa kuku hao
LikeLike
Mwang'oko Milamo
July 8, 2014 at 11:09 pm
habar zenu jaman,
mie nu kijana nko mwanza na nnapenda sana ufugaji wa kuku wa kisasa,naombeni ushauri wenu nianze na kuku wap kati ya mayai au wa nyama na pia mtaji wake waweza kuwa kias gani
naombeni msaada wenu
asantenu
LikeLike
Goodluck
July 1, 2014 at 5:03 pm
Kama hujawahi kufuga kabisa ni vema ukaanza na kuku wachache ambao litakua ndio darasa lako. Jua ya kua licha ya kua na faida ufugaji wa kuku unachangamoto nyingi hivyo unapoingia katika utekelezaji ndipo utaziona mfano magonjwa. Hivyo anza na kuku 50 ama 100
LikeLike
Mwang'oko Milamo
July 8, 2014 at 11:03 pm
Habari wapendwa,mimi nafuga kuku wa mayai kwa awamu ya pili sasa,awamu ya kwanza nilikuwa na kuku 200 nimewauza april lakini hao kuku walikuwa wananyonyoka manyoya sana nimejaribu kubadilisha chakula lakini sikufanikiwa,sasa nina kuku 500 wa mayai ninatamanu sana waendelee vizuri bila kunyonyoka manyoa,naomba ushauri nifanyeje na tatizo ni nini hasa?
LikeLike
Mrs imelda Liwa
July 13, 2014 at 5:36 pm
Pia naomba mnisaidie mchanganyo wa chakula cha kuku kuanzia siku ya kwanza mpk wanayotaga
LikeLike
Mrs imelda Liwa
July 13, 2014 at 5:39 pm
Nashukuru kwa kunipa hamasa zaidi kwani mmi nimepata ujuzi zaidi kwa kuangalia banda nzuri ningeomba mnisaidie jinsi ya kuchanganya chakula na maji yachanganywe na nni kwa ajili ya kinga
LikeLike
robert kway
July 27, 2014 at 8:25 pm
Naomba kufahamu kuku mmoja wa mayai anahitaji eneo la sq. Mita ngapi? Utaratibu wa chanjo kuanzia ninapomnunua akiwa kifaranga, anakula kilo ngapi kwa siku?
LikeLike
Latifa Msangi
August 2, 2014 at 3:43 pm
dogo Latifa unataka kufuga kuku mmoja au
LikeLike
Gonsalva
August 4, 2014 at 11:16 am
Hbr wapendwa nimependa ufugaji wa kuku na mi nna mpango wa kufunga kuku wa nyama nnaomben maelekezo
LikeLike
bertha shirima
August 8, 2014 at 5:58 pm
nitapata wapi ya incubstor
LikeLike
rnaluyaga
August 17, 2014 at 2:34 pm
Ninazo manual incubators za mayai 60 ukiwa tayari nitafute kwa namba zifuatazo 0763 330 800, 0787 330 800, 0713 330 800
LikeLike
Mgawe Revocatus
August 17, 2014 at 11:50 pm
natamani nianze ufugaji wa kuku wa kienyeji nkwa ajiri ya nyama na mayai. naomba elimu so far ninao 150.kama darasa nilitamani nipanue mradi hadi kuku 2000-5000. naomba msaada wa jinsi ya kuandaa mabanda, kupata incubator ya hadi mayai 2000. na jinsi ya kuandaa vyakula vyao
LikeLike
Mhana RJ
September 2, 2014 at 11:06 pm
Naomba jane uwe mwalimu wangu kweli natamani kufika ulipofika
LikeLike
ngao kahema
September 9, 2014 at 12:40 pm
Nataka kuanza kufugakuku wa mayai ni dawa gani ambayo ni nzuri kwa kuwalinda kuku wangu na mambo gan natakiwa kuyazingatia sana ili kuwa na kuku bora
Mahenge niko dar
LikeLike
Mahenge
September 15, 2014 at 4:53 pm
Habari za kazi wapendwa!Hongereni wote kwa ujasiriamali, tunamshukuru sana alieyanzisha hii blogu. Lakini shida yangu kubwa ninyoiona naona kama maswali mengi hayajibiwi, naomba tusaidiane wapendwa kutoa ufahamu wetu kuhusu ufugaji kwa wale tusiojua vizuri na Mungu atawaneemesha mpaka mshangae. Pls wapendwa tusaidiane ktk hili!Kila la kheri na Mungu abariki kazi za mikono yenu nyote!
LikeLike
mama sam
September 17, 2014 at 9:41 am
Hivi kuna incubators zinazotumia umeme wa jua?
LikeLike
mama sam
September 17, 2014 at 12:18 pm
Habari mkuu zipo Na ninatengeneza inatumia watts 60
LikeLike
baba collin
September 21, 2014 at 10:15 am
BABA COLLIN NINAOMBA WASILIANO YAKO.
LikeLike
Mgawe Revocatus
September 21, 2014 at 7:53 pm
hongereni sana kwa kazi nzuri napenda sana na niko karibuni ss na mm kuweza kuanza biashara hii
LikeLike
rashidy
September 18, 2014 at 12:05 am
Zipo incubator za umeme wa jua. ninatengeneza ufanisi wake ni 89% inatumia watt 60. inacontrol joto automatic. kugeuza ni mannua ndani ya sekunde 3 unakua umegeuza mayai yote. inabeba mayai 90. . natengeneza kwa laki 1.70. natumia cool box kutengenezea. 0754078015
LikeLike
baba collin
September 21, 2014 at 10:20 am
Pia ninauza vifaranga wa malawi . Sh. 2000 akiwa na siku moja na kila wiki inaongezeka sh. 500. anakua amepata chanjo zote. 0754078015 niko mbeya
LikeLike
baba collin
September 21, 2014 at 10:23 am
habari baba Collin.
npo Dodoma je naweza kupata vifaranga wa mayai kwa bei ya 1700 kwa mmoja?nahitaji vifaranga 500 ndg yangu
LikeLike
mwamsema mwamsema
June 6, 2015 at 3:54 pm
nataka kujua nikitaka kufuga kuku wa mayai wapatao 500 natakiwa kuwa na kias gani cha pesa mpaka waanze kutaga?
LikeLike
peter
September 26, 2014 at 12:19 pm
ni blog nzuri sana
LikeLike
malipesa
October 7, 2014 at 12:37 am
Mimi ndio nimeanza ufugaji wa kuku wa mayai naitaji ushauri zaidi kuhusu magonjwa na soko
LikeLike
malipesa
October 7, 2014 at 12:39 am
asanten kwa elimu nzur
LikeLike
George Mwambene
October 25, 2014 at 4:14 pm
Habari zenu ndugu zangu,naomba nipate uzowefu wa Vifaranga vya Amadori,vinachukua muda gani mpaka kuwa kuku wa kufaa kuliwa,na naomba mnisaidie number za kampuni ya Amadori. number yangu 0784717042 au email.cmpuzu@gmail.com
LikeLike
christopher
November 13, 2014 at 4:08 pm
Jamani habari zenu,jina langu naitwa Noah Shaban Kasote.Elimu inayopatikana kwenye blog hii ni kubwa mno,hebu basi tujaribu kuitendea kazi(kuiishi)itatufaa sana
LikeLike
Noah Shaban Kasote
November 30, 2014 at 8:54 pm
Nimependa sana ufugaji wa kuku. Ni ninampango wa kuanza kufuga.
LikeLike
yohana jackson
December 20, 2014 at 6:27 pm
NI BANDA BORA KABISA SISI WATAALAMU WA MIFUGO TUNASHAURI JAMII KUJENGA MABANDA KAMA HAYA NA KUWA NA UFUGAJI WA MALENGO KAMA UWEZO NI MDOGO BASI UNAWEZA KUJENGA KWA MFUMO HUU BANDA DOGO KWA KUTUMIA MALIGHAFI ZINAZOPATIKANA KWA URAHISI KATIKA MAZINGIRA YANAYOKUZUNGUKA.
KAHEMA KIVARIA
LIVESTOCK FIELD OFFICER, MKINGA DISTRICT TANGA
CELL. 0659775800, E-MAIL; kahemakivaria@yahoo.com
KWA MSAADA TUWASILIANE TUTAELEKEZANA KWANI DUNIA NI KIJIJI BADILIKA SASA.
LikeLike
KAHEMA KIVARIA
December 21, 2014 at 3:10 pm
Mimi ni mfugaji nahitaji glop la wafugaji ili kujifunza zaidi.
LikeLike
John P Mwandika
December 21, 2014 at 3:37 pm
natafuta mashine ya kuangulia vifaranga nitahipata wapi kwa mwanza namba yangu ya simu ni 0765855583
LikeLike
muniru nasuhi
January 11, 2015 at 12:01 pm
nijuavyo mimi utaweza kuipata ktk ofisi za sido. mfano ukiwa dar waone sido karibu na tazara. na hata ukiwa huko mwanza uaweza ukaghalamia ili kupata mashhine bora na zenye uhakika
LikeLike
mwenda
January 15, 2015 at 6:11 pm
Nitafute kwa namba zifuatazo nikusaidie kupata incubetors hapa Mwanza zipo nyingi sana auto na manual 0763330800/0713330800/0787330800
LikeLike
Mgawe Revocatus
January 15, 2015 at 10:28 pm
Habari ndugu, naulizi soko la uhakika la kuku wa kisasa (Broilers), kwani ndio nataka kuanza kufuga.
LikeLike
Neema
February 23, 2015 at 1:52 pm
Habari ndugu, naulizia soko la uhakika la kuku wa kisasa (Broilers), kwani ndio nataka kuanza kufuga., tafadhali kwa anae fahamu tuwasiliane kwa na. 0766842252
LikeLike
Neema
February 23, 2015 at 1:54 pm
hongeren sana wadau nmependa elimu mnayoitoa.nami nitaifanyia kaz
ipasavyo
LikeLike
nyangulo mdogo
March 14, 2015 at 1:23 am
Kwanza ya yote asanteni kwa kupewa vwasaaa juu.
Pills ni kwamba nimejsribu sana ku-register Kafka j.f. kuweza kuchangia au ninapoona jambo jema nashindwa kufanya Chang ro wote.
LikeLike
helen
April 19, 2015 at 9:33 am
watu wengne sivizuri kutumia namba isiyo yako kuweka kwenye wateja unaowatarifu kuhusu upatikanaji wa mari kama una simu usitumie namba isiyo yako natafuta bata mzinga na bata bukini kama kuna mtu anao hapa mwanza tuwasiliane kwa namba 0765855583 nipo maheneo ya gana
LikeLike
muniru nasuhi
May 2, 2015 at 12:38 pm
asante sana kaka kuniunganisha. Nimesoma michango ya wadau wengine hapo juu, kwakweli ni elimu kubwa sana sijawahi ipata bali kwengine bali hapa.
LikeLike
thadei glorims
May 11, 2015 at 1:59 pm
nilitaka kujua kuku wa kizungu wa mayai..wanachukua mda gan toka wazaliwe hadi waanze kutaga?
LikeLike
sweetbert richard
May 27, 2015 at 8:33 am
habari ndg sweetbert Richard….kuku wa kizungu wa mayai au kwajina lengine LAYERS wanachukua miez 4 kamili kutaga kama utafuata ufugaj bora,zaid ya hapo ni kuanzia miez 4 na nusu.KAMA NIMEPATIA NI KUTOKANA NA UWEZO WA MUNGU KAMA NIMEKOSEA NI KUTOKANA NA UCHACHE WA ELIMU YANGU.Mwamsema mwamsema
LikeLike
mwamsema mwamsema
June 6, 2015 at 3:43 pm
Naomba kuuliza mabati ya asbesto yaliotumika miaka mingi ya nafaa kujengea bamda la kuku
LikeLike
george saulo
June 5, 2015 at 9:59 am
mm nahitaji vifaranga kama 500 nipo ifakara nitavipataje
LikeLike
mikdady juma
June 11, 2015 at 3:41 am
jamani mie nina eneo kubwa la kufugia na ninapenda sana kufuga kuku tatizo sina mtaji ninaomba kama kuna mtu anafahamu NGO’S ambayo wanaweza kutoa mkopo hata kama kwa kurudisha mkopo huo nitarudisha. 0784159427 , 0655159527
LikeLike
MBELYA GIGI
August 1, 2015 at 9:00 pm
naomba mnisaidieni jinsi yakutengeneza banda la kuku lililo bora kwa ufugaji wa kuku wa kienyeji na mfano wake munionyeshe kwa picha
mfano wa banda hilo
LikeLike
abelly
August 27, 2015 at 6:41 am
Hongera sana nimeona banda lako linashawishi japo ni post ya muda vp bado unaendelea natamani kujifunza mengi, mfano naona banda liko wazi sana kuku wanakingwa vp na baridi hasa nyakati za masika
LikeLike
Martin
September 27, 2015 at 7:24 am
Naomba kujua vipimo vya banda la kuku wa kienyeji wastan 100
LikeLike
DENIS MSHINDO
October 15, 2015 at 6:32 am
wadau hongereni sana kwa somo hili mujarrabu kwelikweli. hakuna haja yakupata mateso sana ukiamua kufika mbali ni kuweka jitihada na kumuomba Mungu. naomba na mm nipate majibu ya swali alilouliza kaka Denis Mshindo hapo juu
LikeLike
Ndosho
October 15, 2015 at 2:25 pm
habari ndugu yangu pole na majukumu . samahani mimi nafuga Bata BUKINI lakini tokea niwanunue hawaongezeki namaanisha hawatagi je nifanyeje ili watage? na nichakula gani niwape?
LikeLike
Januarius
November 6, 2015 at 8:11 pm
Ni mara ya kwanza kuingia kwenye mtandao huu,kwa kweli nimefaidika kutokana na mambo nilioyoweza kuyapata humu.Nawashukuruni kwa michango yenu kwani imenivutia sana.
LikeLike
zunny
November 12, 2015 at 4:00 pm
aisee very interesting na mm natarajia kufug kuku ngoja nvute subira alzie maxomo
LikeLike
mkapa bhulash
November 28, 2015 at 12:42 am
Kama mko na group whatsspp au telegram au lolote naomba mniunge kwa namba tie +255715246322
LikeLike
Kenneth Mwazembe
December 10, 2015 at 7:16 pm
japo ni muda mrefu sana tangu picha hiyo ya banda imepwekwa hapo bado ni nzuri ajabu na tupo wengi sana ambao tutaendelea kuitumia kama mfano na hakika inapendeza sana na kusababisha mtu apate mwamko na machungu ya kufanya kitu. Daima kila mtu duniani anatafuta jinsi ya ”kutoka” i.e kufanikiwa na hakika zipo njia nyingi tu ila wengi wetu tupo kama tumefungwa bongo na kushindwa kufikiri. Basi sasa na tuamke japo elimu yetu ndio inatubana uwezo wa kufikiri basi elimu hii ya pembeni itusaidie kuamka na kufanikiwa ndoto zetu. nimependa wazo la mwandishi kule juu kuwa tutengeneze kitu kama kamtandao fulani ka watu wenye obi moja
LikeLike
Deogratias
January 21, 2016 at 1:35 pm
Mimi ni Mfugaji Nina KUKU 2000 Kwa sasa natafuta soko no 0655390880 broiler.
LikeLike
John Mwandika
January 21, 2016 at 2:11 pm
Kwa wale wote wanao hitaji Kuku wanyama na kienyeji wanapatikana
Tupo dar & mosh
0743584661
LikeLike
Deogratius
January 23, 2016 at 10:40 pm
Nimependa hili darasa, Mimi ni mfugaji Ila sina uzoefu naomba kama kuna group mniunganisha Kwa 0763977770
LikeLike
Tatu
February 17, 2016 at 8:48 am
Pia ningependa kuona sample ya Banda linalotakiwa na kujua/kujifunza mbinu za ufugaji ili niweze timiza ndo to zangu, nipo Dar. Ahsanteni
LikeLike
Tatu
February 17, 2016 at 8:54 am
samahani na nkihitaji hao kuku wa mayai ntapataje
LikeLike
hafidh
October 12, 2017 at 5:07 pm
nashukuru kukutana na nyinyi mimi nataka kuanza kufuga kuku wa kienyeji ambao wameishaanza kutaga niitawapata wapi nielekezeni wapi nitawanunua na anza na kuku 25
LikeLike
edith lyaruu
February 19, 2016 at 11:01 am
Wapendwa habari zunu…
Nimevutiwa sanaa na mawazo yenu, na mimi nataka kuanzisha ufugaji wa kuku wa kienyeji kama kuna mtu ana ramani ya banda la kuku naomba anisaidie jmn..
natafuta ramani ambayo ni simple na ni cheap zaidi. Asanteni sana..
LikeLike
Jose
February 29, 2016 at 2:54 pm
HABARI ZENU WADAU?
NAWAKARIBISHA MJIPATIE HUDUMA ZIFUATAZO KWA AJILI YA UFUGAJI WA KUKU KIBIASHARA;
1; VIFARANGA WA KIENYEJI KUKU JAMII YA KULOIER, WENYE SIFA ZIFUATAZO:
Wanafugwa kienyeji; huachiwa huru kama kuku wa kienyeji au hufugwa kisasa ndani ya banda.
Hawapati magonjwa kirahisi.
Wanaanza kutaga wakiwa na miezi 5.
Majogoo huwa na uzito hadi kilo 5 na Mitetea 3.5 hadi 4.
Wanataga mayai 250 na zaidi kwa mwaka.
Mayai yake yamechavushwa(fertile), ila hawaatamii mayai, hutotoleshwa kwa Incubetors.
Wana rangi tofauti tofauti
Ni mchanganyiko wa mitetea na majogoo.
BEI ZETU NI KAMA ZIFUATAZO;
Jedwali elekezi la bei za vifaranga wa siku moja
JINSIA 1-4 5-9 10-14 15-24 25-49 50-99 100+ IDADI CHANJO.
MCHANGANYIKO 3,300 3,200 3,100 2,950 2,800 2,650 2,500 ….. ……….
TETEA 4,000 3,900 3,800 3,650 3,500 3,350 3,200 ….. ……….
JOGOO 2,900 2,800 2,700 2,550 2,400 2,250 2,100 ….. ……….
2; UANGUAJI WA MAYAI.
3: PIA TUNATOA HUDUMA NDOGO NDOGO ZIKIWEMO;
Huduma Ndogo na za ziada;
: Mafunzo-ushauri kwa wafugaji kuku na bata.
: Mikataba na wafugaji wa kuku na bata.
: Ujenzi wa Mabanda ya kisasa na bora.
: Usafirishaji wa Vifaranga Mikoa ya Arusha, Tanga, Dar, Manyara.
: Soko kwa Mazao ya kuku na bata.
: Matangazo ya ufugaji na bidhaa za kuku na bata.
: Unyonyoaji kuku.
: Ufungaji wa vifaa vya kisasa vya maji na vyakula mabandani.
: Utayarishaji wa michanganuo ya ufugaji bora kibiashara
: Uwezeshaji wafugaji wadogo katika kuongeza mitaji.
: Uchanganyaji wa chakula cha mifugo.
: Uongezaji dhamani mazao ya nyamanyama.
TUPO MKOANI KILIMANJARO, WILAYA YA MOSHI MJINI (MANISPA), KATA YA KARIWA CHINI.
KWA MAWASILIANO; TUANDIKIE Email: eligijohn@gmail.com NAUTAJIBIWA MARA,
PIA WAWEZA KUTUPATA KWA NAMBA ZA SIMU ZIFUATAZO;
TIGO; +255713399973,
AIRTEL; +255788684824,
VODACOM +255758634806.
KARIBUNI WOTE.
LikeLike
KUNDA J.
June 9, 2016 at 9:58 am
hongera nami nimekubali kupitian mafunzo haya
LikeLike
adautitasiani
June 17, 2016 at 5:13 pm
habari zenu wapendwa leo kwa mara ya kwanza nimeingia hapa mambo ni mazuri hongereni sana kwa kaz nzuri. nami natarajia kuwa mfugaji wa kuku wa kienyeji namalizia ujenzi wa banda naamini nitajua mengi sana kupitia hapa. Mungu awatangulie katika mradi huu mzuri na wenye faida kubwa
LikeLike
GISELA TARIMO
July 19, 2016 at 2:23 pm
wapendwa nimefurahiswa sana na mafunzo na ushauri wa ufugaji wa kuku wa kienyeji,mimi nimeanza kufuga ingawa napata changamoto za magonjwa hasa vidonda na kushusha mbawa,naomba kupatiwa utaalamu zaidi kwani nataka kuwa mfugaji wa mfano,pia natamani kufuga bata wa kawaida naomba kupata utaalamu wake zaidi.
LikeLike
bernadetaha maketa
July 28, 2016 at 1:17 pm
Jamani, nimefurahi sana kuona hili gruop la wafugaji wa kuku au wajasiliamali. Mimi ni mpenzi wa ujasaliamali kwa ujumula. Nilikuwa aina ya mambanda nikapata banda zuri ambalo limenisababisha kuona mawazo na mafunzo mbali mbali kutoka kwa wadau. Mimi ndo nimeanza kufuga nimeanza na kuku kama kumi. kwasasa natafuta kuku wa Kuloiler na kuchi au mayai yake, au vifaranga. aliye navyo naomba simu yake. Mimi naitwa Conso Muzale. simu yangu ni 0789 524 333. Pia naomba kuunganishwa kwenye kundi hili jamani.
LikeLike
Consolatha Panda Muzale
July 28, 2016 at 5:04 pm
MIMI NI MWANACHAMA WA KUNDI HILI NILIANZA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI
NIKAACHA.
SASA NAFUGA KUCHI NINAO WAKUBWA NA WADOGO MAYAI PIA
0763 330800
0787 330800
0713 330800
IKIWA UNAHITAJI NITAFUTE LAKINI UJIPANGE NA BEI PIA
LikeLike
REVOCATUS MGAWE
July 28, 2016 at 10:16 pm
Asante sana Mgawe, ntakutafuta. Blessed.
LikeLike
Consolatha Panda Muzale
July 29, 2016 at 8:18 am
asanteni jamani kama kunagroup whatsaapp naomba mniunge 0769864843
LikeLike
emanuel abel
August 5, 2016 at 7:07 pm
nataka kufuga kuku 500 je ni mtaji kiasi gani nianze nao
LikeLike
KAPERE
August 11, 2016 at 5:05 pm
Habari, naomba kuwa mmoja wa wanachama wa kundi hili, nimepitia baadhi ya comments na naoa upo mwanga mkubwa wa kujifunza mengi. Nafuga kuku pia wa kienyeji. Msaada.. kuku 250 wanahitajika kula chakula kiasi gani
LikeLike
Jacqueline
August 19, 2016 at 11:13 am
habari zenu wadau, nimependa na nimevutika na ufugaji na nna eneo la ft 75 kwa 60, ambalo cjajenga hata banda, na tatizo ni mtaji kuna mdau atanikopesha? pia c vaya kuja kukagua eneo lenyewe.
LikeLike
abbas khamis
August 30, 2016 at 4:13 pm
Habari mihangaiko , naomba picha za namna ya kutengeza mabanda ya kufugia kuku wa kisasa au kienyeji
LikeLike
Asagwile Kasake Mwasi
September 13, 2016 at 3:34 pm
kuku mia mbili wanakaa kwenye banda LA ukubwa gani
LikeLike
david luwaha
September 22, 2016 at 8:25 am
Asante kwa michango yenu, nimejifunza mengi sana. Tafadhari naomba namba za mfugaji yeyote alie karibu na wilaya ya kyela
LikeLike
Edwin
October 12, 2016 at 2:38 pm
wadau kwa hesabu za haraka haraka linaweza ku cost bei gani mpaka kukamilika kwa banda kama hilo
LikeLike
khasco
October 12, 2016 at 3:07 pm
Jaman mm ni mfugaji wa vifaranga lakn sijapata soko LA vifaranga na sijui nifanyeje kila mm napatikana pande za mwika moshi
LikeLike
Joshua
April 28, 2017 at 12:28 am
Naomba tuwasiliane kwa namba yangu hii 0752166507
LikeLike
Felix Michael
April 16, 2018 at 11:58 pm