Du! Ee bwana eee… bonge ya ajali!
Ni gari namba T 489 ARN.
Ni eneo la Njiapanda Segerea, Barabara ya Nyerere. Wakaazi wakishangaa lori lililoyumba na kufanya kreti za za kinywaji kumwagika na kulamba vumbi. Bahati nzuri hakuna liyethubutu kunywa au kufanya uhalifu mwingine, mfano, kujaribu kuproa vinywaji vilivyosalimika. Ila kama kawaida, hakuna dogo mjini. Watu kibao. Ipo haja ya kutoendekeza sana kudodosadodosa baadhi ya mambo yanapotokea. Wapo waliouliza, je, ingekuwa petroli, watu bado wangebaki hapo huku kumbukumbu za matukio kama ya kule Mbeya na la hivi karibuni kule Nakuru Kenya ambapo lori la mafuta lilipata ajali na watu kujaribu kujichotea mafuta hayo? Watu wapatao 130 waliteketea kwa moto na wengine wengi kujeruhiwa.
Leave a Reply