Ni katika makutano ya barabara za Bibi Titi Mohammed na Uhuru. Chunguza vizuri. Kuna nguzo yenye kuelekeza barabara ya Uhuru. Chini ya nguzo hiyo kuna mtu amekaa. Amejishika tama. Kuza kidogo hiyo picha ili umwone vizuri.
Tunapata tafakari nzito. Ni miaka 47 tokea Uhuru. Hali ya uchumi wetu ikoje? Hali ya maisha ya watu wetu ikoje? Maisha yamekuwa magumu zaidi. Uhakika wa kesho unazidi kutoweka. Uhuru tulio nao una maana gani? Hivi kwa nini tufike mahali ambapo watu wetu wengi wako kama huyu? Hawaishi kujishika tama? Kwa nini? Kwa nini watu wasukumwe na kuishia katika point ya kulipuka kama walivyolipuka kule Afrika ya Kusini? Niliwahi kuona lori limeandikwa ‘Sheria duniani, haki mbinguni’. Tutafakari. Tujadili. Tunakoenda siko. Azimio la Zanzibar limekuja na mengi. Haya ndiyo yanayozidi kututesa leo. Tumeweka kando ‘Ujamaa na Kujitegemea’. Tumebaki kuomba hata chakula wakati kila mahali katika Tanzania ukiweka mbegu au mche utaota na kukua. Sera. Siasa. Uongozi. Elimu. DUNI.