simbadeo2000

Bendera ya Taifa Letu …

dscf0047.jpg

Picha hii imepigwa jana saa 12.15 jioni pale ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Huenda mimi nimepitwa na wakati. Nilipokuwa kwenye mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria nilijifunza kuwa Bendera ya Taifa hushushwa kutoka kwenye mlingoti kila ifikapo saa 12 kamili jioni.

Inawezekana ni mimi ndiye niliyepitwa na wakati au inawezekana kabisa wale wenye jukumu la kushusha bendera hii pale ofisini kwa Mzee Kandoro walipitiwa wakati saa za mwishomwisho za 2007 zikiyoyoma.

Inawezekana pia ni ishara kuwa Watanzania huwa hatujali muda. Tunapanga wenyewe lakini ni sisi sisi ndiyo tunaovunja ahadi za muda tulizoweka. Wakati ni mali. Nidhamu katika kutunza muda ni muhimu kwa maendeleo ya aina yoyote ile.

 Nawatakia HERI na MAFANIKIO katika mwaka huu mpya wa 2008 ambao sasa hivi una umri wa nusu saa hivi.

Kila la kheri.

No Comments Yet »

Say something?Comments RSS TrackBack URI

About author

I am a citizen of Tanzania. I live in Dar es Salaam, commercial city of Tanzania. I am an editor, particularly dealing with books as well as other publications and related activities: editing, translating, supervising design and layout, monitoring printing, warehousing and dissemination of the books. I am also an author: I write children's story books, school textbooks and adult books. I undertake translation tasks from English to Kiswahili and vice versa. I do book indexing, that is preparing an index for a professional book. Contact: kakasimba@gmail.com . Feel free to get in touch with me.

Search

Navigation

Categories:

Links:

Archives:

Feeds