Mavazi … Chaguo lako
Mitindo ya mavazi ya siku hizi, inaniacha hoi. Sawa, kila mmoja ana fursa ya kuchagua avae namna gani … lakini hakuna mipaka kidogo walau … kuwastahi wengine. Labda mimi ni mtu mwenye mawazo mgando … lakini kuna umuhimu baadhi ya wadada wakasaidiwa kidogo katika uvaaji wao.
Lakini hili linanikumbusha jinsi suala la usawa wa kijinsia lilivyo na safari ndefu. Kwa nini stejini ukute mwanamuziki wa kiume yuko kwenye suti au mavazi yanayosetiri sehemu kubwa ya mwili huku mwanamuziki wa kike akiwa robo tatu uchi? Sio Bongo tu … hata kule ambako wanasema harakati za kudai usawa zimeanzia … why? Labda msomaji wewe una maoni fulani. Si vibaya ukitushirikisha. Tupo pamoja.




Kuvaa kama tutakavyo sawa..nakubaliana nawe kwa kweli wakati mwingine akina dada wanavaa kiasi kwamba unatamani kumpa kumpa nguo ndefu..sasa sijui ni kutaka kuonyesha mwili au nini? Sasa si afadhali tu hata kuacha kuvaa kabisa ..Halafu ebu fikiria kwa mfano TZ tuna minguo kibao na nzuri kabisa…mafundi wapo sijui tatizo liko wapi?….
yasinta/kapulya
June 17, 2012 at 5:07 pm
Mi nadhani malezi pia yanachangia pia kuiga makundi yasiofaa. Na inavyoonekana kwa kizazi hiki kilipofikia baada ya miaka kama mitano mbele wadada wengi watatembea uchi. Mungu atusaidie wadada tuweze kujitambua, kujiheshimu na kuishi katika maadili mazuri ya Kiafrika.
dorine
June 18, 2012 at 10:58 am