
Kikosi kamili cha Sitakishari Veteran Sports Club katika Bonanza Maalumu la kusherehekea kutimiza kwa mwaka mmoja tangu timu hiyo ianzishwe rasmi. Iliichapa timu ya Ukonga kwa mabao 2 – 0. Timu nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Boko, Ukonga, Pugu, Kitunda na Air Wing. Kandanda safi ilisindikizwa na mchezo wa kuvuta kamba na burudani safi ya muziki.

Kulia ni Mh. Stambuli, Diwani wa Kata ya Kipawa aliyekuwa mgeni rasmi katika Bonanza hilo; kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Sitakishari Veterani Sports Club, Mr Morris; Kulia kwa Bwa Stambuli ni Mr Elly Ngwala, aliyekuwa DJ na mhamasishaji mkuu.

Mwanadada mshika kibendera alimudu vema mechi zote zipatazo nane alizosimamia tangu asubuhi.

Washikaji kibao walikuwepo.

Mambo ya kuvuta kamba hayakukosekana. Mpaka tunakwenda press, Bonanza lilikuwa bado likiendelea.