
Historia hii itunzwe. Ni hazina kubwa itakayolisaidia Taifa hili katika miaka ijayo. Hao wanaoitwa ‘waendelezaji’ waende kuendeleeza jiji huko pembezoni, siyo hapa katikati.
Na mvua inapotua jijini Dar mambo huwa hivi mitaani:

Mitaa hubaki mitupu.

Na baada ya mitaro ya maji machafu kuziba, basi maji hufurika barabarani. Hali hiyo inapotokea, unachagua moja kati ya mawili – au unajitosa kukanyaka maji hayo au kulipa sh 100 ili uvushwe katika maji machafu kwa kubebwa kwenye mkokoteni. Mababa wa Jiji, kazi mnayo!

Kikosi kamili cha Sitakishari Veteran Sports Club katika Bonanza Maalumu la kusherehekea kutimiza kwa mwaka mmoja tangu timu hiyo ianzishwe rasmi. Iliichapa timu ya Ukonga kwa mabao 2 – 0. Timu nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Boko, Ukonga, Pugu, Kitunda na Air Wing. Kandanda safi ilisindikizwa na mchezo wa kuvuta kamba na burudani safi ya muziki.

Kulia ni Mh. Stambuli, Diwani wa Kata ya Kipawa aliyekuwa mgeni rasmi katika Bonanza hilo; kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Sitakishari Veterani Sports Club, Mr Morris; Kulia kwa Bwa Stambuli ni Mr Elly Ngwala, aliyekuwa DJ na mhamasishaji mkuu.

Mwanadada mshika kibendera alimudu vema mechi zote zipatazo nane alizosimamia tangu asubuhi.

Washikaji kibao walikuwepo.

Mambo ya kuvuta kamba hayakukosekana. Mpaka tunakwenda press, Bonanza lilikuwa bado likiendelea.

Ndiyo. Kiatu kimetulia. Na mguu kimepata. Ila Bongo yetu kwa kutotunza mazingira, kiboko. Hebu cheki hiyo chupa hapo pembeni.