simbadeo2000

Tuna historia … tuitunze

Mar 29
1 Comment

dscf0028

Historia hii itunzwe. Ni hazina kubwa itakayolisaidia Taifa hili katika miaka ijayo. Hao wanaoitwa ‘waendelezaji’ waende kuendeleeza jiji huko pembezoni, siyo hapa katikati.

Na mvua inapotua jijini Dar mambo huwa hivi mitaani:

dscf0034

Mitaa hubaki mitupu.

dscf0035

Na baada ya mitaro ya maji machafu kuziba, basi maji hufurika barabarani. Hali hiyo inapotokea, unachagua moja kati ya mawili – au unajitosa kukanyaka maji hayo au kulipa sh 100 ili uvushwe katika maji machafu kwa kubebwa kwenye mkokoteni. Mababa wa Jiji, kazi mnayo!


Posted in Siasa na jamii

Sitakishari Veterani yatimiza mwaka …

dscf0063

Kikosi kamili cha Sitakishari Veteran Sports Club katika Bonanza Maalumu la kusherehekea kutimiza kwa mwaka mmoja tangu timu hiyo ianzishwe rasmi. Iliichapa timu ya Ukonga kwa mabao 2 – 0. Timu nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Boko, Ukonga, Pugu, Kitunda na Air Wing. Kandanda safi ilisindikizwa na mchezo wa kuvuta kamba na burudani safi ya muziki.

dscf0061

Kulia ni Mh. Stambuli, Diwani wa Kata ya Kipawa aliyekuwa mgeni rasmi katika Bonanza hilo; kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Sitakishari Veterani Sports Club, Mr Morris; Kulia kwa Bwa Stambuli ni Mr Elly Ngwala, aliyekuwa DJ na mhamasishaji mkuu.

dscf0050

Mwanadada mshika kibendera alimudu vema mechi zote zipatazo nane alizosimamia tangu asubuhi.

dscf0075

Washikaji kibao walikuwepo.

dscf0070

Mambo ya kuvuta kamba hayakukosekana. Mpaka tunakwenda press, Bonanza lilikuwa bado likiendelea.


Posted in Siasa na jamii

Kiatu …

Mar 29
1 Comment

dscf0023

Ndiyo. Kiatu kimetulia. Na mguu kimepata. Ila Bongo yetu kwa kutotunza mazingira, kiboko. Hebu cheki hiyo chupa hapo pembeni.


Posted in Siasa na jamii

About author

I am a citizen of Tanzania. I live in Dar es Salaam, commercial city of Tanzania. I am an editor, particularly dealing with books as well as other publications and related activities: editing, translating, supervising design and layout, monitoring printing, warehousing and dissemination of the books. I am also an author: I write children's story books, school textbooks and adult books. I undertake translation tasks from English to Kiswahili and vice versa. I do book indexing, that is preparing an index for a professional book. Contact: kakasimba@gmail.com . Feel free to get in touch with me.

Search

Navigation

Categories:

Links:

Archives:

Feeds