
Ni Abdallah. Mwenyeji wa Mtwara. Anasema kazi yake hii inalipa zaidi kuliko kupalilia mikorosho kule Mtwara. Hapa jamii nzima ina wajibu. Nini kiwe vipaumbele vya Taifa letu: kuchuuza mali zilizotengenezwa na wenzetu wa nje au kutilia mkazo uzalishaji unaoliletea Taifa hili fedha za kigeni? Je, kwa nini kwa mfano isifike mahali Bw Abdallah akaona kuwa inalipa zaidi sana kupalilia korosho kuliko kuchuuza soksi (cheap) za kutoka Uchina? CCM ilyo madarakani ina kazi ya kuwaeleza wananchi mkakati wake wa kubadili kitendaguro hiki.