
Mlimani City, Dar es Salaam. Ingefaa kuwa na maeneo ya namna hii sehemu nyingi za Dar es Salaam na mikoani. Mahali pa kununua na kuuza. Wawekezaji wapewe uendeshaji wa masoko yetu hata yale tunayoita ‘Soko Mjinga’. Hii haimaanishi kuwa ‘wawekezaji lazima wawe wa kutoka nje. Watanzania wenzetu wanaweza kuendesha sehemu kama hizi na kuweka viwango bora vya ubora.

Mlimani City in the making. Ni eneo la kupendeza. Kama si kubananisha sana nyumba, ingefaa nyumba nyingi mitaani zijengwe kwa muundo huo – hasa katika high density areas – kwani makazi bora ni muhimu kwa maendeleo ya kiakili, kiafya, kiroho na kwa aina zote za ukuaji. Inafaa kutembelea hapa.