
Kijani ni afya. Utembeapo eneo lenye mimea kwa wingi tena inayotunzwa vizuri, unajisikia kuwa na hali tofauti katika akili, mwili na hata roho yako. Kijani ni afya.
Imefika wakati tusambaze ukijani kama huu mahali mbalimbali katika jiji hili. Mazingira ya namna hii yatachangia katika kuongeza ubora wa afya zetu. Tunapokuwa na afya njema, tuna nafsi ya kufiriki vizuri zaidi na kwa hiyo kujiletea maendeleo sisi wenyewe na taifa letu. Tushikamane kutunza mazingira ili mazingira yatutunze na kutuletea tija.
Picha inaonyesha eneo lililo karibu na makutano ya Barabara za Ohio, Bibi Titi na Ali Hassan Mwinyi.

Hii ni kuwatakia ‘A Happy Valentine’s Day’. Pichani mdau wa blog hii, Anna, wa Njia Panda Segerea, Dar es Salaam.

Kituo cha Basi cha Banda la Ngozi, Barabara ya Nyerere, Dar es Salaam. Ni saa 11.10 jioni.
Imagine. Ulikuwa na siku ngumu. Siku ambapo ulitumia akili na nguvu nyingi katika kazi zako. Inapofika saa ya kutoka kazini, kituoni magari ya abiria yanakupita tu yakiwa yamejaa. Pengine ni wakati sasa tutafute ufumbuzi wa kudumu kuhusu usafiri wa umma ili mtu asisubiri zaidi ya dakika tano kituoni.

Ni Abdallah. Mwenyeji wa Mtwara. Anasema kazi yake hii inalipa zaidi kuliko kupalilia mikorosho kule Mtwara. Hapa jamii nzima ina wajibu. Nini kiwe vipaumbele vya Taifa letu: kuchuuza mali zilizotengenezwa na wenzetu wa nje au kutilia mkazo uzalishaji unaoliletea Taifa hili fedha za kigeni? Je, kwa nini kwa mfano isifike mahali Bw Abdallah akaona kuwa inalipa zaidi sana kupalilia korosho kuliko kuchuuza soksi (cheap) za kutoka Uchina? CCM ilyo madarakani ina kazi ya kuwaeleza wananchi mkakati wake wa kubadili kitendaguro hiki.

Ni gari namba T 489 ARN.

Ni eneo la Njiapanda Segerea, Barabara ya Nyerere. Wakaazi wakishangaa lori lililoyumba na kufanya kreti za za kinywaji kumwagika na kulamba vumbi. Bahati nzuri hakuna liyethubutu kunywa au kufanya uhalifu mwingine, mfano, kujaribu kuproa vinywaji vilivyosalimika. Ila kama kawaida, hakuna dogo mjini. Watu kibao. Ipo haja ya kutoendekeza sana kudodosadodosa baadhi ya mambo yanapotokea. Wapo waliouliza, je, ingekuwa petroli, watu bado wangebaki hapo huku kumbukumbu za matukio kama ya kule Mbeya na la hivi karibuni kule Nakuru Kenya ambapo lori la mafuta lilipata ajali na watu kujaribu kujichotea mafuta hayo? Watu wapatao 130 waliteketea kwa moto na wengine wengi kujeruhiwa.

Mlimani City, Dar es Salaam. Ingefaa kuwa na maeneo ya namna hii sehemu nyingi za Dar es Salaam na mikoani. Mahali pa kununua na kuuza. Wawekezaji wapewe uendeshaji wa masoko yetu hata yale tunayoita ‘Soko Mjinga’. Hii haimaanishi kuwa ‘wawekezaji lazima wawe wa kutoka nje. Watanzania wenzetu wanaweza kuendesha sehemu kama hizi na kuweka viwango bora vya ubora.

Mlimani City in the making. Ni eneo la kupendeza. Kama si kubananisha sana nyumba, ingefaa nyumba nyingi mitaani zijengwe kwa muundo huo – hasa katika high density areas – kwani makazi bora ni muhimu kwa maendeleo ya kiakili, kiafya, kiroho na kwa aina zote za ukuaji. Inafaa kutembelea hapa.

Maisha ubishi. Ni ujumbe muruwa. Tafsiri nyingi. Mojawapo ni kuwa tusikubali kushindwa – hasa kama tuna sababu ya kutoshindwa. Falsafa hiyo tunaweza kuitafsiri katika maisha yetu mmojammoja au katika familia, jamii ndogondogo mpaka ngazi ya Taifa. Maisha ubishi. Nimekubali.